POPULARITY
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya wahamiaji na wakimbizi nchini Libya, na wakimbizi wajasiriamali katika makazi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Makala inatupeleka Jerusalemu Mashariki, na mashinani nchini Chad, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM, limeeleza mshtuko mkubwa na wasiwasi wake kufuatia kugunduliwa kwa makaburi mawili nchini Libya walimozikwa wahamiaji kadhaa, baadhi yao wakiwa na majeraha ya risasi.Katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma, kutokana na ufadhili wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), kundi la vijana wanajishughulisha na ufugaji wa wadudu nyenje (Crickets) ili kukabiliana na changamoto ya utapiamlo miongoni mwa watoto wachanga.Katika makala Sharon Jebichii anakupeleka Mashariki ya Kati kumulika ziara aliyofanya Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA huko Ukingo wa Magharibi na Gaza ili kujionea hali halisi ya raia.Na mashinani kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu, UNFPA, nampisha Daralssalam, kutoka Sudan ambaye alikuwa Mhadhiri Chuo Kikuu lakini sasa mkimbizi nchini Chad akieleza changamoto alizopitia na kuomba jamii ya kimataifa isaidie wanawake wa Sudan.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Huko Mashariki ya Kati Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA Tom Fletcher alifanya ziara ya siku tatu huko Ukingo wa Magharibi na Gaza ili kujionea hali halisi ya raia. Katika Sharon Jebichii amefuatilia ziara yake na kutuandalia makala hii..
Hii leo jaridani tunaangazia magonjwa ya mfumo wa kupumua vikiwemo virusi vya metapneumovirus, na watoto waathirika wa vita Gaza. Makala inatupeleka nchini Mali na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Huku kukiwa na ripoti za kuongezeka kwa maambukizi ya magonjwa ya mfumo wa kupumua vikiwemo virusi vya metapneumovirus (HMPV) wakati huu wa msimu wa baridi nchini China na kuleta hofu ulimwenguni kuhusu uwezekano wa kutokea kwa janga jingine la ugonjwa kama ilivyokuwa Covid-19, mamlaka ya afya nchini humo inasema kiwango na nguvu za ugonjwa huo viko chini ikilinganishwa na wakati kama huu mwaka jana, ameeleza Hans Kluge, Mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni kanda ya Ulaya akisisitiza ulimwengu kupata taarifa sahihi.Baada ya miezi 14 ya vita Gaza maelfu ya watu wakiwemo watoto wamesalia na ulemavu wa maisha kwa kulazimika kukatwa viungo kutokana na kujeruhiwa katika vita inayoendelea kwa miezi 15 akiwemo mtoto wa umri wa miaka 7 Mahmmoud ambaye sasa amepooza baada ya kupigwa risasi mgongoni na anahitaji huduma za haraka za afya ili akatibiwe limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Magharibi mwa Afrika kusikia jinsi raia wa taifa la Mali walioko ughaibuni wanavyoleta nuru kwa wakulima wa mpunga nchini mwao.Mashinani fursa ni yake Hilda, Mama mwenye umri wa miaka 31 ambaye ni mkimbizi kutoka Burundi anayeishi katika makazi ya wakimbizi nchini Tanzania, anashukuru mfuko wa msaada wa marekani wa kitengo cha Idadi ya watu, wakimbizi na uhamiaji, PRM (Population, Refugees, and Migration Bureau, PRM) kwa huduma za afya ya watoto na kinamama wajawazitito kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa ya kughudumia wakimbizi UNHCR.