Podcasts about septemba

  • 16PODCASTS
  • 504EPISODES
  • 22mAVG DURATION
  • 1MONTHLY NEW EPISODE
  • Feb 1, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about septemba

Latest podcast episodes about septemba

Jukwaa la Michezo
AFCON 2025: Uganda, Tanzania kundi moja katika mashindano ya mwezi Disemba

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Feb 1, 2025 23:57


Hii leo tumeangazia yaliyozungumziwa kwenye mkutano mkuu wa jinsia wa Afrika Mashariki jijini Nairobi, shirikisho la kimataifa la mchezo wa baiskeli yapinga madai kuwa Rwanda itapokonywa haki za kuandaa mashindano ya chipukizi ya dunia mwezi Septemba kufuatia mzozo unaoendelea DRC, uchambuzi wa droo ya AFCON 2025, maandalizi ya CHAN 2024 tarehe mpya zatajwa na uchaguzi wa CAF mwaka huu. Pia tumechabua hatua ya mchujo mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya na tetesi za uhamisho ulaya.

Habari za UN
Msichana Bangladesh: Sikufahamu ufundi bomba ni nini, sasa ILO imeniwezesha

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 1:40


Nchini Bangladesh, mradi wa kuimarisha stadi na kufungua fursa za kiuchumi, ISEC miongoni mwa wanawake na vijana, umewezesha wasichana kuvunja mwiko na kuingia kwenye tasnia ambazo zimezoeleka kuwa ni za wanaume, mathalani ufundi bomba. Mradi huo unaolenga wanufaika 24,000 wenye umri kati ya miaka 18 na 35 unatekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO kwa kushirikiana na serikali ya Bangladesh.Video ya ILO hapa Cox's Bazaar inamleta kwako mmoja wa wanufaika hao ambaye hata hivyo jina lake halikutajwa, akiwa ameshikilia vifaa vya ufundi bomba anasema, awali sikufahamu kuhusu hii kozi hadi nilipofahamu kupitia Idara ya Maendeleo ya Vijana. Hii ni mara ya kwanza fursa hii imetufikia katika shule ya sekondari ya juu ya Moheshkhali. Tunajifunza stadi badala ya kupoteza muda nyumbani itanisaidia maisha yangu ya baadaye.Nikihitimu masomo naungana na kaka kwenye duka lakeAnakiri kuwa kabla ya kushiriki mafunzo haya hakuwa anafahamu kabisa ufundi bomba ni kitu gani. Lakini sasa amejifunza kuhusu vifaa mbalimbali ikiwemo msumeno wa mabomba, spana na kadhalika.ILOMradi wa kuimarisha stadi na kufungua fursa za kiuchumi, ISEC miongoni mwa wanawake na vijana, umewezesha wasichana Cox's Bazaar nchini Bangladesh.Na ndoto yake ni kwamba nikihitimu masomo nitakwenda kuungana na kaka yangu kwenye duka lake linalounza vifaa vya ujenzi. Nataka niwe mjasiriamali kama yeye, nijitegemee na nisaidie familia yangu. Siku hizi kwenye nyingi zilizoendelea na hata hapa Bangladesh wasichana wanafanya aina zote za kazi.Wanaweza kufanya kazi ngumu kama wanaume, nami nataka kuwa hivyo.Video ya ILO inamalizika mnufaika huyu amekamilisha kufunga bomba na sasa maji yanatoka, na mkufunzi anatumia maji hayo kunawa mikono.Malengo namba 4, 5, na 8 ya SDGs yanatekelezwaMradi huu ulizinduliwa mwezi Septemba mwaka 2023 ukifadhiliwa na…

Habari za UN
UN: Vifo vitokanavyo na baridi Gaza vinazuilika, usitishaji mapigano na misaada ndio jawabu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 3, 2025 1:58


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM leo limeonya juu ya vifo vitokanavyo na msimu wa baridi kali Gaza likisema limesikitishwa sana na athari mbaya za mvua za msimu wa baridi na baridi kali kwa Wapalestina waliokimbia makazi yao na kuishi katika mazingira magumu huko Gaza, kwani hilo ni janga la kibinadamu lisilo na kifani. Kupitia taarifa iliyotolewaleo mjini Geneva Uswisi Mkurugenzi Mkuu wa IOM Amy Pope  amesema "Watu walio katika mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na takriban watoto wachanga saba, wamekufa kutokana na baridi kali au hypothermia, na vifo hivi vya kusikitisha vinasisitiza haja ya haraka ya makazi na msaada mwingine wa kibinadamu kuwafikia watu wa Gaza mara moja," Ameongeza kuwa hali hii inachochea janga zaidi la kibinadamu ambalo tayari linawakumba watu waUkanda wa Gaza. Mvua kubwa na mafuriko yameyakumba makazi ya wakimbizi wa ndani yaliyojengwa kwa mahema na kulazimisha familia kuachwa katika maeneo ya wazi kwenye hali mbaya ya baridi, zikijitahidi kutengeneza mahema yaliyoharibika kutokana na matumizi ya miezi kadhaa. © UNRWAChakula kinagawiwa kwa watu waliokimbia makazi yao huko Jabalia, kaskazini mwa Gaza.Vikwazo vya Israel ni changamoto kwa misaadaPia IOM imesema vikwazo vya utaratibu wa kufikia wenye uhitaji, kama ilivyoripotiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA, vimezuia kwa kiasi kikubwa utoaji wa misaada, huku watu 285,000 pekee wakipokea msaada wa makazi tangu Septemba 2024. Kwa mujibu wa IOM hadi kufikia Katikati ya Desemba mwaka jana inakadiriwa kuwa watu wapatao 945,000 bado wanahitaji msaada wa haraka wa kukabiliana na msimu wa baridi ikiwemo nguo za kuongeza joto, mablanketi na tepu za kuima mahema dhidi ya mvua na baridi. Tangu Katikati ya Novemba mwaka jana IOM imewasilisha karibu vifaa 180,000 vya makazi ya dharura kwa washirika ndani ya Gaza na ina zaidi ya vifaa milioni 1.5 vya msimu wa baridi ikiwemo mahema, vifaa vya kuziba  na vitanda ambavyo viko tayari kwenye maghala na sehemu zavivuko, lakini vikwazo vikali vya ufikiaji vinawazuia kufikia wenye uhitaji. © UNICEF/Abed ZaqoutWavulana wawili wakibeba chupa za maji katika kambi ya wakimbizi inayofadhiliwa na UNWRA huko Khan Younis kusini mwa Gaza.Usitihsaji mapigano ndio suluhuIOM imesisitiza wito wake wa dharura wa kusitisha mapigano ili kuwezesha utoaji salama na wa haraka wa msaada wa kuokoa maisha kwa wale wanaouhitaji sana. Pia inasisitiza wito wake kwa pande zote kuzingatia sheria za kimataifa za kibinadamu, kuhakikisha ulinzi wa raia, kuachiliwa kwa mateka wote na kuruhusu ufikiaji salama, wa haraka, usiozuiliwa na endelevu wa wenye uhitaji. Watu wa Gaza wanastahili usalama, makazi na utu. IOM iko tayari kuhamasisha misaada na kusaidia jamii zilizofurushwa, lakini fursa ya ufikiaji wa kibinadamu lazima itolewe ili kuwezesha hili amesisitiza mkuu wa IOM. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema Licha ya hali ngumu, timu za UNRWA zinaendesha makao yote ya Umoja wa Mataifa, na kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu wanaohitaji. Limeongeza kuwa Vita vilipoanza karibu miezi 15 iliyopita, UNRWA iligeuza shule zake, vituo vya afya, na maghala kuwa makazi na kuna wakati ambapo vita ikiendelea UNRWA ilipokea watu milioni 1 waliokimbia makazi yao 

Habari za UN
COP29 Georgina Magesa: Watoto wana haki ya kuishi katika mazingira salama

