POPULARITY
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa ikitupeleka nchini DRC, Sierra Leone na Ghana. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno "MISHEMISHE.”Leo ni Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani ambayo mwaka huu inajikita na maudhui ya “mustakabali wa ulinzi wa amani.”Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema walinda amani wa Umoja wa Matafa wako katika changamoto kubwa “Leo hii, walinda amani wanakabiliwa na hali zinazozidi kuwa ngumu katika dunia inayozidi kuwa na changamoto, ikiwemo uugawanyika na kutofautiana kwa mitazamo duniani kunazidi kuongezeka, operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa, hatari zaidi kutokana na wingi wa vitisho kama vile ugaidi na walinda amani kulengwa kwa makusudi kupitia taarifa potofu zenye madhara makubwa na changamoto zinazovuka mipaka kuanzia janga la mabadiliko ya tabianchi hadi uhalifu wa kimataifa.Kikosi cha 11 cha Tanzania kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeungana na walinda amani wengine kuadhimisha Siku ya Walinda Amani Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika Mavivi, yakiongozwa na Brigedia Jenerali Diamond Meshack Madie, Mnadhimu Mkuu wa Vikosi vya MONUSCO.Shirika la Umja wa Mataifa la Mazingira UNEP limezindua mpango mpya wa dola milioni 15 kusaidia uwekezaji endelevu katika Bonde la Kongo – moja ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia duniani. Mpango huu unalenga kufungua fursa za biashara rafiki kwa mazingira kwa wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta za kijani. Msitu wa mvua wa Bonde la Kongo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kaboni duniani na ni makazi ya watu zaidi ya milioni 75, wakiwemo jamii za asili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Katika makala haya, tutazungumza na watu muhimu kama vile mgonjwa wa UKIMWI, daktari, na mkunga anayeelimisha kuhusu jinsi ya kuzuia watoto kuambukizwa virusi vya UKIMWI wakati wanapozaliwa. Pamoja, tutafahamu changamoto, mafanikio na hatua zinazochukuliwa katika vita hivi.
Leo ikiwa ni siku ya watoto duniani ikirejelea tarehe 20 Novemba mwaka 1954 kwa mara ya kwanza kabisa ilipoanzishwa na Umoja wa Mataifa ili kusongesha umoja na kujitambua miongoni mwa watoto duniani. Kisha siku hii ikaongezwa nguvu na Azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Watoto duniani mwaka 1959 na hatimaye mwaka 1989 Baraza hilo lililopitisha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto, CRC. Mkataba unatambua haki kuu nne za msingi za mtoto: Kuishi, Kuendelezwa, Kulindwa na Kushirikishwa. Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limefanya maadhimisho ya kimataifa huko Copenhagen Denmark, na Madina Jubilate, Mchechemu wa UNICEF Tanzania kwa Tabianchi anaelezea alivyoshiriki.
Washiriki wa Sherehe za kimataifa za mwaka huu wa 2024 za kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Chakula zilizofanyika leo katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) jijini Roma Italia wamesisitiza haja ya upatikanaji wa vyakula mbalimbali vya kutosha, vyenye lishe, bei nafuu na salama.Ni maadhimisho ambayo yamewaleta wadau wa kilimo na chakula kutoka kote duniani lakini yanakuja huku kukiwa na mvutano na mizozo ya kimataifa na majanga ya tabianchi ambayo ni miongoni mwa mambo yanayochangia changamoto ya mamia ya mamilioni ya watu duniani kote kukabiliwa na njaa na mabilioni ya watu kushindwa kumudu chakula bora, FAO inaeleza katika taarifa iliyochapishwa katika ukurasa wake wa wavuti.Katika hotuba yake ya