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele, hali ya usalama na kibinadamu huko Ukanda wa Gaza inazidi kuzorota huku raia na hata wafanyakazi wa kutoa misaada wakisalia wamepigwa butwaa kwani mashambulizi kutoka Israeli yanaendelea kila uchao. Naanzia ndani ya hospitali ya Kamal Adwan kaskazini mwa Gaza, mtoto aliyejeruhiwa amebebwa akilia kwa uchungu. Kwingineko mgonjwa mwingine anatolewa kwenye gari la wagonjwa! Ni taswira iliyozoeleka sasa Gaza.Louise Wateridge ambaye ni Afisa Mwandamizi wa Masuala ya Dharura katika shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa kutoka Gaza Kati amesema hali si hali.Anasema, “mambo kwa kweli yanazidi kuwa mabaya hapa. Kukata tamaa ni kila mahali. Namaanisha, watu unaozungumza nao, na wafanyakazi wenzangu niliozungumza nao hawajui sasa wafanye nini. Hawafahamu waende wapi. Unaweza kusikia nyuma yangu milio ya makombora ikiendelea.”Bi. Wateridge akaendelea kusema kuwa, “kutokuwa na matumaini ndio neno pekee lililosalia Gaza. Unafahamu watu milioni 2.2. Inabidi umkumbushe kila mtu kwamba wamenasa. Hakuna njia ya kutoka nje ya Ukanda wa Gaza na mashambulio ya mabomu yanaendelea mchana kutwa na usiku kucha.”Hali ikiendelea hivyo hii leo huko katikati mwa Gaza, hapo jana jeshi la Israeli lilishambulia na kuharibu kwa kiasi kikubwa ofisi ya UNRWA iliyoko Ukingo wa Magharibi, ofisi ambayo ilikuwa inategemewa zaidi katika kutoa msaada kwa wakimbizi zaidi ya 14,000 wa kipalestina wanaoishi katika kambi ya Nur Shams.UNRWA kupitia mtandao wa X imesema kitendo cha kushambulia ofis iza UN lazima kikome na badala yake zilindwe wakati wote.
Hali Gaza inaendelea kuwa tete wakati ucheleweshwji wa kuhamisha wagonjwa hususan watoto wanaohitaji msaada wa haraka wa huduma za afya imekuwa ni hukumu ya kifo kwao huku maelfu ya watu wakiendelea kukosa mahitaji ya muhimu ya kila siku ikiwemo chakula kama mkate, yameonya leo mashirika ya Umoja wa Mataifa.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limeonya kwamba idadi ya watoto wanaohamishwa Gaza kwa ajili ya huduma za dharura za matibabu imeshuka sana hadi kufikia mtoto mmoja kwa siku na kusema kiwango hiki kikiendelea itachukua zaidi ya miaka 7 kuhamisha watoto 2500 wanaohitaji huduma ya dharura ya matibabu.Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva Uswis msemaji wa UNICEF James Elder amesema “matokeo yake watoto wanakufa Gaza sio tu kutokana na mabomu na risasi na makombora yanayofurusmishwa lakini kwa sababu hata kama miujiza inatokea , hata kama mabomu yanalipuka na nyumba kuporomoka, na vifo kuongezeka watoto wananusurika, lakini kisha wanazuiliwa kuondoka Gaza Kwenda kupokea huduma za afya zitakazookoa maisha yao.”Ameongeza kuwa tangu Januari hadi Mei mwaka huu kwa wastan watoto 296 walihamishwa kwa mwezi kwenda kupata matibabu lakini tangu kufungwa kivuko cha Rafah idadi imeshuka hadi watoto 22 kwa mwezi.Kwa upande wake shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA linasema maisha ya kawaida yanazidi kuwa jinamizi kwani kukidhi mahitaji ya msingi kama chakula ni mtihani mkubwa wengi mathalani katika mji wa Deir al-Balah hata mkate ambao ni chakula kikuu kupatikana ni changamoto,Kila mtu katika Ukanga wa Gaza anakabiliwa na hatari ya baa la njaa kutokana na kuendelea kwa mashambulizi ya mabomu, ghasia, kuharibiwa kwa mashamba na wahudumu wa kibinadamu kushindwa kuwafikia wenye uhitaji.Wataalam wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu nao wamesema wanahofia hali mbaya ya Wapalestina wenye ulemavu ambao wamekwama Gaza, wakionya kwamba watu hao wenye ulemavu wanakabiliwa na hatari za ulinzi ikiwemo kutoepuka kifo na majeraha wakati wa mashambulizi ya vikosi vya Israel na hili ni janga juu ya janga wamesema.Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA likimulika Ukingo wa Magharibi limesema “Makumi ya jamii zinakabiliwa na ongezeko la mashambulizi na vikwazo vya kufikia ardhi yao wakati wa mavuno ya mizeituni ya mwaka huu. Kati ya matukio yote yanayohusiana na walowezi, matukio 104 yamesababisha hasara au uharibifu mkubwa wa mali tangu kuanza kwa mwezi huu wa Oktoba ”.