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 4:01


Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 unaoendelea huko Baku Azerbaijan umeleta pia watoto na vijana wanaharakati wa mazingiria kutoka kote ulimwenguni na kuwapatia fursa kuketi katika meza moja na viongozi ili kuhakikisha mustakabali wao umewekwa katika ajenda ya mkataba huo. Jukumu lao kama wachechemuzi wa mabadiliko chanya na hitaji la mazungumzo na ushirikiano kati ya vizazi lilitambuliwa rasmi katika matokeo ya Mkutano wa Zama Zijazo, SOTF mnamo Septemba 2024.Georgina Magesa, msichana mwenye umri wa miaka tisa na mwanaharakati wa mazingira, ambaye amewakilisha watoto wenzake kutoka Tanzania katika Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 huko Baku, Azerbaijan. Anatoa ujumbe mahsusi akianza kwa kusistiza kuwa watoto pia wana mchango katika kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi.“Watoto wenzangu duniani kote, nyie pia mnaweza kuleta mabadiliko chanya. Anza na hatua ndogo pia muwe na ndoto kubwa. Panda miti. Hifadhi maji. Jifunze kuhusu mazingira yetu. Kwa Pamoja vitendo vyetu vidogo vitageuka mabadiliko makubwa”Katika mwaka huu wa 2024 ambao viwango vya joto duniani vimevunja rekodi duniani, watoto na vijana wanaendelea kupaza sauti zao wakihimiza viongozi wa dunia kuchukua hatua za haraka zinazohitajika ili kushughulikia janga la mabadiliko ya tabianchi. Georgina anasema Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF liko mstari wa mbele, lakini sasa ni wakati wa mshikamano kwa ajili ya mazingira bora kwa watoto wa leo, na wa zama zijazo..“Kwa viongozi wa dunia walioko hapa leo, hii si kazi ya UNICEF pekee. UNICEF inafanya kazi nzuri na sisi watoto, lakini tunahitaji msaada wako ili kujenga ulimwengu wa kesho ambapo hakuna mtoto anayepaswa kuchagua kati ya afya na elimu yake; ambapo hakuna mtoto anayekunywa maji yasiyo salama; hakuna mtoto anayekosa shule kwa sababu ya masuala yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi; na ambapo kila mtoto ana nafasi ya kuwa na afya bora na elimu bora.”Georgina anatamatisha kwa kusisitiza kuwa janga la mabadiliko ya tabianchi limenyima watoto haki zao hivyo kwa kila mtu...“Kumbuka unapolinda mazingira unalinda afya, elimu na ndoto za watoto. Mtoto mwenye afya bora na elimu bora anaweza kubadilisha ulimwengu.”Ama kweli watoto wana haki ya kuishi katika mazingira salama!

Habari za UN
UN: Mashambulizi ya anga ya Israel yalazimisha kampeni ya chanjo kusitishwa Gaza Kaskazini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 23, 2024 2:45


Mashambulizi makali ya anga kutoka kwa jeshi la Israel, idadi kubwa ya watu kutawanywa na ukosefu wa fursa ya kufika Gaza Kaskakzini vimelazimisha kuahirishwa kwa kameni ya chanjo kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya Duniani WHO, la kuhudumia watoto UNICEF na la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA. Asante Anold, kampeni hiyo iliyoahirishwa ilitakiwa kuanza leo n ani duru ya mwisho ya chango ya kampeni iliyolenga kuwachanja watoto 119,279 kote Gaza Kaskazini kwa dozi ya pili ya chanjo ya polio aina ya nOPV2, lakini hali ya sasa imefanya iwe vigumu kwa familia kupeleka watoto wao kwenye vituo vya chanjo, na kwa wahudumu wa afya kuendesha huduma kwa usalama.Mashambulizi ya makombora yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya kiraia yamepunguza maeneo yanayokubaliwa kwa usitishaji wa uhasama kwa mnajili ya masuala ya kibinadamu kuwa kwenye Jiji la Gaza pekee, ikilinganishwa na wakati wa awamu ya kwanza ya chanjo iliyofanyika tarehe 1-12 Septemba 2024.Hali hii inahatarisha kufikiwa kwa lengo la angalau asilimia 90 ya watoto kuchanjwa, jambo ambalo ni muhimu ili kukomesha usambaaji wa virusi vya polio na kulinda afya za watoto.WHO na UNICEF wamesema kuwa kucheleweshwa kwa chanjo ya polio kunaweza kuongeza hatari ya virusi kuenea zaidi Gaza na maeneo Jirani na kuchelewesha utoaji wa dozi ya pili ya chanjo ndani ya wiki sita kunapunguza uwezo wa chanjo hiyo kuimarisha kinga za watoto na kuzuia maambukizi.Tangu  duru ya pili ilipoanza tarehe 14 Oktoba 2024, jumla ya watoto 442,855 wenye umri wa chini ya miaka kumi wamefanikiwa kuchanjwa katika maeneo ya kati na kusini mwa Gaza.UNICEF na WHO wanatoa wito kwa pande zote zinazohusika katika mzozo kutekeleza usitishaji mapigano  wa kibinadamu na kuhakikisha kuwa raia, wahudumu wa afya, na miundombinu ya kiraia kama shule na hospitali inakingwa dhidi ya mashambulizi.Mashirika hayo yamesisitiza umuhimu wa kuanza tena kampeni ya chanjo mara moja ili kuzuia kupooza kwa watoto na kuimarisha kinga dhidi ya polio.Katika juhudi za kuhakikisha huduma bora, takribani watoto 357,802 pia walipatiwa virutubisho vya vitamini A kama sehemu ya juhudi za kuunganisha chanjo ya polio na huduma zingine muhimu za afya.Mashirika ya WHO na UNICEF ymesisitiza kuwa kusitisha vita na kuwezesha chanjo ni hatua muhimu ili kuzuia mlipuko wa polio kuendelea na kulinda afya ya watoto wote Gaza.

Habari za UN
UN Ripoti: Uwezekano wa kifo cha Dag Hammarskjöld kuwa ni hila unaongezeka kutokana na taarifa mpya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 18, 2024 2:02


Ripoti nyingine mpya ya tathimini ya uchunguzi wa hali na mazingira ya kifo cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 1961 Dag Hammarskjöld imetolewa leo ikiwa na vipengele vinne vipya vikiongeza uwezekano kwamba kifo hicho cha ajali ya ndege kilikuwa ni hila. Asante Anold kwanza ikumbukwe kuwa hii sio ripoti ya kwanza na huenda isiwe ya mwisho ya kutathimini hali na mazingira yliyochangia ajali ya ndege iliyokatili maisha ya Dag Hammarskjöld tarehe 17 Septemba 1961 akiwa njia kuelekea Congo ambayo sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Cngo DRC, kujadili usitishwaji wa uhasama ila ni ripoti ya karibuni zaidiRipoti inasema mwenyekiti wa jopo la tathimini ya uchunguzi jaji mkuu wa zamani wa Tanzania Mohamed Chande Othman amepokea taarifa mpya muhimu kutoka kwa nchi wanachama ambazo zinajumuisha maeneo haya Mosi:  uingiliaji unaowezekana wa Nchi Wanachama wa mawasiliano husika.Pili: Uwezo wa wanajeshi wa Katanga, au wengine, wa kufanya shambulio linalowezekana kwenye ndege ya SE-BDY,Tatu: kuwepo kwa askari wa kigeni na wafanyakazi wa kijasusi katika eneo hilo la tukioNa nne: Taarifa zaidi mpya zinazohusiana na muktadha na matukio yanayozunguka kifo hicho mwaka 1961.Jaji Othman amemkabidi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ripoti hii ya tathimini ambaye naye ameiwasilisha kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.Na kufuatiia tathimini hii Guterres amesema anaizingatia ingawa kihistoria kumekuwa na nadharia nyingi zilizotolewa kama sababu inayowezekana ya ajali hiyo, na anazichukulia nadharia hizo nyingi kuwa zisizo na uthibitisho.Hata hivyo mwenyekiti wa jopo la tathimini anasema  nadharia nyingine ambayo inabaki na inakubalika ni kwamba shambulio la nje au tishio lilikuwa sababu ya ajali.Pia amesema kuwa dhana mbadala zinazoonekana kuwepo ni kwamba ajali hiyo ilitokana na hujuma, au makosa ya kibinadamu yasiyokusudiwa.Katibu mkuu amekaribisha ushirikiano uliotolewa na baadhi ya nchi wanachama katika tathimini hiyo lakini bado jopo la tathimini linaaminikuna baadhi ya nchi wanachama wana taarifa muhimu ambazo hawajataka kuzitoa.

