POPULARITY
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, imetahadharisha umma kuhusu kuenea kwa kasi kwa ugonjwa wa Ebola.
Send us Fan MailMheshimiwa Balozi Mobhare Matinyi akizungumza mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho wa kibalozi kwa Mheshimiwa Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, katika hafla iliyofanyika kwenye Ikulu ya Algiers tarehe 10 Juni, 2026. Balozi Mobhare Matinyi anayeiwakilisha Tanzania nchini Algeria, ametoa wito kwa Watanzania kutumia fursa za ushirikiano mzuri baina ya nchi hizi kufaidika katika nyanja mbalimbali.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umetamatishwa leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Idhaa hii imepata fursa ya kuzungumza na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya mkutano huu muhimu, Mtanzania Zuleikha Tambwe. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo..Hatari ya Ebola wakati wa Kombe la Dunia la Soka 2026 ni ndogo na hakuna sababu ya mashabiki kubadili mipango yao ya safari kuelekea Canada, Mexico na Marekani, limesema Shirika la Afya Duniani WHO kombe hilo liking'oa nanga leo. Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Ulaya, Hans Henri P. Kluge, amesema hakuna wagonjwa wa Ebola katika nchi hizo wala Ulaya na amesisitiza, “Safirini kama kawaida na furahieni mashindano hayo.” WHO imefafanua kuwa Ebola haisambai kwa njia ya hewa na visa vingi vipo katika maeneo ya mbali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Annalena Baerbock, amehitimisha ziara ya siku mbili jijini Nairobi nchini Kenya, ambapo amesisitiza nafasi muhimu ya Umoja wa Mataifa katika kuendeleza maendeleo, amani na ushirikiano barani Afrika. "Kila siku Umoja wa Mataifa na washirika wake huokoa maisha. Bila UN, mamilioni ya watoto wasingepata elimu kupitia UNICEF wala chanjo muhimu kupitia WHOna tusingekuwa na ushirikiano kama huu."Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, uliokuwa unafanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani umefikia tamati leo. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.” Kibaya Laibuta, Jaji wa Mahakama ya Rufani nchini Kenya, ambaye pia ni mlemavu aliyeoona au kipofu, ameshiriki na anaeleza alivyouona mkutano huu.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Kesho kutwa Alhamisi ya Juni 11, macho na masikio yanaelekezwa Mexico, Canada na hapa Marekani kwa ajili ya fainali za kombe la dunia kwa mpira wa miguu, au soka al maarufu kabumbu. Ingawa hivyo zama za sasa za mchezo huo maarufu zaidi duniani zinakumbwa na madhara ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Ongezeko la joto kali linavuruga mechi na kuzua wasiwasi kuhusu mustakabali wa mchezo huo. Ni kwa kuzingatia hilo, Sekretarieti ya Mkataba wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, UNFCCC inamulika suala hilo na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike kwani hivi sasa madhara ya joto kali kwenye kabumbu ni dhahiri. Feissal Kirwa anamulika hilo kupitia video iliyoandaliwa na UNFCCC.Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Takriban watoto milioni 138 duniani kote bado wako katika ajira za watoto, wakiwemo watoto milioni 54 wanaofanya kazi hatarishi. Hayo yamo katika ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa ILO. Katika ujumbe wakwe kwenye ripoti hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Gilbert F. Houngbo, ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka ili kubadili hali hii.“Habari njema ni kwamba hadi sasa tuna wagonjwa 19 ambao wamepona, hivyo utambuzi wa mapema na matibabu vinaokoa maisha,” Huyo ni Mkurugenzi wa Operesheni za Tahadhari na Hatua za Dharura za Afya wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani (WHO), Dkt. Abdirahman Mahamud, akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva leo kwa njia ya video kutoka Bunia katika Jimbo la Ituri, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, jimbo ambalo linachangia asilimia 94 ya wagonjwa wote wa Ebola.Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umeanza leo Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York na utaendelea hadi 11 Juni. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.” Washiriki wanajadili namna ya kutokomeza ukandamizaji, ukatili na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu, kuimarisha mifumo ya huduma na msaada, pamoja na kuongeza ushiriki na uwakilishi wao katika maisha ya kisiasa na umma.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "MKWARUZO."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kumeundwa miungano miwili ya kisiasa. Kundi la kwanza linaitwa "C4" linalounga mkono mabadiliko ya katiba, chini ya rais Felix Tshisekedi. Nao vigogo wa upinzani wakiongozwa na Martin Fayulu, Moïse Katumbi na wengine, wao wameunda C64" vuguvugu linalopinga marekebisho yoyote na kuilinda katiba ya sasa. Nini hatima ya makundi haya ? Tunachambua.
Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema zaidi ya watu 900 wanashukiwa kuwa wameambukizwa ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Shirika la Afya Duniani limetangaza mlipuko wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda ni dharura ya afya ya umma inayotia wasiwasi kimataifa.WHO inasema mlipuko huo hauja fikia vigezo vya dharura ya janga, lakini nchi zinazo changia mipaka ya ardhi na DRC ziko katika hatari kubwa ya usambaaji zaidi.Kwa wakazi wa Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wamekuwa na mambo mengi ya kuhofia kutokana na uhasama ambao umekuwa ukiendelea kati ya vikosi vya serikali na wapiganaji waasi.Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema Jumatatu itafungua vituo vitatu vya matibabu, kwa ajili ya watu walioambukizwa virusi vya Ebola katika jimbo la Ituri.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW70 uliofanyika mwezi Machi mwaka huu hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo tulipata fursa ya kuzungumza na washiriki wakiwemo wawakilishi wa mashirika ya wanawake. Miongoni mwao ni Severina Lemachokoti kutoka asasi ya kiraia ya Naretu Girls and Women Empowerment Programme iliyoko kaunti ya Samburu nchini Kenya, ambaye katika mahojiano na Flora Nducha ameelezea jinsi mila na desturi kwa wanawake na wasichana kutorithi chochote kwenye jamii yao zinavyoanza kuyoyoma. Pia tunamsikia kutoka Salome Gatakaa Araka wa FODDAJ ambalo ni Jukwaa la Maendeleo ya Wanawake, Demokrasia na Haki, nchini Kenya ni shirika la kiraia ambalo mwaka huu kwa mara nyingine lilishiriki mkutano huo wa CSW70. Baada ya kushriki vikao mmoja wa viongozi wa shirika hilo amezungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa na ndio msingi wa mahojiano haya.Tunakuletea pia muhtasari wa habari zikiwemo za hali ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, na Sudan, pamoja na masuala ya afya tukimulika yanaoendelea kuhusu virusi vya Hanta au Hantavirus.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi amedokeza juu ya uwezekano wa kuwania muhula wa tatu, na kuchelewesha uchaguzi mkuu unaotarajiwa katika muda wa miaka miwili ijayo.
Hatua ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kuingia kwenye makubaliano na Marekani ili kuwapokea wahamiaji haramu waliofukuzwa nchini humo, kumezua mjadala mzito katika nchi hiyo inayoendelea kukabiliwa na utovu wa usalama, hasa maeneo ya Mashariki. Kwanini kuna mvutano ?
Taarifa kuu wiki hii ni ripoti ya tume ya uchunguzi nchini Tanzania iliyosema watu 518 walifariki wakati wa ghasia za uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka uliopita. Tunaangazia pia taarifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo licha makubaliano ya kusitisha vita kati ya waasi wa M23/AFC na serikali ya Kinshasa, kuendelea kushuhudiwa kwa mapigano ya mara kwa mara. Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Leo wa 14 alikamilisha ziara ya siku kumi barani Afrika juma hili; na katika mzozo wa Mashariki ya kati, Marekani yaongeza muda wa kusitisha mapigano na Iran, hatua sawa ikichukuliwa kati ya Israeli na Lebanon.
James Swan, ambaye ni Mwakilishi Maalum mpya wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, leo Ijumaa amewasili huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kwanza ya kuendeleza juhudi za amani kwenye eneo hilo la mashariki mwa nchi lililogubikwa na vita. Assumpta Massoi na taarifa kamili
Hii leo jaridani tunaangazia ziara ya Mwakilishi Maalum mpya wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini DRC James Swan, vijana na biashara ndogo ndogo katika ukanda wa Gaza, na hali ya kibinadamu kwa wakimbizi wanaorejea kwao katika jimbo la Upper Nile Sudan Kusini.James Swan, ambaye ni Mwakilishi Maalum mpya wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, leo Ijumaa amewasili huko Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kwanza ya kuendeleza juhudi za amani kwenye eneo hilo la mashariki mwa nchi lililogubikwa na vita.Hili ngumu ya kiuchumi inayoendelea kuzorota katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel imewafanya vijana waliokuwa wakisoma vyuo vikuu na wahitimu kuhangaika kufanya kazi ndogo ndogo ili kujikimu baada ya ndoto zao za masomo na taaluma kuvurugwa na vita iliyodumu kwa miaka mitatu.Mwaka mmoja baada ya mapigano makubwa kusababisha vifo na kuwafanya maelfu ya watu kuyahama makazi yao mjini Nasir, jimbo la Upper Nile, dalili za ahuweni zinaanza kuonekana. Wakazi wanarejea polepole, wakijenga upya maisha yao na kurejesha hali ya kawaida kwa msaada wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya mauaji wa wanawake na wasichana Gaza, ukatili wa kijinsia na wa kingono unaotumiwa kama silaha ya vita Sudan, na msaada wa dawa na matibabu ya bure nchini DRC yanyoendeshwa na walinda amani wa MONUSCO kutoka Tanzania.Uchambuzi mpya wa utafiti uliotolewa leo Aprili 17 na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake, UN Women umeweka wazi kuwa zaidi ya wanawake na wasichana 38,000 wameauawa kati ya mwezi Oktoba mwaka 2023 na Desemba 2025 huko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ikiwa ni wastani wa takribani wanawake na wasichana 47 wanaouawa kila siku. Anold Kayanda ameufuatilia utafiti huo na kutuandalia taarifa ifuatayo.Ukatili wa kijinsia na wa kingono unatumiwa kama silaha ya vita nchini Sudan, jambo ambalo limesahaulika huku migogoro ikiendelea katika maeneo mengi mengi kote duniani amesema Tonderai Chikuhwa, Mshauri Mwandamizi wa Sera katika Ofisi ya Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Ukatili wa kijinsia katika Migogoro, katika mahojiano na Khaled Mohamed wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa.Raia wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waishio mji wa Oicha uliopo Mavivi katika Jimbo la Kivu Kaskazini, wamewashukuru walinda amani kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Kikundi cha Tano Cha Utayari (TANZQRF-05), kinachohudumu chini ya mwamvuli wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini humo (MONUSCO) kwa kutoa msaada wa dawa na huduma za kitabibu kwenye Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mji wa Oicha wiki hii.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Raia wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waishio mji wa Oicha uliopo Mavivi katika Jimbo la Kivu Kaskazini, wamewashukuru walinda amani kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Kikundi cha Tano Cha Utayari (TANZQRF-05), kinachohudumu chini ya mwamvuli wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini humo (MONUSCO) kwa kutoa msaada wa dawa na huduma za kitabibu kwenye Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mji wa Oicha wiki hii. Private Habibu Shaban alikuwa shuhuda wa tukio hilo ungana naye kwa taarifa hii
Uganda ni moja ya nchi zinazohifadhi wakimbizi wengi zaidi duniani. Kwa Afrika ni ya kwanza ikihifadhi wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Burundi, rwanda, Sudan, Sudan Kusini na hata Kenya. Katika mada kwa kina hii tunaangazia wakimbizi kutoka Sudan ambao Uganda iliwapokea na kuwapa makazi katika Makazi ya Wakimbizi ya Kiryandongo yaliyoko magharibi mwa nchi. Abdelmonem Makki wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa hivi karibuni ameyatembelea makazi hayo na kuzungumza na wakimbizi hao kutoka Sudan. Na sasa kwa lugha ya Kiswahili, Feissal Kirwa wa Idhaa hii anasimulia.