Tume hiyo huru imeyasema hayo katika taarifa mpya ya msimamo wa kisheriia iliyotolewa mjini Geneva Uswis kuhusu eneo linalokaliwa la Palestina ikiwemo Jerusalem Mashariki ambayo imeweka wazi maoni ya tume kuhusiana na wajibu wa serikali na jinsi Baraza Kuu na Baraza la Usalama linavyoweza kutambua na kutekeleza mbinu na hatua sahihi zinazohitajika kwa kazi hiyo hadi mwisho wa ukaliwaji huo, na kwa haraka iwezekanavyo.Tume ihiyo imebaini kwamba maoni ya ushauri ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki kuhusu matokeo ya Kisheria yanayotokana na sera na desturi za Israel katika eneo linalokaliwa la Palestina ikiwa ni pamoja na Jerusalem Mashariki ni wenye mamlaka na usio na utata kwa kusema kwamba kuendelea kuwepo kwa Israel katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu ni kinyume cha sheria na sheria ya kimataifa.Taarifa hiyo ikitolewa Geneva Gaza kwenyenyewe hali inaendelea kuwa tete, kwa mujibu wa Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestinna UNRWA Phillipe Lazzarini, kwani shule nyingine ya UNRWA imeshambuliwa leo Jabalia Kaskazini mwa Gaza, watu kadhaa wameripotiwa kuuawa na miongoni mwao Watoto wengi waliokuwa wakipata hifadhi katika jengo hilo.Lazzarini amesema hili ni shambulio la tatu dhidi ya majengo ya UNRWA kwa wiki moja. Na pia wafanyakazi wa shirika hilo wanaendelea kuuawa sasa wameffikia 231 tangu kuanza kwa vita hii Oktoba mwaka jana.Naye msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF James Elder akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva Uswisi hii leo amesema “Gaza ni mfano halisi wa ulimwengu wa kuzimu duniani kwa watoto milioni moja wa eneo hilo. Na hali inazidi kuwa mbaya, siku baada ya siku, tunapoona athari za kutisha za mashambulizi ya anga ya kila siku na operesheni za kijeshi za Israek kwa watoto wa Kipalestina.”Nalo shirika la kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA likiangazia Ukingo wa Magharibi limesema “Vikosi vya Israel vimekuwa vikitumia mbinu mbaya za vita katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, na kuibua wasiwasi mkubwa juu ya matumizi ya nguvu kupita kiasi na kuongeza mahitaji ya kibinadamu ya watu.” Ameelezea wasiwasi kuhusu mashambulizi ya walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina na miti yao ya mizeituni wakati huu wa mavuno ya kila mwaka.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mwanza kaskazini Magharibi mwa Tanzania kupata ufafanuzi wa athari za moshi wa kuni kwa binadamu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na sauti kutoka mashinani.Miaka 63 tangu kifo cha ajali ya ndege cha Katibu Mkuu wa pili wa Umoja wa Mataifa Dag Hammarskjöld huko Ndola Zambia, bado majibu hayajapatikana ya nini kilisababisha ajali hiyo wakati akielekea kusaka amani kwa iliyokuwa Congo, sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limesema kampeni ya chanjo eneo la kaskazini mwa Gaza imeendelea leo jumanne licha ya tukio la jana la jeshi la Israeli kuzuia kwa saa nane msafara wa wafanyakazi waliokuwa wanasafiri kwenda kutoa huduma hiyo.Na leo septemba 10, mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA78 unakunja jamvi baada ya mwaka mzima wa mikutano na mijadala, na hivyo kuashiria kuanza kwa mkutano wa 79 ambapo kuanzia tarehe 22 vitaanza vikao vya ngazi ya juu na Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu. Rais anayemaliza muda wake ni Balozi Dennis Francis kutoka Trinidad na Tobago na anayempatia kijiti ni Philemon Yang kutoka Cameroon.Katika mashinani, tunamulika mwaka mmoja tangu kimbunga Daniel kipige mji wa Dema mashariki mwa Libya na vitongoji vyake na kuleta mvua kubwa iliyosababisha mafuriko yaliyoua zaidi ya watu 5,000, na kuacha makovu hadi sasa. Maelezo ya Hawa Bu Zqeeba aliyempoteza baba yake katika mafuriko hayo yanakupatia taswira halisi ya makovu.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Vuta nikuvute ikiendelea Gaza kuhusu ufikishaji, usambazaji na utoaji wa chanjo dhidi ya polio wakati huu ambapo makombora yanaendelea kurindima kutoka jeshi la Israeli, hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO, limethibitisha kubainika kwa mgonjwa mmoja wa polio, ikiwa ni miaka 25 tangu ugonjwa huo utokomezwe eneo hilo. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.(Taarifa ya Assumpta Massoi)Ni kwamba tarehe 20 mwezi uliopita wa Julai, mtoto huyo mwenye umri wa miezi 10 alilazwa katika hospitali ya Al-Aqsa akiwa ana homa kali, anatapika, anahara huku akiwa hana nguvu mwilini, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA katika ripoti yake ya 130 kutolewa tangu vita ianze huko Gaza, ikimulika Gaza, Ukingo wa Magharibi na Yerusalem Mashariki.Tarehe 22 Wizara ya Afya kwenye eneo linalokaliwa la Palestina likathibitisha ugonjwa wa polio virusi namba 2 kwa mtoto huyo ambaye hakuwa amepatiwa chanjo kutoka Deir al-Balah huko Gaza. Siku tatu baadaye yaani tarehe 25 Julai mtoto huyo akapooza sehemu ya chini ya mguu wake. Hivi sasa anaendelea na matibabu na hali yake ni nzuri.Uchunguzi uliofanywa na Kituo cha Marekani cha Kudhibiti na Kuzuia magonjwa, CDC ukaunganisha virusi hivyo na aina ya ile iliyobainika kwenye mazingira huko Gaza mwezi Juni mwaka huu.Sasa WHO imethibitisha kuwa ni polio ambapo Mkurugenzi Mkuu wa UNRWA Philippe Lazzarini kupitia mtandao wa X amesema “inasikitisha sana kwamba mtoto huyo amepooza kutokana na Polio. Polio haitotofautisha kati ya watoto wa Palestina na Israeli. Kuchelewecha sitisho la mapigano kwa misingi ya kiutu kutaongeza hatari ya ugonjwa huo kusambaa zaidi kwa watoto.”Awamu mbili za utoaji chanjo zimepangwa kuanza wiki zijazo na UNRWA imesema wataalamu wake wa afya na kupitia kliniki zake tembezi watasaidia usambazaji kwa ushirikiano na WHO na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Makala hii imeangazia kuuawa kwa kiongozi wa kundi la Hamas, Ismail Haniyeh nchini Iran, mazishi yake yalifanyika Doha, Urusi, mataifa ya Magharibi wabadilishana wafungwa, waziri mkuu wa DRC Judith Suminwa aongoza kumbukumbu ya mauaji ya halaiki ya wakongo maarufu, Genocost, yaliyojiri nchini Kenya, na mgomo wa wafanyabiashara wa Uganda, hukumu dhidi ya dikteta wa zamani wa nchini Guinea na kwengineko duniani.
