Podcasts about kabla

  • 39PODCASTS
  • 115EPISODES
  • 19mAVG DURATION
  • 1MONTHLY NEW EPISODE
  • May 28, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about kabla

Latest podcast episodes about kabla

Siha Njema
Mipango tofauti ya matibabu ya matatizo ya Tezi koo ambayo hutumika Afrika

Siha Njema

Play Episode Listen Later May 28, 2025 10:06


Kabla mgonjwa yeyote kuanzishwa kwenye  matibabu, awe ana tatizo la tezi koo kuzalisha homoni kupitiliza au kushindwa kuzalisha, ni sharti vipimo maalum kufanyika Kipimo cha kwanzo ni inaangazia homoni tofauti inayozalishwa na tezi koo na hii mtu yeyote anaweza kufanya katika wakati wa kufanya vipimo kujua hali yake ya afya ,hapa mtu si lazima awe ameonesha dalili za tezi koo kuwa na tatizo.Kipimo cha pili ambacho ni muhimu huzingatia zaidi  viwango vya  homoni tatu muhimu zinazozalishwa na tezi koo ambayo ni  (TSH), thyroxine (T4), na  triiodothyronine (T3) .Matokeo yataamua ni mpango gani wa matibabu mgonjwa atapewa  dawa,kudhibiti homoni au kuzalisha homoni mbadala tezi koo inaposhindza kazi yake.Kando na dawa kama mpango wa matibabu ,wagonjwa wenye uvimbe wanaweza kushauriwa kufanya upasuaji kuondoa tezi koo ,sehemu yake au yote.Kuna pia mpango wa kutumia mianzi na madini ya Iodine maarufu kama Radioiodine mpango ambao ni sharti kufanywa kwa ueledi mkubwa na kwenye vituo vya afya vilivyo na vifaa vya viwango vya juu.

Superception
Ep. 114 - Hervé Kabla, multi-entrepreneur et auteur du livre "Comment planter sa boîte en 50 leçons"

Superception

Play Episode Listen Later Apr 27, 2025 81:50


Thème : les défis de l'entrepreneuriat. Hervé Kabla commente notamment son parcours (01:32), sa motivation pour écrire ”Comment planter sa boîte en 50 leçons” et l'écho rencontré par ce livre (24:35), la création d'entreprise avec des associés (32:21), le risque de quitter un emploi salarié et l'opportunité du congé pour création d'entreprise (35:22), les enjeux d'encadrement (43:29), le coût de l'avant-vente et les difficultés de la vente (46:03), les risques du télé-travail (51:40), l'importance de la culture d'entreprise (56:18), le rôle de la chance (59:37), les leçons et traces de son expérience (01:03:44), la situation française en matière d'encouragement à la création d'entreprise (01:09:50) et sa nouvelle aventure entrepreneuriale (01:15:43).

Wimbi la Siasa
Tanzania: CHADEMA yashinikiza mabadiliko kabla ya Uchaguzi Mkuu

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 9:54


Mwezi Oktoba 2025, wananchi wa Tanzania, watashiriki kwenye uchaguzi Mkuu, kuwachagua madiwani, wabunge na rais. Hata hivyo, chama kikuu cha upinzani cha CHADEMA, kikiongozwa na Mwenyekiti wake, Tundu Lissu, kinashinikiza mageuzi kwenye sheria za uchaguzi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo.Je, kitafanikiwa katika harakati zake ?

Jioni - Voice of America
Mawaziri wa mambo ya nje wa UAE wanakutana Misri kabla ya mkutano wa viongozi wa kukabiliana na pendekezo la Trump kuutwaa ukanda wa Gaza. - Machi 03, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 29:58


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Habari za UN
Kutana na Celestin Mbaruku mkimbizi mnufaika wa Mpango wa Utambuzi wa Ujuzi wa Awali nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 28, 2025 3:25


Kama mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Celestin Mbaruku hakuwa na fursa ya ajira rasmi hadi alipothibitishwa ujuzi wake kupitia mpango wa Serikali ya Kenya wa Utambuzi wa Ujuzi wa Awali, uliotengenezwa kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO.Kupitia ILO Celestin Mbaruku ni mnufaika wa ufadhili wa PROSPECTS, ushirikiano wa kimataifa unaojumuisha mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa ukilenga kuboresha upatikanaji wa elimu, ulinzi wa jamii, na ajira yenye hadhi kwa jamii zinazowakaribisha wakimbizi na watu waliolazimika kuhama makazi yao.Kimakosa, Celestin Mbaruku akiwa nchini mwake DRC alidhaniwa kuwa muasi, akafungwa lakini akamudu kutoroka hadi Kenya.Kabla ya masaibu haya, huko DRC alikuwa Mwalimu anayesimamia nidhamu katika shule alikokuwa anafanya kazi ya lakini kwa kuwa vyeti vyake vilipotea, hata alipovuka kuingia Kenya, hakuwa na uthibitisho wa kiwango cha elimu yake licha ya kuwa ana diploma ya mbinu za ufundishaji.Na hapo ndipo ikabidi achomoe kibindoni ujuzi wake mwingine. Ujuzi binafsi, ufundi wa kushona nguo.Celestin sasa anafundisha wanawake wadogo shughuli za kushona nguo.Hatimaye mwaka jana, 2024, kupitia mpango wa Serikali ya Kenya wa Utambuzi wa Ujuzi wa Awali (RPL), uliotengenezwa kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO utaalamu wake wa kushona nguo ambao haukuwa na cheti, ukathibitishwa rasmi na akapata cheti, hali ambayo imemfungulia milango ya kuomba ajira rasmi.

Habari za UN
Asante IFAD kwa kutuwezesha watu wenye ulemavu Liberia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 22, 2025 1:57


Nchini Liberia, mradi unaotekelezwa na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD umejengea uwezo watu wenye ulemavu wa kuona na kuwawezesha kuongeza vipato na vile vile uhakika wa kupata chakula. Simulizi ya Sabrina Moshi wa redio washirika SAUT FM mkoani Mwanza nchini Tanzania, inaelezea zaidi.Tuko kaunti ya Lofa, kaskazini kabisa mwa Liberia, magharibi mwa Afrika, tunakutana na Hawa Kamara, yeye ni mlemavu wa kutoona. Yeye pamoja na wenzake wa chama cha watu wenye ulemavu wa kutoona hapa Lofa, wanathibitisha kuwa unapoamua kufanya kitu, hakuna kinachokuzuia.Kupitia mradi wa Mabadiliko ya kilimo kwa wakulima wadogo na uchechemuzi wa kilimo biashara au STAR-P, mavuno ya mpunga kwenye shamba la kikundi hicho, yameongezeka kwa asilimia 300.Hawa anasema, “Mwanzoni hatukuwa na kitu kabisa. Tulihangaika sana kulima mpunga. Lakini baada ya IFAD kutufikia katika maisha yetu na kutusaidia, mambo yalianza kubadilika. Walitupatia pembejeo na mbegu za ubora wa juu kuanzisha mashamba. Tulitumia mbegu hizo kupanda kwenye mashamba yetu Bakadu.”Awali walilima ekari 1.2 tu, lakini baada ya kupatiwa vifaa vya kisasa vya kilimo wameweza kulima hadi ekari 4.3.Mavuno ya mpunga yameongezeka. Wanasagisha mashine, kiasi cham chele wanauza na ziada ni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.Hawa akiwa kwenye shamba lake la mpunga anasema,“Kabla ya STAR-P nilijihisi nimepotea na mpweke. Lakini sasa ninaweza kulima mwenyewe shambani, na ninaweza kujihudumia mimi na pia familia yangu. Zamani niliacha shule. Lakini baada ya kuanza mradi huu, nimerejea shuleni na ninataka kuwa mhasibu mkubwa duniani.”