Awamu ya tisa ya mazungumzo ya amani kati ya waasi wa M23/AFC na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, yalianza siku ya Jumatatu Aprili 13 nchini Uswizi. Ujumbe wa Qatar ambao ni wasuluhishi, akiwemo mjumbe wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika Massad Boulos, wanashiriki. Nini Ajenda ya mazungumzo haya ? Raia wa DRC wategeme nini ? Tunachambua.
Hii leo jaridani tunamulika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC), hali Mashariki ya Kati, Amerika ya Kati, kilimo cha migomba kinachohimili mabadiliko ya tabianchi huko Pemba, Zanzibar nchini Tanzania na katika kujifunza lugha ya Kiswahili ni uchambuzi wa neno, 'Nyapanyapa.'MUHTASARIMabaraza ya Umoja wa Mataifa lile la Usalama na lile la Haki za Binadamu kwa nyakati tofauti yajadili hali ya usalama na haki za binadamu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Huko Mashariki ya Kati hali ya usalama na kibinadamu yazidi kuwa tete Lebanon na Ukanda wa Gaza kutokana na mashambulizi yanayoendelea kila uchao.Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO azungumzia hali tete ya afya nchini Cuba kutokana na kutokuwepo kwa huduma ya uhakika ya umeme.MADA KWA KINA: Jinsimafunzo ya kilimo cha migomba kinachohimili mabadiliko ya tabianchi yalivyoanza kuonesha matokeo chanya huko Pemba, Zanzibar nchini Tanzania. Mradi ni wa FAO kwa kushirikiana na SMZ.JIFUNZE KISWAHILI- Mchambuzi wetu Onni Sigalla kutoka BAKITA Tanzania anafafanua maana ya neno 'Nyapanyapa.'Karibu na mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina leo baada ya takribani wiki mbili mkutano wa 70 wa CSW70 unakunja jamvi. Maudhui yalikuwa kuendeleza Haki, Sheria na Kuchagiza Hatua kwa ajili ya wanawake na wasichana, na sasa washiriki wanaeleza Idhaa hii wanachoondoka nacho.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo akizungumza na waandishi wa habari Mjini Brussels Ubelgiji kuhusu kinachoendelea Mashariki ya Kati akiwa a na Rais wa Baraza la Muungano wa Ulaya António Costa, ametoa ujumbe mahsusi kwa wahusika wakuu wa mzozo huo. Amesema “Kwanza kwa Marekani na Israel, ni wakati muafaka kumaliza vita hivi ambavyo viko hatarini kutodhibitiwa kabisa, vikisababisha mateso makubwa kwa raia, na athari zake zinaenea katika uchumi wa dunia kwa kiwango cha kutisha, zikiwa na uwezekano wa kusababisha madhara makubwa zaidi hasa kwa nchi zenye maendeleo duni”Kisha ujumbe wake wa pili ni “Kwa Iran, acheni kushambulia majirani zenu. Hawakuwa sehemu ya mgogoro huu. Baraza la Usalama limelaani mashambulizi haya na kuamuru yasitishwe, pamoja na kuagiza kufunguliwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz.”Na kuelekea Siku ya Kimataifa ya Furaha hapo Kesho Machi 20 raia Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, eneo lililoghubikwa na mizozo ya silaha wanaeleza furaha kwao inamaanisha nini.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Wanawake kutoka jumuiya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wana jiandaa kwa sherehe maalum ya siku ya wanawake.