ufunguzi Mkurugenzi Mkuu wa FAO, QU Dongyu, amesema mifumo ya kilimo cha chakula inabidi "kusaidia wakulima wadogo, wakulima wa ngazi ya familia na wafanyabiashara wadogo katika mnyororo wa thamani ambao katika nchi nyingi ni wa msingi katika kufanya vyakula vyenye lishe, vya aina mbalimbali vipatikane kwa wote, na kuhifadhi tamaduni za jadi za chakula.” Ujumbe huo wa mkuu wa FAO unafanana na ujumbe wa Papa Francis ambaye amesisitiza wafanya uamuzi wa kisiasa na kiuchumi katika ngazi ya kimataifa lazima wasikilize matakwa ya wale walio chini kabisa katika mnyororo wa chakula.Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia video amesema, "kuna kitu hakiko sawa katika ulimwengu ambao njaa na utapiamlo ni ukweli wa maisha kwa mabilioni ya watoto, wanawake na wanaume." Akasema ulimwengu usio na njaa unawezekana, lakini "mifumo ya chakula inahitaji mabadiliko makubwa," ili kuwa na ufanisi zaidi, ujumuishi, mnepo na endelevu.Gérardine Mukeshimana, Makamu wa Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ametoa wito wa "uwekezaji wa haraka, wa pamoja na thabiti kwa wakulima maskini wa vijijini kutambua kwa ngazi ya chini kabisa haki yao ya msingi ya chakula chenye lishe." Akabainisha kuwa wakulima wadogo wanazalisha karibu nusu ya chakula cha dunia, ingawa pia wanakabiliwa na njaa na umaskini.Mfalme Letsie III wa Lesotho, ambaye ni Balozi Mwema Maalum wa FAO katika upande wa lishe anaeleza anavyoiunga mkono FAO kwa “kujaribu kuwa mtetezi mwaminifu na mwenye kujitolea katika masuala ya lishe, katika masuala ya uhakika wa chakula.” Anasema, “na mara kwa mara, mimi hutembelea sehemu nyingine za bara la Afrika nikivaa kofia yangu ya FAO, hasa kuhimiza serikali na viongozi kama bara kuwekeza zaidi katika masuala ya lishe na masuala ya uhakika wa chakula.”.
Makala wimbi la siasa inaangazia maadhimisho ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kundi la Hamas, litekeleze shambulio baya zaidi kuwahi kutekelezwa huko Israeli, tukio ambalo lilianzisha vita ambayo imesababisha vifo kwa maelfu ya raia wa Kipalestina na maandamano duniani kote kupinga vita hiyo, wakati huu mzozo huo ukihofiwa kuenea katika mashariki ya kati. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka na waalikwa wake
Jumamosi ulimwengu unaadhimisha Siku ya Walimu Duniani, tarehe iliyotengwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuwaenzi walimu kote duniani, na kuangazia changamoto wanazopitia na mafaniko wanayojivunia.
Karibu katika Makala Changu Chako Chako Changu jumapili ya leo ambapo nakulrtea Makala maalum kuhusu maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 14 tangu Ple RFI Kiswahili ilipoanza kupeperusha matangazo yake mubashara kutoka nchini Tanzania ambapo ilikuwa idhaa ya kwanza ya Kimataifa kutangaza ikiwa Afrika mashariki. Na kwenye Muziki nitakuletea Burudani ya Muziki wa Idd Aziz Kiswahili kitukuzwe wakati huu tukielekea kuadhimisha siku ya Kiswahili duniani. Mimi naitwa Ali Bilali, Bienvenue ama Karibu. Kumbuka pia kumfollow mtangazaji wako Ali Bilali kwa kubonyeza hapa @billy_bilali
Makala haya Ali Bilali anazungumzia kuhsu maadhimisho ya miaka 64 ya Uhuru wa DRC.
Karibu ungane nami Elizabeth Masanja katika kipindi cha Pro Life utetezi wa uhai, Wakufunzi wetu leo Wanazungumzia kuelekea kilele cha Maadhimisho ya miaka Thelathini ya Pro Life Tanzania. Inaongozwa na kauli mbiu: (Miaka Thelathini ya Utume wa uhai Tanzania, Tumedumu, tumestawisha, tumetikisa kuta za utamaduni wa kifo. L'articolo Je, wafahamu maadhisho ya Pro life Tanzania? proviene da Radio Maria.