Habari za UN
01 OKTOBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 1, 2024 11:00


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ikiwa Mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA79, umekunja jamvi jana Jumatatu, tunaangazia sehemu ya pili ya mahojiano na mmoja wa washiriki wa mjadala huo waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari, na sauti za mashinani, kulikoni?Baada ya siku 6 za viongozi wa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa kutoa hotuba kuhusu masuala muhimu yanayogusa dunia hivi sasa, wakizingatia maudhui ya kutomwacha nyuma mtu yeyote, hatimaye Mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umekunja jamvi Jumatatu ya Septemba 30 jijini New York, Marekani.Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO limesema kufuatia tangazo la serikali ya Rwanda juu ya mlipuko wa ugonjwa wa homa ya virusi vya marburg tarehe 27 mwezi uliopita, hadi sasa watu 8 wamefariki dunia kati ya 26 waliothibitishwa kuugua ugonjwa huo, mara ya kwanza kuripotiwa Rwanda. Rwanda inashirikiana na wadau ikiwemo WHO kudhibiti kusambaa kwa virusi vya ugonjwa huo ambao hadi sasa hauna chanjo wala tiba. Asilimia 70 ya wagonjwa ni wahudumu wa afya kutoka vituo viwili vya afya kwenye mji mkuu Kigali.Na baada ya jeshi la Israeli hapo jana kujulisha Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Mpito nchini Lebanon, UNIFIL juu ya nia yake ya kuanza mashambulizi ya ardhini dhidi ya wapiganaji wa Hezbollah nchini humo, hii leo ujumbe huo umesema licha ya hatari inayoendelea ya mashambulizi, walinda amani wamejipanga. UNIFIL imesema mara kwa mara wanabadili mwenendo na operesheni zao na tayari wana mipango ya kutekeleza iwapo itahitajika kufanya hivyo. IDF na Hezbollah wamekuwa wanashambuliana kusini mwa Lebanon.Mashinani leo ikiwa ni siku ya Kimataifa ya Wazee Duniani tunakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kusikia ujumbe kutoka kwa mmoja ya wazee, ana maoni gani?Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
30 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 30, 2024 12:16


Hii leo jaridani tunaangazia amani na usalama nchini DRC, na suala la elimu katika malengo ya maendeleo endelevu tukimulika wanafunzi Kilifi nchini Kenya. Makala tunasalia na mada hiyo hiyo ya elimu na mashiani inamulika sheria za kibnadamu.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo wameelezwa jinsi ushindani wa uchimbaji kupita kiasi na biashara ya maliasili huko Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC unavyozidi kuchochea mapigano kwenye eneo hilo, madini kama vile dhahabu na Koltani.Maelfu ya watoto katika Kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya kwa miaka mitatu iliyopita wamelazimika kuacha shule kutokana na umasikini na ukame na mafuriko yaliyochangiwa na mabadiliko ya tabianchi. Lakini sasa wizara ya elimu ya Kenya kwa kushirikiana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, wakfu wa Education Above all na wadau wengine juhudi zinafanyika kuwarejesha watoto shuleni.Makala leo inatupeleka Paris Ufaransa katika makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO kuzungmzia juhudi za shirika hili katika kuhakikisha kwamba wanafunzi walio katika maeneo ya migogoro wanaendelea na masomo yao na wenzao waliohamishwa wanapata ufikiaji wa elimu juu katika nchi zilizowapokea.Katika mashinani fursa ni yake Mirjana Spoljaric Egger, Rais wa Kamati ya Kimataifa ya chama cha Msalaba Mwekundu ICRC akitoa wito wa kutafakari machungu yanayowakumba waathirika wa mizozo wakati wa mazungumzo yake na waandishi wa habari kandoni mwa mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA79.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
Keita: Dhahabu na Koltani vyazidi kushamirisha mapigano Mashariki mwa DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 30, 2024 1:36


Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo wameelezwa jinsi ushindani wa uchimbaji kupita kiasi na biashara ya maliasili huko Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC unavyozidi kuchochea mapigano kwenye eneo hilo, madini kama vile dhahabu na Koltani. Hayo yamo kwenye ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa iliyowasilishwa mbele ya Baraza la Usalama na Mwakilishi wake Maalum nchini DR Congo, Bintou Keita, ikianzia tarehe 20 Juni hadi 19 mwezi huu wa Septemba.Bi. Keita amesema “jimboni Ituri, mapigano yaliyoshamiri hivi karibuni yamechochewa na vikundi vilivyojihami vikijaribu kudhibiti machimbo ya madini. Kwa kuwa faida imeongezeka kwa kupanua machimbo ya dhahabu, vikundi vilivyojihami vimegeuka kuwa wajasiriamali wa madini. Vikundi ya kijamii na jeshi la serikali lisilo na uwezo kifedha wakihaha kudhibiti makundi ambayo yameimarika kijeshi na kifedha.”Mwakikilishi huyo ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe waUmoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MMONUSCO, amesema jimboni Kivu Kaskazini, M23 inazidi kuimarisha udhibiti wake wa maeneo ya Masisi na Rutshuru jimboni Kivu Kaskazini, na hivyo wameweza kudhibiti kabisa uzalishaji wa madini  ya Koltani.Ameongeza kuwa “biashara kutoka eneo la Rubaya linalokadiriwa kuchangia zaidi ya asilimia 15 ya uzalishaji wa madini ya Tantalum, imepatia M23 dola 300,000 kila mwezi. Hii inatia hofu na lazima ikomeshwe,.”Wajumbe pia walipata ripoti kutoka kwa Thérèse Nzale-Kove, mwanaharakati wa haki za wanawake kutoka Mfuko kwa Ajili ya Wanawake wa DRC au FFC.Bi. Nzale-Kove amesema kuondoka kwa MONUSCO jambo ambalo limesharidhiwa lazima kuzingatie changamoto za mifumo ya ulinzi wa haki za binadamu na ukosefu wa haki za kijamii na madhara yake.Ametaka kuzingatiwa kwa tathmini za kile walichojifunza baada ya MONUSCO kuondoka majimbo ya Tanganyika na Kivu Kusini.Kwa sasa MONUSCO imesalia jimbo la Kivu Kaskazini na inatakiwa iwe imeondoka kabisa DRC ifikapo mwisho wa mwaka huu.

Alfajiri - Voice of America
Watu 8 wafariki dunia nchini Rwanda kutokana na virus vya Marburg - Septemba 30, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 30, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
27 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 27, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea kipindi maalum. Leo mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia siku ya nne, miongoni mwa wahutubiaji ni Tanzania. Kabla ya kupanda katika mimbari ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuketi na mwakilishi wa taifa hilo katika mjadala huu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kuzungumza naye masuala kadhaa ikiwemo mzigo wa madeni kwa nchi zinazoendelea  na pia nafasi ya wanawake katika nyanja ya kimataifa. Lakini kwanza alitaka kufahamu Waziri Mkuu Majaliwa amekuja na ujumbe gani kutoka Tanzania kwenye mjadala huu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari.Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu nchini Lebanon, Imran Riza, akizungumza kutoka mji mkuu wa Lebanon, Beirut, kwa njia ya video amewaeleza waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi leo kwamba katika Lebanon kipaumbele kwa sasa ni kuhakikisha usitishaji mapigano wa haraka ili kukomesha mateso zaidi ya raia na uharibifu. Bwana Riza amesisitiza tena wito kwa jamii ya wahudumu wa  kibinadamu kwa nchi zote kutumia ushawishi wao kusaidia katika kupunguza machafuko kwa dharura.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya Wanawake UN Women inaangazia athari kubwa za janga la kibinadamu linaloongezeka kwa wanawake na wasichana wa Sudan, wakiwemo milioni 5.8 ambao ni wakimbizi wa ndani.Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Geneva, Uswisi imetoa wito kwa mamlaka ya Haiti na jumuiya ya kimataifa kufanya zaidi kulinda watu na kuzuia mateso zaidi na kwamba hicho ndicho kinapaswa kuwa kipaumbele. Takwimu za hivi karibuni kutoka Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa takribani watu 3,661 wameuawa nchini Haiti tangu Januari mwaka huu.”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Wakenya watoa maoni yao kuhusu pendekezo la kuongezwa kwa muda wa kuhudumu wa muhula wa Rais na wabunge. - Septemba 27, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 27, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

muda rais septemba
Habari za UN
26 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 26, 2024 11:32