Alfajiri - Voice of America
Trump ahotubia maelfu ya wafuasi wake Jumapili siku moja kabla ya kuapishwa kuwa Rais - Januari 20, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 20, 2025 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

LE BONHEUR C'EST LES AUTRES
Hervé Kabla : "Le bonheur c'est un souvenir"

LE BONHEUR C'EST LES AUTRES

Play Episode Listen Later Jan 14, 2025 28:25


Hervé Kabla est un homme brillant. Polytechnicien, à la fois ingénieur et spécialiste du marketing digital, il s'est depuis quelques années intéressé à la généalogie et a publié récemment chez Amazon « le guide pratique de la généalogie 2.0 » à l'attention des béotiens dans ce domaine.Interrogé dans un café bruyant de la Place de l'Alma à Paris, il nous délivre sa vision du bonheur qui, pour lui, est synonyme de souvenir. Il n'est donc pas question de profiter du moment présent mais de se remémorer les petits et les grands plaisirs passés.L'homme, sympathique, exprime aussi sa capacité à douter dans ces termes : « Le doute est le moteur essentiel de la vie ».Ecoutez ce nouvel épisode du podcast « Le Bonheur c'est Les Autres ». Hébergé par Ausha. Visitez ausha.co/politique-de-confidentialite pour plus d'informations.

SBS Swahili - SBS Swahili
Levi "Wazazi wasi harakishe kuwatuma watoto ng'ambo kabla hawaja komaa"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 31, 2024 20:49


Wazazi wengi huwa na ndoto za kuwatuma watoto wao ng'ambo kufanya elimu ya juu.

Radio Maria Tanzania
Mfahamu mfalme Herode enzi za Utawala wake kabla ya kuja Kristo.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Nov 13, 2024 48:39


Karibu uungane nami Happiness Mlewa , katika  kipindi cha Ujumbe wa Biblia, Leo nipo na Padre Titus Amigu  kutoka  Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) Jimbo Kuu Katoliki Mwanza, akiendelea kufundisha juu ya   kukoseana na kusamehana akiwatazama Wafalme mbalimbali, leo anamzungumzia Mfalme Herode. L'articolo Mfahamu mfalme Herode enzi za Utawala wake kabla ya kuja Kristo. proviene da Radio Maria.

Habari za UN
WFP: Bila msaada wa kibinadamu Wasudan watakufa kwa njaa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 28, 2024 1:35


Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, (WFP) leo kwa mara nyingine tena limetahadharisha kwamba bila msaada wa kibinadamu nchini Sudan, mamia ya maelfu wanaweza kufa kwa njaa. Vita vya kikatili nchini Sudan vimesababisha janga kubwa zaidi la njaa duniani, imeandika WFP katika ukurasa wake wa X leo Oktoba 28 na kufafanua zaidi kwamba mtu mmoja kati ya watu wawili nchini humo anatatizika kupata mlo kila siku.WFP inaeleza kuwa njaa imethibitishwa Kaskazini mwa Darfur na mahitaji ya kibinadamu ni makubwa sana.Kabla ya taarifa hii ya leo ya WFP, jana kupitia pia ukurasa wa mtandao wa X, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Cindy McCain ambaye hivi karibuni alikuwa Sudan mojawapo ya maeneo yenye njaa zaidi duniani, ambapo watu milioni 25 wanakabiliwa na njaa kali ameandika kwamba WFP iko Sudan inatoa msaada wa kuokoa maisha lakini wanahitaji kwa haraka mambo matatu ambayo ni kuwafikia watu ili kuwasaidia, misaada kuweza kupita katika kila kivuko na usaidizi zaidi wa kimataifa kwa Wasudani walio katika mazingira hatarishi.Kwa miaka mingi, Sudan imekuwa ikisumbuka na migogoro. Mgogoro wa hivi karibuni zaidi, ulioanza Aprili mwaka jana 2023, umezua janga baya zaidi duniani la watu kuhama makwao na janga kubwa zaidi la njaa duniani linalosambaa Sudan, Sudan Kusini na Chad.

Alfajiri - Voice of America
Zaidi wa wamarekani milioni 15 tayari wamepiga kura za mapema wiki mbilli kabla ya siku ya uchaguzi kufika. - Oktoba 23, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 23, 2024 29:57


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
27 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 27, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea kipindi maalum. Leo mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia siku ya nne, miongoni mwa wahutubiaji ni Tanzania. Kabla ya kupanda katika mimbari ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuketi na mwakilishi wa taifa hilo katika mjadala huu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kuzungumza naye masuala kadhaa ikiwemo mzigo wa madeni kwa nchi zinazoendelea  na pia nafasi ya wanawake katika nyanja ya kimataifa. Lakini kwanza alitaka kufahamu Waziri Mkuu Majaliwa amekuja na ujumbe gani kutoka Tanzania kwenye mjadala huu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari.Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu nchini Lebanon, Imran Riza, akizungumza kutoka mji mkuu wa Lebanon, Beirut, kwa njia ya video amewaeleza waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi leo kwamba katika Lebanon kipaumbele kwa sasa ni kuhakikisha usitishaji mapigano wa haraka ili kukomesha mateso zaidi ya raia na uharibifu. Bwana Riza amesisitiza tena wito kwa jamii ya wahudumu wa  kibinadamu kwa nchi zote kutumia ushawishi wao kusaidia katika kupunguza machafuko kwa dharura.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya Wanawake UN Women inaangazia athari kubwa za janga la kibinadamu linaloongezeka kwa wanawake na wasichana wa Sudan, wakiwemo milioni 5.8 ambao ni wakimbizi wa ndani.Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Geneva, Uswisi imetoa wito kwa mamlaka ya Haiti na jumuiya ya kimataifa kufanya zaidi kulinda watu na kuzuia mateso zaidi na kwamba hicho ndicho kinapaswa kuwa kipaumbele. Takwimu za hivi karibuni kutoka Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa takribani watu 3,661 wameuawa nchini Haiti tangu Januari mwaka huu.”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
ECW yarejesha matumaini kwa msichana Fatima wa Nigeria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 3:12


