POPULARITY
Mradi wa "operesheni rejea shuleni" unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na wizara ya elimu ya Kenya, shirika liliso la kiserikali la Hapag Lloyd na wadau wengine kwa kuzipa fedha familia zisizojiweza kuendesha shughuli za kiuchumi, umerejesha mautumaini ya elimu kwa mamia ya watoto katika Kaunti ya Kwale Pwani ya Kenya ambao waliacha shule sababu ya umasikini. Flora Nducha na maelezo zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu nchini Ukraine na upatikanaji wa elimu nchini Kenya. Makala tunakupeleka nchini Sudan Kusini, na amashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Ukraine imehitimisha kwamba vikosi vya kijeshi vya Urusi vimetenda uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu, hasa mauaji, kupitia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (drones) yaliyoelekezwa dhidi ya raia.Mradi wa "operesheni rejea shuleni" unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na wizara ya elimu ya Kenya, shirika liliso la kiserikali la Hapag Lloyd na wadau wengine kwa kuzipa fedha familia zisizojiweza kuendesha shughuli za kiuchumi, umerejesha mautumaini ya elimu kwa mamia ya watoto katika Kaunti ya Kwale Pwani ya Kenya ambao waliacha shule sababu ya umasikini. Katika makala ikielekea siku ya walinda amani kesho Mei 29, tunamulika harakati za walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini SUdan Kusini za kulinda raia na mwenyeji wako katika makala hii iliyoandaliwa kupitia video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani Sudan Kusini, UNMISS ni Sharon Jebichii.Na katika mashinani huku machafuko yakiendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, wafanyakazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wako mashinani mjini Goma na maeneo mengine yaliyoathirika ili kutoa msaada muhimu, ikiwa ni pamoja na kufanikisha nia ya wakimbizi wanaorejea nchini mwao Rwanda. Raab na Ruusi ni baadhi yao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Kesho ikiwa ni siku ya nyuki duniani ikimulika umuhimu wa nyuki tunakupeleka nchini Kenya, katika kijiji cha Embulmbul, ambapo mradi wa ufugaji nyuki uliofanikishwa na Shirika la Marekani la Misaada ya maendeleo, USAID, kwa kushirikiana na Idara ya Misitu ya Kenya, KFS na wadau wengine, umeleta tija kwa wenyeji. Mmoja wa wanufaika hao ni mwanamazingira Christopher Mureithi ambaye ni kiongozi wa kikundi cha kufuga nyuki katika msitu wa Ololua ambao wamefanikiwa sio tu kuboresha uzalishaji wa asali, bali pia kuchangia katika uhifadhi wa bioanuwai na misitu. Katika makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii Bwana Mureithi anaanza kwa kueleza mafanikio yao.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na wadau wameleta neema kwa watoto wanaoishi na ulemavu katika Kaunti ya Kisumu Magharibi mwa Kenya baada ya kuwapa msaada wa vifaa ikiwemo viti mwendo na viungo bandia kupitia mradi wa ubunifu kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, msaada uliobadili maisha yao. Flora Nducha amefuatilia tabasamu la mama ambaye mwanye amenufaika na kiungo bandia ungana naye kwa tarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia mvutano unaoendelea barani Asia kati ya majirani wawili India na Pakistani, na msaada wa mguu bandia uliowezesha mtototo nchini Kenya kwenda shule. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakwenda katika ukanda wa Gaza.Huko barani Asia majirani wawili India na Pakistani wameendelea kuoneshana mvutano kati yao kwenye eneo la Jammu na Kashmiri tangu tarehe 22 mwezi uliopita wa Aprili baada ya shambulizi huko Pahalgam. Katibu Mkuu ametoa wito kwa mara nyingine tena.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na wadau wameleta neema kwa watoto wanaoishi na ulemavu katika Kaunti ya Kisumu Magharibi mwa Kenya baada ya kuwapa msaada wa vifaa ikiwemo viti mwendo na viungo bandia kupitia mradi wa ubunifu kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, msaada uliobadili maisha yao.Makala katika wiki ya chanjo duniani, iliyotamatishwa tarehe 30 wiki iliyopita, mtaa wa Butiama, ulioko Mtoni Kijichi katika wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania ulishuhudia wazazi na walezi wakijitokeza kuwapatia watoto wao chanjo muhimu za kuwalinda dhidi ya maradhi hatari. Miongoni mwao ni Hija Halfani ambaye alimpeleka mtoto wake mwenye umri wa siku 42 kupata chanjo yake ya kwanza.”Na mashinani mashinani, kama sehemu ya juhudi za kutoa nafasi ya kujieleza kisanii na kuwaunga mkono Wapalestina kihisia (emotional support), UNRWA imeandaa maonesho ya sanaa katika Shule ya Al-Rimal, ambayo sasa ni makazi ya wakimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, na watoto walipata fursa ya kuonesha kazi za sanaa zinazoakisi(reflect) madhila wanayopitia wakati wa vita kati ya Israeli na Hamas ambavyo bado vinaendelea. Malak Fayad, msichana mkimbizi kutoka Beit Hanoun ni mmoja wao akionesha sanaa yake.….Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Hii leo jaridani tuanaangazia masuala ya ufadhili wa huduma za afya, na kilimo cha cacao nchini Liberia. Makala inatupeleka nchini DRC na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Baada ya Serikali ya Marekani kutoa tangazo jipya sasa kwamba itaendelea kufadhili huduma zinazolenga vita dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na VVU na Ukimwi (UNAIDS) limeeleza kuupokea uamuzi huo kwa furaha na kuuita wa kuokoa maisha.Kilimo bora cha kakao huko Liberia kimemwondolea uchovu na kukosa kulala, mkazi wa kaunti ya Nimba, kaskazini mashariki mwa Liberia, baada ya mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD nchini humo kumwezesha sio tu kugeukia kilimo, bali pia kuajiri vijana wengine na hivyo kufanikisha lengo la Umoja wa Mataifa la kuondokana na umaskini.Makala inatupeleka kwenye msitu wa bonde la mto Congo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC wa pili kwa ukubwa duniani unaofyonza kiasi kikubwa cha hewa ukaa, ambako mradi wa Umoja wa Mataifa wa kulinda bayoanuwai na kupambana na umasikini UNREDD unaleta nuru kwa jamii na mazingira.Na mashinani fursa ni yake fursa ni yake Esther Wangoi Mbugua, Mama mfugaji nyuki kutoka Kaunti ya Kajiado nchini Kenya ambaye alizungumza na washirika wetu Redio Domus akieleza kuwa ameweza kujipatia kipato na kumudu mahitaji ya familia yake kupitia mradi wa ufugajji nyuki.Mwenyeji wako niAnold Kayanda karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia jitihada za kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Maburg nchini Rwanda, na juhudi za kuchunguza virusi vya VVU nchini Ghana. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini DRC, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limeipongeza serikali ya Rwanda kwa kufanikiwa kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Maburg. Hii leo Rwanda imetangaza mwisho wa mlipuko wa hivi karibuni wa ugonjwa huo baada ya kutokuwepo maambukizi mapya katika siku 42 na mgonjwa wa mwisho akiwa amepimwa mara mbili bila kukutwa na ugonjwa kama matakwa ya WHO yanavyotaka ili kutangaza kuisha kwa mlipuko wa magonjwa namna hii.Mwaka 2020 Ghana iliripoti kuwa na watu 350,000 wanaioshi na virusi vya Ukimwi na kati yao hao 31,000 walikuwa ni wajawazito. Jambo lililoshtua ni kwamba ni sehemu ndogo mno ya wajawazito hao ndio walipimwa kufahamu iwapo wana VVU au la. Jambo lililofanya serikali kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kuchukua hatua.Makala inatupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyokoko Kaunti ya Turkana Kaskazini Magharibi mwa Kenya kukukutanisha na mkimbizi kutoka Somalia anayetumia mpira wa kikapu anatumia mpira wa vikapu kuhamasisha jamii yake na kupinga mil ana desturi zisizofaa.Mashinani ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mpira wa Kikapu, fursa ni yake Danny Batachoka, mwanariadha wa Paralimpiki kutoka Goma nchini Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo, DRC ambaye kupitia video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO, anasema ana ndoto ya kuwa mmoja wa wachezaji wakubwa wa mpira wa vikapu katika kitengo chake.” Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Makala haya yanazungumzia hatua za wanawake na wasichana katika eneo la Opapo, Kaunti ya Migori nchini Kenya, kwa msaada wa mashirika yasiyo ya kiserikali na serikali ya kaunti, wameanzisha kiwanda cha kuchakata samaki, kuboresha biashara ya samaki, na kuongeza thamani kwa kutengeneza bidhaa kama soseji na baga,hivyo kuinua uchumi
Makala haya yanazungumzia hatua za wanawake na wasichana katika eneo la Opapo, Kaunti ya Migori nchini Kenya, kwa msaada wa mashirika yasiyo ya kiserikali na serikali ya kaunti, wameanzisha kiwanda cha kuchakata samaki, kuboresha biashara ya samaki, na kuongeza thamani kwa kutengeneza bidhaa kama soseji na baga,hivyo kuinua uchumi
Katika miji ya pwani ya Kenya, vita dhidi ya uraibu vimepata mwelekeo mpya wa kusisimua. Kupitia miradi ya kimazingira, vijana kutoka vituo vya kuwarekebisha tabia hawajizuia tu na mihadarati, bali wanabadili jamii zao pia kupitia miradi hiyo. Mwanahabari wetu Victor Moturi alitembelea Mtopanga, Kaunti ya Mombasa, ambako vijana wamepata matumaini kutokana na utunzaji wa mazingira huku wakipata riziki.
Hii leo jaridani tunaangazia mashauriano huko Busan kuhusu matumizi ya plastiki, na ripoti ya UNODC kuhusu UKIMWI na kudhibiti dawa za kulevya katika magereza. Makala inaturejesha Havana Cuba na mashinani inatupeleka nchini Kenya, kulikoni?Vuta nikuvute kwenye mashauriano huko Busan, Korea Kusini kuhusu mkataba wenye nguvu za kisheria dhidi ya uchafuzi utokanao na matumizi ya plastiki na kulinda mazingira ya baharini imefikia ukingoni kwa mkutano kuahirishwa na wawakilishi wa nchi zilizokuwa zinashiriki kuridhia rasimu mpya yenye ibara 32 itakayojadiliwa mwakani.Wakati jana Desemba Mosi Ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya UKIMWI kwa kuhamasisha haki za binadamu ili kufanikisha vita dhidi ya ugonjwa huu hatari, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inajivunia miaka 25 ya kujiunga na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) katika kushughulikia janga la Virusi Vya UKIMWI (VVU) miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kulevya na miaka 20 ya kazi ya kupambana na UKIMWI magerezani.Makala leo inamulika jinsi bidhaa za kitamaduni zinavyotumika kukuza na kuendeleza mila na desturi za Kiswahili mkoani Tanga Kaskazini mwa Tanzania. Je ni bidhaa zipi hizo na zinatumika vipi? Tuungane na Flora Nducha aliyeyabaini hayo hivi karibuni alipokuwa Havana Cuba kwenye kongamano la kimataifa la Kiswahili.Na mashinani tunasikiliza manufaa ya ufadhili wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD kwa wakulima kutoka kwake Sharon Kirui kutoka Kaunti ya Nakuru nchini Kenya ambaye ni mnufaika wa vocha za kielektroniki za ununuzi kutoka kwa IFAD na ameweza kupanua biashara yake ya kilimo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia machafuko katika ukanda wa Gaza na masuala ya afya nchini Kenya. Makala inatupeleka nchini DRC kumsikia mkimbizi mjasiriamali na mnufaika wa pesa taslimu kutoka WFP, na mashinani tunakupeleka nchini Lebanonon kwa waathirika wa vita.Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele, hali ya usalama na kibinadamu huko Ukanda wa Gaza inazidi kuzorota huku raia na hata wafanyakazi wa kutoa misaada wakisalia wamepigwa butwaa kwani mashambulizi kutoka Israeli yanaendelea kila uchao.Serikali ya Kaunti ya Lamu katika pwani ya kaskazini ya Kenya, kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), wanaendesha shughuli ya kuwafikia wanajamii ili kubadilishana taarifa kuhusu jinsi watu wanaweza kuwalinda watoto na familia zao dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu na kutoa huduma za maji, vifaa vya kujisafi na usafi kwa jamii zilizoathirika. Kutoka katika video iliyoandaliwa na UNICEF.Makala George Musubao, mwandishi wetu wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC anazungumza na mkimbizi Esther Josephine aliyeko kambi ya Bulengo nje kidogo ya mji wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini ambaye amenufaika na msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP.Mashinani tutakuwa Lebanon, kumsikia mama aliyenusurika kifo na wanawe kutokana na makombora ya Israel.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Serikali ya Kaunti ya Lamu katika pwani ya kaskazini ya Kenya, kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), wanaendesha shughuli ya kuwafikia wanajamii ili kubadilishana taarifa kuhusu jinsi watu wanaweza kuwalinda watoto na familia zao dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu na kutoa huduma za maji, vifaa vya kujisafi na usafi kwa jamii zilizoathirika. Kutoka katika video iliyoandaliwa na UNICEF.Wamekaa chini ya mti, wanawake kwa wanaume. Nyuma ni nyumba ya makuti na matumbawe, Lamu, Pwani ya Kenya. Muelimishaji wa masuala ya afya anawaeleza namna ya kuweka mazingira safi ili kupambana na kipindupindu. Mwanajuma Kahidi yamewahi kumkuta. Anaposema Cholera anamaanisha hiyo hiyo kipindupindu iliyokuwa imetishia Uhai wake na familia yake.“Nilipopata maambukizi ya Kipindupindu nilihisi siko sawa kwa sababu nilikosa nguvu na nikakosa raha na nikapoteza nuru ya macho ndio nikakimbilia hospitali. Huo ugonjwa ulipitia kwenye maji na chakula. Mimi na watoto wangu tulipatwa na kipindupindu. Mimi nilichukua siku tatu. Watoto wangu wote mmoja baada ya mwingine walichukua siku nane nane. Madaktari wanajibidiisha sana juu yetu. Baada ya siku kadhaa wanajitokeza na kutuuliza, je mnafanya juhudi tulizowaambia?”Leila Abrar ni Mshauri katika UNICEF anayehusika na mabadiliko ya tabia katika jamii anasema, "kiwango cha ufahamu ni cha juu zaidi kuliko tulipokuwa tunaanza uelimishaji. Na pia tunaambiwa kuwa kiwango cha unawaji mikono kimeongezeka. Mabadiliko ya kijamii na tabia kwa kweli yanahusu kushirikisha jamii, kuwezesha jamii.