Hali ya usalama kuendelea kuzorota mashariki mwa DRC baada ya waasi wa M23 kuteka miji kadhaa kama Nyanzale na maeneo jirani, wabunge nchini Uingereza kupinga mpango wa kuwapeleka wahamiaji nchini Rwanda, uchaguzi wa urais kufanyika marchi 24 nchini Senegal, mpya wa 32 wa jumuiya ya kujihami ya nchi za Magharibi, NATO, lakini pia hali ya Israeli na kwengineko duniani.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alijadili mageuzi ya kiutawala na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas wakati wa mkutano wao leo Jumatano katika Ukingo wa Magharibi, pamoja na juhudi za kuimarisha misaada ya kibinadamu kwa watu wa Ukanda wa Gaza.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili inaangazia mkutano wa nchi ya Uchina na viongozi wa Afrika uliofanyika wiki kadhaa zilizopita, pamoja na ziara za viongozi wa nchi za Marekani, Uingereza na Ujermani kwenye nchi za Afrika Mashariki na Magharibi.Ziara zao zinaashiria nini katika muktadha wa kiuchumi? Emmanuel Makundi amezungumza na Profesa Wetengere Kitojo, kuangazia haya kwa kina.
Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili inaangazia mkutano wa nchi ya Uchina na viongozi wa Afrika uliofanyika wiki kadhaa zilizopita, pamoja na ziara za viongozi wa nchi za Marekani, Uingereza na Ujermani kwenye nchi za Afrika Mashariki na Magharibi.Ziara zao zinaashiria nini katika muktadha wa kiuchumi? Emmanuel Makundi amezungumza na Profesa Wetengere Kitojo, kuangazia haya kwa kina.
Wimbi la siasa imeangazia yaliyojiri nchini Niger baada ya maafisa wa jeshi kumng'atusha madarakani Mohammed Bazoum aliyechaguliwa chini ya misingi ya kidemokrasia, hali inayoendelea kwa sasa pamoja na juhudi za Ecowass kutaka kurejeshwa kwa utawala wa kiraia, na kuachiwa huru kwa rais Bazoum. Kuchambua hili wachambuzi Mali Ali akiwa kwenye Visiwa vya Mayote, pamoja na Hajji Kaburu akiwa jijini Daresalaam nchini Tanzania.
Kongamano kati ya Urusi na nchi za Afrika limeanza wakati huu Moscow ikizituhumu nchi za Magharibi haswa Marekani kwa hujuma kwa kushinikiza nchi za Afrika kutohudhuria.Rais wa Urusi Vladmir Putin hii leo amewapokea viongozi hao katika mji wa Saint Petersburg.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Rais wa Kenya, William Ruto alisisitiza Afrika kuwa na useme kwenye taasisi za kifedha za kimataifa pamoja na kutaka masharti ya ulipaji madeni kuangaziwa upya.Tumekuuliza msikilizaji, Unaamini nchi za Magharibi zinatumia madeni kuzinyonya nchi za Afrika?Mataifa ya Afrika yafanye nini kuepuka madeni
Rais wa Kenya, William Ruto alisisitiza Afrika kuwa na useme kwenye taasisi za kifedha za kimataifa pamoja na kutaka masharti ya ulipaji madeni kuangaziwa upya.Tumekuuliza msikilizaji, Unaamini nchi za Magharibi zinatumia madeni kuzinyonya nchi za Afrika?Mataifa ya Afrika yafanye nini kuepuka madeni
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo leo ninatupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, kama ilivyo sehemu nyingi za Afrika Mashariki nako lugha ya kiswahili inatajwa kuwa chombo chenye nguvu sana kinachoingilia kati ujenzi wa amani na pia katika biashara hasa kwa wakaazi wa mji wa Goma katika jimbo la Kivu Kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Kiswahili ndio lugha ya kwanza nchini DRC yenye idadi kuwa ya wazungumzaji katika mikoa ya Mashariki na Magharibi mwa nchi ambako inatumiwa hata kwenye vyombo vya habari kama Redio na televisheni. Pia tunaangazi ripoti ya UNFPA ya idadi ya watu Duniani. Mashinani tunakupeleka nchini Haiti, kulikoni?Mwenyenji wako ni Leah Mushi, karibu!
Wanachama wa Jumuiya ya DR Congo wanao ishi mjini Sydney, walijumuika katika hafla maalum yaku adhimisha miaka 63 ya uhuru wa nchi yao pendwa.