Alipokuwa na umri wa miaka 10 mnamo mwaka 2015, Fatima na familia yake walilazimika kutoroka nyumbani kwao Konduga, ili kuepuka mashambulizi kutoka kwa makundi yenye silaha. Konduga iko kilomita 25 kusini mashariki mwa mji wa Maiduguri, kaskazini mashariki mwa Nigeria.Familia ya Fatima haikuwa na namna ya kumuandikisha katika shule yoyote rasmi. Alitumia muda wake mwingi kuuza chakula.Shukrani kwa usaidizi wa mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri yaani Education Cannot Wait (ECW) na wadau wake wa kimkakati, Fatima sasa amesajiliwa katika mpango mesto unaolenga kuwapa elimu wasichana walio nje ya shule.Msichana huyu ni mmoja wa walengwa 250 wa programu ya miezi mitano ya kusoma, kuandika na kuhesabu, ambayo imemwezesha kusoma kwa lugha ya Kihausa na hata kuandika jina lake kama anavyoeleza."Niliingia katika shule ya ufundi baada ya kusikia kuihusu wakati nilipokuwa nimeenda kuuza chakua. Mara moja nilihifadhi kile nilichoenda kuuza kisha nikajiandikisha jina langu. Wale ambao tulikuwa hatuendi shule tulitambuliwa na kuchaguliwa. Tulifundishwa jinsi ya kusoma na kuandika. Kabla hapo nilikuwa siwezi hata kuandika jina langu.”Sehemu ya pili ya programu hii mseto ilihusisha kipengele cha ufundi ambapo wasichana wanaoishi katika mazingira hatarishi hupata mafunzo ya ufundi kwa muda wa miezi mitatu. Mpango unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, Norwegian Refugee Council (NRC) na Save the Children."Pia, sasa ninajua namba, na ninaweza kupima watu  ninaposhona." Anasema Fatima ambaye katika kipengengele cha ufundi yeye amechagua ushoni wa nguo.Mpango huu tayari umewanufaisha wasichana balehe 600 tangu kuanzishwa kwake, na kuwapa vifaa vya kuanzia na ujuzi wa kujitegemea. Fatima naye ana matumaini.“Nataka kujifunza stadi hii ili niwahishimishe wazazi wangu na wawe na furaha. Nikimaliza kujifunza nataka kuwa mtu wa kuwashonea ndugu zangu nguo.”Kama ambavyo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anatoa wito kwa nchi zote kuwekeza katika elimu na kufanya juhudi za kila namna kulinda elimu na maeneo ya kusomea, kulinda wanafunzi na walimu,  Mkurugenzi Mtendaji wa Education Cannot Wait (ECW) Yasmine Sherif, anaeleza namna ambavyo mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri umejizatiti kuendelea kuiunga mkono elimu kote duniani wakati huo akitoa wito kwa kila anayeweza kuwaongezea nguvu afanye hivyo."Kuna ustahimilivu na watoto hawa wamepitia kiwewe na mambo mengi. Ni lazima tuwepo kwa ajili yao, na tunaweza kuona matokeo. Tunatazamia kuufanya tena mpango huu mwaka katika mwaka huu, tunatarajia kufanya hivyo kwa takribani dola milioni 15, kama sio zaidi. Ikiwa nyinyi nyote mtakuja na kutusaidia kuongeza."

Jioni - Voice of America
Maelfu ya waandamanji wakusanyika nje ya jengo la bunge la Marekani kabla ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, kulihutubia. - Agosti 07, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 7, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Maelfu ya waandamanaji wakusanyika nje ya jengo la bunge la Marekani kabla ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kulihutubia. - Julai 24, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 24, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

VOA Express - Voice of America
Baadhi ya michezo ya Olimpiki yaanza Ufaransa hata kabla ya tarehe rasmi ya ufunguzi mwishoni mwa wiki. - Julai 24, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 24, 2024 30:00


VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.

Jioni - Voice of America
Kiongozi wa upinzani Kenya asema kuwa haki inahitajika kabla ya mazungumzo na serikali - Julai 21, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 21, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Radio Maria Tanzania
Je, Marehemu akifanyiwa maombi anaweza kusamehewa dhambi zake pasipo yeye kutubu kabla ya kifo chake?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Apr 22, 2024 23:11


Karibu katika kipindi cha Maswali yahusuyo Imani na Frateli Caspary Nyiihwil, kutoka Seminari Kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho Jimbo kuu la Songea Swali la Msikilizaji linalojibiwa linasema Ni halali kufanya ibada ya wafu na Je marehemu akifanyiwa maombi anaweza kusamehewa dhambi zake pasipo yeye kutubu kabla ya kifo chake? L'articolo Je, Marehemu akifanyiwa maombi anaweza kusamehewa dhambi zake pasipo yeye kutubu kabla ya kifo chake? proviene da Radio Maria.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Maadhimisho ya miaka 30 mauaji ya kimbari nchini Rwanda, uteuzi wa waziri mkuu mpya DRC

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Apr 6, 2024 20:18


Ni makala maalum, kuhusu kumbukumbu ya miaka 30 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994, tunahoji mchakato wa maridhiano umefikia wapi miaka 30 baadaye..... hali iko vipi kwa sasa. na dunia imepata  somo gani? Pia kuhusu mauaji hayo, tutarejelea kauli ya Rais Emanuel Macron iliyoonekana kuwa inalenga kutuliza hisia za waathiriwa.Huko DRC uteuzi wa Judith Tuluka Suminwa, mwanamke wa kwanza kuwa waziri mkuu. Mahakama nchini Uganda ilitoa uamuzi wake kuhusu sheria dhidi ya ushoga. Kabla ya kwenda Kenya, Sudani..pamoja na Senegal ambako Bassirou DF aliapishwa kuwa rais mpya, tutakwenda Israeli na maeneo mengine duniani.

Alfajiri - Voice of America
Rais Joe Biden asifu mafanikio ya utawala wake miezi michache kabla ya uchaguzi wa rais - Machi 08, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 8, 2024 29:59


Kwa Undani - Voice of America
Je, makubaliano yatapatikana kati ya Israel na Hamas kusitisha vita kabla ya Ramadan? - Machi 07, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 7, 2024 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

Alfajiri - Voice of America
Marekani ina matumaini kuwa sitisho la mapigano katika vita vya Gaza linaweza kupatikana kabla ya Ramadhani - Machi 05, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 5, 2024 29:59


Jioni - Voice of America
Chama cha madaktari na wauguzi cha Kenya chatoa ilani ya siku 7 kwa serikali, kabla ya kuitisha mgomo wa kitaifa. - Machi 04, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 4, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Israel inasema jeshi lake limetayarisha mpango wa kuwahamisha wakaazi wa Gaza kabla ya uvamizi unaohofiwa huko Rafah. - Februari 26, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 26, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

VOA Express - Voice of America
Ushauri kuhusiana na tahathari za kuchukua kabla ya kukutana na wapenzi mliopatana kupitia mitandao ya kijamii - Februari 12, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 12, 2024 29:59


VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.

VOA Express - Voice of America
Wavulana wengi nchini Uganda waacha shule kabla ya kuhitimu elimu ya msingi kulingana na wadau wa elimu - Januari 26, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 26, 2024 29:59


Dr Boaz Mkumbo
Zingatia haya kabla ya kutumia mafuta ya Olive Oil

Dr Boaz Mkumbo

Play Episode Listen Later Jan 6, 2024 2:16


Katika epsod hii utajifunzza juu ya mambo ya kuzingatia kabla ya kutumia mafuta ya Oil. kitabu cha sayansi ya mapishi ni kitabu kinachotoa muongozo wa lishe bora na kukusaidia kubadilisha  jiko lako kuandokana na magonjwa ya lishe kilichoandikwa na Dr Kitundu Boaz K (@drboazmkumbomd) kwa mahitaji ya nakala ya kitabu cha sayansi ya mapishi wasiliana nasi kwa simu namba  Jiunge na programu ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa ya NHC WAEIGHTLOSS BOOT CAMP Fuata Taratibu hizi za Malipo ili kujiunga. TIGO PESA LIPA NO: 7780779 MPESA LIPA NO: 5567920 JINA: HEALTHY EATING COMPANY LIMITED Ukisha Lipia Nitumie SMS, EMAIL na MAJINA YAKO kwenye meseji Moja usajili Uanze Leo na Masomo Utumiwe Leo Leo. Namba ya Whatsapp Ya Kutuma Taarifa zako: 0767 030 160 AU WASILIANA NASI SIMU: +255767 074 124 +255787 999 994   Usisahahu KUSUBCRIBE kwa elimu zaidi kuhusu magonjwa ya lishe kama vile KISUKARI KITAMBI NA UZITO MKUBWA SHINIKIZON LA DAMU (PRESHA) MVURUGIKO WA HOMONI UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME TEZI DUME MAGONJWA YA GOITA   Tufuatilie katika mitandao ya kijamii INSTAGRAM https://www.instagram.com/sayansiyama... https://www.instagram.com/nsambohealt... FACEBOOK https://www.facebook.com/drboazmkumboMD BLOG https://blog.heaprogram.co.tz/ WEBSITE https://heaprogram.co.tz/ http://nsambohealthcare.tilda.ws/  

Alfajiri - Voice of America
Kampeni za uchaguzi DRC zimemalizika rasmi na sasa raia wanasubiri saa chache kabla ya vituo vya kupiga kura kufunguliwa rasmi nchini humo. - Desemba 19, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 19, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

humo kura sasa raia kabla uchaguzi desemba kupiga kampeni chache
Jioni - Voice of America
LIve Talk: Hali ni ya wasi wasi DRC wiki mbili kabla ya uchaguzi mkuu kutokana na ukosefu wa usalama na upungufu wa vifaa vya uchaguzi - Desemba 08, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 8, 2023 59:57


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wahamiaji wanahitaji taarifa gani kabla waje Australia?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Oct 5, 2023 11:17


Kila mwezi makumi yama elfu ya wahamiaji huwasili katika miji mbali mbali nchini Australia.