Hii leo jaridani tunaangazia janga la nja linalokumba wananchi waathirika wa mizozo nchini Sudan, na simulizi za walinda amani wa UNIFIL nchini Lebanon. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Haiti, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, (WFP) leo kwa mara nyingine tena limetahadharisha kwamba bila msaada wa kibinadamu nchini Sudan, mamia ya maelfu wanaweza kufa kwa njaa.Kikosi cha muda cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon, UNIFIL, ambapo, katikati ya mvutano unaoongezeka kati ya Lebanon na Israel, walinda amani walioko katika makao makuu ya UNIFIL huko Naqoura wamekuwa wakivumilia mazingira magumu. Ushuhuda wa hivi karibuni kutoka kwa walinda amani hao unaonesha ukubwa wa changamoto wanazokabiliana nazo, ikiwemo vitisho vilivyoongezeka kutoka kwa shughuli za kijeshi za Israel zilizo karibu na eneo hilo, vizuizi vya kusafiri, na changamoto za uendeshaji wa shughuli.Makala inatupeleka Nairobi Kenya kwa washindi waliotwaa tuzo ya “Mtu Bora wa Mwaka wa Umoja wa Mataifa 2024” ambao ni kampuni ya Craftskills Wind Energy International Limited wamiliki wa mradi wa nishati ya upepo ya Kipeto Energy iliyoko Kaunti ya Kajiado nchini Kenya.Katika mashinani mashinani leo tutakuwa Haiti ambapo nafasi ni yake Andre Rose, mama wa kijana Kerby, akieleza jinsi msaada wa kifedha unaotolewa na Shirika la UNICEF umekuwa mkombozi kwa familia yake iliyolazimika kukimbia makazi yao kutokana na ghasia za magenge ya uhalifu nchini Haiti.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Kampuni ya Craftskills Wind Energy International Limited wamiliki wa mradi wa nishati ya umeme itokanayo na upepo ya Kipeto Energy iliyoko Kaunti ya Kajiado nchini Kenya wamejitwalia tuzo ya “Mtu Bora wa Mwaka wa Umoja wa Mataifa. 2024”Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo anasema ushindi huo ni kwa watu wa Kaunti ya Kajiado nchini Kenya ambao ni wanaufaika wakubwa wa mradi kwani sio tu umewaletea umeme, bali pia umewainua kiuchumi na kijamii kwa miradi mingine mbalimbali kama inabobainisha makala hii iliyoandaliwa na Flora Nducha..
Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa COP16 katika mji wa Santiago de Cali au Cali huko nchini Colombia na ufugaji nyuki Turakana nchini Kenya. Pia tunakupeleka nchini Somalia kufutilia programu wa WFP wa mlo shuleni na mashinani inatupeleka nchini Lebanon.Mkutano wa 16 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa bayonuai (COP16) umeng'oa nanga leo katika mji wa Santiago de Cali au Cali huko nchini Colombia ambapo mataifa 196 yatajadili jinsi ya kusitisha na kubadili mwelekeo wa kudorora kwa ulimwengu wa asili.Kila siku, mamilioni ya watoto kote ulimwenguni huenda shule wakiwa na njaa, wengi wao wakiteseka na utapiamlo sugu ambao huathiri ukuaji wa kiakili na utendaji wao katika masomo. Wanaobahatika huweza tu kumaliza masomo yao na kufanikiwa maishani kutokana na programu ya ‘mlo ya shuleni' inayoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula Duniani (WFP). Mfano wa wanufaika hao ni El-Khidir Daloum, Mkurugenzi wa sasa wa WFP nchini Somalia.Makala inatupeleka Kaunti ya Turkana Kaskazini mwa Kenya moja ya maeneo kame ambako mradi wa ufugaji nyuki wa WFP umekuwa mkombozi kwa wakulima walioathirika na mabadiliko ya tabianchi.Mashinani fursa ni yake Waffiyah Diyah kutoka Lebanon ambaye ni muathirika wa vita vilivyolazimisha maelfu ya watu kufangasha viragoanaelezea hali ya familia yake baada ya kukimbia mashambulizi na kupoteza kila kitu, lakini sasa anapokea msaada kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM).Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Kaunti ya Turkana Kaskazini mwa Kenya moja ya maeneo kame mradi wa ufugaji nyuki wa WFP umekuwa mkombozi kwa wakulima walioathirika na mabadiliko ya tabianchi.Katika kaunti hii vumbi linalotimuka katika eneo tambarare lisilo na miti linakufanya kujiuliza je Nini kizuri kinaweza kufanyika hapa kwenye ukame uliotamalaki? Lakini cha kustaajabisha ni kwamba kwa kuwezeshwa mengi yanawezekana ikiwemo njia bora za kuhakikisha uhakika wa chakula na hata kubadili maisha ya watu kama anavyosema mkulima wa nyuki Nadipo Lotelei mnufaika wa mradi wa mizinga ya nyuki kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP. “Hatua iliyochukuliwa na WFP kutupatia mizinga ya nyuki imekuja kama nyota ya jaha kwangu kwa sababu siwezi kutembea umbali mrefu kutokana na ajali niliyopata. Mradi huu umenisaidia sana mimi ili kuweza kusaidia watoto wangu na mke wangu. Mke wangu ameweza kuanzisha biashara ya duka kutokana na faida niliyopata ambayo sasa inatumika kama chnzo cha kipato cha mahitaji ya kaya yetu.”Nadipo ni miongoni mwa wafuga nyuki 1,900 katika kaunti ya Turkana ambao wamepewa mafunzo ya ufugaji nyuki na vifaa kupitia mradi wa WFP kwa ushirikiano na shirika binafsi la HIVE ambalo mwenyekiti mtendaji wake ni Christopher Nzuki. “Tunahusika katika ufungaji na usambazaji wa vifaa. Na wakati huohuo tunatoa mafunzo kwa wafugaji nyuki na kisha kuwapatia masoko. Tunachukua kila kitu wanachozalisha.”Ufugaji wa nyuki wa kisasa si kazi kubwa, na pia unatumia nafasi ndogo na maji kidogo. Nyuki huchavusha asilimia 80 ya miti ya maua ikiwemo mazao ya chakula. Huzalisha asali, nta, mafuta na sumu, bidhaa ambazo huuzwa kwa gharama kubwa sokoni. Kwa sasa WFP inasaidia karibu wafugaji wa nyuki 5,000 katika kaunti 9 nchini Kenya lakini lengo ni kuwafikia wengi zaidi na mradi huu kama anavyosema afisa wa WFP Timothy Koskei. “Dhamira yetu mwisho wa yote ni kuwafikia wastani wa wafuga nyuki 10,000 katika kaunti 9 na kuvuna takriban tani 600 za asali.” Kwa mujibu wa WFP nyuki wana uwezo mkubwa na wanaweza kutoa mavuno mengi ambayo ni neema kwa familia sisizojiweza katika maeneo haya kame. Mkurugenzi wa WFP nchini Kenya Lauren Landis anasema mradi umezaa matunda. “Hivi sasa tunasikia kutoka miongoni mwa wanaufaika ambao awali walikuwa wakipokea msaada wa chakula ,ambao sasa sio tu wanazalisha asali kwa ajili ya faida bali pia wanafikiria kuongeza ununuzi wa pembejeo zaidi kutoka kwa Hive. Hivyo tunachokishuhudia ni mchakato ulio wazi ambapo mtu anatoka kuwa mpokea msaada na kuwa mteja, kuwa mpokeaji wa faida na si mpokeaji wa msaada wa chakula.”Kwa mafanikio haya WFP inasema itaendelea kupanua wigo wa mradi huu ili kunufaisha familia nyingi zaidi.
Maelfu ya watoto katika Kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya kwa miaka mitatu iliyopita wamelazimika kuacha shule kutokana na umasikini na ukame na mafuriko yaliyochangiwa na mabadiliko ya tabianchi. Lakini sasa wizara ya elimu ya Kenya kwa kushirikiana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, wakfu wa Education Above all na wadau wengine juhudi zinafanyika kuwarejesha watoto shuleni. “Niliacha shule darasa la nne ilikuwa mwaka 2022, kwasababu shuleni walikuwa wananirejesha nyumbani nikalete ada. Sasa nikifika nyumbani wazazi wanasema hawana”Huyo ni David Tumaini kijana mwenye umri wa miaka hivi sasa 16 mmoja wa wanafunzi waliolazimiika kukatiza masomo miaka miwili iliyopita katika shule ya msingi ya Soyosoyo kutokana na umasikini. Kwa miezi kadhaa alihaha kusaka njia ya kuendelea na masomo."Nilikaa nyumbani kwa muda wa miezi mitano, wakati wenzangu wanakwenda shule na ni siku za masomo na wewe uko nyumbani. Hii inakufanya ujihisi kama wewe si mtu muhimu.”Hisia kama hizo na mustakbali wa watoto hao ndio kilicholisukuma shirika la UNICEF kuanzisha mradi wa “Elimisha mtoto” likishirikisha wizara ya elimu ya kenya na wadau wengine ili kuhakikisha watoto kama David wanarejea shuleni. Elizabeth Waitha ni afisa elimu wa UNICEF.“Tuliweza kubaini Kaunti 16 ambazo zilikuwa na watoto zaidi ya 10,000 ambao wanaendi shuleni, na hii ilikuwa ni kwa shule za msingi tu. Na tukaangalia ni jinsi gani ya kuhakikisha mazingira bora ya kusoma kwa watoto waliosajiliwa kwenye mradi. Na tumeweza kuwasaidia zaidi ya wanafunzi milioni kwa vifaa vya shule na pia kwa waalimu vifaa vya kuandikia kama chaki, kalamu na vingine.”Na ndipo David akasikia kuhusu mradi huo,“Nilipata taarifa kutoka kwa walimu ya kwamba kuna mradi ambao unawasaidia watoto walioacha shule ili warehjee shuleni kuendelea na masomo. Sasa nilipokuja shuleni nikaambiwa wewe tutakusajili katika huu mradi wa msaada , ndipo nikaweza kurejea masomoni, hadi sasa nipo shuleni kwa sababu ya msaada huu. Vitu ambavyo nilipewa ni pamoja na mkoba wa madaftari, vitabu, kalamu na vifutio.”Hii imemrejeshea David matumaini ya ndoto yake“Mimi nikimaliza kusoma nataka kuwa Daktari ili kusaidia wagonjwa. Na katika kusaidia wagonjwa mshahara nitakaolipwa ntajisaidia mwenyewe na pia kusaidia familia yangu”Kupitia mradi huu mbali ya vifaa umewezesha zaidi ya watoto 256,000 kurejea shuleni na bado wanaendelea na masomo.
Hii leo jaridani tunaangazia amani na usalama nchini DRC, na suala la elimu katika malengo ya maendeleo endelevu tukimulika wanafunzi Kilifi nchini Kenya. Makala tunasalia na mada hiyo hiyo ya elimu na mashiani inamulika sheria za kibnadamu.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo wameelezwa jinsi ushindani wa uchimbaji kupita kiasi na biashara ya maliasili huko Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC unavyozidi kuchochea mapigano kwenye eneo hilo, madini kama vile dhahabu na Koltani.Maelfu ya watoto katika Kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya kwa miaka mitatu iliyopita wamelazimika kuacha shule kutokana na umasikini na ukame na mafuriko yaliyochangiwa na mabadiliko ya tabianchi. Lakini sasa wizara ya elimu ya Kenya kwa kushirikiana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, wakfu wa Education Above all na wadau wengine juhudi zinafanyika kuwarejesha watoto shuleni.Makala leo inatupeleka Paris Ufaransa katika makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO kuzungmzia juhudi za shirika hili katika kuhakikisha kwamba wanafunzi walio katika maeneo ya migogoro wanaendelea na masomo yao na wenzao waliohamishwa wanapata ufikiaji wa elimu juu katika nchi zilizowapokea.Katika mashinani fursa ni yake Mirjana Spoljaric Egger, Rais wa Kamati ya Kimataifa ya chama cha Msalaba Mwekundu ICRC akitoa wito wa kutafakari machungu yanayowakumba waathirika wa mizozo wakati wa mazungumzo yake na waandishi wa habari kandoni mwa mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA79.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia suala la elimu katika maeneo ya migogoro, na msaada wa kibinadamu huko Upper Nile nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Nigeria na mashinani nchini Afghanistan, kulikoni??Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kulinda elimu isishambuliwe wakati wa mizozo kutokana na umuhimu wake kwa watoto na jamii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema miaka ya karibuni imeshuhudia ongezeko kubwa la mashambulizi dhidi ya wanafunzi, walimu na shule duniani kote. Hivyo ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa siku hii.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umewaeleza wananchi wa Kaunti ya Nasir au Keich Kon iliyoko jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini kuwa ili waweze kurejeshewa huduma za misaada ya kibinadamu ni vyema wakafikia makubaliano ya kusitisha mapigano.Makala inatupeleka Maiduguri nchini Nigeria kusikia namna mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri yaani Education Cannot Wait (ECW) kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto (UNICEF) na wadau wengine wanarejesha matumaini kwa waliokosa elimu rasmi hasa kutokana na hali mbayá ya usalama katika maeneo yao.Na katika mashinani, fursa ni yake Faeza, mfanyakazi wa kiwanda cha kutengeneza biskuti nchini Afghanistan, mradi unaowezeshwa na shirika la WFP akitueleza manufaa ya mradi huo kwa jamii iliyoathirika na vita hasa wanawake na watoto.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umewaeleza wananchi wa Kaunti ya Nasir au Keich Kon iliyoko jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini kuwa ili waweze kurejeshewa huduma za misaada ya kibinadamu ni vyema wakafikia makubaliano ya kusitisha mapigano. UNMISS pamoja na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu walifikia uamuzi wa kusitisha huduma zao katika kaunti ya Nasir kutokana nae eneo hilo kutofikika na pia ukosefu wa usalama uliosababishwa na mapigano ya mara kwa mara baina ya wanajamii wa kuanti hiyo, na pia mapigano na kaunti za jirani.Hata hivyo mwanzoni mwa mwezi huu wa Septemba kilifanyika kikao kilichowaleta pamoja wadau na wananchi baada ya kupatikana uongozi mpya wa kaunti hiyo ambapo katika kikao hicho, wadau wa misaada ya kibinadamu ikiwemo Umoja wa Mataifa waliombwa kurejesha operesheni zao hususan UNMISS, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani (WFP) na wadau wa Sekta ya afya.Paul Ebikwo ni afisa wa masuala ya kiraia wa UNMISS na akawaeleza anaelewa wasiwasi wao.“Wasiwasi wenu ni wa halali, ni wa kweli, tunaelewa. Lakini mkiongeza mizozo ndani yake, mnafanya mambo kuwa mabaya zaidi, kwa hivyo hebu tufanye maamuzi ya kuachana, na kuweka kando migogoro na sote tufikirie jinsi ya kutatua maswala haya.”Bwana Ebikwo aliongeza kuwa suluhu zote za kuzuia ghasia lazima ziongozwe na wanajamii wenyewe huku akitoa wito kwa makundi ya vijana wanaotumia silaha kujiepusha na mapigano na kutafuta amani.Majadiliano yalihitimishwa kwa wote kukubaliana kuwa na dhamira ya pamoja ya kutafuta njia za kuleta jamii hususani vijana pamoja kwa ajili ya upatanisho na ujenzi wa amani ili kusaidia kurejesha utulivu na kuwezesha jamii katika kaunti ya Nasir kupata ahueni na maendeleo baada ya kuteseka kwa muda mrefu.