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika hospitali ya kanda Bugando, mkoani Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania kumulika chanzo na madhara ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa au UVIDA. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na katika kujifunza Kiswahili tunabisha hodi nchini Zimbabwe, kulikoni?Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa leo kandoni mwa mjadala mkuu ulioingia siku ya tatu moja ya mada zinazopewa uzito ni usugu wa vijiuavijiumbe maradhi au Anti-Microbial Resistance (AMR). Katika taarifa ya Pamoja iluyotolewa kwenye mkutno huo na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO, la mazingira UNEP, la chakula  na kilimo FAO na shirika la afya ya Wanyama duniani WOAH, usugu wa viua vijiumbe maradhi unahusika moja kwa moja na vifo milioni 1.3 na kuchangia vingine milioni 5 kila mwaka.Pia katika katika Mjadala Mkuu wa baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA79 miongoni mwa waliopanda katika mimbari leo kuhutubia ni Rais wa Jamhuri ya Kenya William Samoei Ruto ambaye amesema “Dunia iko katika wakati wa changamoto kubwa za kiusalama, ahati ya chata ya Umoja wa Mataifa kuokoa viizazi kutokana na vita iiko katika hatihati.” Aesema nadhariaya wao dhidi yetu ni chachu ya changamoto kubwa ikiwemo vita. Kuanzia Gaza, Darfur, Ukraine, Yemen, Mashariki mwa DRC , Sudan, Sahel na uhalifunchini Haiti,migogoro inasambaratisha maisha na uwezi wa watukuishi katika kiwangocha kihistoria.”Naye Rais wa Malawi Lazarus McCarthy Chakwera, amesema kila nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa inahusiana na nchi nyingine katika mambo matatu, ushirikiano migogoro na ushindani ulio na usawa, hivyo jinsi ya kushughulikia masuala hayo ndio itaamua mustakbali wa vizazi vvya kesho hasa ushirikiano unaofaidisha wote, ushindani ulio na usawa na utatuzi wa migogoro. Amesisitiza kuwa ushirikiano ni kitu cha muhimu sana na mfano mzuri ni nchi yake Malawi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili fursa ni yake Mary Chigumira kutoka Zimbabwe, mmoja wa waafrika aliyefika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa Jijini New York kwa ajili ya Mkutano wa Zama Zijazo uliokamilika hivi majuzi akieleza anavyotamani kujifunza zaidi lugha ya Kiswahili.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Alfajiri - Septemba 26, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 26, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

septemba
Habari za UN
25 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 25, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa wanaharakati wa malengo ya maendeleo endelevu ambao wamekuja hapa makao makuu ya umoja wa mataifa kuwa sehemu ya utatuzi katika mijadala mikuu ya UNGA79. Makala tunasalia hapa makao makuu na mashinani tunakwenda DRC.Viongozi wa dunia wakiendelea kuhutubia kwenye Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hapa New York, Marekani, kandoni kunafanyika Mkutano wa Ngazi ya Juu  ukimulika madhara ya ongezeko la kina baharí  kutokana na kina cha baharí.Mjadala mkuu wa wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 79 umeingia siku ya pili hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa nasi tunaendelea kuzungumza na washhiriki mbalimbali wakiwemo kutoka asasi za kiraia kusikia maoni yao kuhusu mkutano huu. Flora Nducha amebahatika kuongea na mmoja wao kutoka nchini Zimbabwe.Katika makala Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na vijana wawili waliozaliwa tayari wakiwa na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi na hivyo wameamua kujitolea kusukuma mapambano dhidi ya ugojwa huo hatari duniani. Katika mikutano inayoendelea hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa wakati huu wa UNGA79 wasichana hawa wadogo wamepata fursa ya kushiriki katika mkutano wa ngazi ya juu uliondaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi UNAIDS.Na mashinani fursa ni yake mwananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC jimboni Kivu Kaskazini akiwasilisha ujumbe wake kwa viongozi wanaoshiriki mjadala Mkuu wa mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataiafa, UNGA79 hapa New York, Marekani.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Afrika Kusini yaanza kufukua miili ya raia yake waliofia Zimbabwe miaka ya 80 wakipigana na ubeberu. - Septemba 25, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 25, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
24 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 24, 2024 9:58


Jaridani tunakuletea mada kwa kina ikiwa hii leo Mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa mataifa UNGA79 umeng'oa nanga hii na tunakutana na mdau anayepigia chepuo malengo ya maendeleo endelevu hasa haki katika lengo namba 4 la Elimu Bora.Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA79 umeanza leo New York, Marekani ambapo Katibu Mkuu wa Antonio Guterres amesema anashawishika kwamba kuna kweli mbili chungu katika zahma zinazokumba dunia hivi sasa: Mosi-Hali ya dunia si endelevu na hatuwezi kuendelea kama ilivyo na pili; changamoto zilizozoko zinatatulika. Kinachohitajika ni kuweko kwa mfumo wa kimataifa wenye uwezo wa kutatua changamoto hizo.Rais Joe Biden wa Marekani ambaye amesema ni hotuba yake ya mwisho mbele ya Baraza hilo kama Rais wa Marekani na kwamba anatambua changamoto zinazokabili dunia ikiwemo vita, tabianchi na demokrasia. Lakini ana matumaini kuna suluhu kwa kuzingatia yote waliyofanya pamoja kwa miongo iliyopita.Huko Lebanon shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR linaomboleza vifo vya watumishi wake wawili waliouawa huko Bekaa Mashariki baada ya kombora lililorushwa na Israeli kuangukia makazi yao jana Septemba 23. UNHCR imerejelea wito wa Katibu Mkuu wa UN ya kwamba mashambulizi yakome.Na katika mashinani tunamsikia kijana mmoja aliyefika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuhudhuria mkutano wa Zama Zijazo uliofunga pazia lake jana, ana wito wa kuwapa viongozi wa ulimwengu ambao wanashiriki katika Mjadala Mkuu wa Baraza la Umoja wa Mataifa ambao wenyewe umefungua pazialake leo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
Vijana - Tumechoka na maneno ya viongozi sasa tunataka vitendo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 24, 2024 7:27


Jana Jumapili ya Septemba 22 viongozi wa dunia walipitisha Mkataba wa Zama Zijazo. Mkataba huu unalenga kukabili changamoto za karne ya 21 kuanzia mizozo, mabadiliko ya tabianchi, haki za binadamu, hadi taarifa potofu na za uongo. Maeneo Matano makuu ni pamoja na maendeleo endelevu, amani na usalama duniani, sayansi na teknolojia, vijana na vizazi vijavyo na marekebisho ya usimamizi wa dunia, kipengele muhimu wakati huu ambapo taasisi za fedha za kimataifa na Umoja wa Mataifa wenyewe wameshindwa kuja na majawabu ya karne ya 21. Mkataba wa Kimataifa wa Kidijitali unaoelenga pamoja na mambo mengine usimamizi bora wa Akili Mnemba, pamoja na Azimio kwa ajili ya Vizazi Vijavyo linalotaka serikali za sasa kutilia maanani vizazi vijavyo zinapopitisha maamuzi yao ya leo, ni sehemu ya viambatanishi vya Mkataba huu wa Zama Zijazo. Assumpta Massoi ametaka kufahamu maoni ya vijana baada ya hatua hii, na ndio mada yetu kwa kina siku ya leo. 

Alfajiri - Voice of America
Alfajiri - Septemba 24, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 24, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

septemba
Habari za UN
23 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 23, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina kama nilivyokujulisha leo ambayo ni kipindi maalum kinachojumuisha hotuba za viongozi wa dunia na watetezi wa haki za binadamu ikiwa ni jana Jumapili Septemba 22 viongozi hao walipitisha Mkataba wa Zama Zijazo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Mkutano wa Zama Zijazo uliofanyika kwa siku nne tangu majuzi tarehe 20 ukianza na siku mbili za vijana kukutana na baadaye viongozi wakuu wa ulimwengu, unakunja jamvi hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Kesho Septemba 24 unaanza Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukitajwa kuwa mkusanyiko mkubwa zaidi wa kidplomasia ulimwenguni unaofanyika kila mwaka. Kwa siku sita viongozi wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa watahutubia ulimwengu.Leo Jumatatu hali ya mvutano imezidi kutanda Mashariki ya Kati huku ripoti za mamia ya mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Israel dhidi ya Hezbollah yakilenga kusini mwa Lebanon na Gaza ikiwa ni pamoja na kambi ya wakimbizi, wameeleza wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa. Hatua hiyo inakuja wakati afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Lebanon Jeanine Hennis-Plasschaert aakianza ziara rasmi nchini Israel kukutana na maafisa wakuu wa serikali, baada ya kusisitiza kwamba "hakuna suluhu ya kijeshi ambayo itafanya pande zote mbili kuwa salama".Na Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali  ya Haki za Binadamu nchini Burundi Fortuné Gaetan Zongo, amehutubia mkutano wa 57 wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu huko Geneva, Uswisi hii leo na kueleza kuwa hali ya kibinadamu katika taifa hilo la Maziwa Makuu bado inatia wasiwasi akitolea mfano tukio la mashinikizo kwa wapenzi waliokuwa wanaishi pamoja huko Ngozi, Kayanza na Kirundo mwezi Machi na Aprili mwaka huu.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Umoja wa Mataifa kwa ushirikiano na serikali ya DRC, waanza mradi mpya wa kuwafunza wanawake kuendesha pikipiki. - Septemba 23, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 23, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
20 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia uondoaji wa taka katika ukanda wa Gaza, na ujumbe wa vijana ambao watashiriki mijadala mikuu hapa makaomakuu ya Umoja wa Mataifa. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini, kulikoni?Hali inazidi kuwa si hali huko Ukanda wa Gaza kwani sasa raia wanakwepa sio tu mashambulizi na magonjwa bali pia nyoka, panya na wadudu ambao wanasambaa kutokana na mazingira machafu. Watu wanajihifadhi kwenye maeneo ya wazi bila mifumo ya majitaka au ya kuondoa maji ya mvua. Timu ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina imefika kupuliza dawa ili kulinda wananchi hao.Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani vijana kutoka kila kona ya dunia wanakutana kuanza kujadili kuhusu mstakabali wao katika zama zijazo. Miongoni mwao ni Jerop Limo kutoka Kenya anayetumia uzoefu wake wa kuishi na Virusi Vya Ukimwi kwa miaka 24 ya umri wake kuhakikisha ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu ambao tayari wanaishi na virusi hivyo.Makala inaturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani ambako mkutano wa Zama Zijazo umen'goa nanga leo kwa siku mbili za kuchua hatua kabla ya kikao cha ngazi ya juu siku ya Jumapili na Jumatatu. Leo Vijana wanapata fursa ya kupaza sauti zao kuhusu dunia na mustakbali wautakao.Na katika mashinani Balozi Mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Tendai Mtawarira, mwanamichezo nguli mstaafu wa mpira wa raga mzaliwa wa Zimbabwe lakini alichezea Afrika Kusini, akizungumzia alichokishuhudia katika safari yake ya kwanza nchini Sudan Kusini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 20 Septemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 16:46