Jioni - Voice of America
Wananchi wa Zimbabwe waiombea amani nchi yao kabla ya uchaguzi wa Agosti 23 - Agosti 20, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 20, 2023 30:00


zimbabwe agosti kabla uchaguzi wananchi
SBS Swahili - SBS Swahili
Ziara ya kombe la dunia ya anza nchini Australia kabla ya michuano hiyo kuanza

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 11, 2023 7:44


Tiketi milioni moja za kombe la dunia, la soka ya wanawake itakayo andaliwa nchini Australia na New Zealand zime uzwa tayari.

Habari za UN
Sitisha uhasama miongoni mwa wakimbizi wa ndani Sudan Kusini: UNMISS 

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 9, 2023 0:02


Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umetoa wito wa kusitishwa mara moja kwa uhasama miongoni mwa wakimbizi wa ndani katika Kambi ya Umoja wa Mataifa ya Ulinzi wa Raia nchini humo kufuatia tukio la jana Alhamis ambapo watu kadhaa waliripotiwa kujeruhiwa na wengine kuuawa.Video iliyorekodiwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) inaonesha gari la wagonjwa la Umoja wa Mataifa likisindikizwa na walinda amani likipita katika barabara ya vumbi katikati ya umati wa wakimbizi wa ndani katika eneo la Malakal nchini Sudan Kusini.  Kila mmoja aliyefanikiwa kusalia na chochote katika anavyovimiliki, amekibebeba kichwani, mgongoni au mkononi.  Jana muda wa mchana ghasia zilizuka kati ya jamii mbili za wakimbizi wa ndani ambazo zimehifadhiwa katika Kambi ya Umoja wa Mataifa ya Ulinzi wa Raia. UNMISS inasema vurugu hizo zilichochewa na tukio la kuchomana visu huku ripoti za awali zikitaja raia watatu kuuawa na wengine 20 kujeruhiwa hadi kufikia jana Alhamisi mchana. Kabla ya hapo, hiyo-hiyo jana Alhamis asubuhi, milio ya risasi ilitanda alfajiri katika mji mkuu wa jimbo la Upper Nile, Malakal, karibu na makazi ya UNMISS.Walinda amani wa UNMISS waliingia kazini haraka kwa kuwa hali ya wasiwasi imekuwa ikiendelea hapa tangu mwisho wa wiki iliyopita, wakati mzozo katika kituo cha maji uliongezeka haraka na kuwa mzozo kamili ambapo mtu mmoja mwenye umri wa miaka 32 aliuawa. Kwa kuwa kambi ya walinda amani iko karibu na kambi ya Umoja wa Mataifa ya ulinzi kwa raia, mara zote walinda amani wako chonjo kuchukua hatua ya haraka pindi tu wanapopokea taarifa ya vurugu. Wakati wa mapigano ya mwezi uliopita, wanajeshi na polisi walinda amani walitumwa mara moja ili kutuliza hali hiyo. Polisi na walinda amani wa kijeshi kwa sasa wanashika doria ndani ya eneo hilo na kuzunguka eneo la nje, kwa ushirikiano na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Sudan Kusini ili kuondoa hofu miongoni mwa jamii iliyokimbia makazi yao. Zaidi ya hayo, walinda amani matabibu katika hospitali ya UNMISS wanatoa huduma ya dharura kwa baadhi ya waliojeruhiwa.  Kwa mujibu wa usajili wa kibayometriki wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM), kufikia Desemba mwaka jana 2022, baadhi ya watu 37,032 waliokimbia makazi yao wanajihifadhi katika Eneo la Ulinzi la Umoja wa Mataifa la Malakal. 

video zaidi umoja polisi raia kila kwa wakati kambi jeshi mataifa kabla unmiss shirika ujumbe wananchi miongoni desemba malakal sudan kusini alhamis alhamisi
Habari za UN
UNAIDS: Ili kutokomeza ukimwi ifikapo 2030 kila mtu lazima ajumuishwe hata watumia mihadarati

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 8, 2023 0:04


Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na vita dhidi ya ukimwi UNAIDS limesema ili kuhakikisha ukimwi unatokomezwa ifikapo mwaka 2030 basi kila mtu anapaswa kujumuishwa katika vita hivyo ikiwemo wafungwa na wanaotumia mihadarati, kwani Mifumo mingi ya magereza inajitahidi kukabiliana na msongamano, rasilimali duni, ufikiaji mdogo wa huduma za afya na huduma zingine za msingi, vurugu na matumizi ya dawa za kulevya.Nchini Moldova, gereza namba 16 la Pruncul moja ya magereza ambako UNAIDS inashirikiana na serikali na mamlaka za afya kuhakikisha wafungwa na hasa wanaotumia mihadarati wanapata huduma za kudhibiti virusi vya ukimwi au VVU na kukabiliana na athari za matumizi ya mihadarati.Shirika hilo linasema mwaka 2021, idadi ya wafungwa magerezani duniani kote iliongezeka kwa asilimia 24 ikilinganishwa na mwaka wa 2020 hadi kufikia zaidi ya watu milioni 10.Kwa mujibu wa takwimu za ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa za kulevya na uhalifu UNODC katika baadhi ya nchi hadi asilimia 50 ya watu walio gerezani hutumia au hujidunga dawa za kulevya ambayo ni moja ya sababu kubwa ya maambukizi ya magonjwa yatokanayo na damu kama vile VVU na hepatitis C.Moldova ni miongoni mwa nchi zilizathirika na matatizo haya kwani tangu mwaka2000, ni magereza machache tu nchini humo yaliyokuwa yakitoa huduma za kupunguza madhara. Lakini sasa kwa msaada wa UNAIDS magereza yote 17 yana huduma na mfungwa yeyote mpya katika jela za nchi hiyo anawajibika kumuona daktari wa magonjwa ya akili, na daktari wa kawaida kwa vipimo na ikihitajika basi anajumuishwa katika mpango wa matibabu.Mfungwa Alexander Godin ni miongoni mwa waathirika anapitia katika milango kadhaa iliyofungwa katika gereza namba hili huku akisindikizwa na mlinzi hadi kwenye duka la dawa gerezani hapo. Hii ni sehemu ya utaratibu wake wa kila siku. Anakuja kuchukua dawa yake ya maji ya methadone baada ya kuacha uraibu wa dawa za kulevya, "Nimekuwa kwenye matibabu mbadala ya methadone kwa miaka 10. Familia yangu ilifanya uamuzi huu. Kabla ya hapo, nilitumia dawa za kulevya, afuni. Kwa hili, pesa zilihitajika, na hapo ndipo shida zilianza katika familia. Familia ilipendekeza niende kujiorodhesha kwenye zahanati inayotoa matibabu na tangu hapo nimekuwa kwenye mpango huo.” Methadone ni tiba inayosaidia watu kukabiliana na dalili za athari za mihadarati, msongo wa mawazo, kupunguza utegemezi wa heroini na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwenye sindano zenye maambukizi.Maria Potrimba, mkuu, idara ya magonjwa ya kuambukiza, Gereza hapa anasema "Ikiwa mgonjwa yuko kwenye matibabu haya mbadala, anafahamu zaidi kuhusu athari na anazingatia zaidi matibabu yake."Maambukizi ya VVU ni asilimia 11 kati ya watu wanaojidunga dawa za kulevya nchini Moldova ambao ni zaidi ya asilimia 0.36 ya watu wote. Na ni moja ya makundi yaliyoathirika zaidi nchini humo.Svetlana Plamadeala, ni mkurugenzi wa UNAIDS nchini Moldova amasema, "Nchini Moldova mzigo wa VVU ni mkubwa zaidi miongoni mwa makundi muhimu na pia huathiri wafungwa. Ofisi UNAIDS nchini humu iliunga mkono serikali kufanya majaribio ya programu za kupunguza madhara na matibabu ya mbadala wa afyuni magerezani tangu mapema mwaka wa 2000. Leo tunasherehekea ukweli kwamba tumepanua wigo wa huduma hizo kutoka kwenye mradi wa majaribio hadi kwenye mfumo mzima wa magereza au kila gereza lina huduma hizo. Ni katika kutoa kipaumbele kwa watu na pia ni kuhusu mtazamo wa afya ya umma.”UNAIDS, na washirika wengine wa Umoja wa Mataifa kwa muda mrefu wamekuwa wakiunga mkono kupanua huduma hizi kwenye magereza yote.Kwa sasa, kulingana na Harm Reduction International, ni nchi 59 pekee duniani ndio zinazotoa huduma hizo katika magereza yake.

