POPULARITY
Hii leo jaridani tunaangazia makumbusho ya mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, na Siku ya Afya Duniani. Makala inamulika nafasi ya michezo katika kusongesha amani na maendeleo, na mashinani tunakwenda nchini Kenya, kulikoni?Dunia inapokumbuka miaka 31 tangu mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametuma ujumbe mzito wa maombolezo na onyo, akitaka mshikamano wa kimataifa kupambana na ongezeko la chuki, mgawanyiko, na misimamo mikali kupitia mifumo ya kidijitali.Leo ni Siku ya Afya Duniani ambayo mwaka huu inangazia suala muhimu kwa afya ya dunia, changamoto maalum wanazokumbana nazo wanawake na wasichana lakini pia vifo vya watoto wachanga, na ili kuhakikisha changamoto hizo zinashughulikiwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO limezindua kampeni ya mwaka mzima ya “Mwanzo wenye afya ni mustakbali wenye matumaini”..Makala inamulika nafasi ya michezo katika kusongesha amani na maendeleo, ambapo Assumpta Massoi amezungumza na Rosemary Mwaipopo, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kiraia la DaySpring Foundation nchini Tanzania. Yeye alikuwa ni miongoni mwa washiriki wa Mkutano wa 69 wa Hali ya Wanawake duniani, CSW69 uliofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa mwezi uliopita wa Machi.Na mashinanileo ikiwa leo ni siku ya afya duniani, kupitia mahojiano yaliyofanikishwa na washirika wetu Radio Domus, fursa ni yake Padri Thaddeus Mukaya wa kanisa la katoliki la Parokia ya Embulbul ambalo pamoja na wadau wengine waliandaa huduma za bure za matibabu kwa wenyeji wa eneo hilo ili kusaidia jamii ambazo haziwezi kujimudu kimaisha.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Siku ya kimataifa ya Michezo kwa ajili ya Maendeleo na Amani imeadhimishwa tarehe 6 mwezi huu wa Aprili maudhui yakiwa Ujumuishaji wa kijamii, hususan makundi ya pembezoni. Umoja wa Mataifa kupitia wavuti wake unasema kuwa siku hii inatambuliwa kutokana na nafasi ya michezo katika kuleta mabadiliko chanya, kuondoa vikwazo na kuvuka mipaka. Na usuli wa maudhui ya mwaka huu ni kwamba fikra potofu kwenye jamii zimesababisha baadhi ya watu kutokana na jinsia yao, umri, au rangi wanashindwa kushiriki kwenye michezo ambayo kwa njia moja au nyingine hutokomeza umaskini kwa kuwezesha washiriki kujipatia kipato. Nchini Tanzania shirika la kiraia la Dayspring Foundation limetambua nafasi ya michezo na limeanza kuchukua hatua. Assumpta Massoi wa Idhaa hii amezungumza na Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Rosemary Mwaipopo ambaye anaanza kwa kuelezea ni kwa nini waliamua kujikita katika kusaka vipaji.
Jioni hii kwenye makala ya Jukwaa la Michezo tumeangazia Congo kufutiliwa kushiriki mashindano ya CHAN 2024, kufutwa kazi kwa kocha wa Rwanda Torsten Spittler, uwanja mpya wa Talanta jijini Nairobi unaendelea kupiga hatua kwenye ujenzi huku ligi ya Tanzania ikitajwa nafasi ya nne katika orodha ya ligi bora Afrika, Kenya yang'ara mashindano ya chipukizi ya tenisi, msururu wa raga ya dunia mkondo wa tatu, fainali za Australian Open na tetesi za uhamisho ulaya na Afrika.
Kipindi cha leo kimeangazia pakubwa droo ya mashindano ya CHAN 2024; adhari ya kuahirishwa kwa kipute na uchambuzi wa makundi. Pia tumetupia jicho raundi ya sita hatua ya makundi mechi za klabu bingwa Afrika, fainali ya mashindano mapya ya wasichana U17, Shujaa yataja kikosi chake cha mkondo wa Perth 7s, Kipchoge akilenga taji la tano la London Marathon, Tyson Fury astaafu ndondi kwa mara ya pili pamoja na mashindano ya tenisi ya Australian Open yakiingia hatua ya robo fainali. Kulingana na droo iliyofanyika Jumatano usiku katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Kenyatta (KICC) jijini Nairobi nchini Kenya, Harambee Stars imepangwa katika 'kundi la kifo' ambapo itamenyana na mabingwa mara mbili Morocco (2018 na 2020) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (2009 na 2016)."Tuko kwenye kundi la kifo," Mariga alikiri, akibainisha uimara wa wapinzani wao."Hizo ni timu kubwa na inamaanisha lazima tuweke juhudi zaidi katika maandalizi."“Wapinzani wetu ni wagumu, tutashiriki mashindano haya kwa mara ya kwanza lakini haijalishi. Tuna wachezaji wazuri ambao wanaweza kutoa changamoto,” alijibu Kenneth Muguna, mmoja wa wachezaji muhimu katika kikosi cha sasa cha Harambee Stars.Pia katika Kundi A kuna Zambia na Angola. Kenya itakuwa mwenyeji wa mashindano haya yanayofanyika kila baada ya miaka miwili kwa wachezaji wa nyumbani pamoja na Tanzania na Uganda.Wenyeji wenza Tanzania wako katika Kundi B ambapo watamenyana na Madagascar, Mauritania, Burkina Faso na Jamhuri ya Afrika ya Kati.“Tusichukulie kundi hili kama jepesi, sisi kama wenyeji lazima tujitayarishe vyema ili tupite awamu ya makundi na hata kushinda kombe, “ alisema rais wa shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) Wallace Karia.Uganda wataongoza Kundi C ambapo watamenyana na Niger na nchi mbili ambazo zitatinga hatua ya mwisho ya mchujo. Mabingwa watetezi Senegal wataanzisha tena uhasama na Nigeria katika kundi D, ambayo pia ina Sudan na Kongo.“Tumecheza dhidi ya Guinea na Niger mara kadhaa, tunajua wanavyocheza. Tumefuzu mara ya nane mashindano haya, na hatujawahi kuaga mashindano kwenye makundi,” alieleza kwa msisimko Moses Magogo, rais wa shirikisho la soka (FUFA) nchini Uganda. Michuano hiyo yenye timu 19 ambayo awali ilipangwa kufanyika Februari 1 hadi 28, iliahirishwa hadi Agosti mwaka huu. Wasaidizi wa droo hiyo walikuwa wachezaji wa zamani - McDonald Mariga wa Kenya, Mrisho Ngasa wa Tanzania na Hassan Wasswa wa Uganda huku mkurugenzi wa mashindano wa CAF, Samson Adamu akisimamia mchakato wa droo.Katika ujumbe wake wa video kabla ya droo hiyo, rais wa CAF Patrice Motsepe alitoa shukrani zake kwa marais William Ruto (Kenya), Samia Suluhu Hassan (Tanzania) na Yoweri Museveni (Uganda) kwa ushirikiano wao kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa mafanikio."Ukarabati wa viwanja, viwanja vya kufanyia mazoezi, miundombinu, hoteli na hospitali katika nchi hizo tatu unaonyesha maendeleo makubwa na motisha, iliyodhihirika wakati wa ziara yangu," ujumbe wake Motsepe ulibainisha."Lengo lilikuwa kuunganisha mataifa matatu ya Afrika Mashariki, pamoja na mengine kutoka sehemu mbalimbali za Afrika."Waziri wa Michezo nchini Kenya Salim Mvurya alipamba hafla hiyo pamoja na wenzake kutoka Uganda na Tanzania, Peter Ogwang na profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko.Droo KamiliKundi A: Kenya, Morocco, Angola, DR Kongo, ZambiaKundi B: Tanzania, Madagascar, Mauritania, Burkina Faso, Jamhuri ya Afrika ya KatiKundi C: Uganda, Niger, Guinea, Q2, Q1Kundi D: Senegal, Kongo, Sudan, Nigeria