Mswada wa serikali ya shirikisho waku ongeza malipo ya uzeeni katika likizo ya wazazi yenye malipo ime idhinishwa na bunge.

habari septemba
Alfajiri - Voice of America
Zoezi la kutoa chanjo dhidi Mpox nchini DRC linaanza Oktoba 2 - Septemba 20, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

mpox oktoba septemba
Habari za UN
19 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 19, 2024 10:55


Hii leo jaridani tuankuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Sudan Kusini kufuatilia changamoto za kibinadamu na jinsi ambavyo mashirika ya Umoja wa Mataifa yanavyozitatua. Pi atunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo na ufafanuzi wa methali.Licha ya kuongezeka kwa majanga duniani, kuanzia umaskini hadi dharura ya tabianchi, Umoja wa Mataifa umesalia na azma yake ya kusongesha amani, maendeleo endelevu na kupunguza machungu yanayowapata binadamu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres katika ripoti yake ya mwaka ya utendaji wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo jijini New York, Marekani kabla ya kuanza kwa Mjadala Mkuu wa  mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA79.Shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi, UNAIDS hii leo limetoa ripoti yake huko Geneva, Uswisi ikionesha kuwa mzigo wa madeni unaokabili nchi za Afrika zilizo Kusini mwa jangwa la Sahara unasababisha zibakie na fedha kidogo kugharimia huduma za afya, pamoja na huduma muhimu zaidi dhidi ya Virusi vya Ukimwi, VVU. Idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU duniani wako eneo hilo lakini mzigo wa madeni unarudisha nyuma maendeleo yaliyopatikana ya kutokomeza Ukimwi ifikapo 2030.Tukisalia na suala hilo hilo la UKIMWI, UNAIDS inasema vijana wawili wanaoishi na Virusi vya Ukimwi na pia wana ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii, Ibanomonde Ngema kutoka Afrika Kusini, na Jerop Limo kutoka Kenya, wako njiani kuja New York, Marekani kushiriki UNGA79 na Mkutano wa Zama Zijazo kwa lengo la kusihi viongozi wa dunia kushirikiana na vijana katika kutokomeza Ukimwi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “Mke ni nguomgomba ni kupalilia.”.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Israel inasema imeanzisha enzi mpya ya vita dhidi ya Hezbollah - Septemba 19, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 19, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
18 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za Umoja wa Mataifa za kukabiliana na ugonjwa wa MPOX barani Afrika. Makala inatupeleka nchini Sudan Kusini kuangazia uhairishwaji wa uchaguzi na mashinani nchini Sudan ambapo vilabu vinatumiwa kuimarisha ulinzi wa wasichana.Kutokana na ombi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (the Global Fund) leo umetangaza kuchangia dola za Marekani milioni 9.5 kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa wa mpox katika majimbo sita kati ya yale yenye viwango vya juu zaidi vya maambukizi nchini humo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Burundi linasema asilimia 33 ya wagonjwa wa homa ya nyani au mpox nchini humo ni watoto wa kwenda shule wenye umri wa kuanzia miaka 5 hadi 19, na hivyo kuwa changamoto mpya wakati familia zinajiandaa kwa mwaka mpya wa masomo.Makala leo inatupeleka Sudan Kusini ambako mwishoni mwa wiki serikali ilitangaza kuahirisha uchaguzi mkuu ambao ulikuwa ufanyike 22 Desemba mwaka huu 2024.Mashinani tuko katika kambi ya wakimbizi ya Zamzam nchini Sudan ambako shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA) linatumia vilabu kufanikisha ulinzi wa wasichana walio hatarini. Sasa Ikhlas Mousa Andulkareem ambaye ni mfanyakazi wa kijamii katika shirika lisilo la kiserikali la Nada ALAzhar, linalopata usaidizi kutoka UNFPA anatueleza jinsi eneo salama kwa wanawake na wasichana litawanufaisha waathiriwa kwenye kambi hii ya Zamzam.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
UNICEF Burundi yachukua hatua mpox isivuruge muhula wa masomo kwa watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 1:53


Nchini Burundi shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linashirikiana na serikali kuhakikisha mlipuko wa ugonjwa wa homa ya nyani au mpox nchini humo hauthiri watoto kurejea shuleni wakati huu ambapo asilimia 33 ya wagonjwa wakiripotiwa kuwa na umri wa kati ya miaka 5 hadi 19. Cecily Kariuki anatupa maelezo zaidi kupitia  video hii ya UNICEF inayotupeleka hospitali ya Prince Louis Rwagasore iliyoko mji mkuu wa taifa hilo la Maziwa Makuu, Afrika, Bujumbura..Video ya UNICEF inaanzia kwenye uwanja wenye mahema yenye nembo ya shirika hilo. Moja kwa moja tunaingia ndani, daktari akitoa maelekezo kwa akina mama walioko na watoto wao wanaougua mpox. Miongoni mwao ni Primitive Nibitanga, mama watoto wawili. Primitive anasema tumelazwa kwa zaidi ya wiki mbili sasa. Nilienda kituo cha afya lakini hawakuweza kumtibu mtoto wangu. Majirani walinishauri nije hapa kliniki. Nilifika na kulazwa. Mtoto wangu alikuwa mahututi, lakini wauguzi walijitahidi kwa kadri ya uwezo wao na haikuchukua muda alipona. Bahati mbayá siku tatu baadaye dada yake alipata dalili zile zile na tukarejea tena hapa.”Daktari Fidel Cishahayoanahusika na usimamizi wa matibabu ya mpox katika hospitali hii ya Prince Rwegasore. Anasema “hatua ya kwanza ilikuwa kutenga hili eneo kwa sababu tulikuwa tunapokea wagonjwa wa mpox na wanaoshukiwa kuwa na maambukizi. Kwa hiyo tuliandaa ili kuwa na eneo la wagonjwa na washukiwa. Tuliandaa pia timu ya wahudumu, wakiwemo madaktari na wauguzi kutoka idara nyingine kwa ajili ya mpox. Wanaopona wanaruhusiwa na kushauriwa kujitenga kwa angalau wiki tatu.” UNICEF tayari imeomba dola milioni 58.8 kusaidia kupambana na mlipuko wa mpox barani Afrika ikiwemo nchini Burundi. Mwakilishi wa UNICEF nchini Burundi France Bégin amesema fedha hizo pamoja na mambo mengine zitasaidia kuwalinda watoto ili warejee shuleni licha ya mlipuko. Vile vile kuepusha kuvurugwa zaidi kwa fursa za wanafunzi kusoma kwani mwaka mpya wa masomo umeanza tarehe 16 mwezi huu wa Septemba.