Makala hii imeangazia mkutano wa tisa kati ya China na Afrika huko Beijing, wafungwa zaidi ya 100 waliuawa katika gereza la makala nchini DRC, Kenya na mkasa wa moto ulivyowaua wanafunzi Kaunti ya Nyeri, uchaguzi kufanyika nchini Tunisia, na nchini Ufaransa Michel Barnier aliteuliwa kuwa waziri Mkuu, miezi miwili baada ya mvutano wa kisiasa nchini Ufaransa, na mambo mengine kwengineko duniani.
Serikali ya Kitaifa na za Kaunti zimeendelea kutangaza kutengwa kwa mabilioni ya pesa kwa ajili ya waathiriwa wa mafuriko nchini na mikakati ya kukabili mafuriko. Wacha fedha hizo zitumiwe ifaavyo na maafisa wanaohusika wawajibishwe kwa matumizi yake.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Mafuriko yanayoshuhudiwa jijini Nairobi na kote nchini yanaonesha wazi uwezo duni wa serikali kujiandaa kwa ajili ya majanga, na pia kuwepo kwa miundomsingi duni kustahimili majanga yanapotokea. Sepetuko inazirai Serikali za Kaunti na ya Kitaifa kuweka mikakati kabambe ya kujiandalia majanga kama mafuriko ili kuepusha mauti yanayoshuhudiwa.
Mabuting Balita l Oktubre 28, 2023 – Sabado l Ika-29 na Linggo sa Karaniwang Panahon Ebanghelyo: Lucas 6:12-16 Umakyat si Hesus sa bundok para manalangin at magpalipas ng magdamag sa pagdarasal sa Diyos. Nang nag umaga na, tinawag n'ya ang kanyang mga alagad at pumili s'ya ng labindalawa sa kanila na tinawag n'yang Apostol: si Simon na pinangalanan n'yang Pedro, si Andres na kapatid nito, si Jaime, si Juan, si Felipe, si Bartolome, si Mateo, si Tomas, si Jaimeng anak ni Alfeo, si Simon na tinaguriang Zelota, si Judas na kamag-anak ni Jaime, at si Judas Iskariote na naging taga-pagkanulo. Pagninilay: “Sino ba naman ako?” takang-takang tanong ng isang dalagang mula sa isang mahirap na pamilya ng Tondo. “Sino ba naman ako para mapili ni Kristo na maging tagasunod niya? Hindi kaya siya nagkakamali lang?” Ito rin marahil ang naisip nila San Simon Makabayan at ni San Judas Tadeo noong tawagin sila ni Hesus upang maging mga apostol niya. Ipinagdiriwang natin ang kapistahan nila ngayon. Kaunti lang ang mga detalyeng nalalaman tungkol sa kanila, pero sila ang pinakamalapit kay Hesus dahil sila'y mga pinsan niya. Nang humayo sila mula sa Jerusalem para ikalat ang Mabuting Balita ng Kaligtasan sa iba't ibang dako ng mundo, nagkitang muli si San Judas at San Simon sa Persia. Magkasama silang nangaral tungkol kay Kristo at libu-libo ang sumampalataya; pero doon din sila parehong naging martir. Mga ordinaryong lalaki sina Simon at Judas na pinili ni Hesus mismo upang turuan ang iba tungkol sa pag-ibig ng Diyos. Mauunawaan natin sa kanilang buhay na kahit na ang pinaka-karaniwang tao, maaaring maging mga banal kapag nagpasya silang sumunod kay Hesus. Ang inyo pong lingkod ang dalagang-Tondong hindi makapaniwala sa tawag ni Kristo. Nanalangin, nag-lakas-loob, at sinubukang tumugon sa hamon ng bokasyon 40 years ago. Napakalaking privilege at biyaya na maibahagi sa inyo ang mabuting balita. Ikaw, kapanalig, tinatawag ka ba ng Panginoon para sumunod sa kanya? Huwag mag-atubili. Kasama natin siya sa bawat hakbang ng ating buhay. Manalangin tayo: Panginoon, sa halimbawa at panalangin nina San Simon at San Judas, patuloy nawang lumago ang Simbahan sapamamagitan ng pagdami ng mga taong naniniwala at sumusunod sa Iyo. Amen.
Mabuting Balita l Oktubre 25, 2023 – Miyerkules l Ika-29 na Linggo sa Karaniwang Panahon Ebanghelyo: Lucas 12:39-48 Sinabi ni Hesus sa kanyang mga alagad: “Isipin ninyo ito: kung nalaman lamang ng may-ari ng bahay kung anong oras ng gabi ang dating ng magnanakaw, hindi sana n'ya pababayaang looban ang kanyang bahay. Kaya maging handa kayo sapagkat dumarating ang Anak ng Tao sa oras na hindi Ninyo inaakala.” Sinabi ni Pedro: “Panginoon, kanino mo ba sinasabi ang talinhagang ito, sa amin ba o sa lahat?” Sumagot ang Panginoon: “Isipin ninyo ito: may tapat at matalinong katiwala na pangangasiwaan ng panginoon sa kanyang tauhan para bigyan sila ng rasyon sa tamang oras. Kung sa pagdating ng kanyang panginoon ay matagpuan s'ya nitong tumutupad nang gayon, mapalad ang lingkod na iyon. Talagang sinasabi ko sa inyo, pangangasiwain s'ya nito sa lahat nitong ari-arian. Ngunit maaari namang maisip ng lingkod na iyon: ‘Matatagalan pang dumating ang aking panginoon.' At simulang pagmalupitan ang mga utusang lalaki at babae, at kumain, uminom at maglasing. Ngunit darating ang panginoon ng lingkod na iyon sa araw na di inaasahan at sa oras na di n'ya nalalaman. Palalayasin n'ya ang katulong na ito at pakikitunguhang gaya ng mga di-dapat. Maraming hampas ang tatanggapin ng katulong na nakaaalam sa kalooban ng kanyang panginoon pero hindi naghanda ni sumunod sa kalooban n'ya. Kaunti lang naman ang tatanggapin ng walang nalalaman sa kalooban n'ya ngunit gumawa ng mga bagay na dapat parusahan. Hihingan nga ng marami ang binigyan ng marami at hihingan nang higit ang pinagkatiwalaan nang higit.” Pagninilay: Ang Mabuting Balita sa araw na ito ay napakahalagang paalala at pagsusuri ng ating sarili, sa kung papano natin ginagawa ang mga bagay na ipinagkakatiwala sa atin. Maganda rin namang masabihan kang napaka-responsable mong tao. Pero hindi lang ang pagiging responsable at magaling ang mahalaga kay Hesus, kundi higit sa lahat, ang pagiging tapat o (faithful). Katapatan na bunga ng buong tiwala, at pagpapahalaga sa malalim na relasyon, ng isang taong nagbibigay ng tiwala sa Kanya. Ang taong tapat ay responsable, hindi lang sa trabaho, kundi may pagpapahalaga din ito sa kapakanan ng mga kasama nito sa anumang gawain – dahil sila rin ay ipinagkatiwala sa atin ng Diyos. Nawawala ang pagiging makasarili sa ganitong disposisyon. Mas katiwa-tiwala at laging handa sa pagdalaw ng Diyos sa ating buhay. Manalangin tayo: Panginoong Hesus, gabayan nawa kami ng aming pananampalataya sa iyo para maging tapat at may pagpapahalaga sa lahat ng bagay at mga taong ipinagkakatiwala Ninyo sa amin. Amen. - Sr. Reajoy San Luis, fsp l Daughters of St. Paul
Gavana wa Kaunti ya Mandera Mohamed Adan Khalif, amesema asilimia 60 ya kaunti yake iko chini ya udhibiti wa Al Shabaab.
Wakati ukame mkali ukiendelea kuathiri Afrika hususan Ukanda wa jangwa la Sahara na kusababisha mamilioni ya watu kuyakimbia makazi yao kwenda kusaka misaada, baadhi ya wananchi waliosalia kwenye maeneo yao wanasema hali ni mbali lakini wamebaki kwa mustakabali wa watoto wao. Miaka 40 ya jua kali na ukame katika pembe ya Afrika, imekuwa na athari kubwa kwa wananchi wengi wasijue hali yao ya kesho itakuwaje kama mama huyo aitwaye Nurta Andow Nurinye mkazi wa Kaunti ya Garissa nchini Kenya. “Nina watoto watano, kabla ya ukame tulikuwa na mifugo, maziwa na nyama. Tangu ukame uje hakuna mvua, Wanyama wamekufa mbuzi, ngamia kila kitu kimekwenda. Maisha yamebadilika, hakuna chakula hakuna maziwa, hatuna kitu chochote, watoto wakirejea kutoka shuleni hakuna kitu chochote.” Lakini kwanini Bi.Nurta na familia yake hawaendi kusaka msaada zaidi kwenye kambi za wakimbizi wa ndani? “Tungeweza kuondoka na kwenda kusaka chakula sehemu nyingine lakini hatuwezi kwenda. Hapa watoto wapo shule, na hapa watoto wanaenda Madrasa na kwa sababu hiyo hatuwezi kufungasha virago na kwenda sehemu nyingine, ni lazima tubaki hapa.” Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa ikiwemo lile la idadi ya watu duniani na afya ya uzazi UNFPA yanafanya kila juhudi kuhakikisha wanawafikia wananchi kama Nurta Nurinye ili kuwafikishia misaada ya kuokoa maisha.
Shirika lisilo la kiserikali la mtopanga River Conservation, linafanya juhudi kurejesha mto huo katik ahali yake ya awali baada ya kuharibiw akutokana na uchafuzi.
Haii ya wasiwasi imeripitiwa baada ya wavamizi kushambulia vijiji viwili katika kaunti ya Lamu nchini Kenya katika kile mamlaka zinasema ni shambulizi la kigaidi.
Jaridani hii leo tunaangazia machafuko nchini Sudan na mchakato wa uchaguzi nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Kenya na Mashinani yunasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu idadi ya watu duniani.Mzozo nchini Sudan ukiingia mwezi wa pili, hii leo Umoja wa Mataifa na wadau wake wamefanyia marekebisho ombi la usaidizi kwa nchi hiyo na sasa linafikia dola bilioni 3 kwa ajili ya kusaidia mamilioni ya watu nchini humo na mamia ya maelfu wengine waliokimbilia nchi jirani kusaka usalama. Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umefanya warsha za majadiliano katika mji wa Torit na Magwi mashariki mwa mji mkuu Juba jimboni Equatorial Mashariki ili kujadili kuhusu utungaji katiba na michakato ya uchaguzi.Makala leo inatupeleka Kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya ambako shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linashirikiana na serikali na wadau wengine kuzisaidia familia zisizojiweza na zilizo hatarini kupitia program ya lishe na elimu ya afya na malezi bora ijulikanayo kama NICHE.Katika mashinani tutasikia ujumbe kuhusu idadi ya watu duniani na jinsi ambavyo inatofoutiana kulingana na nchi.Mwenyeji wako ni Anold Kyanda, Karibu!
Kaunti ya Kilifi iliyoko Pwani ya Kenya ni moja ya maeneo ambako mradi wa majaribio wa elimu ya malezi na lishe kwa watoto unaendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ukifanyika kwa ushirikiano na serikali na wadau wengine,lengo kubwa likiwa ni kuzisaidia familia zisizojiweza na zilizo hatarini kupitia program ya lishe na elimu ya afya ziweze kutoa malezi bora kwa watoto wao huku zikikabiliana na ukatili katika familia hasa dhidi ya watoto.Mradi huu umeleta faraja kubwa kwa familia nyingi za kauti hiyo tuungane na Flora Nducha katika Makala hii kwa undani zaidi.