Leo kwenye makala ya kwanza kabisa ya Jukwaa la Michezo mwaka 2025, tumeangazia raundi ya nne hatua ya makundi mechi za Ligi ya vilabu bingwa Afrika. Mwanariadha mkenya Beatrice Chebet avunja rekodi yake ya dunia huku raia wa Eritrea mwendesha baiskeli Biniam Girmay akishinda tuzo la Afrika wakati uo huo mashindano ya magari ya Dakar Rally na Kombe la Mapinduzi yaking'oa nanga. Lakini pia tutatupia jicho tetesi za uhamisho ulaya na michuano ya tenisi ya Brisbane Open inayoendelea.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Kila mmoja achukue hatua kuondokana na vikwazo vya ujumuishaji watu wenye ulemavu - GuterresUmoja wa Mataifa uko tayari kufanya kazi na Kamati ya Kimataifa ya Michezo ya Olimpiki ya Watu wenye Ulemavu (Paralympic) ili kufikia maono ya jamii shirikishi, jumuishi na endelevu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito michuano ya Paralympic iking'oa leo jijini Paris, Ufaransa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Bwana Guterres aliyeko ziarani nchini Timor Leste, barani Asia, ametuma ujumbe kwa Mkutano wa Kimataifa wa Ujumuishaji watu wenye Ulemavu unaofanyika katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris Ufaransa ambako michezo ya Olimpiki ya watu wenye ulemavu, Paralimpiki 2024 imeanza kutimua vumbi leo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaamini Michezo ya Olimpiki ya Watu wenye Ulemavu inahimiza kila mtu, kuanzia kwa serikali, mamlaka za mitaa na watoa uamuzi kila mahali, kuchukua hatua ili kuondokana na vikwazo vya ushirikishwaji kamili na wa maana wa watu wenye ulemavu na Umoja wa Mataifa unaahidi kushiriki kikamilifu kutimiza lengo hilo.Aidha katika mkutano huu wa ngazi za juu, UNESCO imeitumia nafasi hiyo kuzindua Kijitabu na mfululizo wa video za mafunzo kuhusu Usawa wa Ulemavu katika Vyombo vya Habari. Kitabu hicho cha mwongozo kina masomo yanayolenga kuwapa wataalamu wa vyombo vya habari maarifa na zana wanazohitaji ili kuhakikisha mashirika yao yanakuwa jumuishi kwa kuwazingatia watu wenye ulemavu.Moja ya vivutio vikubwa katika paralimpiki za mwaka huu zitakazofanyika hadi tarehe 8 ya mwezi ujao Septemba ni timu ya wakimbizi wanane waliopelekwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.
Hii leo jaridani tunamulika kupelekwa kwa chanjo dhidi ya polio huko Gaza; mkimbizi wa Burundi aliyerejea nyumbani kutoka Tanzania ainuliwa kiuchumi; makala ni mkimbizi wa Sudan aliyeko ugenini naye awezeshwa kijasiriamali na mashinani tunabisha hodi nchini Rwanda kumulika usawa wa kijinsia kwenye michezo.Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linapeleka Gaza huko Mashairki ya Kati dozi milioni 1.2 za chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio aina ya 2, wakati huu ambapo ugonjwa huo hatari umethibitishwa kuweko eneo hilo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.Kwa wakimbizi, kurejea nyumbani ni jambo moja na kuanza upya ni jambo lingine. Wengi wao hawana chaguo lingine isipokuwa kuanza maisha yao upya. Mkoani Makamba, nchini Burundi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) wanawawezesha waliorejea nyumbani kujijenga upya na kwa tija. Miongoni mwao ni Emelyne Kabura kama anavyosimulia Bosco CosmasKatika makala Evarist Mapesa anatuletea simulizi ya mkimbizi wa Sudan ambaye sasa anaishi Sudan Kusini. Baada ya kupitia madhila lukuki amewezeshwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na sasa anajishughulisha na ujasiriamali.Na sasa ni mashinani Christelle Umuhoza, Mkurugenzi wa Programu wa Rwanda katika shirika la Shooting Touch, kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO nchini humo, anaeleza umuhimu wa michezo katika kuondoa vikwazo vya kijinsia.
Tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya Olimpiki hapo jana raia wa St Lucia Julien Alfred akishindia taifa lake medali ya kwanza ya Olimpiki, Sudan Kusini yaaga mashindano ya basketboli kibingwa, uchambuzi wa wanariadha wa Afrika Mashariki wanaotarajiwa kushiriki nusu fainali na fainali kadhaa leo usiku na kesho, uchambuzi wa mechi za nusu fainali ya soka lakini pia kwenye mjadala tunazungumzia kashfa ya jinsia ya mabondia Angela Carini na Imane Khelif
Joshua Cheptegei ashinda medali ya dhahabu kwenye mbio za mita 10,000 huku Malkia Strikers ikibanduliwa mashindanoni. Morocco na Misri zafuzu nusu fainali huku waafrika kwenye uogeleaji wakifanya vibaya. Pia tutakufahamisha matokeo ya judo, basketboli, kuendesha basikeli na jedwali la medali ambapo Uchina inazidi kuongoza jedwali hilo
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Makala imeangazia hafla ya ufunguzi wa michezo ya Olimpiki ya Paris siku ya Ijumaa ya wiki hii, huku miundombinu ya treni za umeme ikishambuliwa, rais William Ruto atangaza baraza la mawaziri akiwajumuisha wanasiasa wanne wa upinzani, kesi dhidi ya kiongozi wa muungano wa waasi Corneille Nangaa jijini Kinshasa nchini DRC, Maandamano na kukamatwa kwa vijana kule Uganda, siasa za Afrika Magharibi, na Kaskazini,Joe Biden ajijiondoa katika ki nyang'anyiro cha uchauguzi huku Kamala Harris akiteuliwa kuwa mgombea wa chama cha Demokratic nchini Marekani.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.