Nånting Om Aktier
128. Kabla upp portföljen med Transtema

Nånting Om Aktier

Play Episode Listen Later Mar 6, 2023 40:16


Ett bolag som handlas 6 gånger EBITDA och växer 12% organiskt låter osannolikt. Men så är fallet för veckans case: Transtema. Transtema installerar och underhåller telekomnäten bestående av koppar, fiber och antenner, dvs. kommunikationsnäten. Transtema ger serivice till allt som blinkar i en teknikbod. Det finns överhängande risker som lurar i vassen i form av höjda personalkostnader och gamla stämningar. Båda dessa punkter samt mycket, mycket mer ses över i veckans avsnitt. I veckans volley tipsar Markus om att lita på sin strategi medan Tim sneglar åt Asien och Kina. Skriv gärna till oss på: nantingomaktier@gmail.com Instagram: @nantingomaktierBetygsätt gärna podden på Spotify och iTunes för att ge oss och Unga Aktiesparare mer spridning.En podd från Unga Aktiesparare.-9.17 - Dagens case36.35 - Veckans VolleySupport this show http://supporter.acast.com/nantingomaktier. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.

Habari za UN
Mradi wa ILO wawezesha wanawake wa kimasai Kenya kujua kusoma, kuandika na kuanzisha biashara

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 27, 2023 0:02


Nchini Kenya, mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO wa ubia wa maendeleo kati ya sekta ya umma na binafsi, PPDP umewezesha wanawake wa jamii ya kimasai katika eneo la Rift Valley kujiinua kiuchumi na kijamii. Thelma Mwadzaya na ripoti kamili kama ilivyoandaliwa na ILO.Mmoja wa wanufaika hao ni Mary Nkisonkoi kutoka kijiji cha Oloshaiki kilichoko eneo la Rift Valley au Bonde la Ufa nchini Kenya.Mary kupitia video ya ILO anasema alikuwa na bahati sana kuchaguliwa kuwa mwezeshaji wa jamii katika mradi wa PPDP.“Kabla ya mradi huu kuanza, wanawake katika eneo letu hawakuwa wanakutana na kuzungumza kwa uwazi na kina matatizo na changamoto zinazowakabili. Hatukuruhusiwa kufanya hivyo labda pale tu ambapo waume zetu walifahamu kile ambacho kinajadiliwa,” anasema Mary.Walikuwa wamezoea kusalia kijijini na kukutana kanisani na baada ya ibadi kila mtu anarejea nyumbani na kuendelea na wajibu wake wa kifamilia. Hatukufahamu kuwa sisi wanawake na akina mama tunaweza kufanya kitu na kusaidia kama jamii au kama wanawake.PPDP ikabisha hodi OloshaikiMradi wa PPDP ukaingia na ukaanza kufundisha wanawake kuhusu jinsia, haki za wanawake na tofauti kati ya mke na mume.“Hii ilituhamasisha kuzungumza na wanaume wetu,” anasema Mary huku akiongeza kwamba alifundishwa kuwa mwezeshaji ili kuwaleta pamoja wanawake na wanaume katika majukwaa ya umma. “Niliwaita wazee wa kijiji, wanawake, viongozi wa vikundi vya kijamii ili kujadili ni jambo gani lifanyike ili kuinua eneo letu.”Mabadiliko chanya ya kujivuniaMary anasema mabadiliko ya kwanza kutokea na ambayo anajivunia ni pale wanawake walipoweza kupata elimu ya watu wazima. “Tulifundishwa na mwalimu kutoka mradi wa PPDP. Tulifundishwa pia jinsi ya kuendesha biashara.”Wanawake wengi walijiunga na darasa kwa sababu “hatukuwa na njia nyingine ya kujipatia kipato. Kwa asili, wanawake hawawezi kuuza ng'ombe au mahindi kwa sababu shamba ni mali ya mume.”Walijipanga vema ili wasikose darasaMary anasema mwanzoni ilikuwa changamoto, lakini walijifunza kujipanga mapema kuhakikisha majukumu ya nyumbani na uchungaji wa mbuzi na ng'ombe unafanyika asubuhi. Ikifika saa 8 adhuhuri watoto wanaporejea nyumbani kutoka shuleni, wanawake walienda darasani.“Wanawake walijifunza alfabeti pamoja nan amba na matokeo yake waliweza kutumia simu za rununu au za kiganjani,” anasema Mary.Baada ya kujua kusoma na kuandika, nini kilifuatia?Mwezashaji huyu wa jamii anasema baada ya darasa la elimu ya watu wazima, walifikiria ni nini tena wanaweza kufanya na kuleta mabadiliko zaidi.“Tulianzisha kikundi cha upatu. Siku yetu ya soko ni jumatano ambako  wanawake wanauza maharage, viazi au mboga za majani. Tuliamua kukutana kila Alhamisi baada ya siku ya soko na kila mwanamke alete dola senti 40 au dola senti 81. Na iwapo mwanamke anataka kukopa fedha kukuza biashara yake, tunamkopesha na atarejesha na riba. Kisha tutampatia tena mwanamke mwingine akuze biashara yake.” Mafanikio mengine sasa wanaume wamepata uelewa wa kuwapatia wake zao nafasi na fursa kwa sababu Mary anasema, “nilipoketi nao kama mwezeshaji, niliwaeleza kuwa akina mama nao wanaweza kuleta kipato nyumbani, wakalipa karo na hata kununua chakula.”Sasa anasema wako huru kuanzisha na kumiliki biashara. Kila mwanamke anaweza kupeleka kitu nyumbani na kuweka mezani, hata kiwe kidogo kiasi gani.Hata shilingi 500 za Kenya saw ana dola 4.10. Tunawaambia waume zetu hiki ndicho nilichopata,” anasema Mary akiongeza kuwa hayo ni mabadiliko makubwa na hatuishi kama tulivyokuwa tunaishi zamani. Mary anasema “ninajiambia katika biashara yangu siku moja nitakuwa miongoni mwa nyota zinazong'ara kwenye eneo hili.” Kupitia ujasiriamali wa kukuza ng'ombe bora, Mary ameweza kujenga nyumba yake na anatamatisha akisema, “wanawake si watu wa kukandamizwa. Pale mwanamke anapoelimishwa, jamii itanufaika zaidi. Kwa hiyo…

Alfajiri - Voice of America
Mpango wa ICC kumfungulia Joseph Kony mashtaka kabla hajakamatwa waibua hisia mseto - Desemba 01, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 1, 2022 29:59


Waathiriwa wa ukatili wa kundi la waasi la Lord's Resistance Army, LRA, nchini Uganda, wamekuwa na maoni mseto, kuhusu mipango ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuanzisha kesi dhidi ya kiongozi mtoro wa kundi hilo, Joseph Kony, bila kuwepo mahakamani.