Maadhimisho ya wiki yawakimbizi yalifanyika kote nchini Australia.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Karibu uungane na Mtangazaji Elizabeth Masanja katika kipindi cha Utume wa Walei, Mwezeshaji Damiani Ndimbo pamoja Varerian Mushi Wajumbe wa kamati ya Uinjilishaji Jimbo kuu la Dar es Salaam. Mada Jumuyia ndogondogo kuelekea maadhimisho miaka ya 50 tangua kuanzisha kwake . L'articolo Fahamu faida ya kuanzisha Jumuyia ndogondogo katika Kanisa na kuelekea Maadhimisho ya Miaka 50. proviene da Radio Maria.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Ungana na Padre Dkt.Clement Kihiyo, Mkuu wa Idara ya Litrujia Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) akituongoza kuangazia Litrujia katika kipindi cha Pasaka & Siku 50 za Maadhimisho ya Pasaka. L'articolo Ifahamu Liturujia katika kipindi cha Pasaka & Siku 50 za Maadhimisho ya Pasaka. proviene da Radio Maria.
Ni makala maalum, kuhusu kumbukumbu ya miaka 30 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994, tunahoji mchakato wa maridhiano umefikia wapi miaka 30 baadaye..... hali iko vipi kwa sasa. na dunia imepata somo gani? Pia kuhusu mauaji hayo, tutarejelea kauli ya Rais Emanuel Macron iliyoonekana kuwa inalenga kutuliza hisia za waathiriwa.Huko DRC uteuzi wa Judith Tuluka Suminwa, mwanamke wa kwanza kuwa waziri mkuu. Mahakama nchini Uganda ilitoa uamuzi wake kuhusu sheria dhidi ya ushoga. Kabla ya kwenda Kenya, Sudani..pamoja na Senegal ambako Bassirou DF aliapishwa kuwa rais mpya, tutakwenda Israeli na maeneo mengine duniani.
VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.
Kumbikizi ya miaka 30 tangu mauaji ya kimbari yaliyosababisha vifo vya watu hadi laki 8 ,kuna wito wa ulimwengu kuhakikisha watuhumiwa zaidi kusakwa na mataifa yaweke mikakati kuzuia mauaji kama haya kutojirudia Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch, sasa linataka jumuiya ya kimataifa kuongeza kasi ya kuwasaka watuhumiwa zaidi wa mauaji ya kimbari ya nchini Rwanda, ambapo mwishoni mwa juma hili, Kigali itafanya kumbukizi ya miaka 30.
Makala haya yameandaliwa na Florence Kiwuwa kwa ushirikiano na Ruben Lukumbuka.
Makala maalum ya changu chako chako changu inafanyika hapa Mombasa pwani ya Kenya katika luktadha wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya lugha ya kifaransa, inayofahamika Kama La Francophonie, ambapo Taasisi inayofundisha watu lugha hii na tamaduni za Ufaransa, Alliance Francaise ya Mombasa, imeandaa maadhimisho haya maalum kwa kuenzi namna ambavyo Francophonie inavyotia fora nchini DRC. Ungana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka moja kwa moja akiwa Alliance francaise ya Mombasa
Matangazo haya yanafuatilia habari zilizojitokeza nyakati za mchana na ambazo hazisikiki sana katika matangazo mengineyo. VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Maadhimisho ya Miaka 60 ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) katika Chuo cha Tumaini Makumira – Arusha leo tarehe 21 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Maadhimisho ya Miaka 60 ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) katika Chuo cha Tumaini Makumira – Arusha leo tarehe 21 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya sherehe za Nanenane jijini Mbeya tarehe 08 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya sherehe za Nanenane jijini Mbeya tarehe 08 Agosti, 2023.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Karibu kuwa nami jumapili hii katika Makala haya ya Changu chako Chako Changu ambapo Jumapili hii nakuletea sehemy atatu na ya mwisho ya makala kuhusu siku ya Kiswahili Duniani Julay 7 iliokwenda sanjari na maadhimisho ya miaka 13 ya rfi kiswahili ambapo Kundi la Less Wanyika liliburudisha. Mimi naitwa Ali Bilali Karibu ama bienvenue.