Makala haya ni sehemu ya pili ya historia ya michuano ya mataifa bingwa barani Afrika CAN.
Karibu kuungana naye Ali Bilali katika Makala ya leo Changu chako chako changu, ambapo anakuletea historia ya kombe la mataifa ya afrika na atiba ya shughuli kutoka Alliance francaise za ukanda na kwenye muziki atakuletea historia fupi ya mwanamuziki rapa kutoka nchini Kenya King Kaka. Kumbuka pia kumfolow kwa instagram @billy_bilali
Miongoni mwa yale tuliyokuandalia ni pamoja na kuanza kwa mashindano ya La Francophonie nchini DRC, maandalizi kuelekea Olimpiki ya mwaka 2024? Uchambuzi wa mechi za Kombe la Dunia soka la kina dada droo ya klabu bingwa barani Afrika na michuano ya Kombe la Dunia mchezo wa netiboli.
“Tunajaribu kuleta michezo na nguvu zake katika mazingira magumu sana ya watu wasiojiweza. Mchezo ni mzuri kwa kuwapa watu matumaini ya siku zijazo.” Anasema Filippo Grandi, Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) akirejelea Timu ya mpira wa miguu ya wanawake wakimbizi wanaoishi nchini Australia baada ya kuokoa maisha yao yaliyokuwa hatarini nchini mwao Afghanistan. Anold Kayanda anasimulia zaidi.
Miongoni mwa tuliyokuandalia ni pamoja na ligi ya mpira wa vikapu barani Afrika kuanza leo nchini Rwanda, Yanga yatinga fainali ya kombe la shirikisho wakati Senegal watawazwa washindi wa kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 17, CAF yatangaza mfumo mpya wa kufuzu kombe la dunia mwaka 2026 na orodha ya mwisho ya wachezaji watakaowania tuzo la Marc-Vivien Foe yatangazwa na RFI/France 24.
Mwanzoni mwa mwezi huu wa April dunia iliadhimisha Siku ya Kimataifa ya michezo kwa maendeo na amani, nchini Sudan Kusini kwa siku mbili mfululizo maelfu ya wananchi walikusanyika kusherehekea tamasha la utamaduni la amani lililoandaliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni ya jimbo la Kaskazini la Bahr El Ghazal.Maelfu ya wananchi walikusanyika kwa ajili ya sherehe hizo katika mji wa Aweil, wakitazama na kushiriki kuimba na kucheza nyimbo na ngoma za kitamaduni. Leah Mushi anasimulia hali ilivyokuwa
Hii leo katika jarida tunamulika upatikanaji wa huduma za maji na za usafi, siku ya furaha, kongamano la kiswahili Zanzibar, Tanzania na changamoto za maji yatokanyo ziwa Kivu mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.Wakati viongozi wa dunia wakijiandaa kuhudhuria mkutano wa kihistoria wa maji wa Umoja wa Mataifa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF llimetoa wito wa uwekezaji wa haraka katika huduma za maji, usafi na usafi wa mazingira (WASH) zilizo na mnepo ili kuwalinda watoto. Leo ni siku ya furaha duniani ambapo Umoja wa Mataifa unasema ni siku ya kutabua umuhimu wa furaha kwa watu wote ulimwenguni kwani ni msingi wa lengo la ubinadamu na pia huchagiza ukuaji wa kiuchumiAnold Kayanda wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amezungumza na Fatma Hamad, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Michezo, Vijana na Michezo katika serikali ya mapinduzi Zanzibar kuhusu Kongamano la Idhaa za Kiswahili lililofanyika visiwani humo. Mashinani: Paschal, mtoto mwenye umri wa miaka 15 ambaye kila siku kabla ya kwenda shule anadamkia Ziwa Kivu jimboni Kivu Kaskazini nchini DR Congo kuokota taka ili kuhakikisha wanaoteka maji hawapati magonjwa.
Tangu shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni lilipoitangaza lugha ya Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha za kimataifa, taasisi mbalimbali zimeendelea kuhamasisha makundi mbalimbali kuitumia lugha hiyo katika masuala mbalimbali ya kijamii kama vile elimu kuhusu mabadiliko ya tabianchi, uchumi, ukatili wa kijinsia na kadhalika. Miongoni mwa makundi muhimu kufanikisha hayo ni waandishi wa habari ambao wana fursa kubwa ya ushawishi kwa jamii kama asemavyo Fatma Hamad,Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Michezo, Vijana na Utamaduni katika serikali ya mapinduzi, Zanzibar alipozungumza baada ya kukamilika kwa Kongamano la Idhaa za Kiswahili lililofanyika kwa siku mbili visiwani humo. Fatma Hamad anaanza kumweleza mwenzetu Anold Kayanda aliyehudhuria Kongamano hilo tathmini ya Kongamano lilivyokuwa.
Didier Deschamps ametangaza kuwa ataendelea kuwa kocha wa timu ya taifa ya soka ya Ufaransa hadi michuano ijayo ya kombe la dunia mwaka 2026. Tunajadili hili na mengine mengi katika Makala ya leo ya Jukwaa la Michezo.
Haya ni makala ya mwisho ya Jukwaa la Michezo kwa mwaka wa 2022. Tunakuletea kwa ufupi, matukio makubwa yaliyotokea viwanjani . Tunakutakia kila la heri katika mwaka mpya wa 2023.Asante kwa kuwa shabiki wetu.
Kwenye Makala ya leo Jumapili 18 12 2022 tunaangazia fainali ya kombe la dunia kati ya Ufaransa dhidi ya Argentina. Sikiliza hapa iwapo ulikosa kwenye radio
Timu ya taifa ya Morrocco imejikatia nafasi katika nusu fainali .Na kwenye makala yetu tumekuuliza Unadhani Morocco inaweza kushinda kombe la dunia? Hadi sasa ni timu ipi imekupendeza na mchezaji wako bora ni nani?Sikiliza Habari Rafiki .
Timu ya taifa ya Morrocco imejikatia nafasi katika nusu fainali .Na kwenye makala yetu tumekuuliza Unadhani Morocco inaweza kushinda kombe la dunia? Hadi sasa ni timu ipi imekupendeza na mchezaji wako bora ni nani?Sikiliza Habari Rafiki .
Makala ya Gurudumu la uchumi wiki hii, inaangazia maonesho ya teknolojia kwa wabunifu wa michezo ya Kidijiti "Video Games", yatakayofanyika mwishoni mwa juma hili, mtayarishaji amezungumza na Douglas Ogeto, CEO wa Ludiqueworks ya nchini Kenya pamoja na Ann Ndanu, mmoja ya waandaji wa maonesho ya NAICCON 2022.