Habari za UN
Kisima cha maji kinatumia nishati ya jua katika shule ya Msingi ya Daley, Garissa nchini Kenya.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2022 0:03


Msaada wa kisima cha maji uliofanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika shule ya Msingi ya Daley kwenye Kijiji cha Daley, Kaunti ya Garissa nchini Kenya, umesaidia sana jamii hasa katika suala la elimu katika eneo hilo la nchi ambayo imekosa mvua ya kutosha kwa misimu mitano mfululizo.Ni wanafunzi wakiwa darasani, kwa uchangamfu wakijadiliana na mwalimu wao kuhusu umuhimu wa maji katika maisha ya kila siku. Nje ya darasa lao kunaonesha wazi hali ya ukame ilivyo ya kutisha. Ardhi imekauka na ni miti michache tu imebaki na ukijani. Kabla ya UNICEF kwa kushirikiana na jamii na serikali kuigilia kati, hali ya kukosekana kwa mvua imesumbua maisha ya wakazi wa hapa ikiwemo upatikanaji wa elimu kwa watoto wa jamii hii ya wafugaji kama asemavyo Mwalimu Mkuu Msaidizi, Wasula Samson Saiya anasema "Tuna takribani wasichana 146 na wavulana 200 jumla wanafunzi 346. Unagundua kwamba wengi wa wanafunzi wanachunga mifugo. Kwa hiyo, wakati wa ukame kama hivi unakuta pia wanahama na wanyama hao kule walikokwenda kulishia ili wawachunge. Kwa hivyo, tunajikuta tuna wanafunzi wachache darasani.” Ili kuitatua hali hiyo, UNICEF ilitoa msaada wa kifedha na kiufundi kuchimba kisima cha chini ya ardhi na kuweka mfumo wa kupaadisha maji kwa kutumia nguvu ya nishati ya jua na pia ujenzi wa upanuzi mpya wa bomba ili kuunganishwa na miundombinu iliyopo ya usambazaji wa maji. Takriban watu 6200 wakiwemo wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Daley na Kituo cha Maendeleo ya Awali ya Watoto (ECDC) wanapata huduma ya maji salama. Aidha, zahanati moja ya afya ina huduma ya maji salama. Osman Aden Abdi, Naibu Mkurugenzi, Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Idara ya Maji ya Kaunti ya Garissa anasema "Faida ni nyingi. Wakati tulipopata kisima, hali ya hatari katika suala la wanyama pori imepungua. Unyanyasaji wa kijinsia pia umepungua kwa sababu kioski hiki cha maji kiko mahali pa wazi sana. Tuna bahati sana kwa sababu umbali ni kama mita 50 tu hadi mahali pa maji. Inaokoa muda linapokuja suala la masomo ... unajua, katika maeneo yetu ni kukavu sana na joto sana. Kwa hivyo, tunawaruhusu wanafunzi kupata maji kila baada ya dakika 30...badala ya kurudi nyumbani. Kuna maeneo kadhaa ambako UNICEF, kwa usaidizi wa serikali ya kaunti imeweka mitambo ya nishati ya jua. Baada ya kisima hiki kilichimbwa na kuwekewa nishati ya jua, hakuhitajiki gharama zaidi, ili kwa muda mrefu jamii ziweze kujikimu zenyewe.” Kufikia Novemba 2022, katika Kaunti ya Garissa, UNICEF tayari imesaidia ukarabati wa mifumo 21 ya usambazaji wa maji na kufikia jumla ya watu 92,279 wanaopata maji salama. 

Alfajiri - Voice of America
Hali ilivyo nchini Qatar saa 48 kabla ya kipute cha Kombe la Dunia kuanza - Novemba 18, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 18, 2022 30:00


Wageni, wachezaji na mashabiki wa mpira wa miguu, wanaendelea kuwasili nchini Qatar, tayari kwa michuaao ya Kombe la Dunia mwaka 2022, ambayo itaanza rasmi kesho kutwa, na kwendelea hadi Desemba 18, wakati fainali itafanyika kwenye uwanja wa Lusail.

Habari za UN
Juhudi za UNICEF Uganda zafanikisha watoto kupata chanjo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 17, 2022 0:03


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na serikali ya Japan , wanaisaidia serikali ya Uganda kuimarisha uwezo wa mfumo wa uhifadhi wa chanjo baada ya mfumo wa afya kuathirika vibaya na janga la COVID-19, lengo likiwa kuhakikisha kila mtoto na kila mtu hasa katika jamii zisizojiweza anapata chanjo za kuokoa maisha. Taarifa zaidi inasomwa studio na Happiness Palangyo wa Redio washirika Uhai FM  (TAARIFA YA HAPPINESS PALANGYO)  Eneo la Lira Kaskazini mwa Uganda ni moja ya maeneo yaliyoathirika kwa kiasi kikubwa na janga la COVID-19 ambalo limeuacha hoi mfumo mzima wa afya ikiwemo huduma za uhifadhi na utoaji chanjo.  Lakini sasa kupitia uwekezaji mkubwa uliofanywa na shirika la UNICEF kwa ufadhili wa serikali ya Japan umerejesha matumaini ya wakazi na hususan watoto kupata chanjo wanazostahili kwani shirika hilo limenunua na kuweka majokofu maalum 115 ya kuhifadhi chanjo ya COVID-19 na kupiga jeki chanjo zingine za kawaida ambazo ni za kuokoa maisha kwa watoto. Dkt. Ochen Buchan Patrick ni afisa wa huduma za afya wilayani Lira anasema  “Huu ni uwekezaji mkubwa ambao utatusaidia sana kutoa huduma zote muhimu kwa saa 24 bila kuingiliwa na ukarabati wa mfumo wa baridi . Mfumo huu mpya sasa unafanya kazi vizuri kwa sababu unatumia  nishati ya sola na ninafurahi kwamba sasa hatuhangaiki kugawanyaganywa gesi na kisha Kwenda kukusanya mitungi. Hivyo gharama za uendeshaji zimepungua kwa kiasi kikubwa , lakini pia mfumo wetu wa baridi wa uhifadhi umeimarika sana.”  Kabla ya mfumo huu mpya wa kuhifadhi chanjo,ilikuwa changamoto kubwa kuwafikia walengwa na chanjo muhimu kama asemavyo Mirriam Adongo afisa wa program ya chanjo katika kituo cha afya cha Ogur  “Tulikuwa tunakwenda hadi Lira mjini kupeleka chanjo. Tulikuwa tunaendesha pikipiki hata wakati wa mvua , na chngamoto ya hali mbaya ya hewa, barabara mbaya vyote vilikuwa vinatusibu, lakini sasa kwa mfumo kuletewa hapa imefanya kuwa rahisi kwetu hata kutoka nje kwa sababu tunaweza kupata chanjo kwa urahisi na pili unatumia sola, kabla ya hapo tulipokuwa na mtambo unaotumia umeme , umeme ukikatika tu ilitulazimu kukimbiza chanjo zote hadi kwenye kituo cha wilaya cha kuhifadhi chanjo mjini ambayo ilikuwa kazi kubwa”  Uongozi wa huduma za afya wa Lira unasema sasa huduma zimeimarika na la msingi lililosalia ni kuhakikisha vifaa hivyo  vinatunzwa vyema na kudumu kwa mufda mrefu ili kuendelea kuihamasisha jamii na kuwapa chanjo muhimu.  Nalo shirika la UNICEF limesema furaha yake ni kuona lengo lililokusudiwa linatima kwani kwao kuwekeza katika vifaa hivyo vya mfumo wa bardidi wa kuhifadhi chanjo ilikuwa muhimu sana kama ilivyo kuwekeza kwenye upatikanaji wa chanjo zenyewe na sasa hata vituo vya afya vya vijijini kabisa vinaweza kuhifadhi chanjo zake, shukran kubwa kwa serikali ya Japan. 