Maelfu ya watu wamevuka na kuingia Sudan Kusini wakikimbia mzozo unaoendelea nchini Sudan. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) liko linawasaidia wanaowasili lakini mzigo huu wa ziada unaweka shinikizo katika shughuli za shirika hilo ambazo tayari ziko katika hali mbaya ya ufadhili.Video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inatupeleka katika Kaunti ya Renk iliyoko kaskazinimashariki mwa nchi ya Sudan Kusini inakopakana na Sudan. Hapa ni kila mtu anajaribu kukumbatia kile alichofanikiwa kutoroka nacho akikwepa mabaya ambayo yangemkumba ikiwa angesalia Sudan ambako tangu tarehe 15 mwezi jana Aprili kunafukuta mapigano makali. Wanaobahatika wanabebwa na magari ya Umoja wa Mataifa, wengine punda na wengine wametembea mwendo mrefu kufika hapa. Kwa mujibu wa WFP, zaidi ya watu 30,000 hadi sasa wamevuka mpaka kutoka Sudan na kuingia Sudan Kusini. Wengi wao ni waliorejea kwani walikimbia madhila hapa Sudan Kusini lakini nako ugenini Sudan kumechafuka, wamerejea. Naimat Khamis, ni mmoja wa waliorejea anasema, "Tulilazimika kuja hapa kwa sababu ya mapigano ya Khartoum…tulilazimika kukimbia haraka iwezekanavyo kwa sababu ya vita…ilikuwa safari ngumu…tunataka kubaki na jamaa zetu hapa kwa sababu tumeteseka sana.” Hassan Abdallaziz, kijana mwenye umri wa miaka 17 huyu yeye ni raia wa Sudan kwa hiyo kwa Sudan Kusini yuko ukimbizi anasema, “Hali ya nchi ilinilazimu kuja hapa. Hakuna kitu kizuri kilichobaki nchini, hakuna kazi, ni machafuko. Mtu yeyote anaweza kupora mali yako, ni kama msitu." WFP tayari inawasaidia waliowasili na wanaowasili ikiwa ni pamoja na kuwapa chakula, kuwapima watoto, wajawazito na wanaonyonyesha, lakini mzigo huu wa ziada unaongeza chumvi kwenye kidonda. Mary-Ellen McGroarty ni Mkurugenzi wa WFP nchini Sudan Kusini akiwa mjini Juba anasema, "Mgogoro huu umekuja katika wakati mbaya zaidi. Unajua nchini Sudan Kusini tunaingia katika msimu wa muambo na msimu wa mvua. Tayari tuna watu milioni 7.4 wanaohitaji msaada wa chakula. Hatuwezi kuwafikia wote kwa sababu ya changamoto za rasilimali. Tumelazimika kupunguza programu zetu kwa sababu ya vikwazo vikali vya ufadhili. Na sasa tena tunalazimika kuweka vipaumbele upya kati ya watu wenye njaa, hawa wapya wanaowasili, ambao wako hatarini sana.”
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Makala ya Dosari Ya Shilingi yalioandaliwa na Oscar Ochieng yanahusu madeni katika kaunti ya Mombasa. Makala haya yanazamia sababu zinazopelekea kaunti hii kushuhudia madeni ya kiwango cha juu ndani ya miaka mitano ya kifedha iliyopita wakati ambapo utawala wa sasa umeunda jopo kung'amua ukweli kuhusu madeni hayo.
Hali ya umasikini inayowakumba wananchi wa kaunti ya Kilifi nchini Kenya, imewasababisha wananchi kugeukia ukataji wa miti ili kujikimu kimaisha, hali hii ikichangia uharibifu wa mazingira.
Kaunti ya Kilifi katika miaka ya hivi karibuni imetajwa kuwa Moja wapo ya kaunti zinazoongoza Kwa idadi kubwa ya wasichana wanaopata mimba za mapema nchini. Takwimu kutoka kwa mfumo wa taarifa za afya nchini yaani Kenya Health Information System zikionyesha kuwa jumla ya wasichana 4,909 walio na umri wa kati ya miaka 15-18 walipata mimba katika kipindi Cha mwezi Januari Hadi Agosti Mwaka 2021. Na kama anavyosimulia Ali Mwalimu kwenye makala haya, mashirika mbalimbali kaunti ya Kilifi yamejitokeza kukabiliana na tatizo hilo.
Nchini Kenya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women kwa ushirikiano na wadau wanajengea uwezo wajenzi wa amani mashinani hata kwenye maeneo yenye changamoto kama vile kambi ya wakimbizi ya Daadab kwenye kaunti ya Garissa nchini humo kwa lengo la kuepusha vijana kutumbukizwa kwenye vikundi vyenye msimamo mkali. UN Women inafanya hivyo kupitia warsha inazoendesha kwa ushirikiano na mashirika ya kiraia ya wanawake kama vile WomanKind Kenya ambapo katika moja ya warsha huko kambini Daadab, Nimo Dubat, mwenyekiti wa chama cha wanawake wachuuzi sokoni anaelezea umuhimu wa warsha hizo akisema, “kwa upande wa usalama, wanawake na vijana ndio wanaweza kufuatilia, sisi ndio vijana tumezaa na tunajua ambaye anaanza kuleta shida nyingi. Katika watoto wetu, mama ndiye mzazi, mama ndiye anajua ambaye anaanza tabia mbaya. Mama ndiye anajua nani ameingia kwenye mtaa mgeni, na nani Jirani yake amepokea mgeni, hata tumetengeneza kikundi cha wanawake wa nyumba 10. Hata kuna wasichana wajumbe wa nyumba 10. Sasa tunataka tupatiwe nguvu, tushikamane na polisi kwenye ulinzi. Mama ndiye anabeba mzigo wa shida yote. NasibaAbdi Farah mkazi wa Daadab na mnufaika wa warsha hiyo iliyojumuisha wanaume na vijana wa kike na wa kiume, hakuficha hisia zake akisema kupitia mafunzo waliyopata akisema kuwa "yule kijana ambaye sitamuona nitauliza kwa wenzake ameenda wapi? Ameenda mpakani? Basi nitaenda kwa mama na kumuuliza mtoto wake ameenda kufanya nini mpakani? Akisema sijamuona? Namueleza tafuta kijana wako na umlete.” Warsha hii ilipatia fursa pia viongozi wa eneo la Daadab kushirkiana na mashirika yenye mtazamo sawa kupitisha na kuridhia na kuanza kutekeleza Mpango wa Utekelezaji wa Kaunti ya Garissa wa kuzuia na kukabiliana na misimamo mikali.
Huku msimu wa Krimasi na Mwaka Mpya ukikaribia Sekta ya Utalii inategemea sana msimu huu kuimarika kutokana na watalii wa mataifa ya kigeni wanaolenga kuzuru maeneo mbalimbali ya kitalii nchini. Mojawapo ya maeneo hayo ni eneo la Pwani hususani Kaunti ya Mombasa. Je, wafanyabiashara hasa wa hoteli za kitalii wamejiandaa vipi msimu huu? Robert Menza amezungumza na Josephat Iha ambaye ni Meneja wa Mauzo katika Mkahawa wa Massai Beach.
Hii leo jarida linamulika ukatili dhidi ya wanawake na wasichana na pia mradi wa kupatia fedha jamii nchini Malawi. Makala tunakwenda nchini Kenya na Mashinani nchini Tanzania.Ripoti ya utafiti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNODC inaonyesha kuwa wanawake na wasichana ndio walio katika hatari kubwa ya kuuawa majumbani, ikionyesha kuwa kwa wastani zaidi ya wanawake au wasichana watano waliuawa kila saa na wenzi wao au jamaa wa familia kwa mwaka 2021. Flora Nducha na taarifa zaidiNchini Malawi,shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF kwa msaada kutoka kwa wadau wake wa maendeleo linatekeleza mradi wa kupatia fedha jamii au MSCTP kwa ajili ya kupunguza umaskini, kukabili utapiamlo halikadhalika kuondokana na utoro shuleni utokanao na wazazi kushindwa kulipa karo.Makala ambapo tunaelekea nchini Kenya katika Kaunti ya Garissa kuangazia hali mbaya ya ukame iliyosababishwa na mabadiliko ya tabianchi na hatua zinazochukuliwa na Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na serikali.Na leo mashinani na tunakwenda nchini Tanzania kusikia ni harakati za kunusuru wanawake dhidi ya ukatili kwa misingi ya umiliki wa ardhi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Umoja wa Mataifa na wadau wake wa masuala ya kibinadamu nchini Kenya wameomba dola milioni 472.6 kusaidia watu milioni 4.3 walioathiriwa na ukame, ili kuunga mkono mwitikio unaoongozwa na Serikali, huku janga hilo likitarajiwa kuwa mbaya zaidi. Hali katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo katika Pembe ya Afrika, ni mbaya. Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua anaeleza kuwa mzigo huu wa janga la mabadiliko ya tabianchi ni mkubwa kwa nchi yake na kwa hivyo ni muhimu jumuiya ya kimataifa ikasaidia lengo hilo la Umoja wa Mataifa kwani hali ya wananchi inazidi kuwa mbaya. Mfano mmoja ni katika Kaunti ya Garissa ambako video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa Mazingira, UNEP, inaonesha hali ya wananchi kuwa maisha yako hatarini. Kutoka Kenya, Mwadishi wetu Thelma Mwadzaya anaeleza zaidi kupitia makala hii.
Hii leo jarida linaangazia ripoti iliyotolewa leo na UNICEF kuhusu ubaguzi wa rangi na ubaguzi dhidi ya watoto na pia habari kutoka Garissa, Kenya, makala ya maandamanano ya wanaharakati huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, kisha mashinani nchini Ethiopia.Ubaguzi wa rangi na ubaguzi mwingine dhidi ya watoto kwa misingi ya makabila, lugha na dini zao umeenea duniani kote na kuleta athari kwenye mfumo wa haki, usawa na hata uwezo wa kujua kusoma, hayo yapo kwenye ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF.Msaada wa kisima cha maji uliofanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika shule ya Msingi ya Daley kwenye Kijiji cha Daley, Kaunti ya Garissa nchini Kenya, umesaidia sana jamii hasa katika suala la elimu katika eneo hilo la nchi ambalo limekosa mvua ya kutosha kwa misimu mitano mfululizo.Makala tunafuatilia maandamanano ya wanaharakati huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, maandamanayo yaliyofanyika tarehe 17 mwezi huu wa Novemba, kulikoni?Mashinani tunakwenda nchini Ethiopia kuona ni kwa vipi mtoto mmoja kwa kuwa ni wa kike analazimika kutumia muda wake kuteka maji badala ya kwenda shuleni.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Msaada wa kisima cha maji uliofanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika shule ya Msingi ya Daley kwenye Kijiji cha Daley, Kaunti ya Garissa nchini Kenya, umesaidia sana jamii hasa katika suala la elimu katika eneo hilo la nchi ambayo imekosa mvua ya kutosha kwa misimu mitano mfululizo.Ni wanafunzi wakiwa darasani, kwa uchangamfu wakijadiliana na mwalimu wao kuhusu umuhimu wa maji katika maisha ya kila siku. Nje ya darasa lao kunaonesha wazi hali ya ukame ilivyo ya kutisha. Ardhi imekauka na ni miti michache tu imebaki na ukijani. Kabla ya UNICEF kwa kushirikiana na jamii na serikali kuigilia kati, hali ya kukosekana kwa mvua imesumbua maisha ya wakazi wa hapa ikiwemo upatikanaji wa elimu kwa watoto wa jamii hii ya wafugaji kama asemavyo Mwalimu Mkuu Msaidizi, Wasula Samson Saiya anasema "Tuna takribani wasichana 146 na wavulana 200 jumla wanafunzi 346. Unagundua kwamba wengi wa wanafunzi wanachunga mifugo. Kwa hiyo, wakati wa ukame kama hivi unakuta pia wanahama na wanyama hao kule walikokwenda kulishia ili wawachunge. Kwa hivyo, tunajikuta tuna wanafunzi wachache darasani.” Ili kuitatua hali hiyo, UNICEF ilitoa msaada wa kifedha na kiufundi kuchimba kisima cha chini ya ardhi na kuweka mfumo wa kupaadisha maji kwa kutumia nguvu ya nishati ya jua na pia ujenzi wa upanuzi mpya wa bomba ili kuunganishwa na miundombinu iliyopo ya usambazaji wa maji. Takriban watu 6200 wakiwemo wanafunzi kutoka Shule ya Msingi ya Daley na Kituo cha Maendeleo ya Awali ya Watoto (ECDC) wanapata huduma ya maji salama. Aidha, zahanati moja ya afya ina huduma ya maji salama. Osman Aden Abdi, Naibu Mkurugenzi, Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Idara ya Maji ya Kaunti ya Garissa anasema "Faida ni nyingi. Wakati tulipopata kisima, hali ya hatari katika suala la wanyama pori imepungua. Unyanyasaji wa kijinsia pia umepungua kwa sababu kioski hiki cha maji kiko mahali pa wazi sana. Tuna bahati sana kwa sababu umbali ni kama mita 50 tu hadi mahali pa maji. Inaokoa muda linapokuja suala la masomo ... unajua, katika maeneo yetu ni kukavu sana na joto sana. Kwa hivyo, tunawaruhusu wanafunzi kupata maji kila baada ya dakika 30...badala ya kurudi nyumbani. Kuna maeneo kadhaa ambako UNICEF, kwa usaidizi wa serikali ya kaunti imeweka mitambo ya nishati ya jua. Baada ya kisima hiki kilichimbwa na kuwekewa nishati ya jua, hakuhitajiki gharama zaidi, ili kwa muda mrefu jamii ziweze kujikimu zenyewe.” Kufikia Novemba 2022, katika Kaunti ya Garissa, UNICEF tayari imesaidia ukarabati wa mifumo 21 ya usambazaji wa maji na kufikia jumla ya watu 92,279 wanaopata maji salama.