Makala ya Gurudumu la uchumi wiki hii, inaangazia maonesho ya teknolojia kwa wabunifu wa michezo ya Kidijiti "Video Games", yatakayofanyika mwishoni mwa juma hili, mtayarishaji amezungumza na Douglas Ogeto, CEO wa Ludiqueworks ya nchini Kenya pamoja na Ann Ndanu, mmoja ya waandaji wa maonesho ya NAICCON 2022.
Kuna changamoto nyingi katika sekta ya michezo nchini Kenya. Waziri wa Michezo, Ababu Namwamba ana kibarua na mwamba mkubwa kurejesha Kenya katika hadhi nzuri kispoti.
Bingwa wa mbio za mita ya 100 Mkenya Ferdinard Omanyala, ndio bingwa wa michezo ya Jumuiya ya Madola. Tunaangazia michezo hayo na mengine mengi yanayotokea viwanjani.
Ni jumapili nyingine tunakutana tena katika Makala haya ya Changu Chako Chako Changu, nakuletea historia ya michezo ya Jumuiya ya madola inayofanyika huko Uingereza, na kwenye le Parler francophone nakuletea ratiba ya tamasha kupitia centre culturel francophone ya Kigali na kwenye Muziki nitakuletea mwanamuziki kutoka nchini Ufaransa wa miondoko ya RNB TayC. Mimi naitwa Ali Bilali Bienvenue.
Jumamosi hii kwenye Jukwaa la Michezo, tunakuletea mkusanyiko wa matukio yote yaliyotokea viwanjani barani Afrika na kwingineko duniani. Watangazaji wako ni George Ajowi na ¨Paul Nzioki.
Leo kwenye Jukwaa la Michezo, tunakuletea uchambuzi wa michuano ya soka kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika, michuano ya CECAFA kwa upande wa wanawake, mashindano ya mchezo wa Tennis, kuwania taji la French Open, miongoni mwa matukio mengine.
Michezo kwa Watoto
Jaridani na Flora Nducha-Kwenye habari kwa ufupi: Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Ulimwenguni, ILO, imebainisha kuwa mtu mmoja kati ya wanne hajisikii kuthaminiwa kazini, huku wale wanaohisi kujumuishwa wakkiwa ni wale walioko katika majukumu ya juu zaidi. Viwango vya juu vya usawa, utofauti na ushirikishwaji vinahusishwa na uvumbuzi mkubwa, tija na utendaji, uajiri na uhifadhi wa vipaji, na ustawi wa wafanyakazi lakini uchunguzi wa ripoti uligundua kuwa ni nusu tu ya waliohojiwa walisema kuwa utofauti na ushirikishwaji vilitambuliwa vya kutosha na kufadhiliwa katika utamaduni na mkakati wa maeneo yao ya kazi. “Ni theluthi moja tu ya makampuni yanayopima ushirikishwaji kwa sasa, ingawa kufanya hivyo ni muhimu kwa maendeleo.” Imeeleza taarifa ya ILO iliyotolewa hii leo mjini Geneva, Uswisi. ====================================================== Mwaka huu wa 2022, takriban watoto milioni 6.3 wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 katika nchi 6 za ukanda wa Sahel wataathirika na tatizo la uzito mdogo ikilinganishwa na urefu wao na hivyo kuweka maisha ya watoto wasiopungua 900,000 hatarini, linaonya kundi la wataalamu wa kufuatilia lishe katika nchi zilizoko Afrika Magharibi na Kati. Kundi hilo la wataalamu linaloundwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa kama vile UNICEF, WFP, WHO na wadau wengine kama Concern na Save the Children, linatoa wito kwa wafadhili na washirika wao kuongeza msaada wao haraka ili kukabiliana na mahitaji ya haraka ya lishe ya watoto walioathiriwa huku wakiimarisha hatua za kuzuia ili kukabiliana na sababu kuu za utapiamlo wa watoto katika eneo hilo. Idadi ya watoto chini ya umri wa miaka 5 wanaotarajiwa kukumbwa na utapiamlo duniani mwaka huu haijawahi kuwa kubwa kiasi hicho, ikionesha ongezeko la asilimia 27 ikilinganishwa na mwaka 2021 na asilimia 62 ikilinganishwa na mwaka 2018. ======================================================= Na ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Michezo kwa Maendeleo na Amani yenye kaulimbiu ‘Kupata Mustakabali Endelevu na Wenye Amani kwa Wote: Mchango wa Michezo, katika ujumbe wake kwa siku hii, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Amina Mohammed amesema, "Michezo ina uwezo wa kuoanisha shauku, nguvu na ari yetu kwenye jambo la pamoja. Na hapo ndipo matumaini yanaweza kusitawishwa, na uaminifu unaweza kurejeshwa. Ni katika umoja wetu, nia ya kutumia nguvu kubwa ya michezo kusaidia kujenga mustakabali bora na endelevu kwa wote." Siku ya Kimataifa ya Michezo kwa Maendeleo na Amani (IDSDP), ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 6 Aprili, inatoa fursa ya kutambua jukumu chanya la michezo na mazoezi ya viungo katika jamii na katika maisha ya watu kote ulimwenguni. Mada kwa kina na tutaelekea nchini Tanzania kusikilia simulizi ya mjasiriamali aliyeshinda nafasi ya tatu katika tuzo za wajasiriamali wadogo katika nchi kumi na tano ulimwenguni kwenye kutekeleza lengo namba moja la malengo ya maendeleo endelevu la kutokomeza umasikini. Pia tutapata mashinani
Michezo kwa Watoto
Mwaka wa 2022, kutakuwa na matukio mbalimbali ya michezo, ikiwemo kombe la dunia, mashindano ya soka kwa mataifa ya Afrika na mashindano ya riadha ya dunia.
Nchini Kenya, Wizara ya Michezo imevunja Shirikisho la soka nchini humo na rais wa Shirikisho hilo Nick Mwendwa kukamatwa kwa madai ya ufisadi. Tunachambua hili na mengine mengi yanayotokea viwanjani barani Afrika na kwingineko duniani.
Australia ni nchi yenye tamaduni ya michezo, na moja ya njia zakusisimua zakujumuika katika jamii ya Australia, nikupitia vilabu vya jamii vya michezo, ambavyo hutoa faida kubwa yaki afya na jamii kwa kila mtu anaye husika.
Leo tunaangazia umuhimu wa Michezo kwa Mwanafunzi kwa Afya ya mwili na akili. Kwenye kipindi hiki utawasikia baadhi ya wadau wakiwakilishaa makundi mbali mbali ya watoto, walezi, wazazi, na wataalamu nchini Tanzania wakiangazia umhimu wa michezo.
Mwanariadha wa Kenya, Agnes Tirop, aliyeuwawa azikwa leo nyumbani kwao katika kaunti ya Nandi nchini humo. Tutaangazia pia mzunguko wa pili wa mechi za kufuzu kwa fainali za kombe la mashirikisho pamoja na klabu bingwa kwa mataifa ya Afrika. Bila kusahau hatua za makundi kwenye kuwania ubingwa wa kombe la klabu bingwa barani Ulaya.