Karibu katika Makala changu Chako Chako Changu ambayo leo ni maalum kabisa kuhusu siku ya kimataifa ya lugha ya Kiswahili ambayo huadhimishwa kila ifikapo Julay 7 ambapo huu ni mwaka wa pili tangu kuanza kuadhimishwa kwa siku hii baada ya shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Sayansi Elimu na Utamaduni kuidhinisha siku hii ili kulinda tamaduni za waswahili siziji kupotea. Mimi naitwa Ali Bilali ambatana name mwanzo hadi Tamati.
Karibu katika Makala haya Changu Chako Chako Changu ambapo jumapili ya leo tunaendeleza sehemu ya pili ya Makala kuhusu maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani, Ali Bilali ndio langu jina Karibu.
MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA KUPAMBANA NA RUSHWA TAREHE 10 JULAI, 2O23- AICC ARUSHA
MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA KUPAMBANA NA RUSHWA TAREHE 10 JULAI, 2O23- AICC ARUSHA
Kila tarehe 7 ulimwengu huungana kuadhimisha siku ya kimataifa ya Kiswahili
Kila tarehe 7 ulimwengu huungana kuadhimisha siku ya kimataifa ya Kiswahili
Makala hii imeangazia hatua ya mahakama ya London Uingereza kuhusu waomba hifadhi kwamba ni kinyume cha sheria na kwamba Rwanda si salama huku Rwanda ikisema itakata rufaa wahamiaji walioko nchini humo. Maadhimisho ya miaka 63 ya uhuru wa DRC na mkutano wa Luanda Angola kuhusu amani ya mashariki ya Nchi hiyo, imeangazia pia yaliyojiri nchini Kenya, Uganda, Sudan an Ethiopia na kwengineko duniani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za kulevya Duniani tarehe 25 Juni, 2023 yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za kulevya Duniani tarehe 25 Juni, 2023 yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha
Maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani yatafanyika wiki ijayo Julai 7 na sasa maandali zi yanafanyika katika kila kona kuhakikisha siku hiyo iliyopewa uzito mkubwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO lakini pia inatumika kama jukwaa la kuziunganisha jamii sio za Afrika tu zinazozungumza Kiswahili ali na nyinginezo zinazokumbatia Kiswahili.Estelle Zadra Afisa Uhusiano wa ofisi ya UNESCO hapa New York. ameeleza kwamba kuna mambo mengi yatakayojiri siku hiyo, “Kuanzia hapa New York hadi Paris, Dar es salaam hadi Nairobi na katika miji mbalimbali ya Afrika tutakuwa na mijadala na matukio ya kitamaduni ili kuwafanya washiriki kuwa sehemu ya lugha hii iliyosheheni ya Kiswahili. Mbali ya matukio ya kijamii kama mazungumzo na mijadala tutakuwa na hafla mbalimbali za kitamaduni, kama dansi, muziki na hata chakula cha kitamaduni.”Hata hivyo nilitaka kufahamu nini maudhui ya mwaka huu na kwanini wameyachagua hayo Etelle hakutafuna maneno, “Kiswahili ni lugha ya umoja na mawasiliano kwa watu wengi sana barani Afrika na nje ya Afrika lakini tunataka kuonyesha kwa jinsi gani Kiswahili kilivyo na uwzekao mkubwa katika zama za kidijitali, hivi sasa jamii zetu zimeunganishwa sana na ni muhimu kila mtu kuwa na fursa ya nyenzo hizo na tunazihitaji kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na mijadala katika jamii zetu na kila mtu kushiri hivyo maudhui ya mwaka huu ni “Kuibua uwezo wa Kiswahili katika zama za kidijitali kwa sababu tunauhakika kwamba Kiswahili kinaweza kutumika kama daraja kuunganisha jamii mbalimbali na kuwezesha ujumuishwaji katika ulimwengu wa kidijitali.”Na ili kuhakikisha maudhui haya yanatimia Estelle amesema wanashirikiana kwa karibu n anchi zote za Afrika Mashariki na za Jumuiya ya maendeleo ya nchi za Kusini mwa afrika SADC ambazo pia zimekikumbatia Kiswahili lakini pia amesema lengo kuu ni kuwafikia vijana hususan wajasiriamali ambao wana hamu ya kutumia nyenzo za kidijitali kujiendeleza na lugha mujarabu kwao ni Kiswahili. Na mwisho Estelle akasema ujumbe wa UNESCO kwa dunia kuhusu siku hii ni kwamba, “Kiswahili sio lugha tu bali ni mkusanyiko mahiri wa urithi uliosheheni wa kitamaduni wa Afrika Mashariki na tunadhani kwa kukumbatia Kiswahili katika zama za kidijitali tunatoa fursa ya kubadilishana utamaduni, kuchagiza ukuaji wa uchumi na uwezeshaji wa kielimu. “ Siku ya lugha ya kiswahili duniani huadhimishwa kila mwaka tareje 7 Julai tangu ilipopitishwa rasmi na UNESCO miaka mwili iliyopita.