Licha ya serkali kuahidi kushughulikia changamoto za wafanyabiashara wadogo wadogo, bado mahangaiko yanashuhudiwa mwezi mmoja baada ya Kenya Kwanza kuchukua hatamu za uongozi. Wengi wa wafanyabiashara hao wanalalamikia kuongezwa kwa bei ya mafuta, na kusababisha hasara katika sekta ya matatu. Charles Macharia, mhudumu wa teksi na Jimmy Mwangi, mhudumu wa matatu wanatishia kugura biashara hii. Mwanahabari wetu Edwin Mbugua amefanya mazungumzo na baadhi ya wafanyabiashara hao katika Kaunti ya Nyeri.
Washikadau mbalimbali wanaunga mkono mpango wa ujenzi wa nyumba kwa bei nafuu unaoendelezwa na serikali, mfano mradi wa Buxton Point katika Kaunti ya Mombasa unaoendelezwa na mfanyabiashara, Suleiman Shahbal na Serikali ya Kaunti ya Mombasa. Robert Menza amezungumza na Martin Kariuki, anayesimamia uuzaji wa nyumba hizo.
Mabuting Balita | Oktubre 19, 2022 - Miyerkules Ika – 29 na Linggo sa Karaniwang Panahon Ebanghelyo: Lucas 12:39-48 Sinabi ni Hesus sa kanyang mga alagad: “Isipin ninyo ito: kung nalaman lamang ng may-ari ng bahay kung anong oras ng gabi ang dating ng magnanakaw, hindi sana n'ya pababayaang looban ang kanyang bahay. Kaya maging handa kayo sapagkat dumarating ang Anak ng Tao sa oras na hindi ninyo inaakala.” Sinabi ni Pedro: “Panginoon, kanino mo ba sinasabi ang talinhagang ito, sa amin ba o sa lahat?” Sumagot ang Panginoon: “Isipin ninyo ito: may tapat at matalinong katiwala na pangangasiwaan ng panginoon sa kanyang tauhan para bigyan sila ng rasyon sa tamang oras. Kung sa pagdating ng kanyang panginoon ay matagpuan s'ya nitong tumutupad nang gayon, mapalad ang lingkod na iyon. Talagang sinasabi ko sa inyo, pangangasiwain s'ya nito sa lahat nitong ari-arian. Ngunit maaari namang maisip ng lingkod na iyon: ‘Matatagalan pang dumating ang aking panginoon.' At simulang pagmalupitan ang mga utusang lalaki at babae, at kumain, uminom at maglasing. Ngunit darating ang panginoon ng lingkod na iyon sa araw na di inaasahan at sa oras na di n'ya nalalaman. Palalayasin n'ya ang katulong na ito at pakikitunguhang gaya ng mga di-dapat. Maraming hampas ang tatanggapin ng katulong na nakaaalam sa kalooban ng kanyang panginoon pero hindi naghanda ni sumunod sa kalooban n'ya. Kaunti lang naman ang tatanggapin ng walang nalalaman sa kalooban n'ya ngunit gumawa ng mga bagay na dapat parusahan. Hihingan nga ng marami ang binigyan ng marami at hihingan nang higit ang pinagkatiwalaan nang higit.” Pagninilay: Sa Ebanghelyo ayon kay San Lucas, ipinakikilala na ang ating Panginoon, sa pamamagitan ng larawan ng isang tao naglakbay patungo sa malayong lugar. Ang kanyang pagtitiwala ng iba't -ibang biyaya, panahon, pagkakataon at sa kanyang mga kasamahan, kanyang mga katiwala. Pero ang mga taong ito may kanya-kanyang pamamaraan upang gamitin ang mga pinagkatiwalang biyayang ito sa kasamahaan man o sa kabutihan. Sabi nga, “Anything that we do here on earth has its echo in eternity.” Sa pagbabalik nung Panginoon ng mga taong ito, makikita niyo ang mga taong gumawa ng may katapatan sa kanila-kanilang mga tungkulin, mayroon ding ilan na hindi ginamit ang panahon at pagkakataong ito. At ginamit ang pagkakatong ito para mag pasasa sa kanilang buhay hanggang sa masaktan, bugbugin ang kanilang mga kasamang mga katiwala. Pinagkakatiwala sa atin ng ating Panginoon ang maraming biyaya. Na ang pagkakakilanlan ng mga Kristiyano, mga taong walang ibang gagawin kundi kabutihan at tanging kabutihan lamang. Pagpupuri sa Diyos at paglilingkod sa ating kapwa. Maratnan nawa tayo ng ating Panginoon sa kanyang muling pagbabalik. Mapabilang sa mga katiwala ng may katapatan at kinagampanan ang tungkulin ipinagkatiwala sa kanila ng ating Panginoon. Pagpalain tayo ng ating Panginoon! Fr. Eugene Dominic Hechanova | Archdiocese of Lipa
Katika Makala Uchumi na Biashara Podcast, mwanahabari wetu wa Kaunti ya Trans Nzoia, Martin Ndiema amesema na wakulima ili kubaini ikiwa wameridhia kupanda mimea iliyoboreshwa kwa njia ya kijenetiki yaani GMO. Wapo ambao wamekumbatia na wengine kuirai serikali kuutafakari upya kuhusu uamuzi huo wa Baraza la Mawaziri wa kupitisha GMO. Aidha, amesema na mtaalamu wa mimea akizamia ubora wa mazao ya mimea ya GMO, soko la kimataifa na usalama wa chakula kwa matumizi ya binadamu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema watoto wengi na hususan wa kike katika jamii zilizoathirika na ukame nchini Kenya ikiwemo Turkana wako katika hatari hasa ya kuozwa mapema kwa sababu familia nyingi zinahaha kuweka mlo mezani na suluhu ya karibu wanayoiona ni kuoza binti zao mapema ili kujikimu. Sasa shirika hilo linashirikiana na mamlaka za huduma ya ulinzi kwa watoto katika maeneo yaliyoathirika ili kuwalinda dhidi ya ajira ndoa za utotoni. Mary Kabora na maelezo zaidi. Carol , hilo si jina lake halisi ila amepewa sababu ya kulinda usalama wake, ana umri wa miaka 11 na anaishi katika Kaunti ya Turkana anasema mjomba wake aliamua kumuoza baada ya hali ya maisha kuzidi kuwa mbaya kutokana na ukame , kwani sasa hawana mbuzi tena, wala hawana chochote na matatizo yamekuwa mengi nyumbani. Lakini Caro mwenye ndoto za kusoma alikataa katakata akisema, “nilisema siwezi kukubali hata kama ni njaa basi wacha niake tu mi siwezi kukubali hicho kitu.” Hii ni changamoto inayozikabili familia nyingi hapa Turkana, kisa ni ukame wa muda mrefu uliowafanya kupoteza uwezo wa kujikimu kimaisha, mazao yamekauka, mifugo imekufa, fedha hakuna na msaada ni changamoto. Kukosekana kwa fedha ya kulipia mtihani ndio kulimponza Carol na kisha, “Mama yangu niliporudishwa nyumbani kwenda kuleta hela ya kulipia mtihani alisema hana hela, hakunipa na hiyo likanifanya nikaacha shule. Na ndio ikafanya wanipe mzee anioe, mimi nikakataa nikasema huyo bwana siwezi kukubali.” Ameendelea kusema kuwa mwanaume huyo mzee alikuja kumchukua na pikipiki akaondoka naye na wakiwa njiani walisimama porini na mwanaume huyo akamnajisi. Mkurugenzi wa huduma ya ulinzi kwa watoto Turkana Julius Yator anasema “Kisa hicho kutoka Turkana South kiliripotiwa na jirani kwenye ofisi ya huduma kwa watoto ambayo ni ofisi yangu, na kuanzia hapo mchakato wa kukamata wahusika na kumuokoa mtoto ukaanza.” UNICEF inashirikiana na ofisi hiyo ili kuwalinda watoto walioathirika na ukame na walio hatarini kama Carol, na hadi sasa watoto 1,600 katika Kaunti hiyo wameshafikiwa na kuokolewa dhidi ya ajira na ndoa za utotoni. Mkuu wa UNICEF ofisi ya kanda ya Lodwar Laban Rotuno Kipsang anasema “kwa kawaida tunaporipoti kesi kama hizo binti huokolewa na anapewa malazi na ushauri nasaha. Ukanda wangu pia unafanya kazi kubwa ya kushirikisha jamii kupitia msaada wa UNICEF peke yetu na washirika wengine, na sasa hivi tuna kampeni inayosema baini na komesha , ili unapoona unazuia ni kama katika kesi hii mtu aliona na akaamua kuripoti na mtoto akaokolewa asiolewe.” Na Carol baada ya kuokolewa anasema anataka kurejea ndoto yake “Nataka kusaidiwa niendelee na shule.”
Leo kwenye Makala Uchumi na Biashara mwanahabari wetu wa Kaunti ya Trans Nzoia, Martin Ndiema anaangazia juhudi zinazowekwa na viongozi wa matabaka mbalimbali Barani Afrika kufanikisha kuwapo kwa sarafu moja inayopendekezwa kuitwa AFRO. Aidha amezamia suala la kuafikia boda huru kustawisha uchumi wa bara hili.
Kaunti ya Turkana nchini Kenya inakabiliwa na ukame wa muda mrefu. Ili kusaidia kuimarisha mifumo ya lishe, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, nchini Kenya limeanzisha mfumo wa simu za mkononi uitwao RapidPro. Huduma hii huwezesha vituo vya afya kushirikishana ujumbe wa lishe na wafanyakazi wa kujitolea wa afya ya jamii, ambao huripoti taarifa na takwimu mbalimbali za kiafya kuhusu jamii zao.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF leo limemteua na kumtangaza mwanaharakati wa mazingira kutoka nchini Uganda Vanessa Nakate kuwa balozi mwema mpya wa shirika hilo. Vanessa Nakate, Balozi mwema wa UNICEF, akiwa ziarani Turkana nchini Kenya alitembelea hospitali ya rufaa ya Lodwar na hapo anazungumza na mtoto Eunice Asukuku ambaye alifikishwa hospitali kwa tatizo la utapiamlo mkali, kuvimba mwili na ukosefu wa damu. Chanzo cha matatizo ni uhaba wa chakula utokanao na ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi. Uteuzi wa Vanessa, mwenye umri wa miaka 25 unafuatia ziara yake kwenye Pembeme ya Afrika ambako alishuhudia jinsi gani mabadiliko ya tabianchi yalivyochangia athari mbaya kwa maisha ya watoto nchini Kenya kutokana na ukame unaoendelea. Pia uteuzi huo ni kuthibitisha ushirikiano wake na shirika la UNICEF na kutambua utetezi wake bora wa kimataifa wa haki za kimazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Vanessa alisafiri wiki iliyopita na UNICEF hadi Kaunti ya Turkana Kaskazini Magharibi mwa Kenya ili kujionea athari za uhaba wa maji na chakula unaosababishwa na ukame mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa katika Pembe ya Afrika katika kipindi cha miaka 40. Katika safari yake ya kwanza na UNICEF, alikutana na jamii zilizo katika kitovu cha athari za mabadiliko ya tabianchi ikiwa ni pamoja na kinamama na watoto wanaopata matibabu ya kuokoa maisha kutokana na utapiamlo mkali na familia zinazonufaika na mifumo ya usambazaji wa maji inayotumia nishati ya jua kwa msaada wa UNICEF. Nitahakikisha sauti za watoto zinasikika Baada ya kuteuliwa kwake Bi. Nakate amesema "Kama balozi mwema wa UNICEF, itakuwa jukumu langu la kwanza kuwasilisha sauti za watoto na watu waliotengwa katika mazungumzo ambayo awali hawakujumuishwa. Jukumu hili na UNICEF litanipa fursa zaidi za kukutana na watoto na vijana katika maeneo yaliyoathiriwa zaidi na mabadiliko ya tabianchi na jukwaa lililopanuliwa la kutetea kwa niaba yao. Nchini Kenya, watu niliokutana nao waliniambia kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi na ukame katika maisha yao, huku misimu minne ya mvua iliyofeli mfululizo ikiwanyima watoto haki zao za msingi.” Ameongeza kuwa moja ya jamii alizokutana nazo imemweleza kuwa haijashuhudia mvua kwa zaidi ya miaka miwili. “Hii ni zaidi ya shida ya chakula na lishe, ni mwelekeo mwingine wa changamoto yetu ya mabadiliko ya tabianchi inayozidi kuwa mbaya.” Ombi la UNICEF la kuboresha na kusaidia maisha ya mamilioni ya watu walioathirika na ukame na kuwajengea mnepo kwa muda mrefu kwenye Pembe ya Afrika na kuzuia athari za ukame kwa miaka ijayo zinagonga mwamba kwani hadi sasa ombi hilo limefadhiliwa kwa asilimia 3% pekee. Akiwa Sopel, kaunti ya Turkana nchini Kenya, Vanessa Nakate alitembelea shule ya msingi na kuzungumza na wanafunzi kuhusu changamoto wanazozipata kutokana na janga la ukame kwenye eneo hilo la Afrika Mashariki. Safari ya uanaharakati ya Vanessa Nakate Vanessa alianza harakati zake Januari 2019 kwa maandamano na ndugu zake na binamu zake katika mitaa ya jiji la Kampala, nchini Uganda, maandamano yaliyochochewa na mwanaharakati mwingine nyota wa mabadiliko ya tabianchi na mazingira Greta Thunberg. Aliendelea kuandamana kila wiki, na kuwa sura inayojulikana katika harakati ya vijana kupiga mabadiliko ya tabianchi duniani kote. Mwaka 2020 alijulikana zaidi ulimwenguni wakati alipoondolewa kwenye picha ya habari aliyokuwemo pamoja na Thunberg na wanaharakati wengine weupe wa mabadiliko ya tabianchi. Kufuatia tukio hilo alochosema Vanessa ni kwamba chombo hicho cha habari "hakikufuta picha tu, bali kilifuta bara zima", kauli ambayo iligonga vichwa vya habari vya kimataifa. Vanessa amesema safari yake haikuwa rahisi “Kama mwanamke mwanaharakati mchanga wa Kiafrika, imenibidi kupigana ili kusikilizwa na vyombo vya habari na watoa maamuzi. Wakati nina bahati ya kuwa na jukwaa sasa, ninakusudia kuendelea kupigania wengine. Watoto walio katika kitovu cha athari za mabadiliko ya tabianchi, kama wale niliokutana nao Turkana, Kenya, ni watu ambao nitapigania katika jukumu langu jipya na UNICEF,” amesema Nakate. Tangu wakati huo Vanessa ametumia jukwaa lake kutetea haki ya masuala ya mabadiliko ya tabianchi kujumuisha kila jamii, haswa wale kutoka sehemu zilizoathiriwa zaidi. Alianzisha Rise Up Movement, jukwaa la kupaza sauti za wanaharakati wa mabadiliko ya tabianchi wa Afrika, pamoja na mradi wa kufunga paneli za sola katika shule za vijijini za Uganda. Amehutubia viongozi wa dunia katika mikutano ya mabadiliko ya tabianchi ya COP25 na COP26 na alionekana na hadithi yake kuchapishwa kwenye jarida la TIME.