Hii leo jaridani tunaangazia habari ya kusikitisha ya kifo cha mfanyakazi wa UNICEF nchini DRC, na ujumbe wa washiriki wa mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW70 leo unaendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York.Shirika la UNICEF limesema limesikitishwa na kushtushwa na kifo cha mfanyakazi wake Karine Buisset kilichotokea katika shambulio linaloripotiwa kufanywa na droni katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhriy a Kidemokrasia ya Congo DRC, eneo ambalo kwa muda mrefu limekumbwa na mapigano na hali mbaya ya kibinadamu. Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, Catherine Russell kupitia mtandao wake wa kijamii wa X, amesema shirika hilo pamoja na wafanyakazi wake duniani wameumizwa sana na tukio hilo.Oluwaseun Ayodeji Osowobi, mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Nigeria amezungumzia umuhimu wa kushirikisha wanaume katika harakati za kupigania haki za wanawake duniani wasichana.Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW70 leo unaendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York ukiwa umeingia siku ya 3. Na vijana hawakusahaulika wamepewa nafasi ya kutoa maoni yao na mapendekezo yao kuhusu maudhui ya mwaka huu ambayo yanasisitiza umuhimu wa kuchukuliwa kwa hatua madhubuti kuhusu haki za wanawake, usawa wa kisheria na ushiriki wa vijana.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, leo limesema limesikitishwa na kushtushwa na kifo cha mfanyakazi wake mmoja, Karine Buisset kilichotokea katika shambulio linaloripotiwa kufanywa na ndege isiyo na rubani yaani droni katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, eneo ambalo kwa muda mrefu limekumbwa na mapigano na hali mbaya ya kibinadamu. Anold Kayanda na taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania ambako UNHCR inasema ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi wa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi. Pia tunakuletea jifunze Kiswahili.Ushirikiano wa kimataifa kupitia mikataba ya kimataifa ya kudhibiti dawa umesaidia watu duniani kote, imesema hii leo Bodi ya Kimataifa ya kudhibiti dawa za kulevya, INCB wakati ikizindua ripoti ya mwaka 2025 kuhusu hali yad awa za kulevya duniani.Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu wamelaani vikali ukatili unaodaiwa kufanywa na kundi la waasi la M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, dhidi ya watetezi wa haki za binadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu.Na leo ikiwa ni siku ya tatu ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) huko The Hague Uholanzi kuthibitisha iwapo kuna ushahidi wa kutosha wa kumfikisha mahakamani Rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte kwa madai ya uhalifu dhidi ya ubinadamu unaohusianana kile kilichoitwa “vita dhidi ya dawa za kulevya” nchini mwake, wakili upande wa utetezi, Nicholas Kaufmann amesema hakuna uhusiano uliothibitishwa kati ya hotuba zake za “kipekee, zenye kauli kali” na mauaji anayotuhumiwa kuyafanya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “ANUIAYE KUKUTUKANA HAKOSI MATANGO”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Redio Duniani likitupeleka nchini Tanzania kusikia jinsi ambavyo redio inavyochochea maendeleo ya kijamii, nchini Uganda kumsikia mkimbizi kutoka DRC, na katika ukanda wa Gaza ambako redio inaunganisha tena jamii ndani ya vifusi.Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.Katika maeneo ya migogoro, duniani redio huwa nguzo ya utulivu na wakati mwingine daraja la kuokoa maisha. Na ndivyo ilivyokuwa kwa mkimbizi Bahati Yohane kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwani kwake, redio haikuwa tu combo cha habari ilikuwa dira ya kuokoa maisha yake.Kabla ya vita vya sasa kuanza katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lilalokaliwa kimabavu na Israel, Redio ilikuwa chombo muhimu kwa umma na kwa hakika umuhimu wake haujakoma isipokuwa huduma ya matangazo ya redio ndio iliyokuwa imekoma kutokana na vituo vya redio kusambaratishwa kwa makombora, lakini sasa juhudi zinafanyika kuirejesha huduma hiyo muhimu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Katika maeneo ya migogoro, redio huwa nguzo ya utulivu. Mathalani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Radio Okapi ya Umoja wa Mataifa imekuwa sauti ya kuaminika na kuwasaidia wakimbizi kusaka usalama tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 kama sehemu ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO. Mmoja wa wakimbizi kutoka Mashariki mwa DRC ambaye sasa anaishi kambi ya wakimbizi ya Kyangwali nchini Uganda amemweleza John Kibego kutoka Redio washirika wetu Kazi Njema FM ya mjini Hoima jinsi matangazo ya redio Okapi yalivyonusuru maisha yake wakati wa vita
Hii leo jaridani Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na Wakili Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kutoka Tanzania aliyehudhuria Mkutano wa Kamisheni ya Maendeleo ya Kijamii (CSocD64).Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yametoa onyo kali kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayowakumba watoto nchini Sudan. Mashirika hayo lile la kuhudumia watoto UNICEF, la afya WHO na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu wamenasema ghasia zisizoisha, njaa na magonjwa vinawasababisha watoto kupoteza Maisha na kudhoofika, huku mashambulizi dhidi ya vituo vya afya na vikwazo vya upatikanaji wa misaada vikizorotesha juhudi za kuwaokoa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, msemaji wa UNICEF, Ricardo Pires, amesema “Katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Darfur Kaskazini, zaidi ya nusu ya watoto wote wanakabiliwa na utapiamlo mkali, si makadirio, si mfano, imethibitishwa.”.Kikosi cha 12 cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania TANZBAT 12 kinachohusumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Condo DRC chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO kimeendelea kudumisha uhusiano wa kijamii na wakazi wa mji wa Beni Mashariki mwa DRC, kwa kutoa msaada wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi katika shule ya msingi Ngite iliyopo eneo la Mavivi. Mkuu wa shule hiyo Neema Nyamwaka amewashukuru walinada amani hao kutoka Tanzania kwa kujali sekta ya elimu.Leo ni siku ya mikunde duniani Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO likisistiza umuhimu kwa chakula hicho kwa lishe na mazingira. Huko Kigoma Tanzania FAO kupitia mpango wa Pamoja wa KJP imekuwa ikitoa mafunzo kwa wakulima kuhusu umuhimu wa mazao ya jamii ya mikunde huyu ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona nchini Vietnam, na harakati za kutokomeza ukeketaji nchini Kenya.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Ninamualika Rashid Malekela aliyeifuatilia kwa kina taarifa hiyo ili atueleza zaidi.Nchini Vietnam taifa lililoko kusini-mashariki mwa Asia, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona anajitahidi kuhakikisha anatimiza ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano licha ya vikwazo anavyokumbana navyo kila uchao, na hii ni kwa sababu si kwamba njia ni rahisi bali kwa sababu dhamira yake ni kubwa zaidi.Ukeketaji au FGM ni jinamizi linalowaandama waathirika maisha yao yote likisababisha changamoto sio tu za kimwili lakini pia za kiafya na kuwaacha na makovu yasiyofutika. Katika Kaunti ya Tana River Kusini Mashariki mwa Kenya tunakutana na manusura na shujaa mwanaharakati wa kupambana na mila hiyo potofu ya ukeketaji Saadia Hussein, raia wa Somalia anayeishi Kenya hivi sasa. Mkurugenzi mtendaji na mwanzilishi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Brighter Society Initiative anatusimulia safari yake ya machungu ya ukeketaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Rashid Malekela ameifuatilia kwa kina taarifa hiyo na anaeleza zaidi.