Mara kwa mara Umoja wa Mataifa umeendelea kusisitiza kuwa vipaji vikiwemo vya michezo vina mchango mkubwa katika kusaidia kuleta maendeleo na amani. Vijana wanapotambuliwa vipawa vyao wanapata shughuli rasmi za kufanya na hivyo kuinua vipato vyao, kuwaondoa katika mazingira hatarishi na faida nyingine za ujumla ambazo muunganiko wake unasaidia kuelekea katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Mwandishi wetu wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na Collince Onyango, muasisi wa mradi unajulikana kama ETCO au Empowering the Community, ambao lengo lake ni kutambua vipawa miongoni mwa vijana wasiokuwa na ajira mtaani Kibera mjini Nairobi na kisha kuwaunganisha na watu au mashirika yatakayowapa ajira.
Karibu kusikiliza jarida ambapo baada ya kusikiliza habari kwa ufupi utasikia mada kwa kuhusu chakula cha asili kutoka Kilimanjaro nchini Tanzania. Mwishoni mwa wiki dunia imeadhimisha siku ya chakula duniani ikibeba maudhui “Hatua zetu ndio mustakbali wetu” kwa ahadi ya kuimarisha mifumo ya chakula na kuhakikisha watu wote mahali popote walipo duniani wanapata lishe bora na mlo kamili. Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO nchini Tanzania limeenda mbali zaidi na kutumia maadhimisho hayo kuelimisha jamii za vijijini si tu kupata lishe bora lakini pia kuhakikisha vyakula vya asili vinaendelea kudumishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Wiki hii mataifa ya Afrika, yapo mbioni kusaka tiketi ya kufuzu kwenye kombe la dunia nchini Qatar mwaka 2022 katika mchezo wa soka. Tunachambua hili na mengine mengi.
Jumamosi hii kwenye Jukwaa la Michezo, miongoni mwa tuliyokuandalia ni pamoja droo ya michuano ya kwanza ya klabu bingwa barani Afrika katika mchezo wa soka kwa upande wa wanawake, michuano ya klabu bingwa barani Ulaya na mashindano ya riadha ya London Marathon mwaka 2021.
Miongoni mwa yale utakayoyasikia jioni hii ni pamoja na: -Msimu mpya wa ligi kuu ya soka waanza nchini Kenya. -Nchini Tanzania Yanga na Simba wanachuana katika mechi ya ngao ya jamii. -Rwanda kuwa mwenyeji wa mashindano ya dunia ya kukimbiza basikeli mwaka 2025. -Chelsea na Manchester United zafungwa katika mechi za ligi kuu zinazoendelea nchini Uingereza.
Nchini Afghanista shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na washirika wengine wa maendeleo wanatoa huduma za msaada wa kisaikolojia kwa watoto zinazohusisha michezo na uchoraji bila kusahau utoaji wa chanjo kwa watoto chini ya miaka 5. Taarifa ya Leah Mushi (Pause) Video ya UNICEF ikionesha watoto wakiwa nje wamezunguka duara huku watoto watatu wakiwa ndani ya duara wakishindana kuruka kamba, na wengine waliozunguka huku watu wazima wakiwapigia makofi. Video hiyo pia inaonesha wengine wakicheza mchezo wa kurushiana na kudaka puto. Hapa ni katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Shahrak -Sabz katika mji wa Herat ambapo vimetengenezwa vituo vinavyohamishika vya kusaidia watoto kisaikolojia kutokana na maswahibu ya migogoro waliyoishuhudia, hivyo vitu kama uchoraji, na kuzungumza na wataalamu wa kisaikolojia vinakuwa faraja kwa watoto hawa. Kwa wale ambao hawawezi kwenda kucheza kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kupata majeraha au ulemavu, kuna timu zaidi ya 4 za wataalamu ambao huwatembelea majumbani kutoa ushauri nasaha kwa watoto, na wazazi wao, na huko nako hutoa burudani na kuwafundisha. Nako katika Kituo cha Afya cha Bab-e-Bargh, kilichowezeshwa na UNICEF huduma za utoaji chanjo, lishe, na huduma nyingine baada ya kujifungua zinaendelea. Jumla ya watoto 120 hupatiwa huduma ya chanjo za kawaida kila siku. Huduma nyingine wapatiwazo ni kuchunguzwa utapiamlo na wenye utapiamlo mkali kutibiwa, pamoja na kutibu magonjwa ya watoto walio chini ya miaka 5. UNICEF wamejidhatiti kuhakikisha huduma za afya zinaendelea nchini Afghanistan kupitia vituo hivi vya afya vinavyo hama hama kutoka eneo moja kwenda eneo jingine, ili kuwafikia walengwa wengi zaidi, ambapo wengi hufatwa katika kambi za wakimbizi wa ndani.
Miongoni mwa matukio makubwa yanayotokea viwanjani, tunayachambèua jioni hii ni pamoja na :- -Michuano ya soka, hatua ya makundi kwa mataifa ya Afrika kufuzu kucheza michuano ya kombe la dunia mwaka 2022 nchini Qatar. -Michuano ya soka, kuwani taji la klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati, CECAFA kwa upande wa wanawake. -Hatua ya nusu fainali, kuwania taji la mchezo wa kikapu kwa mataifa ya Afrika, inayoendelea jijini Kigali nchini Rwanda.