Habari za UN
Mradi wa kusoma na kuandika waleta manufaa kwa wanafunzi Zambia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 14, 2022 0:02


Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF nchini Zambia kwa kushirikiana na serikali ya Zambia na Taasisi ya Hampel wanaendesha programu iitwayo Catch Up yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi wa shule za msingi nchini humo kupata matokeo bora ya masomo ya hisabati na kusoma hususan wale waliokuwa na ufaulu mdogo wa masomo hayo na sasa matokeo chanja yameanza kuonekana, tuungane na Leah Mushi kwa Taarifa zaidi. Taarifa ya Leah Mushi Katika jimbo la Luapula nchini Zambia, video ya UNICEF inamuonesha mwalimu akitumia mbinu mbali mbali ikiwemo kutumia ubao , kuchora kwenye sakafu na chaki na hata kurusha mawe ili kuwaelimisha wanafunzi somo la hisabati. Wanafunzi hawa ni miongoni mwa zaidi ya wanafunzi 80,000 wanaopata masomo ya ziada ya somo hili la hisabati lakini likiwa na mbinu pia za kuwafanya wajue kusoma kupitia programu ya Catch up. Judith Chama ni mwalimu wa programu hiyo katika shule ya msingi Chiseta anasema hapo awali hali ilikuwa si nzuri “Kabla ya kuja kwa program ya Catch up, wanafunzi wetu walikuwa hawawezi kusoma nambari kama elf umoja na mbili, lakini baada ya kuanza kwa masomo mpaka sasa, wanafunzi ambao nipo nao darasani kwangu wanaweza kusoma 5366.” Katika shule nyingine ya msingi ya Pembeshi mwalimu Caroline Nsemiwe anasema mzazi wa mtoto mmoja alimpa ushuhuda kuwa mwanae ameimarika sana kwenye kusoma, hapo awali alikuwa anasoma herufi moja moja lakini sasa anaweza kusoma neno kamili. Kauli yake hii inaungwa mkono na wazazi Esther Bwalya na Akim Mulenge “Nikiangalia mtoto wangu alipokuwa awali na alipo sasa napata furaha sana, kuna utofauti mkubwa. “Watoto wetu wangekuwa nyuma sana kama wasingefikiwa na program hii mapema kwasababu Watoto walio darasa la 3,4 na la 5 wanafanya vizuri zaidi kuliko wale walio darasa la 6 na 7”. Habari hizi njema pia zinawapa furaha wafadhili wa mradi huo na kupongeza ushirikiano wanaopata kutoka kwenye uongozi wa jimbo la Luapula na wanaaamini matokeo hayo yatakuwa na manufaa bora zaidi kadri siku zinavyozidi kwenda. Kwa sasa programu hii inatekelezwa katika wilaya nne za jimbo la Luapula, na mwaka 2023 inategemewa kuanza kutekelezwa katika wilaya zote za jimbo hilo.  

Habari za UN
Walimu wasio na sifa ni moja ya sababu za janga la elimu duniani- UNICEF

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 16, 2022 2:31


Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani ukianza leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limetoa taarifa inayoeleza idadi ya Watoto wasiojua kusoma imeongezeka ulimwenguni ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita.Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Assumpta Massoi Jijini New York, Marekani katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, UNICEF wameweka mfano wa darasa kando mwa bustani ya mawaridi, darasa hili linaitwa “Darasa la Mgogoro wa kujifunza”, lengo ni kufikisha ujumbe wa changamoto ya elimu duniani hivi sasa.  Katika kuhakikisha wanafikisha ujumbe wa changamoto ya elimu UNICEF wameweka mfano wa darasa kando mwa bustani ya mawaridi katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, darasa hili linaitwa “Darasa la Mgogoro wa kujifunza”. Darasa hili limewekwa ubao na madawati lakini theluthi moja ya madawati hayo yametengenezwa kwa mbao na kuwekwa mabegi ya mgongoni ikiwakilisha theluthi moja ya Watoto wenye umri wa miaka 10 wanaokadiriwa kuwa na uwezo wa kusoma na kuelewa ulimwenguni. Kabla ya Janga la COVID-19 miaka miwili iliyopita watoto waliojua kusoma wenye umri wa miaka 10 ulimwenguni walikuwa nusu lakini sasa UNICEF linasema idadi yao ni theluthi moja hii ikiwa sawa na mtoto mmoja kati ya watatu ndio mwenye uwezo wa kusoma na kuelewa hadithi fupi. Katika taarifa yake iliyotolewa jijini New York Marekani Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF Catherine Russell ameeleza sababu za kuporomoka kwa uwezo wa Watoto kujua kusoma ni shule zilifungwa muda mrefu kipindi cha janga la CORONA na kuwaacha mamilioni ya Watoto bila ujuzi wa msingi wa kusoma na kuhesabu, elimu haikuwa bora na kufichua mapungufu mengi ndio maana idadi ya Watoto wasiojua kusoma na kuhesabu imeongezeka kwa kiwango cha kushtusha na kuonya hii ni hatari kwa Maisha ya baadae ya watu wote duniani. Taarifa hiyo imemnukuu Bi Russelle akisema “Mifumo yetu ya elimu ndio mwelekeo wa maisha yetu ya baadae. Tunahitaji kubadili mwelekeo wa sasa au itatubidi kukabiliana na matokeo ya kushindwa kuelimisha kizazi chote. Viwango vya chini vya kujifunza vya leo inamaanisha fursa ndogo kesho.” Wakati viongozi wakikutana katika Mkutano wa marekebisho ya mfumo wa elimu UNICEF imetoa wito kwa serikali kujitolea kuwafikisha Watoto elimu bora kwa kuongeza uwekezaji kwenye elimu, kuweka mazingira salama ya kujifunzia, kuandikisha Watoto wengi shule na kuboresha maslahi ya walimu. Mkuu huyo wa UNICEF amesema hali ya sasa ni mbaya “Shule hazina rasilimali, walimu wanalipwa ujira mdogo, walimu wengine wasio na sifa wanaajiriwa, msongamano wa wanafunzi madarasani, mitaala ya kizamani na vyote hivi vinasababisha Watoto kushindwa kufikia uwezo wa juu wa ufaulu.”  

Jioni - Voice of America
Raila, Ruto wahutubia mikutano ya mwisho ya kampeni kabla ya uchaguzi mkuu - Agosti 06, 2022

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 6, 2022 29:59


Odinga anayepeperusha bendera ya muungano wa Azimio la Umoja One Kenya na viongozi wa mrengo huo pamoja na wafuasi wao, walikusanyika katika uwanja wa michezo wa Kasarani huku Ruto, anayewania kwa tiketi ya chama cha UDA chini ya muungano wa Kenya Kwanza akijiunga na wenzake kwenye uwanja wa Nyayo.

uda ruto agosti odinga kabla mkuu azimio uchaguzi mkuu kampeni
SBS Swahili - SBS Swahili
Fikiri kwa makini kabla upige simu kwa 000

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 19, 2022 13:17


Jeshi la polisi lina wahamasisha wa Australia watumie namba ya (000) kwa dharura tu, na wawasiliene na polisi kwa matukio mengine yasiyo ya dharura kupitia namba zingine za huduma.