Hii leo ni Siku ya Kimataifa ya Uelewa Kuhusu Ualbino na kama ilivyo ada ya kila Jumanne tunakuletea mada kwa kina ambapo tutamsikia mwanamuziki Roben X akieleza kuhusu maisha yake ya Ualbino. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za DRC, Myanmar na Ukraine. Mashinani tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa tukikuletea ujumbe kuhusu ujumuishaji na uajiri wa watu wenye ualbino.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limesema imeshtushwa na shambulio dhidi ya kambi ya wakimbizi wa ndani lililofanyika jana Jumatatu katika jimbo la Ituri, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Nchini Ukraine Umoja wa Mataifa unashirikisha serikali ya taifa hilo na ya Shirikisho la Urusi ili kuhakikisha upatikanaji wa fursa ya kuwafikia raia wote walioathiriwa na uharibifu mkubwa wa bwawa la Kakhovka.Na mwezi mmoja baada ya kimbunga Mocha kupiga Magharibi mwa Myanmar, mratibu mkazi na wa misaada ya kibinadamu wa umoja wa Mataifa Ramanathan Balakrishnan amesema leo kwamba baraza la uongozi wa jimbo la Rakhine limesitisha fursa ya kufikisha misada ya kibinadamu katika jimbo hilo na hivyo kuathiri usambazaji wa misaada ya kuokoa Maisha katika jamii zilizoathirika.Na katika mashinani leo nampisha Mtaalam Huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wenye ualbino.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina aambapo tutasalia hapa makao makuu kusikiliza msimamo wa Tanzania kuhusu Umoja wa Mataifa kufuatia mazungumzo yetu na Mwakilishi mpya wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Hussein Kattanga. Pia tunaluletea habari kwa ufupi zikiwemo za machafuko nchini Sudan, njaa uliokithiri katikati mwa Afrika na ukosefu wa elimu ka wasichana nchini Afghanistan. Mashinani tunakupeleka nchini Malawi, kulikoni?Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk, ametoa wito wa kusitishwa uhasama mara moja nchini Sudan akilisihi jeshi la serikali SAF na vikosi vya upinzani Rapid Support Forces RSF kurejea katika meza ya mazungumzo.Kiwango cha kutokuwa na uhakika wa chakula katika nchi za Magharibi na katikati mwa afrika kinaratajiwa kuwa cha juu Zaidi mwaka huu katika kipindi cha miaka 10 huku kikitishia kusambaza njaa katika nchi nyingine za pwani na zile zinazokabiliwa na mizozo kama Burkina Faso na Mali kwa mujibu wa utafiti mpya uliotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP.Na utafiti mpya uliofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP unaonyesha kwamba bila wasichana kuendelea na masomo na wanawake kufanya kazi nchini Afghanistan matarajio ya kujikwamua kiuchumi kwa taifa hilo yatasalia kuwa ndoto.Na katika mashini tutaelekea nchini Malawi kushuhudia furaha ya wenyeji baada ya kupata hakikisho la chakula kufuatia kilimo kinachostahimili mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, Karibu!
Nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO kupitia mradi wake FISH4ACP limepokea matokeo ya Utafiti kuhusu Usawa wa Kinjisia katika Masuala ya Uvuvi, moja ya hoja ambayo ikitekelezwa vema itasaidia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hasa la kutokomeza njaa na kuondokana na umaskini.Uzinduzi wa matokeo hayo umefanyika wakati wa kikao cha siku mbili hapa mkoani Kigoma na unatoka na Utafiti kuhusu Usawa wa kijinsia katika mnyororo wa thamani wa mazao ya Uvuvi Ziwa Tanganyika ukishirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wavuvi, wachakataji, wasafarishaji, Jeshi la Polisi, serikali na wadau wa maendeleo.Devotha Songorwa wa Redio washirika Kids Time FM nchini Tanzania ndio shuhuda wetu wa uzinduzi huo uliofanyika katika Mkoa wa Kigoma, Magharibi mwa Taifa hilo la Afrika Mashariki amezungumza na Afisa Mtaalamu Mnyororo wa Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji, kutoka FAO nchini Tanzania anayesimamia mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma nchini Tanzania, Hashim Muumin, ambaye amempatia muhtasari wa matokeo ya utafiti huo kutokana na mradi huo wa miaka mitano unaotekelezwa katika nchi 12 za Afrika ikiwemo Tanzania .“Imeonekana uvuvi ni suala la kiume zaidi kuliko wanawake lakini kwa utafiti tulioufanya tuliona asilimia 78 ya wachakataji ni wanawake na asilimia 99 ya wavuvi ni wanaume na kuna masuala ambayo yanawakwaza kina wanawake na wanaume wavuvi katika kujikwamua kiuchumi,” amesema Afisa huyo.Ameeleza kuwa utafiti huo utasaidia kubaini changamoto zinazokabili masuala ya Jinsia na fursa zake katka Ziwa Tanganyika ili kutoa mwamko kwa wanawake na watu wenye ulemavu kujihusisha na Uvuvi kuinua kipato chao.“Shirika la FAO limeanzisha dawati la jinsia katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambalo linafanya kazi na sisi kama mradi wa FISH4ACP tunafanya kazi kwa karibu sana kuhakikisha sera, mikakati na sheria za Serikali zinatekelezwa,” amebainisha Hashim.
Hii leo jaridani tunaangazia wasichana waliotekwa nyara katika shule ya bweni huko Chibok Nigeria ambapo mpaka sasa 96 bado wapo utumwani, na matokeo ya mradi wa FISH4ACP nchini Tanzania. Makala tunakupeleka nchini Rwanda na Mashinani nchini Jamhuri ya Congo, Brazaville, kulikoni?Ikiwa ni miaka tisa imepita tangu wasichana 276 kutekwa nyara wakiwa katika shule ya bweni huko Chibok Nigeria ambapo mpaka sasa 96 bado wapo utumwani, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limetaka wadau kusaidia katika kuwekeza zaidi katika usalama wa wanafunzi mashuleni kwani bado vitendo vya utekaji vinaendelea nchini humo.Nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO kupitia mradi wake FISH4ACP limepokea matokeo ya Utafiti kuhusu Usawa wa Kinjisia katika Masuala ya Uvuvi, moja ya hoja ambayo ikitekelezwa vema itasaidia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hasa la kutokomeza njaa na kuondokana na umaskini. Devotha Songorwa wa Redio washirika Kids Time FM nchini Tanzania ndio shuhuda wetu wa uzinduzi huo uliofanyika katika Mkoa wa Kigoma, Magharibi mwa Taifa hilo la Afrika Mashariki.Katika tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa kusikiliza simulizi ya manusura wa mauaji ya kimbari dhidi ya watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, ikiwa leo Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lina kumbukizi maalum ya mauaji hayo.Na katika mashini tutaelekea katika mji mkuu wa Jamhuri ya Congo, Brazaville kusikia ushauri kutoka kwa mwanamke ambaye amekuwa akiishi na Virusi vya Ukimwi, VVU kwa miaka 24.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, Karibu!
Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo:Angola yatakiwa kubadili sheria ya kuengua watu wenye ulemavu katika kusimamia haki zao.TANBATT 6 wanaohudumu chini ya MINUSCA washiriki huduma ya kutoa matibabu na kukabidhi msaada wa dawa katika zahanati ya WAPO, Berberati, Mambéré-Kadéï.Mradi wa ufumbuzi wa tatizo la maji kwa kutumia teknolojia ya nishati ya jua wahakikisha upatikanaji wa maji safi na salama mkoani Kigoma, Magharibi mwa Tanzania.UNICEF yafadhili mafunzo ya kuwaelimisha walimu nchini Rwanda ili kuwashauri wanafunzi.