Sikiliza Chambuzi mbalimbali nikiwepo pia "Mlimani Radio 106.5", nikifanya na wadau mbalimbali akiwemo muongozaji wa kipindi hicho ndg. Robert MIHAYO, Kila siku ya J3-Ijum. Saa 3:30 - 4:00 Asubuhi.... Siku hii Tulikua na Suzan Richard. --- Send in a voice message: https://anchor.fm/aucland-mudu/message
Leo kwenye Makala ya Jukwaa la Michezo tuliyokuandalia ni pamoja na -Mashindano ya kuwania taji la mchezo wa kikapu barani Afrika yanayoendelea nchini Rwanda. -Michuano ya soka kuwania taji la klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati kwa upande wa wanawake. -Droo ya michuano ya soka, klabu bingwa barani Afrika. -Christiano Ronaldo kurejea Manchester United -Mashindano ya Olimpiki kwa walemavu yanayoendelea jijini Tokyo nchini Japan
Sikiliza Chambuzi mbalimbali nikiwepo pia "Mlimani Radio 106.5", nikifanya na wadau mbalimbali akiwemo muongozaji wa kipindi hicho ndg. Robert MIHAYO, Kila siku ya J3-Ijum. Saa 3:30 - 4:00 Asubuhi. --- Send in a voice message: https://anchor.fm/aucland-mudu/message
Mashindano ya kimataifa ya Olimpiki ya watu wenye ulemavu yameanza rasmi hii leo mjini Tokyo Japani yakihusisha washiriki wa michezo mbalimbali kutoka kila pembe ya dunia wakiwemo wakimbizi. (TAATIFA YA FLORA NDUCHA) Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR mashindano hayo yanayojumuisha wanamichezo kutoka mataifa 160 kwenye michezo muhimu ya watu wenye ulemavu katika historia mwaka huu yana timu wa wakimbizi yenye washiriki sita wanaume watato na mwanamke mmoja wanaoshindana kwenye michezo mbalimbali ikiwemo kuogelea, kurusha tufe, mashindano ya boti na taekwondo. Huyo ni Parfait Hakizimana mkimbizi wa Burundi anayeishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Mahama nchini Rwanda mmoja wa wanamichezo hao 6 wenye ulemavu wa timu ya wakimbizi akisema siku alipojua kuwa anashiriki mashindano ya Olmpiki Tokyo alifurahi sana na kuona milango imeanza kufunguka. Safari ya Parfait haikuwa rahisi amepitia zahma kubwa, machafuko na vita vilivyomwachia kilema cha maisha baada ya kupugwa risasi mwaka 1996 akiwa na umri wa miaka 6 tu na kupooza kabisa mkono wake wa kushoto, siku ambayo pia mama yake mzazi aliuawa. Lakini kama wasemavyo wahenga yaliyopita si ndwele bali kuganga yajayo Parfai anaganga yajayo kupitia michezo ambayo inampa nguvu, matumaini na ujasiri mkubwa. “Michezo inatusaidia kuwa na ujasiri hata kama maisha ni magumu. Taekwondo ni maisha yangu, Napenda taekwondo kwani inanisaidia kusahau wakati mgumu nilioupitia katika maisha yangu.” Na kabla ya kuelekea Tokyo Parfait alipata fursa ya kuwaaga wanamichezo wenzake, kocha wake, ndugu jamaa na marafiki n ahata kupokea baraka toka kwa mkewe Irene “Kwangu ni furaha kubwa sana Mungu amzidishie na kumfungulia njia nzuri na ampatie nguvu ili afanikiwe tuje kusikia kuwa huko ameshinda” Kilichosalia sasa kwa Parfai ambaye pia amekuwa mwalimu wa taekwondo kwa wakimbizi wengine kambini Mahama ni kupeperusha vyema Tokyo bendera ya wakimbizi na kutimiza ndoto yake huku akitakiwa kila la heri na kushangiliwa na watu milioni 82 waliotawanywa kote duniani wakiwemo milioni 12 kati yao wanaoishi la ulemavu.
Mashindano ya riadha ya dunia kwa vijana wasiozidi miaka 20 yanaendelea kushika kasi jijini Nairobi nchini Kenya, droo ya michuano ya soka kuwania taji la mataifa ya Afrika AFCON 2021 ni baadhi ya matukio tunachojadili Jumamosi hii.
Kenya itakuwa mwenyeji wa mashindano ya riadha ya dunia kwa chipukizi wasiozidi miaka 20. Express FC ya Uganda ndio mabingwa wa taji la CECAFA katika mchezo wa soka.
Michezo ya Olimpiki iliyokuwa inaendelea jijini Tokyo nchini Japan kwa wiki mbili kati ya Julai 23 mpaka Agosti 08 2021, imemalizika jijini Tokyo nchini Japan. Jiji la Paris nchini Ufaransa sasa limepokea kijiti cha kuandaa michezo ijayo ya Olimpiki itakayofanyika mwaka 2024 nchini Ufaransa. Tunachambua kwa kina namna michezo hiyo ilivyokuwa huko Japan, baada ya kuahirishwa kwa mwaka mmoja kufuatia janga la Corona.
Sikiliza Chambuzi mbalimbali nikiwepo pia "Mlimani Radio 106.5", nikifanya na wadau mbalimbali akiwemo muongozaji wa kipindi hicho ndg. MIHAYO, Kila siku ya J3-Ijum. Saa 3:30 - 4:00 Asubuhi. --- Send in a voice message: https://anchor.fm/aucland-mudu/message
Bara la Afrika, limeanza vibaya kwenye Michezo ya Olimpiki inayoendelea jijini Tokyo nchini Japan. Tunachambua
Michezo ya Olimpiki, iliyocheleweshwa kwa mwaka mmoja kutokana na janga la Covid 19, imeanza rasmi huko jijini Tokyo nchini Japan. Tunajadili nafasi ya mataifa ya Afrika Mashariki na Kati.
Michezo iliyocheleweswa ya Olimpiki kutokana na janga la Covid 19 inafungua milango yake jijini Tokyo nchini Japan, nini thathmini yako na matarajio yako ?
Miongoni mwa yale tunayokuandalia ni pamoja na fainali ya klabu bingwa barani Afrika katika mchezo wa soka, maandalizi ya michezo ya Olimpiki na kumalizika kwa mashindano ya kukimbiza basikeli ya Tour de France.
Italia ndio mabingwa soka barani Ulaya. Mserbia Novak Djokovic ashinda taji la Wimbeledon katika mchezo wa Tennis nchini Uingereza. Tunaangazia hili na mengine mengi yanayotokea barani Afrika.
Michuano ya kuwania taji la soka barani Ulaya, yamefikia katika hatua ya nusu fainali. Michuano ya Tennis ya Wimbledon, kukimbiza baiskeli Tour de France, tunajadili haya na mengine mengi.
Mashindano ya dunia ya kukimbiza magari, Kenya Safari Rally, yaanendelea kupamba moto, tutakuletea pia ripoti kutoka Rwanda kuhusu bingwa wa soka nchini humo na michuano ya nusu fainali, kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika.
Miongoni mwa yale tuliyokuandalia Jumamosi hii kwenye Jukwaa la Michezo ni pamoja na , rais wa Shirikisho nchini DRC Constatine Omar ajiuzulu nchini Rwanda, ligi kuu ya soka yafika katika hatua ya mwondoano na michuano ya soka, kuwania taji la bara Ulaya inaendelea.
Michuano ya soka kuwania taji la bara Ulaya, imeanza kutifua vumbi. Mashindano ya kuwania taji la French Open katika mchezo wa Tennis, yanafika tamati jijini Paris. Tunajadili, haya na mengine mengi.
Miongoni mwa yale tunayajadili Jumamosi hii kwenye Jukwaa la Michezoni hatua ya Naomi Osaka kujiondoa kwenye michezo ya mwaka huu ya Tennis ya French Open, lakini pia maandalizi ya michezo ya Olimpiki yatakayofanyika kati ya Juni na Julai jijini Tokyo nchini Japan.
Michuano ya soka hatua ya robo fainali, mzunguko wa pili, kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika, ligi ya mchezo wa kikapu barani Afrika na kumalizika kwa michuano ya soka katika ligi mbalimbali barani Ulaya.
Michuano ya soka hatua ya robo fainali, mzunguko wa pili, kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika, ligi ya mchezo wa kikapu barani Afrika na kumalizika kwa michuano ya soka katika ligi mbalimbali barani Ulaya.