Habari za UN
Mabadiliko ya sera kuhusu bahari ni muhimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 28, 2022 1:32


Mkutano wa pili wa kimataifa kuhusu bahari unaendelea huko Lisbon, Ureno. Mkutano huu umeanza tarehe 27 mwezi huu wa Juni na utamalizika tarehe 1 Julai 2022. Kabla ya kuanza kwa kikao cha ngazi ya juu, mkutano ulitanguliwa na jukwaa la vijana likileta pamoja wanaharakati na wachechemuzi vijana kuhusu masuala ya baharí wakionesha ubunifu wao wa jinsi ya kutatua dharura ya baharí, kama alivyooiita Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres .Miongoni mwa washiriki ni kijana Nancy Iraba mwanasayansi wa masuala ya bahari kutoka Chuo Kikuu cha Dare es salaam nchini Tanzania. Hapa akihoijwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa anaelezea jukwaa linajikita na nini.

Habari za UN
Sikufahamu kuhusu zao la mwani, sasa limenibadilishia maisha yangu- Marinda

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 27, 2022 3:37


Wakati mkutano wa dunia kuhusu bahari umeanza leo huko Lisbon nchini ureno kujadili namna ya kuhakikisha bahari inalindwa ili jamii zinufaike na uchumi utokanao na shughuli za kwenye bahari au uchumi wa buluu sambamba na faida nyingine nyingi, tunaelekea kijiji cha Kibuyuni, eneo la Shimoni, kaunti ya Kwale nchini Kenya kusikia jinsi maisha ya wakulima wa zao la mwani linalolimwa baharini yalivyobadilika baada ya mradi wa shamba la mfano la mwani ulioanzishwa na Taasisi ya Utafiti wa Majini na Uvuvi ya Kenya KMFRI kuleta manufaa kwa wanakijiji zaidi ya 2500 wa kijiji hicho. Kabla ya mradi huo maisha ya wanakijiji hao yalikuwa duni na jengo pekee lililokuwa limeezekwa mabati lilikuwa ni msikiti, lakini sasa wananchi hawa wana uhakika wakupata dola 300 kila baada ya siku 45. Ni kwa vipi basi, tuungane na Leah Mushi katika makala hii iliyofanikishwa na kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC nchini Kenya,

Habari za UN
IFAD yatatua mzozo wa maji baina ya wakulima na wafugaji nchini Sudan

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 31, 2022 2:34


Dunia hivi sasa imegubikwa na picha za mapigano huko Ukraine, lakini taifa hilo si sehemu pekee duniani inayokabiliwa na mizozo. Barani Afrika nchini Sudan, mapigano ya mara kwa mara ya kugombea maji na ardhi ya malisho kati ya wakulima na wafugaji yamekuwa yakisababisha majeruhi na wakati mwingine vifo, mabadiliko ya tabianchi yakizidisha hali mbaya zaidi.   Hata hivyo Umoja wa Mataifa kupitia mfuko wake wa maendeleo ya kilimo, IFAD na serikali wameweza kuketisha wakulima na wafugaji na angalau kuleta amani. Ni kwa vipi? Happinnes Pallangyo wa radio washirika Radio Uhai FM iliyoko Tabora nchini Tanzania anafafanua katika taarifa hii iliyofanikishwa na IFAD.  Taswira ya wanawake na watoto wakichota maji kutoka kwenye mabomba ya maji.   Pembeni nako kuna kisima cha maji kwa ajili ya mifugo.   Kulikoni katika taifa hili lenye mivutano itokanayo na uhaba wa maji na malisho?   Awdeeyer Abdullah Omer ambaye ni mfugaji anasimulia.  Anasema “zamani hali ilikuwa ni ngumu. Kabla ya ujenzi wa kituo hiki cha maji, tuliteka maji kutoka kisima kichafu. Wakati mwingine hakuna maji kabisa. Tulilazimika kutembeza punda wetu hadi mbali sana. Lakini sasa tunashukuru kuwepo kwa kituo hiki cha maji.”  Ujenzi wa kituo hiki ni miongoni mwa majawabu kutoka IFAD ili kuzuia mapigano ya wakulima na wafugaji.   Mabadiliko ya tabianchi yanakausha siyo tu maji na mimea bali eneo la malisho linasinyaa na wakulima wanashindwa pia kulima.  Nats.. Dkt. Mohammed Ahmed Hassan, Mtaalam wa IFAD anasema walifanya utafiti wa njia za wanyama ambako huko walijenga vituo vya maji ya kunywa kwa ajili ya wanyama.  Halikadhalika, IFAD na serikali ya Sudan pia walianzisha na kufadhili kituo cha utatuzi wa mizozo na ujenzi wa amani ambapo mizozo kati ya wakulima na wafugaji inapoibuka, basi hufika kituoni kwa ajili ya mashauriano.  Katika kipindi cha miaka 5 kituo kimoja huko Kordofan kimetatua zaidi ya mizozo mikubwa 35 ikiwemo katika eneo la Om Rowaba.  Meya wa mji huo Hassan Yaseem  El Hassan ambaye pia ni mshiriki kwenye kituo hicho anafafanua.  “Tunajaribu kuleta mafanikio kwa pande zote na kufanikisha makubaliano.”  Tangu mwaka 2018, mradi huu umewezesha ujenzi wa zaidi ya 190 vituo vya kuhifadhi maji vinavyosaidia zaidi ya kaya 78,000 kwenye eneo hilo la Sudan.  Wafugaji hawa wa kuhamahama penginepo watalazimika kuendelea kukabiliana na mabadilliko ya tabianchi, lakini suala la kugombea maji limesalia historia.

Sheria Poa Podcast
Mikataba ya wachumba kabla ya Ndoa (Prenups) - Tanzania

Sheria Poa Podcast

Play Episode Listen Later Aug 11, 2021 28:08


Mikataba ya wachumba kabla ya ndoa (Prenups) ni mikataba ambayo wanandoa watarajiwa huingia kuhusu mali walizochuma kabla ya kufungua ndoa husika. Aina hii ya mikataba lengo lake kuu huwa ni kuhakikisha mali ambazo wanandoa wamechuma kabla ya ndoa husika hazitokuwa mali za pamoja za wanandoa hao endapo ndoa hiyo itavunjika. Katika kipindi cha leo tupo na Wakili msomi Emmanuel Bakilana, ambaye anatufafanulia kuhusu mikataba hii, madhumuni yake, faida na hasara zake kwenye jamii yetu ya kitanzania na sisi kama jamii tunahitaji aina hii ya mikataba. Kwa maelezo zaidi kuhusu wazungumzaji; Privaty Rugambwa https://www.linkedin.com/in/privaty-patiensi-rugambwa-5078554a/ https://www.irglobal.com/advisor/privaty-patiensi-rugambwa/ Emmanuel Bakilana https://tz.linkedin.com/in/emmanuel-g-bakilana-846405123 Kwa maelezo zaidi juu ya Mikataba ya wanandoa kabla ya ndoa Kupakua Sheria The Law of Marriage Act [CAP 29 RE 2019] https://rita.go.tz/eng/laws/History%20Laws/Marriage%20Ordinance,%20(cap%2029).pdf Tovuti https://www.investopedia.com/terms/p/prenuptialagreement.asp https://www.graysons.co.uk/advice/prenuptial-agreements/ https://brittontime.com/2021/02/22/what-is-a-prenup-and-how-do-they-work/ --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/sheriapoa/message