Hii leo jaridani tunaangazia lugha ya Kiswhaili na ripoti ya dawa za Kulevya ya UNODC 2023. Makala tunakupeleka nchini Pakistan na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Kuendelea kwa ongezeko la usambazaji haramu wa dawa za kulevya na mitandao ya usambazaji inayoendelea kukua inazidisha mizozo ya kimataifa na changamoto za huduma za afya na utekelezaji wa sheria, imesema Ripoti ya Dunia ya Dawa ya mwaka huu 2023 iliyozinduliwa leo na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC).Maadhimisho ya pili ya siku ya lugha ya Kiswahili duniani yatafanyika wiki ijayo Julai 7 na sasa maandali zi yanafanyika katika kila kona kuhakikisha siku hiyo iliyopewa uzito mkubwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO lakini pia inatumika kama jukwaa la kuziunganisha jamii sio za Afrika tu zinazozungumza Kiswahili ali na nyinginezo zinazokumbatia Kiswahili. Katika makala na leo ikiwa ni siku ya Siku ya Kimataifa ya Kupinga Matumizi Mabaya ya dawa Za Kulevya na Usafirishaji Haramu kauli mbiu ya mwaka huu inasema, “Watu kwanza: acha unyanyapaa na ubaguzi, imarisha kinga”. Tunaelekea nchini Pakistan kusikia kisa cha binti aliyedumbukia kwenye uraibu wa dawa za kulevya na kupoteza kila kitu.Mashinani tutaelekea Kalobeyei huko Kakuma nchini Kenya kusikiliza jinsi ambavyo wakimbizi wanavyoishi kwa utengamano na jamii za wenyeji nchini humo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa dhidi ya Ajira au Utumikishaji wa Watoto ambayo inakusudia kutumika kama kichocheo cha kuongeza harakati za kimataifa dhidi ya ajira au utumikishwaji kwa watoto na ikisisitiza uhusiano kati ya haki za kijamii na ajira kwa watoto, kama ilivyo kwa nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Mataifa, Tanzania nayo imeungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hii ambapo maadhimisho hayo yamefanyika Kitaifa katika kijiji cha Gua, Kata ya Gua katika Halmashauri ya Wilaya ya Songwe Mkoani Songwe. Kupitia siku hii muhimu kwa Watoto ulimwenguni kote, baadhi ya watoto kutoka Shule ya Msingi Gua wametoa maoni yao kuhusu umuhimu wa maadhimisho haya, miongoni mwao ni, Grace yeye ni muelimishaji jamii kuhusu utumikishwaji wa mtoto kwenye mashamba ya tumbaku, hapa anazungumzia hali ya utumikishwaji ilivyo kwa sasa, Kwa upande wake Innocent David Pesa amewashauri wazazi na walezi juu ya athari za utumikishwaji wa mtoto, Maadhimisho ya mwaka huu yanaenda Sambamba na kauli mbiu isemayo “Haki za Jamii kwa Wote, Tokomeza utumikishwaji wa Mtoto”
Maadhimisho haya yanafanyika wakati huu ripoti ya hivi punde ya shirika la mazingira la umoja wa mataifa UNEP ikipendekeza mabadiliko ya mifumo ili kuabiliana na chanzo cha uchafuzi wa plastiki.