Hii leo jaridani kesho ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa saratani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika hatua ambazo ni uzinduzi wa Mpango wa Utekelezaji wa Kitaifa wa kutokomeza saratani ifikapo mwaka 2030.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani, WHO, leo limetoa ombi la dola bilioni moja ili kukabiliana na majanga ya afya mwaka 2026 katika dharura 36 zilizo mbaya zaidi duniani. Ombi hilo linalenga kusaidia huduma za afya zinazookoa maisha katika nchi zilizoathiriwa na migogoro na majanga, zikiwemo Gaza, Sudan, Haiti na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Mashariki ya Kati, wakati muda ukiendelea kuyoyoma kwa maelfu ya wagonjwa mahututi huko Gaza, kufunguliwa tena kwa kivuko cha Rafah kunaleta mwanga wa matumaini. Kivuko hicho kilifunguliwa Jumatatu baada ya kufungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, chini ya mpango wa amani unaoungwa mkono na Marekani, na kuruhusu uhamisho wa kwanza wa wagonjwa tangu mwaka 2025.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo liimesema linaongeza juhudi zake zamsaada wa msimu wa baridi nchini Ukraine huku watoto na familia wakikabiliwa na kukatika kwa umeme, kukosa vipasha joto na maji kufuatia mashambulizi yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya nishati na baridi kali. Tangu Novemba, shirika hilo limesambaza jenereta 106 kote nchini kusaidia huduma za maji na mifumo ya kupasha joto, huku takribani jenereta 150 zaidi zikitarajiwa kuwasili katika wiki zijazo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "KUNVI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya ambako wasichana juhudi za kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) zimewezesha vijana wa kike kushiriki masomo ya Teknolojia ya Habari na Maewasiliano, TEHAMA na kujifunza stadi za teknolojia ili waweze kuedeleza biashara ya mtandaoni pamoja na matumizi mengine.Zaidi ya watu nusu milioni wameathiriwa na mafuriko makubwa katika mikoa ya kusini na kati ya Msumbiji, huku mvua kubwa ikiendelea kuvuruga usafiri, huduma za afya na njia za ugavi. Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA nchini humo, Paola Emerson, amewaambia waandishi wa habari huko Geneva, Uswisi kuwa majimbo ya Gaza, Sofala na Maputo ndiyo yaliyoathirika vibaya zaidi.Huko Mashariki ya Kati mapema leo Jumanne, vikosi vya Israel vimebomoa kwa tingatinga makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, huko Yerusalemu Mashariki eneo linalokaliwa kimabavu na Israel. Mkuu wa UNRWA, Philippe Lazzarini, amelieleza tukio hilo kama “shambulio lisilo na kifani dhidi ya Umoja wa Mataifa,”.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, leo imesema imeanza kutekeleza mpango wa kurejesha kwa hatua mamlaka ya dola katika mji wa Uvira, mashariki mwa nchi hiyo, kufuatia kuondoka kwa kundi lenye silaha la AFC/M23. Serikali inasema vikosi vya usalama, polisi na huduma nyingine za serikali vinarejea ili kulinda raia, kulinda mali na kuleta utulivu katika eneo hilo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu ONNI SIGALA Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno “ KING'ANI”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika mwaka mpya 2026 kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ambao wanaendelea kukabiliwa na hali ngumu ya maisha katika kambi za wakimbizi na katika makazi ambayo ni magofu na vifusi vya nyumba zilizoharibiwa wakati wa vita baina ya Jeshi la Israel na Wanamgambo wa Hamas.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linasema licha ya sitisho la mapigano huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, maisha ya watoto bado yako katika hali tete, huku zaidi ya watoto 100 wakiwa wameuawa tangu Oktoba mwaka jana lilipoanza sitisho hilo.Vinywaji vyenye sukari na vileo vinazidi kuwa nafuu kwa bei kutokana na viwango vya kodi kwa muda mrefu kuwa vya chini katika nchi nyingi, jambo linalochochea unene kupita kiasi, ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya moyo, saratani na maradhi mengineyo hasa miongoni mwa watoto na vijana balehe, zimesema ripoti mpya mbili zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Ituri, mashariki mwa nchi hiyo ambako ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umepatia mafunzo ya ujasiriamali wafungwa kwenye gereza kuu lililoko Bunia, ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "MAHULUCHI"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Karibu katika muziki Ijumaa, makala maalumu ya RFI Kiswahili inayokuletea vibao vya kukumbukwa vilivyoacha alama kubwa katika historia ya muziki wa dunia.Wiki hii tunasafiri kimuziki kutoka Marekani, kupitia Karibiani, hadi Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, tukifurahia nyimbo zenye ujumbe wa furaha, mapenzi, imani na utu. Safari yetu inaanza nchini Marekani kwa kibao “Celebration” cha kundi la Kool & The Gang wimbo uliogeuka kuwa nembo ya sherehe duniani kote, ukiwahamasisha watu kusahau huzuni na kusherehekea maisha. Kutoka hapo tunatua Karibiani kupitia “Jamaica Farewell” wa Don Williams, wimbo wenye ladha ya country na mguso wa kisiwa, unaoelezea mapenzi, kumbukumbu na uchungu wa kuaga ardhi unayoipenda. Safari inaendelea nyumbani Afrika Mashariki kwa kibao cha Kiswahili “Mulofa wangu” cha marehemu Daudi Kabaka kutoka Kenya, wimbo wa mapenzi uliojaa hisia nzito na lugha tamu, unaothibitisha ubora wa muziki wa zamani wa Afrika Mashariki. Tunafunga safari yetu Afrika ya Kati kwa “Le Bon Samaritain” wa gwiji wa rumba Papa Noël kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wimbo unaochanganya ala za gitaa za kipekee na ujumbe wa utu, huruma na kusaidiana katika jamii.