Michuano ya mchezo wa soka, hatua ya robo fainali, kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika zinachezwa katika mataifa mbalimbali barani Afrika. Tunajadili hili na matukio mengine yanatokea viwanjani wikiendi na wiki hii.
Miongoni mwa yale tunayokuletea kwenye Jukwaa la Michezo ni pamoja na kuahirishwa kwa mchezo wa ligi kuu ya soka nchini Tanzania miongoni mwa matukio mengine kama mashindano ya kukimbiza magari yaendayo kwa kasi Langalanga.
Miongoni mwa matukio makubwa yaliyotokea wiki hii viwanjani ni pamoja na fainali ya klabu bingwa barani Afrika katika mchezo wa wavu kwa upande wa wanawake lakini pia droo ya robo fainali kuwania taji la klabu bingwa na Shirikisho soka barani Afrika bila kusahau mashindano ya kukimbiza baiskeli ya Tour de Rwanda.
Leo kwenye Jukwaa la Michezo, tunaangazia matukio muhimu yaliyotokea viwanjani, ikiwemo mashindano ya kukimbiza magari Safari Rally nchini Kenya.
Michezo kwa Watoto
Michezo kwa Watoto
Bingwa mara mbili wa Michezo ya Olimpiki katika mbio za Mita 800 mwanadada Caster Semenya kutoka Afrika Kusini, anataka kufuzu katika Michezo ya mwaka huu nchini Japan kukimbia mbio za Mita 5,000. Dennis Onyango, kipa wa siku nyingi wa timu ya taifa ya soka ya Uganda, ametangaza kustaafu. Tunajadili haya na mengine mengi.
Mechi za soka hatua ya makundi kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika, zimekamilishwa katika viwanja mbalimbali barani Afrika. Tunachambua kwa kina.
Klabu ya Simba SC ya Tanzania, na Al Ahly ya Misri, zimefuzu katika hatua ya robof fainali kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika. Simba iliishinda AS Vita Club mabao 4-1 lakini Al Ahly ya Misri ilitoka sare ya mabao 2-2 na Al Al-Merrikh ya Sudan. Tunajadili hili na mengine mengi.
Music and Sports History | Free Audiobooks | Famous Speeches | Podcast by Henry Gindt
Thanks for listening to Henry Gindt's "Sports Legends" documentary series. On today's episode: Cristiano Ronaldo. Don't forget to subscribe to this podcast and you'll get all the other free podcast episodes of Sports Legends as they're released. If you subscribe, you can also come back to this podcast and listen to the rest of the episode when you have more time, as well as listen to the next episodes in this free podcast series. Cristiano Ronaldo career/ team history: Sporting CP (2002–2003) | Manchester United (2003–2009) | Real Madrid (2009–2018) | Juventus (2018 - present) | Listen to this FREE episode as well on your favorite podcast app, including: Google Podcasts (free episode): https://podcasts.google.com/feed/aHR0cHM6Ly9hbmNob3IuZm0vcy80ODQxYmIyNC9wb2RjYXN0L3Jzcw== Apple Podcasts (free episode): https://podcasts.apple.com/us/podcast/listen-learn-grow-share/id1550813532?mt=2&ls=1 Audible, Amazon Music (free episode): https://www.amazon.com/Listen-Learn-Podcast-Learning-GoCheezy-com/dp/B08JJTM9VV Spotify Podcasts (free episode): https://open.spotify.com/show/7oDExb9mvUYnHGlM3nFyHI Free YouTube Channel, YouTube Music: https://www.youtube.com/channel/UCtVLgC42ozVmfWVPtJfJLhw #ronaldo #cr #juventus #football #soccer #cristianoronaldo #realmadrid #lionelmessi #messi Languages and Subtitles supported: ASSISTIR (ou ESCUTAR) Documentário Esportivo Cristiano Ronaldo Gratuito MIRAR (o ESCUCHAR) el documental deportivo gratuito de Cristiano Ronaldo شاهد (أو استمع إلى) فيلم وثائقي رياضي مجاني كريستيانو رونالدو নিখরচায় ক্রিশ্চিয়ানো রোনালদো স্পোর্টস ডকুমেন্টারি দেখুন (বা তালিকাবদ্ধ করুন) 观看(或收听)免费的克里斯蒂亚诺·罗纳尔多体育纪录片 POGLEDAJTE (ili SLUŠAJTE) Besplatni dokumentarni film Cristiana Ronalda SLEDUJTE (nebo POSLOUCHEJTE) zdarma dokumentární film Cristiana Ronalda SE (eller LYT til) Gratis Cristiano Ronaldo Sportsdokumentar KATSO (tai KUUNTELE) ilmainen Cristiano Ronaldon urheiludokumentti REGARDER (ou ÉCOUTER) le documentaire sportif gratuit de Cristiano Ronaldo SEHEN (oder HÖREN) Kostenlose Cristiano Ronaldo Sportdokumentation ΠΑΡΑΚΟΛΟΥΘΗΣΤΕ (ή ΑΚΟΛΟΥΘΕΙΤΕ) Δωρεάν ντοκιμαντέρ Cristiano Ronaldo નિ Cશુલ્ક ક્રિસ્ટીઆનો રોનાલ્ડો રમતો દસ્તાવેજી જુઓ (અથવા સૂચિબદ્ધ કરો) צפה (או האזין) לסרט התיעודי הספורטיבי של כריסטיאנו רונאלדו בחינם देखो (या सूची) फ्री क्रिस्टियानो रोनाल्डो खेल वृत्तचित्र TONTON (atau DENGARKAN) Dokumenter Olahraga Cristiano Ronaldo Gratis GUARDA (o ASCOLTA) Documentario sportivo gratuito su Cristiano Ronaldo 無料のクリスティアーノロナウドスポーツドキュメンタリーを見る(または聞く) 무료 크리스티아누 호날두 스포츠 다큐멘터리 시청 (또는 듣기) TONTON (atau DAFTAR ke) Dokumentari Sukan Cristiano Ronaldo Percuma സ Crist ജന്യ ക്രിസ്റ്റ്യാനോ റൊണാൾഡോ സ്പോർട്സ് ഡോക്യുമെന്ററി കാണുക (അല്ലെങ്കിൽ കേൾക്കുക) विनामूल्य क्रिस्टियानो रोनाल्डो स्पोर्ट्स डॉक्यूमेंटरी (पहा किंवा सूचीबद्ध करा) SE (eller LYTT på) Gratis Cristiano Ronaldo sportsdokumentar ମାଗଣା କ୍ରିଷ୍ଟିଆନୋ ରୋନାଲଡୋ ସ୍ପୋର୍ଟସ୍ ଡକ୍ୟୁମେଣ୍ଟାରୀ ଦେଖନ୍ତୁ (କିମ୍ବା ଶୁଣନ୍ତୁ) | مستند ورزشی کریستیانو رونالدو را تماشا کنید (یا به آنها گوش دهید) OBEJRZYJ (lub SŁUCHAJ) Bezpłatny dokument sportowy Cristiano Ronaldo ਦੇਖੋ (ਜਾਂ ਸੂਚੀਬੱਧ) ਮੁਫਤ ਕ੍ਰਿਸਟਿਅਨੋ ਰੋਨਾਲਡੋ ਸਪੋਰਟਸ ਦਸਤਾਵੇਜ਼ੀ VEZI (sau ASCULTĂ) documentar gratuit despre sportul Cristiano Ronaldo СМОТРЕТЬ (или СЛУШАТЬ) бесплатный документальный фильм о спорте Криштиану Роналду ПОГЛЕДАЈТЕ (или СЛУШАЈТЕ) Бесплатни документарни филм о Кристијану Роналду TAZAMA (au SIKILIZA) Hati ya Michezo ya Cristiano Ronaldo ya Bure Titta på (eller lyssna på) gratis Cristiano Ronaldo sportdokumentär இலவச கிறிஸ்டியானோ ரொனால்டோ விளையாட்டு ஆவணப்படத்தைப் பாருங்கள் (அல்லது கேட்கவும்) ดู (หรือฟัง) สารคดีกีฬาฟรีของ Cristiano Ronaldo Ücretsiz Cristiano Ronaldo Spor Belgeseli'ni İZLEYİN (veya DİNLEYİN) ПЕРЕГЛЯНУТИ (або СЛУХАТИ) Безкоштовний спортивний документальний фільм про Кріштіану Роналду دیکھو مفت (یا فہرست میں) مفت کرسٹیانو رونالڈو کھیلوں کی دستاویزی فلم XEM (hoặc NGHE) Phim tài liệu thể thao Cristiano Ronaldo miễn phí --- Support this podcast: https://anchor.fm/henry-gindt/support
Timu za taifa za mchezo wa soka za Comoros na Gambia, zimefuzu katika michuano ya bara Afrika, AFCON itakayofanyika mwaka 2022 nchini Cameroon, lakini mataifa mengine kama DRC , Kenya, Tanzania, yakishindwa kufuzu. Tunajadili hili kwa kina.