Kaunti ya Mombasa imekuwa ikishuhudia mkurupuko wa homa zinazosababishwa na mbu ikiwemo homa ya Dengue, Chikungunya na Malaria. Magonjwa ambayo yanasababishwa na aina Fulani ya mbu. Mhariri wetu Ruth Keah katika Makala yafuatayo,ameeleza juhudi mbalimbali zilizochukuliwa na wadau wa afya kuhakikisha kuwa inatokomeza magonjwa hayo.
Kaunti ya Mombasa imekuwa ikishuhudia mkurupuko wa homa zinazosababishwa na mbu ikiwemo homa ya Dengue, Chikungunya na Malaria. Magonjwa ambayo yanasababishwa na aina Fulani ya mbu. Mhariri wetu Ruth Keah katika Makala yafuatayo,ameeleza juhudi mbalimbali zilizochukuliwa na wadau wa afya kuhakikisha kuwa inatokomeza magonjwa hayo.
Tunamulika matukio ya maamuzi ya Raila Odinga kwenda mahakamani na uchaguzi wa magavana katika Kaunti za Kakamega na Mombasa na changamoto za sensa nchini Tanzania halikadhalika uchaguzi wa Angola ambapo chama tawala kinaongoza na kuelekea kupata ushindi.
ATBP7 BUSINESS SEGMENT: MALAPIT NA MAUBOS ANG STANDARD AT 3-IN-1 IDEAL SIOMAI FOOD CARTS! VERY LIMITED OFFER ONLY! Kaunti na lang ang Promo Carts na natitira kaya humabol ka na!! Sa halagang 14,998 makakapag-start kana ng sarili mong negosyo! Ideal Siomai Standard Franchise - P14,998 Ideal Siomai Stall Lifetime Franchise 2-Layer Steamer Acrylic Gulaman Container Stove Burner And Regulator 1k Worth Of Initial Products San ka pa kumpleto na, ikaw nalang kulang! Ito Ang Food Cart na pwede mong ipagmalaki kasi super ganda super tibay pa. May iba pa kaming mga Food Carts na pagpipilian. Be a franchisee today! Ano pa hinihintay mo? ORDER AND FRANCHISE NOW! PLS PM, TEXT, OR CALL Globe 09774548445 Landline 0275274062 You may watch the actual YouTube Video: https://youtu.be/1okASdViYwg PLEASE LIKE AND SUBSCRIBE TO MY OFFICIAL YOUTUBE CHANNEL ATBP7: https://www.youtube.com/channel/UCXuH33Fq0jp3Q9C1d9i0DWA Follow Carla Lalie Flamenco Francisco: Facebook: https://www.facebook.com/ricarlaf Twitter: https://twitter.com/DUCHESSCarla22 Pinterest: https://www.pinterest.ph/Pretty_Ricarla/ Instagram: https://www.instagram.com/pretty_ricarla/ Spotify: https://open.spotify.com/show/5LgQKypoXxW68uQNEMn8Eq?si=c855c1fc33034071 If you want to earn extra money using applications, you can also click the links below for your free subscription and more. *WORDPRESS https://wordpress.com/refer-a-friend/... *PH TODAY https://l.facebook.com/l.php?u=https%... *ENTIREWEB https://l.facebook.com/l.php?u=https%... *FEATURE POINTS https://featu.re/XAMG5Z *PAID TO READ EMAIL https://www.paid-to-read-email.com/?r=1852090 *FRANCHISING BUSINESSES: "Ideal Siomai AND Pure Obsession" HURRY UP!! Book An appointment with us for Business Orientation, Food Tasting, Process Training, and Cart Viewing. Siguradong kikita ang Franchise mo!! FRANCHISE NOW! FOR INQUIRIES: PLS PM, TEXT, OR CALL Globe 09774548445 Landline 0275274062
Wakati Kenya ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu tarehe 9 mwezi ujao wa Agosti, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo linatoa wito kwa serikali itakayoingia madarakani ipatie kipaumbele hifadhi ya jamii ikiwemo kupatia fedha familia zilizo hatarini kama njia mojawapo ya kupunguza umaskini. UNICEF inatoa wito huo wakati huu ambapo mradi wake wa majaribio kupatia fedha famiilia maskini zenye watoto umeanza kuzaa matunda kama anavyoelezea Anold Kayanda katika taarifa hii. Huyo ni Monika Muema, mkazi wa Kaunti ya Kajiado nchini Kenya. Yeye ni bibi na mlezi wa wajukuu watano na binti yake ambaye ni kiziwi. Monika ni mnufaika wa mradi wa UNICEF wa kupatia fedha kaya maskini ambapo kila mwezi hupatiwa takribani dola 17 ili kuweza kulea wajukuu zake akiwemo Alice mwanafunzi wa darasa la 7. Monika anatumia fedha anazopata kusuka vikapu. Ukosefu wa fursa za ajira na changamoto itokanayo na COVID-19 ilifanya hali kuwa mbaya zaidi na watoto wakashindwa hata kwenda shule. Susan Momanyi, afisa wa UNICEF Kenya anasema, “hapa Kenya kaya milioni 1.4 zimeandikishwa kwenye mradi wa hifadhi ya jamii, na hivoy kuacha takribani watoto milioni 12 wanoahitaji huduma hiyo. Ndio maana UNICEF inatoa wito kwa serikali ijayo ya Kenya kuongeza bajeti kwenye hifadhi ya jamii kwa asilimia 1.7 ya pato lake la ndani, kiwango ambacho ni sawa na nchi zingine za kipato cha kati ili kila mtoto anufaike.” Sasa hata walimu wa Alice shuleni wanasema wameona tofauti tangu bibi yake aanze kunufaika na mradi wa kupatiwa fedha kwani mahudhurio ni bora halikadhalika sare za shule.
Hii leo jaridani ni siku ya mada kwa kina, halikadhalika kuna Habari kwa Ufupi bila kusahau kujifunza lugha ya Kiswahili. Mada kwa kina inakupeleka Kaunti ya Migori nchini Kenya kumulika harakati za Umoja wa Mataifa kusaidia wakulima kuondokana na kilimo hatarishi cha tumbaku. Habari kwa ufupi inaangazia wito wa kufunguliwa kwa hospitali tegemewa huko Cameroon ambayo imefungwa baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha. Kisha ni Kenya wito wa kutakiwa kuzingatia uhuru wa msingi wa raia na kuepusha ghasia kuelekea uchaguzi mkuu na mwishoni ni pongezi kwa ubia wa chanjo duniani, GAVI kwa kutenga fedha kufanikisha usambazaji wa chanjo dhidi ya Malaria barani Afrika. Katika kiswahili, je wafahamu maana ya methali Hata ugali kiporo huchoma? Basi karibu sana na mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.
Wasaga-nafaka mjini Kitale, Kaunti ya Trans Nzoia wanasema hawatakubali kuuza unga wa pakiti ya kilo 2 kwa shilingi 100 hadi serikali itakapowafidia. Mmoja wao kwa jina Robert Wanyonyi anasema kufikia sasa hakuna mikakati iliyowekwa kuhusu jinsi watakavyofidiwa na serikali. Anasema mkutano wa Jumatano katika Ikulu ulihudhuriwa na wachache, wengi wao wakiachwa nje. Hata hivyo, amekiri kwamba wateja wamekosa kununua unga wakishinikiza kuuziwa kwa shilingi 100. Katika mahojiano na Martin Ndiema, Wanyonyi anasema huenda wasaga-nafaka wakatapa hasara iwapo hawatafidiwa. Wakenya nao wanaipongeza serikali kwa kupunguza bei ya unga wa mahindi.
Wakenya wameendelea kulalamikia kupanda kwa gharama ya maisha, serikali nayo ikizidisha deni hadi trilioni 10 sasa. Aidha, wabunge na maseneta wamelaumiwa kwa kupitisha pendekezo la kuongeza deni la taifa kutoka shilingi trilioni 9, hadi 10 hali inayochangia kupanda kwa bei za bidhaa. Mike Ekutan ametangamana na Wakenya mjini Lodwar, Kaunti ya Turkana.
Moja ya malengo ya Mkutano wa bahari unaoendelea Lisbon, Ureno, ni kujadili namna ambavyo dunia inaweza kuendelea kunufaika kiuchumi kutokana na uwepo wa bahari. Ajenda hiyo inakuwa muhimu kwa kuwa tayari ni dhahiri shairi kuwa baharí imekuwa mkombozi wa kiuchumi kwa watu wengi duniani. Mfano wa wazi ni Amiri Juma Amiri, mkazi wa kijiji cha Kibuyuni katika Kaunti ya Kwale huko Pwani ya Kenya, mkulima wa zao la mwani ambalo hulimwa baharini. Taarifa ya Anold Kayanda. "Mimi katika hii kazi ya mwani nilikuwa siifanyi.Nilikuwa ninafanya kazi ya uvuvi." Huyo ni mzee Amiri Juma Amiri, mkazi wa kijiji cha Kibuyuni katika Kaunti ya Kwale huko Pwani ya Kenya. Wakati Bwana Amiri akifanya shughuli za uvuvi, mkewe alikuwa analima mwani baharini, lakini nguvu zikamtupa mkono, hapo ndipo bwana amirí akaingia kusaidia na amejikuta amekuwa kinara wa kilimo cha mwani. "Katika wale wakulima ninaweza kusema ni mtu wa kwanza au wa pili kwa ile kulima zaidi." Bwana Amiri akiwa amesimama si mbali kutoka katika ufukwe wa bahari ya hindi na mkononi akiwa ameshika mimea ya mwani iliyofungwa kwa kamba ambazo huisaidia mimea hiyo kuelea kwenye maji, anasema uvuvi ulikuwa haumlipi kwa kiwango anachofaidika nacho katika ukulima wa mwani, "Kule baharini katika uvuvi naona mapato yake ni madogo kwa sababu yalikuwa hayakidhi mahitaji yangu katika familia. Ukienda pwani (kuvua samaki) utapata kula, utapata mambo mambo mengine kidogo lakini kuhusu mambo kama ugonjwa, kuhusu mambo ya kusomesha watoto, yalikuwa kidogo yananisumbua." Lakini sasa mambo yamebadilika, "Ninapata pesa za mwani ninasomesha (ada za shule), kama kumetokea mambo ya ugonjwa pia kidogo ninajisaidia. Pia kwa wakati huu tulionao, ukiona kama mambo yamekuwa magumu zaidi nikienda kwa kile kikundi chetu pia ninaweza kusaidiwa nikajisaidia na mimi." Faida anazozipata mzee Amiri kutokana na kilimo hiki cha baharini si hizo pekee, hakika mwani umembadilishia maisha yake "Nilikuwa ninaishi nyumba ya matope...nilikuwa ninaishi nyumba ya matope. Lakini nilipoanza kilimo cha mwani hiki, mwaka wa kwanza ule kuuza mwani niliuza tani tatu na nusu. Nilipouza, nilipopata zile pesa niliamua kuuza nyumba ya jiwe na sasa hivi niko na nyumba ya jiwe inaenda chumba cha tatu sasa. Kila nikivuna ninaongeza chumba. Kwa hivyo kwa upande wangu mimi huu mwani, ndio umeniwezesha zaidi kuliko yale mambo ya uvuvi." Mwani ni aina ya mimea inayoota na kukua kwenye maji na inapokomaa na kuvunwa inatumika katika matumizi mbalimbali ya binadamu na wanyama miongoni ikiwa ni kusindika vyakula, dawa na mbolea.