Maadhimisho ya miaka 58 ya maandamano yaliyosababisha umwagikaji damu hapo mwaka wa 1965, katika siku iliyokuja kujulikana kama “Bloody Sunday” yalifanyika Jumapili katika mji wa Selma, Alabama, wakati ambapo Rais Joe Biden anakabiliwa na ukosoaji kutoka kwa wapiga kura.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Na Padre Leonard Maliva Paroko wa Parokia ya Isimani Jimbo la Iringa
Na Padre Paul Chiwangu Katibu Mtendaji wa Idara ya Litrurjia ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
Na Padre Dominic Mavula C.PP.S Mkurugenzi wa Matangazo Radio Maria Tanzania
Karibu kusikiliza jarida, Flora Nducha anakuletea yale yaliyojiri kutoka Umoja wa Mataifa ikiwemo;- 1. Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupinga umasikini ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema lazima hatua za dharura zichukuliwe, tena kwa kuzingatia watu na utu. 2. Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF nchini Uganda kwakushirikiana na serikali ya Japan wanaisaidia serikali ya Uganda kuimarisha mifumo ya afya ili watoto wote waweze kupata chanjo. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO nchini Tanzania wameadhimisha siku ya chakula duniani kwa kugawa maziwa kwa wanafunzi na kuhamasisha umuhimu wa lishe kwa wanafunzi. Na mwisho utamsikia mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakuka duniani WFP nchini Haiti akizungumzia hali mbaya inayowakumba wananchi wa nchi hiyo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Maadhimisho ya Miaka 10 ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) tarehe 09 Septemba, 2022
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Maadhimisho ya Miaka 10 ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) tarehe 09 Septemba, 2022
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Kizimkazi yaliyofanyika katika uwanja wa Dimbani, Kusini Unguja tarehe 05 Septemba, 2022
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Kizimkazi yaliyofanyika katika uwanja wa Dimbani, Kusini Unguja tarehe 05 Septemba, 2022
Taarifa kwa Umma Kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Ushirikiano wa Uchumi kati ya Tanzania na Jimbo la Zhejiang la nchini China. o la Zhejiang (CCPIT- Zhejiang Sub Council) Ndugu Chen Zongyao jijini Hangzhou. Zhejiang ni mojawapo ya Majimbo ya China yenye nguvu kubwa ya kiuchumi ikiwa na GDP ya Dola za Kimarekani Bilioni 849 na GDP per capital ya Dola za Kimarekani 14,907. Kutokana na utajiri wa Jimbo hilo, zipo fursa nyingi za biashara na uwekezaji.
Karibu msikilizaji kuwa nami Jumapili hii katika Makala haya ya Changu Chako Chako Changu, leo nakuletea Historia ya Kiswahili ambayo imeanza kuadhimishwa kwa mara ya kwanza mwaka huu Julay 7 kote duniani, nitakuletea pia ratiba ya shughuli za kitamaduni kutoka Centre culturel francais ya huko Kigali na kwenye Muziki nitakuletea sehemu ya Tamasha la mwanamuziki Lafouine alioifanya huko Kigali nchini Rwanda Juma lililopita. Mimi naitwa Ali Bilali Bienvenue.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa Maadhimisho ya Miaka 25 (Silver Jubilee) ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa Maadhimisho ya Miaka 25 (Silver Jubilee) ya Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC).
Maadhimisho hayo yaliongozwa na rais Uhuru Kenyatta na kuhudhuriwa na takriban watu 30,000 kwenye bustani ya Uhuru wakiwemo viongozi wa ngazi za juu, bila kuwepo kwa naibu rais William Ruto ambaye ofisi yake ilisema hakualikwa.
Maadhimisho ya miaka themanini ya shambulizi la Darwin yalifanyika jana, katika ibada maalum katika wilaya ya Kaskazini.
Maadhimisho ya #SikuYaAfyaYaAkiliDuniani: Uzoefu wangu binafsi na nyenzo zilizonisaidia Get full access to Barua Ya Chahali at www.baruayachahali.com/subscribe
Maadhimisho ya #SikuYaAfyaYaAkiliDuniani: Uzoefu wangu binafsi na nyenzo zilizonisaidia