Habari za UN
Mfuko wa Kimataifa yatoa karibia dola milioni 10 kukabiliana na mpox DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 1:49


Kutokana na ombi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria (the Global Fund) leo umetangaza kuchangia dola za Marekani milioni 9.5 kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa wa mpox katika majimbo sita kati ya yale yenye viwango vya juu zaidi vya maambukizi nchini humo.  Tangazo hilo lililotolewa leo Septemba 18 katika makao makuu ya Mfuko huo wa kimataifa unaofahamika kama The Global Fund, mjini Geneva, Uswisi imeeleza kuwa fedha hizo zinaelekezwa katika katika jimbo la Equateur, Ubangi Kusini, Sankuru, Tshopo, Kivu Kusini, Kivu Kaskazini na Kinshasa, jimbo lenye msongamano mkubwa wa watu milioni 17.

Alfajiri - Voice of America
Wachambuzi wa siasa Tanzania waitaka serikali kuanzisha uchunguzi huru juu ya mauaji ya baadhi ya wanasiasa wa upinzani - Septemba 18, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
17 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 17, 2024 9:54


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Nairobi Kenya ambako tutamsikiamwanamuziki nyota, mjasiriamali na mwanaharakati wa haki za wanawake Lizi Ogumbo. Pia tunakuletea habari kwa ufufpi na mashinani.Vurugu dhidi ya wapinzani wa serikali nchini Venezuela zimefurutu ada, imesema tume huru ya uchunguzi ikitaja kukamatwa, ukatili wa kingono na utesaji kama mbinu zitumiwazo na serikali ya Rais Nicolas Maduro ili aendelee kuweko madarani.Mwaka 2024 ukiripotiwa kuwa na idadi kubwa ya chaguzi kwenye nchi zaidi ya 60 ambako zaidi ya watu bilioni 1 watapiga kura kuchagua viongozi wao wa umma, wataalamu wa Umoja wa Mataia wanaelezea hofu yao juu ya kitendo cha watu kutoweshwa katika kipindi hicho ili kunyamazisha demokrasia, kitendo ambacho wamesema kinabinya uhuru wa kupiga kura.Na hii leo matokeo ya utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa yameonesha kuwa licha ya majanga yanayoendelea kukumba dunia, nchi wanachama zimeendelea kujizatiti kuanzisha huduma za serikali mtandao ili wananchi waweze kupata huduma mbali mbali kidijitali, ambapo ripoti inazitaja Denmark, Estonia na Singapore kushika nafasi ya juu kati ya nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa, kwa mawanda na ubora wa huduma za serikali mtandaoni.Katika mashinani Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP nchini Bangladesh Stefan Liller anatueleza kiwango cha athari za mafuriko makubwa yaliyoikumba nchi hiyo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 17 Septemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 17, 2024 18:49


Mwanaume anaye shukiwa kuhusika katika jaribio laku muuwa Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump, amefunguliwa mashtaka ya uhalifu wakutumia bunduki.

rais habari septemba
Habari za UN
16 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 16, 2024 9:56


Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN wa Tabaka la Ozoni, na mssada wa kibinadamu kwa wenyeji wa kisiwa kidogo cha Carriacou, Grenada waliokumbwa na kimbunga Beryl. Makal tunakupeleka nchini Nigeria na mashinani nchini Sudan.Pamoja na chapisho lililotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa (WMO) kuangazia ushahidi unaoongezeka kwamba tabaka la ozoni kwa hakika liko mbioni kurejea katika hali nzuri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake maalumu kwa ajili ya siku ya leo ya Kimataifa ya Uhifadhi wa Tabaka la Ozoni amesisitiza mataifa yote ulimwenguni kuidhinisha na kutekeleza maazimio ya maboresho ya Itifaki ya Montreal yaliyozaa Marekebisho ya Kigali kwa lengo la kupunguza gesi chafuzi zenye nguvu zinazoongeza joto duniani.Kimbunga Beryl, kilichopiga tarehe 1 Julai 2024, kimewaacha wakazi wa kisiwa kidogo cha Carriacou, Grenada, na athari kubwa . Kufuatia changamoto zinazowakabili wasamaria kutoka maeneo mbalimbali likiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) wamewasaidia kurejesha matumaini kama anavyosimulia Anthony St. Hilaire manusura wa kimbunga hicho.Makala inatupeleka Maiduguri Nigeria ambako mafuriko yanayoshuhudiwa baada ya bwawa la Alau kupasua kingo zake kutokana na mvua kubwa hayajawahi kuonekana katika miaka ya karibuni. Shirika la Umoja wa Matifa la mpango wa chakula duniani WFP ni mdau Mkubwa katika kufikisha misaada kwa waathirika na mkuu wa ofisi yake ya Maiduguri Emmanuel Bigenimana anaeleza alichokishuhudia.Na katika mashinani Aziza, mama wa watoto wanne kutoka Sudan ambaye alikuwa mhudumu wa kibinadamu na sasa amejikuta mkimbizi nchini Uganda baada ya kukimbia nyumbani kwao Sudan kufuatia mapigano yaliyoanza Aprili 2023. Nyumba yao iliporwa kila kitu na sasa akiwa ukimbizi anasimulia maisha yalivyo tangu ahamishwe na kuwa mkimbizi huku akinufaika na msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
Walinda amani wa Tanzania wang'ara katika ulinzi wa amani nchini Afrika ya Kati, CAR

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 13, 2024 2:33


Umoja wa Mataifa umewatunuku nishani Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kikosi cha 7 kutoka Tanzania TANBAT 7 kinachohudumu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR chini ya mwamvuli wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo (MINUSCA) kimetunukiwa nishani za Umoja wa Mataifa mnamo tarehe10 Septemba 2024. Afisa Habari wa kikosi hicho, Kapteni Emanuel Ngonela alikuwa shuhuda na ametuandalia makala hii.

Habari za UN
13 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 13, 2024 9:40


Hii leo jaridani tunaangazia chanjo za polio katika ukanda wa Gaza, na kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda. Makala inatupeleka nchini CAR na mashinani tutaelekea Gambella, Ethiopia, kulikoni?Zaidi ya watoto 560,000 wamepokea chanjo dhidi ya virusi vya polio aina ya pili (cVDPV2) kwenye Ukanda wa Gaza katika duru ya kwanza ya kampeni kubwa ya chanjo iliyomalizima jana yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa.Mnara wa kudumu wa kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda umesimikwa kwenye bustani ya makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York kuhakikisha kilichotokea hakitosahaulika na      asilani kisitokee tena.Makala inatupeleka nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati ambako Umoja wa Mataifa umewatunuku nishani Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kikosi cha 7 kutoka Tanzania TANBAT 7 kinachohudumu chini ya mwamvuli wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo CAR (MINUSCA).Na katika mashinani tutaelekea Gambella, Ethiopia ambapo kupitia video ya UNICEF, tunakutanisha na Ariet, mtoto wa umri wamiaka 10 aliyekumbwa na utekaji baada ya kijiji chake kuvamiwa. Ariet anaeleza jinsi alivyofurahi baada ya kupata msaada wa UNICEF, ili kurejea kwenye maisha ya kawaida.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Kinyua "karibuni tusherehekee uafrika wetu kupitia soka ACT"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 13, 2024 7:09


Wanachama wa jumuiya yawa Afrika wanao ishi Canberra, ACT wanajiandaa kushiriki katika kombe la Afrika kesho Jumamosi 14 Septemba 2024.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 13 Septemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 13, 2024 17:55


Mdhibiti wa vyombo vya habari nchini, atapewa mamlaka yakuchukua hatua dhidi ya makampuni ya teknolojia kama Meta na X, kwa usambazaji wa habari potofu na habari feki katika mitandao yao.

habari septemba
Habari za UN
12 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 12, 2024 9:59