In 2019, 29-year-old Irene Gakwa made a big move: she flew from her home in Kenya to the United States to start a new life. Irene had always loved helping people, and she was going to turn that love into a career by studying nursing. Fortunately, Irene already had a support system in the states: her two brothers, Chris and Kennedy lived in Boise, Idaho, and she was going to join them. Everything was going according to plan, and Irene even fell in love. But her family alleges that her boyfriend was no Prince Charming. They say that he was controlling and worked to isolate Irene from her family.On February 24, 2022, Irene had a video call with her parents. She hasn't been seen since. Did she, as her boyfriend claims, decide to pack up and move once again, or has something much worse happened to Irene?If you have any information regarding the disappearance of Irene Gakwa, or if you've seen a grey or silver Subaru Crosstrek with Idaho license plates that may have been seen trespassing on private property or in rural parts of Campbell County between February 24 and March 20, please contact the Gillette Police Department at 307-682-5155.Iwapo una habari yoyote kuhusu kutoweka kwa Irene Gakwa, au ikiwa umeona Subaru Crosstrek ya kijivu au ya fedha yenye nambari za leseni za Idaho ambayo inaweza kuwa ilionekana ikiingilia mali ya kibinafsi au katika maeneo ya mashambani ya Kaunti ya Campbell kati ya Februari 24 na Machi 20. , tafadhali wasiliana na Idara ya Polisi ya Gillette kwa 307-682-5155.We are proud members of Spreaker Prime and The Darkcast Network.Find us everywhere: https://linktr.ee/attwgpodGet episodes early and ad-free on Patreon: https://patreon.com/attwgpodMerch store: https://www.teepublic.com/stores/attwgpodFor a full list of our sources, please visit our blog: https://andthentheyweregone.com/blogThis week's promo is brought to you by Partial list of sources:https://namus.nij.ojp.gov/case/MP90106https://whereisirene.com/index.phphttps://juryfile.com/2022/04/21/irene-gakwa/https://diasporamessenger.com/2022/05/online-love-ended-in-agony-for-missing-kenyan-woman-irene-gakwa-in-us/https://www.news-journal.com/fianc-of-missing-woman-arrested-for-allegedly-stealing-from-her/article_f5a7498c-ff3c-5e33-a7cd-9ac556a8cb5e.htmlhttps://county17.com/2022/05/11/person-of-interest-arrested-in-gillette-missing-woman-case/
Bi. Mwansa, mwanamke mwenye umri wa miaka 70 amekuwa akijihusisha na upishi wa vyakula mbalimbali ambavyo huviuza kwa wateja kila siku, biashara ambayo ameifanya kwa zaidi ya miaka arubaini sasa. Biashara hii aliitegemea sana kuyakidhi mahitaji yake pamoja na wanawe kukiwamo kugharimia karo ya ya wanawe. Mwanamke huyu ambaye ni mkazi wa Majengo, Mvita katika Kaunti ya Mombasa anajihuisha na upishi wa chapati na maharagwe ya nazi. Vyakula vingine ambavyo pia Bi. Mwansa hupika ni mikate ya sinia na mitai. Kupanda kwa gharama ya bidhaa za upishi ukiwamo ya unga wa ngano, mafuta ya kupikia miongoni mwa bidhaa nyingine ambapo huzitumia kwa upishi kumemwathiri sana. Mwanahabari wetu wa Mombasa Robert Menza amezungumza naye katika Uchumi na Biashara Podcast
Mabadiliko ya tabianchi yanayoendelea kukumba Dunia kila uchao hayajaacha wakulima salama. Nchini Kenya, wakulima vijana katika kaunti ya Nyeri, miaka miwili iliyopita walitegemea mto wa jirani na maji ya mvua kumwagilia mashamba yao ya mboga za majani. Hata hivyo ukame na mvua zisizotabirika vilivyosababishwa na mabadiliko ya tabianchi vilikatisha wakulima tamaa. Lakini Umoja wa Mataifa kupitia mfuko wake wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD ulisikia kilio cha wakulima hao vijana na kupatia fedha mashirika mawili: KCEP CRAL linalohusika na programu ya kuboresha nafaka na mnepo pamoja na UTanRMP la usimamizi wa bonde la mto Tana ambao waliwezesha wakulima kupatiwa vifaa ikiwemo vya umwagiliaji. Sasa hali ni shwari kwa vipi? Ungana na Assumpta Massoi katika makala hii.
One of the great liabilities of life is that all too many people find themselves living amid a great period of social change, and yet they fail to develop the new attitudes, the new mental responses, that the new situation demands. They end up sleeping through a revolution. And I submit that nothing will be [...] Read More... The post Tuloy-Tuloy Na Pag-Ibig Kahit Kaunti appeared first on Open Table Metropolitan Community Church.
Jarida la Jumatatu Aprili 25 kwanza ni habari kwa ufupi- Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) umelaani vikali unyanyasaji na ukatili wa kingono ulioenea, mauaji ikiwa ni pamoja na watu kukatwa vichwa, kuchomwa moto raia wakiwa hai, na mashambulizi dhidi ya wahudumu wa misaada ya kibinadamu katika Kaunti ya Leer. ============================ Leo ni siku ya malaria duniani mwaka huu ikibeba maudhui “Tumia ubunifu ili kupunguza mzigo wa ugonjwa wa malaria na kuokoa maisha”. Kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO hakuna chombo kimoja kinachopatikana leo duniani ambacho kitatatua tatizo la malaria hivyom shirika hilo linataka uwekezaji na uvumbuzi utakaoleta mbinu mpya za kudhibiti vijidudu, uchunguzi, dawa za malaria na zana zingine ili kuharakisha kasi ya maendeleo dhidi ya kutokomeza ugonjwa huo wa malaria. ============================= Na jukwaa la 21 la Umoja wa Mataifa la watun wa asili, leo limefungua pazia jijini New York Marekani. Jukwaa hilo linalofanyika ana kwa ana na kwa njia ya mtandao likiwaleta pamoja watu kutoka kila pembe ya dunia mwaka huu linajikita na maudhui “Watu wa asili, biashara, uhuru na msingi wa haki za binadamu wanazostahili ikiwa ni pamoja na ya ridhaa kabla na baada ya taarifa”. MADA KWA KINA: Ikiwa ni siku ya Malaria Duniani mada kwa kina leo inaangazia Malaria kuhusu mbinu mpya za kudhibiti ugonjwa huo ikiwememo chanjo na utafiti wa matumizi ya Toxorhynchites aina ya mbu ambaye anakula mbu wengine hususan mbu aina ya Anopheles ambaye anaeneza ugonjwa wa Malaria. Mwenyeji wako leo ni Leah Mushi.
John 14:18-20 ESV 18 “I will not leave you as orphans; I will come to you. 19 Yet a little while and the world will see me no more, but you will see me. Because I live, you also will live. 20 In that day you will know that I am in my Father, and you in me, and I in you ----- 18 Hindi ko kayo iiwang nag-iisa, ako'y darating sa inyo. 19 Kaunti pang panahon at hindi na ako makikita ng sanlibutan, ngunit makikita ninyo ako; sapagkat ako'y nabubuhay ay mabubuhay rin kayo. 20 Sa araw na iyon ay malalaman ninyong ako'y nasa aking Ama, at kayo'y nasa akin, at ako'y nasa inyo. BECAUSE I LIVE, YOU ALSO WILL LIVE Jesus was leaving but He assured them that they won't be orphans. In the ancient world, being an orphan was even more tragic than in our times today. They were surely homeless and penniless, so that they were dependent entirely on the charity of strangers. This was not the end of their relationship with Him. They won't be abandoned or left without any help. The help comes from the Helper, the promised Holy Spirit. Jesus has explicitly claimed that His task be over and He will be gone from the world. However, it would spark a movement in the lives of the disciples. They will live because Jesus lives. [1 Cor 15:21] The best is yet to come although their predicament was gloomy at that time. In Christ, we have passed from death to life (John 5:24; 1 John 3:14). Why? It's because of the death and resurrection of Jesus (Rom 5:21; 6:8; John 14:6). This particular promise from Christ is the ultimate answer to our struggles in this world (Rom 8:18, 28). Christians have the guarantee of redemption and restoration at the end of our earthly lives (Heb 11:14–16). ---------------------- Visit and FOLLOW Gospel Light Filipino on YouTube, Facebook and Instagram
Leo katika kitengo hiki tunaandazia mahangaiko ya waendeshaji pikipiki kufuatia msako katika harakati za kuinadhifisha sekta ya bodaboda. Msako huo ambao hata hivyo ulisitishwa kuruhusu mazungumzo, umesababisha madhara wahudumu hao wanaokiri ndoa zao zinayumba, wake zao wakiwatoroka kwa kutokuwa na fedha. Mwanahabari wetu wa Kaunti ya Trans Nzoia , Martin Ndiema ametangamana na baadhi yao na kufanya mahojiano nao.
Biashara za ufuoni katika Kaunti ya Kilifi zimesadia vijana wengi kujimudu kimaisha na kuacha uraibu wa mihadarati. Gibson Kombe ni baharia na mwanzilishi wa fuo moja maarufu[vidazini beach, Kilifi ambaye amefungua biashara mbalimbali katika fuo hiyo na pia kuwaajiri vijana wengi na kuwawezesha kuanza kujimudu kimaisha kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Mwanahabari wetu Marion Kithi anatupambia sehemu hii.
Day 8 Nasaan ang ipinanganak na hari ng mga Judio? Nakita namin sa silangan ang kanyang bituin, kaya't naparito kami upang siya'y sambahin. Mateo 2:2 Paulit-ulit na kinikiliti ng Biblia ang ating isipan kung gaano katiyak ang mga pangyayari noon. Paano nadala ng “bituing” ito ang mga mago mula sa silangan patungong Jerusalem? Hindi sinabi ng Biblia na dinala ng bituin ang mga mago o nanguna ito sa kanila papunta sa Jerusalem. Sinabi lang na may nakita silang bituin sa silangan (Mateo 2:2) at pumunta sila sa Jerusalem. At paano nanguna sa kanila ang bituin sa limang-milyang paglalakbay nila mula Jerusalem patungong Bethlehem, gaya ng sinasabi sa Mateo 2:9? At paano ito tumigil sa tapat ng kinaroroonan ng sanggol? Ang sagot? Hindi natin alam. Napakaraming pagsisikap upang maipaliwanag ito batay sa mga planeta o kometa o supernovas o mahimalang ilaw. Hindi lang talaga natin alam. At gusto ko kayong payuhang huwag maging abala sa mga teorya na tentatibo lamang at walang masyadong espiritwal na halaga. Nakikipagsapalaran akong magbigay ng generalization upang balaan kayo: Ang mga taong abala sa mga ganitong bagay — kung paano naging gabay ang bituin at paano nahati ang Red Sea at paano dumating ang manna at paano nabuhay si Jonah sa loob ng isda at paano nagkukulay-dugo ang buwan — ay madalas mga taong tinatawag kong may mentalidad para sa marginal. Hindi mo nakikita sa kanila ang malalim na pag-ibig sa mga sentral na bagay ng ebanghelyo: ang kabanalan ng Diyos, ang kapangitan ng kasalanan, ang kawalan ng kakayahan ng tao, ang kamatayan ni Cristo, ang pagbibigay-katwiran sa pamamagitan lamang ng pananampalataya, ang pagpapawalang-sala ng Espiritu, ang kaluwalhatian ng pagbabalik ni Cristo, at ang panghuling paghuhukom. Tila lagi ka nilang nililihis sa daan gamit ang isang bagong artikulo o libro na exciting para sa kanila, na tumatalakay sa isang bagay na marginal. Kaunti lamang ang pagdiriwang sa malalaking sentral na katotohanan. Ngunit malinaw na makikita sa usapin ng bituin na ginagawa nito ang isang bagay na hindi nito kayang gawin mag-isa: Ginagabayan nito ang mga mago patungo sa Anak ng Diyos upang sambahin Siya. Sa biblikal na kaisipan, iisa lamang ang nasa likod ng ginagawa ng mga bituin: ang Diyos mismo. Hayaang maging malinaw ang aral: Ginagabayan ng Diyos ang mga dayuhan kay Cristo upang Siya'y sambahin. At ginagawa Niya ito sa pamamagitan ng paggamit ng pandaigdigan — malamang ay universal — na impluwensiya at kapangyarihan. Pinapakita ni Lucas ang pag-impluwensiya ng Diyos sa Roman Empire upang magkaroon ng census sa eksaktong panahon para dalhin ang isang mahalagang birhen sa Bethlehem upang matupad ang propesiya sa kanyang panganganak. Pinakita ni Mateo ang pag-impluwensiya ng Diyos sa mga bituin sa langit para dalhin ang iilang dayuhan sa Bethlehem upang sambahin nila ang Anak. Ito ang disenyo ng Diyos. Ginawa Niya ito noon. Ginagawa pa rin Niya ito ngayon. Layunin Niyang sambahin ng mga bansa — lahat ng mga bansa (Mateo 24:14) — ang Kanyang Anak. Ito ang kalooban ng Diyos para sa lahat ng tao sa iyong opisina at sa iyong classroom at sa iyong kapitbahayan at sa iyong tahanan. Sabi sa Juan 4:23, “Sapagkat ganyan ang uri ng pagsambang ninanais ng Ama.” Sa simula ng Mateo, mayroon tayong “Halina't silipin” na pattern. Ngunit sa pagtatapos ay naging “ipahayag sa iba” ang pattern na ito. Pumunta ang mga mago at nakita ito. Tayo'y dapat humayo at magpahayag. Ngunit hindi nagkakaiba ang layunin at kapangyarihan ng Diyos sa pagtitipon ng mga bansa upang sambahin ang Kanyang Anak. Ang pagma-magnify ng naglalagablab na pagsamba kay Cristo sa mga bansa ang dahilan kung bakit mayroong daigdig.
Kuhusu historia na utamaduni, tunaangazia utafiti wa shughuli, asili, na tamaduni ya binadamu zaidi ya miaka Milioni tatu iliyopita, katika êneo la Turkana, nchini Kenya uliofanywa na Profesa Mfaransa Sonia Harmand kwa ushirikiano na Makavazi ya taifa ya Kenya.
Edna Dhababu mwenye umri wa miaka 27, mkazi wa Rabai katika Kaunti ya Kilifi ni mfanyabiashara anyejihusisha na uuzaji wa mavazi ya utamaduni wa Jamii ya Mijikenda. Si hilo tu, Dhahabu pia hukodisha mavazi hayo kwa wateja ambao huwa na hafla mbalimbali zikiwamo za ukumbusho wa kuzaliwa na harusi. Mwanahabari wetu Robert Menza ametangamana naye na kufanya mahojiano ya moja kwa moja.