Hii leo jaridani tunaangazia hali nchini Venezuela operesheni ya kijeshi ya Marekani, afya ya uzazi Tana River nchini Kenya, na wanawake wakimbizi wa DR Congo wanaopitia ukatili wa kijinsia wakikimbia machafuko. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana leo katika kikao cha dharura baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela tarehe 3 Januari mwaka huu, hatua iliyozua hofu ya kuongezeka kwa hali ya kutokuwa na utulivu nchini humo na katika eneo zima.Huko nchini Kenya katika kaunti ya Tana River, hali mbaya ya hewa na migogoro imesababisha takriban watu 140,000 kuyahama makazi yao. Upatikanaji wa huduma za afya nao umekuwa mgumu na kuongeza magumu hususani kwa wanawake na watoto. Katika kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Afya nchini humo inashirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO katika kutoa huduma za afya kipaumbele kikielekezwa kwenye masuala ya uzazi salama.Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA), nchini Burundi, linaongeza juhudi zake kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) wanaokimbia mapigano yanayoendelea mashariki taifa hilo la Maziwa Makuu ili kulinda afya, usalama na utu wao na wa jamii zinazowapokea.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA), nchini Burundi, linaongeza juhudi zake kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) wanaokimbia mapigano yanayoendelea mashariki taifa hilo la Maziwa Makuu ili kulinda afya, usalama na utu wao na wa jamii zinazowapokea. Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia wakimbizi kutoka DR Congo wanaokimbilia Burundi, lishe bora kwa watot nchini Zambia, na afya ya uzazi na msaada wa UNFPA kwa wasichana vijana nchini Kenya. Kilio cha wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC cha kupatiwa msaada ukiwemo wa chakula kimeitikiwa na Japani, moja ya mdau wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP ambapo shirika hilo limepatiwa dola laki sita na elfu ishirini na tano.Nchini Zambia, mafunzo ya mapishi yanayotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto, UNICEF, kwa wanawake yamefanikiwa kubadilisha namna familia zinavyowalisha watoto wao, kwa kutumia vyakula ambavyo tayari vinapatikana katika mazingira yao.Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya watu, UNFP limechukua hatua kukabiliana na changamoto ya mimba za utotoni zinazochochewa na vikwazo vya kijamii na utamaduni pamoja na upungufu wa huduma za afya ya uzazi na kijinsia zinazofaa kwa vijana. Msichana mmoja anasimulia masaibu aliyopita.Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!
Kilio cha wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC cha kupatiwa msaada ukiwemo wa chakula kimeitikiwa na Japani, moja ya mdau wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP ambapo shirika hilo limepatiwa dola laki sita na elfu ishirini na tano, kama anavyosimulia Assumpta Massoi.
Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya WFP ya uhakika wa chakula mwaka 2026 duniani, wakimbizi kutoka DRC, waliovuka mpaka na kuingia Burundi, na kilimo cha umwagiliaji kwa jamii za Hirshabelle nchini Somalia. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema ukosefu wa chakula utaendelea kuwa katika viwango vya kutisha katika mwaka ujao wa 2026, huku mamilioni ya watu wakikabiliwa na njaa kali duniani.Kutana na Maseka ambaye ni miongoni mwa makumi ya maelfu ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waliovuka mpaka na kuingia nchi Jirani ya Burundi baada ya ghasia kulazimisha familia yake kukimbia mashariki mwa DRC.Jamii za wakulima katika mkoa wa middle Shabelle, Somalia, zimeathiriwa vibaya na ukame na mafuriko yanayodhoofisha kilimo na uhakika wa chakula. Ili kukabiliana na hili, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), Somalia kwa ufadhili wa Serikali ya Uswisi imetekeleza mradi wa BRiMS unaolenga kuimarisha mnepo kwa wakulima kupitia ukarabati wa miundombinu ya vijijini, urejeshaji wa mifumo ya umwagiliaji, na kuijengea jamii uwezo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Kutana na Maseka ambaye ni miongoni mwa makumi ya maelfu ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waliovuka mpaka na kuingia nchi Jirani ya Burundi baada ya ghasia kulazimisha familia yake kukimbia mashariki mwa DRC. Flora Nducha na taarifa zaidi
Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili, akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia tiba asili, machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na ubakaji unaotumika kama silaha ya vita nchini humo humo.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, linaweka mkazo mpya wa kisayansi katika tiba asili au mitishamba, wakati mawaziri, wanasayansi na viongozi wa jamii za asili kutoka zaidi ya nchi 100 wakikutana mjini New Delhi India kuanzia leo kuangazia mchango wa tiba za asili.Kuongezeka kwa machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumesababisha watu wengi kuyahama makazi yao ndani na kumbilia kusaka hofadhi nchi Jirani ya Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wakimbizi limeeleza mpaka sasa karibu wakimbizi 64,000 tayari wamewasili Burundi, na idadi ikitarajiwa kuongezeka.Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili, akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Kuongezeka kwa machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumesababisha watu wengi kuyahama makazi yao ndani na kumbilia kusaka hifadhi nchi Jirani ya Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wakimbizi limeeleza mpaka sasa karibu wakimbizi 64,000 tayari wamewasili Burundi, na idadi ikitarajiwa kuongezeka. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Sudan Kusini kufuatilia mradi wa kilimo cha mpunga ulivyoleta ustawi kwa jamii ya katikati mwa Sudan unaofanikishwa kwa msaada wa mafunzo wa walinda amani wa UN kutoka Korea Kusini wanaohudumu katika UNMISS kupitia wanasayansi na wakulima wa eneo la Bor katika. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa methali.Mapigano makali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 70, kuwafurusha watu zaidi ya 200,000, na kusitisha msaada wa chakula kwa maelfu. Umoja wa Mataifa unasema hali katika Kivu Kusini imezorota kwa kasi, huku msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP ukisimama na shule zaidi ya 30 zikigeuzwa makazi ya dharura. Katika taarifa yake, Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq, amesema hali imefikia kiwango cha hatari, akionya: “Familia zinazoishi kwa njaa sasa zinagawana chakula chao cha mwisho na watu waliokimbia makazi. Hii ni dharura inayovuka mipaka.” UN inazitaka pande zote kusitisha mapigano mara moja na kuruhusu misaada kufika kwa walio hatarini.Mkutano wa kikao cha 7 wa Baraza La Mazingira la Umoja wa Mataifa UNE-7 unaeelekea ukingoni jijini Nairobi Kenya na miongoni mwa washiriki ni kijana mwanaharakati wa mazingira kutoka asasi ya Umoja wa Mataifa YUNA nchini Tanzania Ally MwamzoraNa leo Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Milima, ukisisitiza umuhimu wa milima kama “kitovu cha maji ya dunia.” Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, takriban asilimia 70 ya maji safi ya Dunia yamehifadhiwa kama theluji au barafu, yakitoa mito inayosambaza maji ya kunywa, kilimo, viwanda, na umeme wa maji na takriban watu bilioni mbili, ikiwa ni pamoja na jamii nyingi za asili, wanategemea maji ya milima kwa mahitaji yao ya kila siku, maisha, na tamaduni zao. Wataalamu wanasisitiza kuwa kulinda mazingira ya milima ni muhimu ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa vizazi vijavyo.Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na leo zinaanza siku 16 za uanaharakati kuelimisha umma kuhusu janga la ukatili wa kijinsia, tunamsikia mmoja wa waathirika wa ukatili wa kingono.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa onyo kali kuhusu ongezeko la ukatili mtandaoni dhidi ya wanawake na wasichana.Ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa na uhalifu UNODC inaonya kwamba mwaka 2024, wanawake na wasichana 50,000 waliuawa na wapenzi au jamaa sawa na mwanamke mmoja kila dakika 10.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) inaonya kwamba uchumi wa Eneo la Palestina Linalokaliwa kwa Mabavu na Israel umerudi nyuma miaka 22 kwa muda usiozidi miaka miwili kwani umeingia katika hali mbaya zaidi ya mdororo kuwahi kurekodiwa, huku miongo ya maendeleo ikifutwa na operesheni za kijeshi zilizodumu kwa muda mrefu pamoja na vizuizi vya muda mrefu.Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya maendeleo na mabadiliko ya tabianchi barani Afrika, mashindano ya mpira wa miguu yanayofahamiaka kama Hope Championship kwa watu waliokatwa viungo katika Gaza na ukatili wa kijinsia.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo ametoa ujumbe mzito kwenye Mkutano wa Muungano wa Afrika AU na Muungano wa Ulaya EU, unaofanyika mjini Luanda, Angola akionya kuwa dunia “inabadilika kwa kiwango cha kutisha,” huku janga la tabianchi, ukosefu wa usawa na mvutano wa kimataifa vikichochea misukosuko mipya duniani.Tukielekea katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake hapo kesho Novemba 25 leo tunakupeleka Kenya kwake Geradline Ndayisenga, raia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) ambaye sasa anaishi ukimbizini kwenye eneo la Kitengela, Kaunti ya Kajiado nchini humo, anasema kama si usaidizi wa ushauri wa nasaha alioupata kutoka shirika la kiraia la Forum for Women Development, Democracy and Justice, FODDAJ nchini humo, basi hajui maisha yake yangalikuwa vipi.Mashindano ya mpira wa miguu yanayofahamiaka kama Hope Championship kwa watu waliokatwa viungo katika Ukanda wa Gaza yamemalizika majuzi baada ya siku nne mfululizo za michuano. Mashindano haya yanaandaliwa na Chama cha Soka cha Watu Waliokatwa Viungo cha Palestina kama sehemu ya juhudi za kuwasaidia majeruhi na kuthibitisha ushiriki wao endelevu katika shughuli rasmi za michezo.Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!
Tukielekea katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake hapo kesho Novemba 25 leo tunakupeleka Kenya kwake Geradline Ndayisenga, raia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) ambaye sasa anaishi ukimbizini kwenye eneo la Kitengela, Kaunti ya Kajiado nchini humo, anasema kama si usaidizi wa ushauri wa nasaha alioupata kutoka shirika la kiraia la Forum for Women Development, Democracy and Justice, FODDAJ nchini humo, basi hajui maisha yake yangalikuwa vipi. Je ilikuwaje? Tuungane na Sheilah Jepngetich kwa simulizi zaidi.
Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ujulikanao kama MONUSCO, leo umelaani vikali mashambulizi makubwa yaliyofanywa na kundi lenye silaha la Allied Democratic Forces ADF kati ya tarehe 13 na 19 Novemba 2025 katika baadhi ya maeneo ya Lubero, jimboni Kivu Kaskazini na kukatili maisha ya raia wengi. Flora Nducha na maelezo zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, mbinu bunifu za kilimo cha kakao nchini Peru, na mradi wa miundombinu wa kupunguza athari ya mafuriko na kugeuza maji ziada kuwa rasilimali muhimu kwa jamii nchini Rwanda.Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ujulikanao kama MONUSCO, leo umelaani vikali mashambulizi makubwa yaliyofanywa na kundi lenye silaha la Allied Democratic Forces ADF kati ya tarehe 13 na 19 Novemba 2025 katika baadhi ya maeneo ya Lubero, jimboni Kivu Kaskazini na kukatili maisha ya raia wengi.Katika msitu wa Amazon upande wa nchi ya Peru, jamii za watu wa asilizimeonesha namna mbinu bunifu za kilimo zinaweza kuongeza uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Yote haya yanakuja wakati dunia ikiendelea kujadili mustakabali wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika mkutano wa Umoja wa Mataifa COP30 unaoendelea huko Belém, Brazil.Mwezi Mei 2023, Rwanda nchi iliyozungukwa na milima ilikumbwa na mafuriko makubwa yaliyosababisha maporomoko ya ardhi na kusababisha maji kutoka katika milima ya volkano, yakiambatana na mawe mazito kuharibu mashamba, makazi na barabara. Baada ya mafuriko hayo ili kupunguza athari za majanga kama hayo, kwa wakati mwingine Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) nchini Rwanda, kwa ufadhili wa Serikali ya Japan, linatekeleza mradi wa Kukabiliana na Majanga Yanayohusiana na Maji katika wilaya za Rutsiro na Burera. Lengo ni kupunguza Athari na kugeuza maji ziada kuwa rasilimali muhimu kwa jamii.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Brazil kwenye mkutano wa COP30, ambako Dkt. Richard Muyungi, Mjumbe maalumu kwenye masuala ya mabadiliko ya tabianchi na mazingira kutoka nchini Tanzania anaeleza ni nini bara la Afrika linahitaji.Umoja wa Mataifa umekaribisha kupitishwa kwa Azimio namba 2803 la Baraza la Usalama kuhusu Gaza hapo jana, ukilitaja kuwa hatua muhimu katika kuimarisha usitishaji mapigano. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, anazitaka pande zote kuheshimu kikamilifu makubaliano hayo na kutafsiri kasi ya kidiplomasia kuwa hatua za dharura na za wazi kwa watu walioko katika eneo hilo. Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Guterres, Stéphane Dujarric, amesema Umoja wa Mataifa umejizatiti kuongeza misaada ya kibinadamu na kuunga mkono jitihada zinazoelekezwa katika hatua inayofuata ya usitishaji mapigano.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), hali ya kibinadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini bado ni tete. Mkurugenzi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu, Kanda ya Afrika Patrick Youssef ambaye amerejea hivi karibuni kutoka DRC amewaleza waandishi wa habari jijini Geneva, Uswisi kwamba raia wa DRC wanaendelea kubeba mzigo mzito wa mapigano, hata wakati shughuli chache za kibiashara zikiendelea kurejea Goma. Ametoa tahadhari kuwa mgogoro huo unakabiliwa na upungufu mkubwa wa ufadhili, ukatili wa kingono unaongezeka, na zaidi ya asilimia 70 ya watu waliojeruhiwa kwa silaha mwaka huu ni raia.Kuanzia leo tarehe 18 inaanza Wiki ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usugu wa Vijiumbemaradhi dhidi ya dawa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linaonya kuwa usugu wa vimelea yaani hali ambapo bakteria, virusi na vijidudu vingine havidhuriki tena kwa dawa tayari unatishia mifumo ya afya, uchumi na uhakika wa chakula. Kwa kaulimbiu “Chukua Hatua Sasa: Linda Leo Yetu, Linda Mustakabali Wetu,” WHO inatoa wito kwa serikali, wahudumu wa afya, wakulima, wadau wa mazingira na umma kuchukua hatua madhubuti kutekeleza ahadi za kisiasa ili kupunguza kuenea kwa maambukizi sugu ya dawa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Jarida hii leo tunamulika harakati za kuzuia mauaji ya kimbari El Fasher, Sudan, hakuna dalili za kumalizika kwa janga la njaa mashariki mwa DRC na furaha kwa watoto waliopatiwa mabegi ya kwenda shule huko Tigray, Ethiopia.Unapokabiliana na ukatili na mauaji ya kimbari ni vema kuhakikisha wanaotekeleza wanafahamu kuwa wanafuatiliwa na kutazamwa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi yao, amesema Chaloka Beyani Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari.Mgogoro katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) unaendelea kuwa mbaya huku mapigano yakizidi, na kusababisha makumi ya maelfu ya watu kukimbia makazi yao na kuzidisha njaa kali, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeeleza leo.Nchini Ethiopia, Kaskazini Magharibi mwa jimbo la Tigray watoto wamefurahia kupatiwa vifaa kwa ajili ya kurejea upya shuleni baada ya vita ya muda mrefu, shukrani kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.