Miongoni mwa matukio makubwa yaliyotokea viwanjani wiki hii, ni michuano ya soka ya klabu bingwa barani Afrika, na maandalizi ya michezo ya Olimpiki jijini Tokyo nchini Japan.
Patrice Motsepe, ndiye rais mpya wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF, anachukua nafasi ya Ahmed Ahmed, baada ya kuidhinishwa na wakuu wa vyama vya soka kutoka mataifa ya bara hilo. Wapenzi wa soka barani Afrika wana matarajio gani ? Tunajadili kwa kina.
Leo katika Makala ya Jukwaa la Michezo miongoni mwa matukio tunakuchambulia ni harakati za kumpata rais mpya wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF, fainali ya mchezo wa soka kwa vijana wasiozidi miaka 20 kati ya Uganda na Ghana nchini Mauritania, miongoni mwa masuala mengine.
Wiki hii, tunaangazia kwa kina kuhusu maandalizi ya uchaguzi wa rais wa Shirikisho la soka barani Afrika, fainali ya vijana kuwania taji la vijana wasiozidi miaka 20 nchini Mauritania, miongoni mwa matukio mengi yaliyotokea viwanjani wiki hii.
Karibu sana katika Jukwaa la Michezo, baada ya kutokuwepo kwa karibu mwaka mmoja, baada ya kuzuka kwa janga la Corona duniani na kuathiri shughuli za michezo. Tumekuandalia uchambuzi wa matukio yatakayofanyika mwaka 2021 licha ya kuendele kuwepo kwa janga la Corona.
Mwinyi zahera ametambulishwa rasmi kuwa kocha Mkuu wa klabu ya Gwambina FC ambayo imepanda daraja msimu wa 2019/20 na itashiriki ligi kuu Bara msimu wa 2020/21. Zahera aliwahi kuifundisha yanga ndani ya ligi msimu wa 2018/19 na alianza nayo msimu wa 2019/20 kabla ya kufungashiwa virago kwa kile kilichoelezwa kuwa aliboronga kwenye michuano ya kimataifa. Kocha huyo amesaini dili la miaka 5 na inaelezwa kuwa ataanza kusajili nyota wake ambao alifanya nao kazi ndani ya Yanga. Wanaotajwa kuibukia Gwambina ni pamoja na Mrisho Ngassa na Kelvin Yondani ambao kwa sasa ni wachezaji huru. Vilevile Waziri wa michezo Tanzania, Dkt Harison Mwakyembe ametangaza uamuzi wa serikali kuendelea kuruhusu idadi ya wachezaji 10 wa kigeni huku idadi ya wachezaji wanaotakiwa kucheza itaratibiwa chini ya baraza la Michezo la Taifa BMT. Amesema bado wizara kwa kushirikiana na BMT na wadau wa soka watakaa kikao kujadili aina ama viwango vya wachezaji wanaopaswa kusajiliwa na kuingia nchini. Amefafanua, "Angalau nchi zilizopo katika nafasi 50 kwa FIFA ndiyo tusajili huko hata kwa daraja la kwanza, ingawa bado hii si sheria ni maoni tuu,ni vyema pia aina ya wachezaji watakaosajiliwa kutoka nje wawe na weledi na uwezo mkubwa.
Karibui miaka mitatu tangu Ahmad Ahmad kuchaguliwa kuwa rais wa shirikisho la kandanda barani Afrika, CAF, shirikisho hilo linakabiliwa na mshororo wa tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya fedha. Tunajadili katika makala ya Jukwaa la Michezo. Ungana na Fredrick Nwaka akiwa na wachambuzi wa soka Juma Mudimi na Bonface Osano
Soka la bara la Afrika, limeendelea kushuhudia changamoto mbalimbali za waamuzi au marefarii, huku baadhi wakikosa maadili kwa kujihusisha na upangaji wa matokeo na kutofuata ipasavyo sheria 17 za mchezo huu unaopendwa duniani, kama ilivyoshuhudiwa nchini Tanzania na uongozi wa nchi hiyo kuchukua hatua.
Rais wa shirikisho la kandanda duniani Fifa Gian Infantino amependekeza fainali za mataifa ya Afrika kuchezw akila baada ya miaka minne badala ya miaka miwili ya sasa. Tunajadili kwa kina katika jukwaa la michezo. Ungana na Fredrick Nwaka akiwa na wachambuzi wa soka Mustapha Mtupa, Samwel John na Bonface Osano
Michuano ya klabu bingwa barani Afrika hatua ya makundi imeendelea kurindima ambapo klabu za TP Mazembe, Mamelody Sundowns, Zamalek ni miongoni mwa klabu zilizofuzu hatua ya robo fainali. Je msisimko wa michuano hiyo umepungua msimu huu? Fredrick Nwaka ameungana na wachambuzi wa soka Mohammed Simbaulanga na Aloyce Mchunga kutathimini kwa kina.