Hii leo jaridani mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, kulikofanyika mashauriano kuhusu mkutano wa zama zijazo, ambapo baadhi ya washiriki wameeleza walichojadili na walichopendekeza. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno “KILIWAZO”.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X amelaani vikali tukio la jana huko Gaza ambapo vikosi vya anga vya Israel vilishambulia makazi ya wakimbizi wa ndani wapatao 12, 000. Katika shambulio hilo wafanyakazi 6 wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA walifariki dunia na kufanya tukio hilo kuwa lenye vifo vingi zaidi vya wafanyakazi wa UNRWA katika tukio moja.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) na wadau wake, jana Septemba 11 huko Gaza wamefanikiwa kuhamisha wagonjwa 97 na watu wengine 155 wenye majeraha makubwa zaidi. Katika unaotajwa kuwa uhamishaji mkubwa wa wagonjwa tangu ule wa Oktoba 2023 wagonjwa walisafirishwa kupitia Kerem Shalom hadi Uwanja wa Ndege wa Ramon nchini Israel kwa safari ya kuelekea Abu Dhabi, Falme za Kiarabu.Tukisalia huko Gaza, takribani robo moja au watu elfu ishirini na mbili na mia tano ya wale waliojeruhiwa huko Gaza kufikia Julai 23 wanakadiriwa kuwa na majeraha ambayo yatabadilisha kabisa maisha yao na kwa hivyo wanahitaji huduma za uangalizi sasa na hata kwa miaka ijayo. Hiyo ni kwa mujibu wa uchambuzi uliotolewa leo na WHO.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “KILIWAZO”.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
11 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 11, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ugonjwa wa homa ya nyani au mpox barani Afrika na kufufuliwa kwa kituo chao cha Redio na Televisheni ya Taifa, RTNC huko Beni nchini DRC. Makala tanakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Ugonjwa wa homa ya nyani au mpox ukisalia kuwa dharura ya afya ya umma duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasaka zaidi ya dola milioni 21 zitakazotumika hadi mwishoni mwa mwaka huu kuongeza harakati dhidi ya ugonjwa huo miongoni mwa wakimbizi katika nchi zilizokumbwa na dharura ya ugonjwa huo, hususan Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.Wakazi wa mji wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wana furaha tele baada ya kufufuliwa kwa kituo chao cha Redio na Televisheni ya Taifa, RTNC. Kupitia msaada wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, wakazi hao sasa wanaweza kusikiliza na kutazama vipindi vyao wanavyovipenda, waandishi wa habari nao, hawafanyi tena kazi chini ya mti.Makala inatupeleka mkoani Kigoma kaskazini magharibi mwa Tanzania kusikia manufaa ya mradi wa Kilimo Tija Kigoma (KiTiKi) unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kwa ufadhili wa Watu wa Jamhuri ya Korea.Na mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani kanda ya Afrika, tunamsikia Shane Prigge mkuu wa mnyororo wa usambazaji, WFP Kenya akieleza jinsi UNHAS ambalo ni shirika la ndege la Umoja wa Mataifa la huduma za kibinadamu linavyowezesha mashirika ya kibinadamu kufanya kazi zao.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
10 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 10, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mwanza kaskazini Magharibi mwa Tanzania kupata ufafanuzi wa athari za moshi wa kuni kwa binadamu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na sauti kutoka mashinani.Miaka 63 tangu kifo cha ajali ya ndege cha Katibu Mkuu wa pili wa Umoja wa Mataifa Dag Hammarskjöld huko Ndola Zambia, bado majibu hayajapatikana ya nini kilisababisha ajali hiyo wakati akielekea kusaka amani kwa iliyokuwa Congo, sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limesema kampeni ya chanjo eneo la kaskazini mwa Gaza imeendelea leo jumanne licha ya tukio la jana la jeshi la Israeli kuzuia kwa saa nane msafara wa wafanyakazi waliokuwa wanasafiri kwenda kutoa huduma hiyo.Na leo septemba 10, mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA78 unakunja jamvi baada ya mwaka mzima wa mikutano na mijadala, na hivyo kuashiria kuanza kwa mkutano wa 79  ambapo kuanzia tarehe 22 vitaanza vikao vya ngazi ya juu na Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu. Rais anayemaliza muda wake ni Balozi Dennis Francis kutoka Trinidad na Tobago na anayempatia kijiti ni Philemon Yang kutoka Cameroon.Katika mashinani, tunamulika mwaka mmoja tangu kimbunga Daniel kipige mji wa Dema mashariki mwa Libya na vitongoji vyake na kuleta mvua kubwa iliyosababisha mafuriko yaliyoua zaidi ya watu 5,000, na kuacha makovu hadi sasa. Maelezo ya Hawa Bu Zqeeba aliyempoteza baba yake katika mafuriko hayo yanakupatia taswira halisi ya makovu.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 10 Septemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 10, 2024 17:24


Wauguzi na wakunga kote jimboni New South Wales, wanao ondoka kazini leo Jumanne 10 Septemba, kinyume na amri za tume ya mahusiano ya serikali ya viwanda kusitisha mgomo maramoja.

Habari za UN
UNMISS: Wananchi wa kaunti ya Nasir watakiwa kuepuka mapigano ili wapelekewe maendeleo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 1:56


Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umewaeleza wananchi wa Kaunti ya Nasir au Keich Kon iliyoko jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini kuwa ili waweze kurejeshewa huduma za misaada ya kibinadamu ni vyema wakafikia makubaliano ya kusitisha mapigano. UNMISS pamoja na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu walifikia uamuzi wa kusitisha huduma zao katika kaunti ya Nasir kutokana nae eneo hilo kutofikika na pia ukosefu wa usalama uliosababishwa na mapigano ya mara kwa mara baina ya wanajamii wa kuanti hiyo, na pia mapigano na kaunti za jirani.Hata hivyo mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba kilifanyika kikao kilichowaleta pamoja wadau na wananchi baada ya kupatikana uongozi mpya wa kaunti hiyo ambapo katika kikao hicho, wadau wa misaada ya kibinadamu ikiwemo Umoja wa Mataifa waliombwa kurejesha operesheni zao hususan UNMISS, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani (WFP) na wadau wa Sekta ya afya.Paul Ebikwo ni afisa wa masuala ya kiraia wa UNMISS na akawaeleza anaelewa wasiwasi wao.“Wasiwasi wenu ni wa halali, ni wa kweli, tunaelewa. Lakini mkiongeza mizozo ndani yake, mnafanya mambo kuwa mabaya zaidi, kwa hivyo hebu tufanye maamuzi ya kuachana, na kuweka kando migogoro na sote tufikirie jinsi ya kutatua maswala haya.”Bwana Ebikwo aliongeza kuwa suluhu zote za kuzuia ghasia lazima ziongozwe na wanajamii wenyewe huku akitoa wito kwa makundi ya vijana wanaotumia silaha kujiepusha na mapigano na kutafuta amani.Majadiliano yalihitimishwa kwa wote kukubaliana kuwa na dhamira ya pamoja ya kutafuta njia za kuleta jamii hususani vijana pamoja kwa ajili ya upatanisho na ujenzi wa amani ili kusaidia kurejesha utulivu na kuwezesha jamii katika kaunti ya Nasir kupata ahueni na maendeleo baada ya kuteseka kwa muda mrefu.

sudan hata wfp umoja sekta lakini mataifa maendeleo unmiss shirika ujumbe kaunti wananchi septemba sudan kusini
Habari za UN
09 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia suala la elimu katika maeneo ya migogoro, na msaada wa kibinadamu huko Upper Nile nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Nigeria na mashinani nchini Afghanistan, kulikoni??Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kulinda elimu isishambuliwe wakati wa mizozo kutokana na umuhimu wake kwa watoto na jamii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema miaka ya karibuni imeshuhudia ongezeko kubwa la mashambulizi dhidi ya wanafunzi, walimu na shule duniani kote. Hivyo ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa siku hii.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umewaeleza wananchi wa Kaunti ya Nasir au Keich Kon iliyoko jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini kuwa ili waweze kurejeshewa huduma za misaada ya kibinadamu ni vyema wakafikia makubaliano ya kusitisha mapigano.Makala inatupeleka Maiduguri nchini Nigeria kusikia namna mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri yaani Education Cannot Wait (ECW) kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto (UNICEF) na wadau wengine wanarejesha matumaini kwa waliokosa elimu rasmi hasa kutokana na hali mbayá ya usalama katika maeneo yao.Na katika mashinani, fursa ni yake Faeza, mfanyakazi wa kiwanda cha kutengeneza biskuti nchini Afghanistan, mradi unaowezeshwa na shirika la WFP akitueleza manufaa ya mradi huo kwa jamii iliyoathirika na vita hasa wanawake na watoto.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
06 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 6, 2024 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia mashambulizi ya kutisha ya kingono nchini Sudan, na mafunzo ya kidijitali. Makala na mashinani tunakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Ujumbe Huru wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa  wa kutafuta ukweli nchini Sudan, leo Septemba 6 jijini Geneva, Uswisi, wametoa wito wa kuwekwa vikwazo vya silaha kote nchini Sudan kutokana na kukithiri kwa vitendo vya kikatili kama vile mashambulizi ya kutisha ya kingono.Uhusiano kati ya teknolojia, elimu, na mabadiliko ya tabianchi ni upi? Hili ndilo limekuwa swala kuu katika mkutano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) uliopewa jina la Wiki ya Kujifunza kwa Kidijitali au Digital Learning Week uliokamilika jana Alhamisi huko Paris Ufaransa. Mkutano huu uliangazia maswala nyeti ya mchango wa teknolojia katika elimu inayolenga maendeleo.Makala tunaelekea DRC ambako George Musubao, Mwandishi wetu wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumza na Mkuu wa kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC-MONUSCO anayemaliza muda wake mwezi huu baada ya kuhudumu kwa mwaka mmoja Brigedia Jenerali Alfred Matambo. Brigedia Jenerali Matambo anaanza kwa kuzungumzia matokeo ya moja ya operesheni  kubwa za kijeshi 15 walizotekeleza dhidi ya makundi yenye silaha likiwemo la CODECO.Na katika mashinani, Daktari Erick Mashimango aliyeko nchini DRC anatueleza kuwa kuenea kwa ugonjwa wa mpox kwa kasi nchini humo ambako kumegharimu maisha ya ziadi ya watu 600 kumewafanya wananchi kuwa tayari kupokea chanjo.Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu! 