Kwenye makala ya juma hili, tunaangazia kwanini biashara ya mkaa imeendelea licha ya Serikali kuipiga marufuku nchini Kenya, makala haya yanaletwa kwenu kwa udhamini wa Shirika la Ufaransa la Maendeleo ya Vyombo vya Habari, CFI
Kwa kuwa jiji la Nairobi huwakilisha Kenya nzima likiwa jiji kuu, yafaa lisimamiwe na idara maalum ya serikali ya taifa wala sio kwa njia za kisiasa. NMS imefanya kazi nzuri kuliko wanasiasa wawili ambao wamekuwa magavana tangu mwaka 2013.
MABUTING BALITA | OKTUBRE 20, 2021 Miyerkules sa Ika–29 na Linggo sa Karaniwang Panahon EBANGHELYO: LUCAS 12:39-48 Sinabi ni Jesus sa kanyang mga alagad: “Isipin ninyo ito: kung nalaman lamang ng may-ari ng bahay kung anong oras ng gabi ang dating ng magnanakaw, hindi sana n'ya pababayaang looban ang kanyang bahay. Kaya maging handa kayo sapagkat dumarating ang Anak ng Tao sa oras na hindi ninyo inaakala.” Sinabi ni Pedro: “Panginoon, kanino mo ba sinasabi ang talinhagang ito, sa amin ba o sa lahat?” Sumagot ang Panginoon: “Isipin ninyo ito: may tapat at matalinong katiwala na pangangasiwaan ng panginoon sa kanyang tauhan para bigyan sila ng rasyon sa tamang oras. Kung sa pagdating ng kanyang panginoon ay matagpuan s'ya nitong tumutupad nang gayon, mapalad ang lingkod na iyon. Talagang sinasabi ko sa inyo, pangangasiwain s'ya nito sa lahat nitong ari-arian. Ngunit maaari namang maisip ng lingkod na iyon: ‘Matatagalan pang dumating ang aking panginoon.' At simulang pagmalupitan ang mga utusang lalaki at babae, at kumain, uminom at maglasing. Ngunit darating ang panginoon ng lingkod na iyon sa araw na di inaasahan at sa oras na di n'ya nalalaman. Palalayasin n'ya ang katulong na ito at pakikitunguhang gaya ng mga di-dapat. Maraming hampas ang tatanggapin ng katulong na nakaaalam sa kalooban ng kanyang panginoon pero hindi naghanda ni sumunod sa kalooban n'ya. Kaunti lang naman ang tatanggapin ng walang nalalaman sa kalooban n'ya ngunit gumawa ng mga bagay na dapat parusahan. Hihingan nga ng marami ang binigyan ng marami at hihingan nang higit ang pinagkatiwalaan nang higit.” PAGNINILAY: Mapagkakatiwalaan ka ba? Marahil kaunti na sa atin ang nakauunawa sa salitang katiwala o yung mga inaatasan ng isang may-ari na mangasiwa, mangalaga o magpatakbo ng isang tahanan, ari-arian o negosyo. Naka-ugat at nakabatay ang salitang ito sa Tiwala. Lubos ang tiwalang ibinibigay ng may-ari sa kanyang katiwala na itataguyod nito ang ipinagkatiwala sa kanya kahit na umalis at malayo ang may-ari. Ganito ang nais na iparating ni Hesus sa mga namumuno sa Bayan ng Diyos at sa lahat ng mga tagapag-lingkod at pastol na nangangalaga sa mga Anak ng Diyos. Tayong lahat ay mga katiwala, mga taga-pangalaga ng mga gawa ng Maylikha maging ng kanyang mga anak dito sa lupa. Huwag nating isawalang-bahala, abusuhin o pabayaan ang mga biyaya na sa atin ipinagkatiwala. Alalahanin natin ang halaga ng bawa't biyaya na pawang hiram lamang natin sa May-ari ng sangnilikha. Hiling ni Hesus na bagama't hindi natin lubos na nalalaman kung kailan babalik ang may-ari, alagaan natin ang lahat ng sa ati'y ipinagkatiwala - mula sa dagat, kabundukan at lahat ng likas na yaman, mula sa mga malilit na kabataan maging ang ating buong bayan. Lahat ay biyaya na sa atin ay ipinagkatiwala. Gamitin natin sa wastong paraan ang kapangyarihan at kakayahang ibinahagi sa atin ng Maykapal upang payabungin at higit pang pagyamanin ang Kanyang mga biyaya, para sa ikatataguyod natin at higit sa lahat sa ikauunlad ng ating kapwa at bansa. Amen. – Cl. Buen Andrew Cruz, SSP | Society of St Paul
Wafanyabiashara wa ngozi katika Kaunti ya Turkana wanakadiria hasara kutokana na ukosefu wa karo baada ya soko na bei ya ngozi kusambaratika. Wakizungumza na mwanahabari wetu wa Turkana, Mike Ekutan wafanyabiashara hao wanalazimika kutupa ngozi za ng'ombe, kondoo na mbuzi kwa kukosa thamani. Hata hivyo, wanaowachinja punda wanapata faida kwani ngozi yake hununuliwa na kupelekwa Uchina.
Steve Opondo, maarufu Mtumba Man kutoka Kaunti ya Kisumu ni mfanyabiashara aliyejipatia umaarufu kutokana na sarakasi zake wakati wa kuuza nguo za mitumba. Anasema aliamua kubuni njia ya kuwavutia wateja wake ambao wengi ni akina dada. Mtumba Man sasa ni jina kubwa; amepewa kandarasi ya miaka mitano katika duka la nguo la Devine Collections hapa jijini Nairobi. Maishani, anatazamia kuwa mfanyabiashara mkubwa. Mtumba Man amezungumza na mwanahabari wetu, Esther Kirong' katika podcast hii.
Moses Wafula, muuza-nyama mjini Kapenguria katika Kaunti ya Pokot Magharibi anasema biashara yake inanawiri kutokana na mazungumzo mazuri na wateja wake. Wafula anasema hoteli, shule na hata hospitali ni wateja wake wakuu. Hofu yake kuu ni kuharibika kwa nyama kwa kukosa friji. Pia anasema nyama ya ng'ombe wa gredi huharibika haraka kulinganishwa na wale wa kiasili. Wafula amezungumza na mwanahabari wetu Moses Kiraese katika podcast hii.
Walinda amani wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS wanaendelea na doria ya barabarani kutoka Tambura hadi Ezo katika Jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini kutathmini hali ya usalama na kibinadamu kufuatia kuzuka kwa mzozo mkali unaoendelea katika eneo hilo. Taarifa ya John Kibego inaeleza zaidi. (Taarifa ya John Kibego) Magari ya UNMISS yanaonekana yakilazimika kupita katika vinjia vyembamba katikakati ya misitu. Walinda amani wanajaribu kila njia ikiwa ni pamoja na kuweka magogo katika maeneo ya barabara yaliyobomoka ili magari yasikwame, waweze kuwahakikishia usalama wananchi wa Sudan Kusini. Mapigano yamelazimisha zaidi ya watu 17,000 kukimbia vijiji vyao katika eneo la Tambura kutafuta hifadhi katika Kaunti jirani ya Ezo. Mmoja wao ni Azande, kijana mdogo wa umri wa miaka 17 akiwa anabubujikwa na machozi anaeleza madhila aliyopitia, “Tulikwenda shambani na wazazi wetu ghafla wanaume watatu walitoka msituni. Waliwakamata wazazi wetu, lakini wadogo zangu wadogo watatu wa kiume na mimi tulifanikiwa kukimbia. Tulienda msituni, ambapo tulikaa mpaka usiku. Kisha tukasikia milio ya risasi. Baada ya hapo, niliingia shambani na kukuta miili ya mama na baba imelala.” Maafisa wa Ulinzi wa Watoto wa UNMISS wana wasiwasi kuhusu athari zinazowezekana za mzozo wa kijamii unaoendelea. Moses Bagari ni Afisa katika kitengo hicho katika eneo la Yambio anasema, "Kuna wasiwasi mwingi wa ulinzi, hasa kwa watoto ambao ndio wako hatarini sana. Hali miongoni mwa wasichana. Inaweza pia kuongeza unyanyasaji wa kingono majumbani na hata uhalifu. Watoto wengi wanaweza kuingizwa katika makundi yenye silaha kwa sababu tumekuwa tukiona vijana wenye silaha karibu na hatuwajui wengi wao. " Maafisa wa Ulinzi na Usaidizi wa UNMISS nao wana wasiwasi vile vile wanapoendelea kuwasiliana na wahudumu wa masuala ya kibinadamu katika juhudi za kuleta msaada unaohitajika.Thomas Bazawi kutoka kitengo hicho anasema, “Zaidi ya watu 17,000 katika Kaunti ya Ezo wanahitaji msaada. Moja ya mahitaji ambayo watu hawa waliohama ni ya chakula, kwa sababu hakuna cha kutosha kwa wote. Wanakaa na jamii inayowakaribisha na shinikizo kubwa limewekwa kwenye rasilimali kidogo zilizopo. Lakini wao wanathamini ukarimu unaotolewa na wenyeji wao. Hitaji la pili ni dawa na huduma ya afya. Idadi ya vituo vya afya na uwezo wao hauwezi kuchukua jamii ya wenyeji na watu waliokimbia makazi yao. UNMISS itatumia ofisi yake kuwasiliana na washirika wa kibinadamu wanaweza kuingilia kuokoa maisha ya watoto na wanawake walio katika mazingira magumu.” Wakati hali tete ikiendelea, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kulinda wafanyakazi wa kibinadamu wanaotoa huduma kwa maelfu ya watu waliokimbia makazi yao katika eneo kubwa la Tambura. TAGS: UNMISS, Sudan Kusini, Tambura
Ili kuongeza ajira kwa vijana na kuboresha usafi katika jamii za Kaunti tatu za Migori, Siaya na Kituyi nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, kwa kushirikiana na wadau wake kama shirika la LIXIL na FINISH INK ya nchini humo, wanatoa mafunzo na ufadhili kwa wajasiriamali wachanga hasa wanaojihusisha na miundombinu ya usafi na kujisafi. Taarifa ya Jason Nyakundi inaeleza zaidi.
Kaunti ya Mombasa ina idadi kubwa ya waraibu wa kike wa mihadharati, ambao wengi wao hujipata wamebakwa wakiwa maskani mwao. Wengi wa waraibu hao hushindwa kutafuta haki baada ya kubakwa,hivyo kuishia kuishi na makovu ya milele. By Athman Luchi
Hatua ya Rais Uhuru Kenyatta kutia saini Mswada wa Fedha wa 2021 inazidi kuwakandamiza wananchi ambao wanalazimika kugharimia ada mpya ya asilimia 16. Aidha, wanawalaumu wabunge kwa kusalia kimya. Wanasema hali hii imechangia talaka katika familia, wanawake wakikosa kabisa kuelewa kuhusu kodi hiyo ya thamani. Pia wameghadhabishwa na jinsi serikali inavyopandisha bei ya mafuta huku ikishindwa kuchimba bidhaa hiyo katika eneo la Lokichar, Kaunti ya Turkana. Mwanahabari wetu Mike Ekutan amefanya mahojiano na wafanyabiashara, wahudumu wa bodaboda vilevile wasomi mjini Lodwar.
Ingawa harakati nyingi za kiuchumi na kijamii zimevurugwa na mlipuko wa COVID-19 Mbunge wa Kaunti ya Kigorobya, nchini Uganda David Karubanga alipokuwa akihojiwa na mwandishi wetu wa nchini humo John Kibego, amewatia moyo wananchi kuendelea kusongesha Malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, kwa kuchapa kazi wakati huu wa kufungwa kwa biashara nyingi ili lengo kuu la kuyatimiza malengo 17 ya maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030 liweze kufikiwa.
Podcast hii inamwangazia jamaa mwenye umri wa miaka 30 ambaye hajui la kufanya baada ya mkewe kumtoroka. Kijana huyo anayefanya kazi katika Kaunti ya Isiolo anasema kwamba siku moja mkewe alimwomba ruhusa ya kwenda kuwaona wazazi wake na hadi sasa hajarejea. Mwanamke huyo aliondoka pamoja na mtoto wao wa umri wa miaka 3 na anapopigiwa simu na mumewe anasema kwamba aliolewa kwingine. Kijana huyu yuko katika njia-panda asijue la kufanya. Mshauri wa masuala ya kijamii, Rachel Mahungu anampa ushauri katika podcast hii.
Biashara ya mahindi mwaka huu ni ngumu kulinganishwa na miaka iliyopita kutokana na bei duni. Aidha, Bodi ya Nafaka na Mazao, NCPB inafanya biashara na mawakala wanaowanyanyasa wakulima. Martin Ndiema amezungumza na Joseph Lamai, mkulima wa mahindi na mkazi wa Kaunti ya Trans Nzoia kuhusu suala hili.
Mwanahabari wetu, Willie Khaemba anashiriki gumzo na mfanyabiashara wa mitungi ya gesi katika Kaunti ya Bungoma, Benson Ojiambo. Anazungumzia faida, changamoto na namna ya kuzikabili ili kufaulu katika biashara hii.
FB Live: May 09, 2021 with Ustadz Ahmad Javier The post Ahmad Javier – FB Live: Kaunti na Lang Natitira appeared first on Ahmad Javier.
Makala hii imeangazia kuzikwa kwa aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa Tanzania John Magufuli katika makaburi ya familia huko mjini Chato, mkoani Geita, Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, na Huko Kenya kaunti tano, likiwemo jiji kuu Nairobi, Kajiado, Kiambu, Machakos na Nakuru, yalifungwa kuanzia Ijumaa ya marchi 26 kwa lengo la kupambana na ongezeko la maambukizi ya COVID-19 nchini humo, huku muda wa watu kutotembea katika kaunti hizo ni kati ya saa mbili usiku mpaka wa saa 10 Alfajiri.Hali nchini DRC, Uchaguzi wa Congo Brazzaville na kwingineko duniani yaliangaziwa katika makala haya
Katika Ushauri wa Kibiashara na Fedha, mwanahabari wetu Moses K. Kiraese anazungumza na Julius Okello, mfanyabiashara wa samaki katika Soko la Kacheliba, Kaunti ya Pokot Magharibi.