Habari za UN
Wachunguzi wa haki za binadamu wataka kuongezwa kwa vikwazo vya silaha Sudan - UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 6, 2024 1:54


Ujumbe Huru wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa  wa kutafuta ukweli nchini Sudan, leo Septemba 6 jijini Geneva, Uswisi, wametoa wito wa kuwekwa vikwazo vya silaha kote nchini Sudan kutokana na kukithiri kwa vitendo vya kikatili kama vile mashambulizi ya kutisha ya kingono.  Ni mbobevu wa sheria duniani, Mohamed Chande Othman, Mwenyekiti wa Ujumbe huo Huru wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa wa Mataifa wa kutafuta ukweli kuhusu yanayoendelea Sudan akiwaeleza waaandishi wa habari leo kwamba, "tangu katikati ya Aprili mwaka 2023, mzozo wa Sudan umeenea hadi majimbo 14 kati ya 18 na kuathiri nchi nzima na ukanda huo, na kuwafanya Wasudan milioni nane kuwa wakimbizi wa ndani kutokana na mzozo huo, na milioni mbili - zaidi ya milioni mbili – kulazimishwa kukimbilia nchi jirani.”Katika ripoti yao hii ya kwanza tangu Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa lilipounda jopo hilo mwaka jana 2023, wajumbe hawa wamesisitiza kwamba pande zote mbili zinazohasimiana yaani wanajeshi wa Jeshi la Sudan (SAF) na Vikosi vya wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF), pamoja na washirika wao, wanahusika na mashambulizi makubwa, ya kiholela na ya moja kwa moja yaliyohusisha mashambulizi ya anga na makombora dhidi ya raia, shule, hospitali, mitandao ya mawasiliano na miundombinu mingine muhimu ya maji na umeme ikionesha kutozingatia kabisa ulinzi wa wasio wapiganaji.Joy Ngozi Ezeilo, mmoja wa wajumbe wa jopo hilo la wataalamu huru anaeleza kwamba, waathirika walisimulia kushambuliwa wakiwa kwenye nyumba zao na kutishiwa kifo au kuumizwa kwa ndugu au watoto wao kabla ya kubakwa na zaidi ya mtu mmoja.”Wachunguzi hao licha ya kupendekeza uwekaji zaidi wa vikwazo vya silaha kwa Sudan, pia wamehimiza kuanzishwa kwa kikosi cha kimataifa cha kulinda amani na ama kiwe chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa au mamlaka nyingine ya kikanda.

Habari za UN
05 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 5, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha nchini Bahrain kufuatilia harakati za vijana za kufanikisha haki za watoto waliozaliwa na usonji au Down Syndrome. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na uchambuzi wa methali “Jawabu la kesho andaa leo.”Awamu ya kwanza ya kampeni ya utoaji chanjo ya polio kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 10 imehamia hii leo eneo la kusini mwa ukanda huo hususan Khan Younis na itakamilika Jumapili hii. Mama mmoja aliyepeleka mtoto wake leo amesema aliposikia tu chanjo inatolewa dhidi ya polio alikimbilia kituo cha jirani cha tiba ili ampatie chanjo kwani anahofia itasambaa kutokana na mazingira machafu ya majitakama wanamoishi. Awamu hii itamalizika Jumapili. Awamu ya Pili itaanza baada ya wiki nne.Nchini China Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anahudhuria mkutano wa China na nchi za Afrika, leo amehutubia mkutano huo na kueleza masuala kadhaa yakusaidia kusongeza nchi za Afrika ikiwemo haja ya kutatua changamoto ya nchi za Afrika kuwa na madeni makubwa na kushindwa kuwekeza katika miradi ya maendeleo, ushirikiano wa kusini -kusini na hitaji la Afrika kuwa na uwakilishi wakudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.Na leo ni siku ya Kimataifa ya ukarimu duniani, mfano mmoja tu wa ukarimu unaoendelea sasa duniani ni ule shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA wanaopokea kutoka kila kona ya dunia kuanzia kwa watu maarufu, asasi za kiraia, mpaka watu binafasi, wote lengo likiwa ni kuwawezesha UNRWA kuhudumia wapalestina milioni mbili walio katikati ya mzozo huko Gaza.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, Mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anafafanua methali “Jawabu la kesho andaa leo.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
4 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 4, 2024 10:00


Ungana na Leah Mushi anayekutea jarida la Umoja wa Mataifa hii leo likiangazia juhudi za Afrika katika kujenga miji endelevu, mapambano ya kutokomeza magonjwa ya kitropiki yasiyopewa kipaumbele, matumizi ya sayansi katika nyanja mbalimbali za maisha na mashinani utasikia juhudi za kuhakikisha mipaka ya nchi inaendelea kuwa wazi hata wakati wa majanga ya asili na migogoro. 

Habari za UN
03 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 3, 2024 9:59


Karibu kusikiliza jarida ambapo hii leo mwenyeji wako Anold Kayanda anakuletea mada kwa kina inayoangazia nafasi ya vijana katika uongozi. pia utasikia muhtasari wa habari na mashinani inayoangazia kampeni ya utoaji chanjo ya polio  huko Ukanda wa Gaza, Mashariki ya Kati. 

gaza sdg karibu mashariki septemba
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 3 Septemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 3, 2024 16:40


Data ya hivi karibuni imeonesha kwa sasa ni ghali zaidi kununua nyumba Adelaide au Perth kuliko Melbourne.

Habari za UN
Kila mmoja achukue hatua kuondokana na vikwazo vya ujumuishaji watu wenye ulemavu - Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 28, 2024 1:33


Kila mmoja achukue hatua kuondokana na vikwazo vya ujumuishaji watu wenye ulemavu - GuterresUmoja wa Mataifa uko tayari kufanya kazi na Kamati ya Kimataifa ya Michezo ya Olimpiki ya Watu wenye Ulemavu (Paralympic) ili kufikia maono ya jamii shirikishi, jumuishi na endelevu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito michuano ya Paralympic iking'oa leo jijini Paris, Ufaransa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Bwana Guterres aliyeko ziarani nchini Timor Leste, barani Asia, ametuma ujumbe kwa Mkutano wa Kimataifa wa Ujumuishaji watu wenye Ulemavu unaofanyika katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris Ufaransa ambako michezo ya Olimpiki ya watu wenye ulemavu, Paralimpiki 2024 imeanza kutimua vumbi leo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaamini Michezo ya Olimpiki ya Watu wenye Ulemavu inahimiza kila mtu, kuanzia kwa serikali, mamlaka za mitaa na watoa uamuzi kila mahali, kuchukua hatua ili kuondokana na vikwazo vya ushirikishwaji kamili na wa maana wa watu wenye ulemavu na Umoja wa Mataifa unaahidi kushiriki kikamilifu kutimiza lengo hilo.Aidha katika mkutano huu wa ngazi za juu, UNESCO imeitumia nafasi hiyo kuzindua Kijitabu na mfululizo wa video za mafunzo  kuhusu Usawa wa Ulemavu katika Vyombo vya Habari. Kitabu hicho cha mwongozo kina masomo yanayolenga kuwapa wataalamu wa vyombo vya habari maarifa na zana wanazohitaji ili kuhakikisha mashirika yao yanakuwa jumuishi kwa kuwazingatia watu wenye ulemavu.Moja ya vivutio vikubwa katika paralimpiki za mwaka huu zitakazofanyika hadi tarehe 8 ya mwezi ujao Septemba ni timu ya wakimbizi wanane waliopelekwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.