Vita ya Ukraine ikiwa inaingia mwaka wake wa pili, wawakilishi mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wametoa maoni yao kufuatia uamuzi kwa njia ya kura uliofanywa na Kikao Maalumu cha dharura cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio jipya la kutaka amani ya haki na ya kudumu nchini Ukraine na kwamba Urusi bila masharti yoyote iondoe mara moja majeshi yake katika ardhi ya Ukraine. Umaalumu wa kikao hiki cha siku mbili kilichokamilika jana jijini, New York, Marekani ni kwa mujibu wa azimio lilipotishwa mwaka 1950 na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwamba Baraza hilo linaweza kushughulikia masuala ya kimataiafa yanayohusu amani na usalama pale ambapo Baraza la Usalama linakuwa limeshindwa kufanya hivyo. Kwa msingi huo kutokana na mara kwa mara Urusi kutumia kura ya turufu katika Baraza la Usalama kuzuia uamuzi wa kuibana, ndipo kikao hiki cha Baraza Kuu kikaitishwa kwa siku mbili Jumatano na Alhamis katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ili nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wapige kura kuiambia Urusi iondoke Ukraine.Awali kabla ya azimio kupigiwa kura, Vassily Nebenzia Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi aliliambia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuwa kufanya uamuzi kwa kuangalia tu yaliyotokea Februari 24 mwaka jana 2022 ni jaribio la makusudi la nchi za Magharibi kuficha sababu za kweli za mzozo huo. Hata hivyo matokeo ya kura yakaonesha kuwa walioinga mkono Urusi ni nchi 7 tu, 31 zikionesha kutokuwa upande wowote huku 141 zikiliunga mkono Azimio. Vita ikome, Urusi iondoke Ukraine.Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nje wa Ukraine, Dmytro Kuleba, mara tu baada ya kupitishwa kwa azimio… anasema “nchi yangu imeridhika na matokeo na ujumbe uko wazi; Haijalishi ni nini Urusi inajaribu na jinsi inavyojaribu kudhoofisha utaratibu wa kimataifa, inashindwa kila mara.” Naye Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa aliwasisitizia wajumbe akisema, “uchokozi ni kinyume cha sheria. Kumvamia jirani ni kinyume cha sheria. Kujimegea kipande cha nchi nyingine ni kinyume cha sheria.” Miongoni mwa nchi 32 ambazo zimepiga kura isiyoonesha kama zinaunga mkono azimio au la pamoja na Burundi, Msumbiji, Ethiopia, Congo, Zimbabwe, Afrika Kusini, China, India na Pakistan. Na zile ambazo zimeiunga mkono Urusi kwa kulipinga azimio hilo la kumaliza vita Ukraine ni Belarus, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea, Eritrea, Mali, Nicaragua, Urusi yenyewe na Syria.
Katika kuhakikisha wanawavutia wakimbizi wa ndani kurejea makwao, ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS, umekarabati na kukabidhi jengo la mahakama pamoja na kujenga jengo jipya la jela huko jimboni Equatorial Magharibi katika kaunti ya Maridi.Nchini Sudan Kusini wananchi waliokuwa wakimbizi wa ndani na sasa wameanza kurejea katika vijiji vyao wanataka kurejea katika mazingira ambayo kuna utawala wa sheria.Sarah Barnet ni kiongozi wa wanawake wa kaunti ya Maridi iliyoko jimboni Equatorial Magharibi, “Tunahitaji kuona haki ikitendeka, hasa kwa wanawake. Kuna kesi nyingi za unyanyasaji wa kijinsia katika jamii yetu, na zinapaswa kushughulikiwa na mahakama. Haki zetu kama wanawake lazima ziheshimiwe.”Kwakutambua hili na kutekeleza jukumu lake la kuhakikisha wanalinda amani na kuimarisha mifumo ya haki nchini Sudan Kusini UNMISS wametekeleza mradi uliogharimu takriban dola 100,000 kwa kukarabati jengo la mahakama ya kaunti ya Maridi na kujenga jengo jipya la jela ili yaweze kutoa huduma ya kuhakikisha sheria zinafuatwa na wale wasiofuata sheria jela mpya iliyojengwa lipo kwa ajili yao.Ibrahim Tahiru ni afisa wa Ulinzi, Mpito na Uunganishaji wa UNMISS na anasema wanachukulia utekelezaji wa miradi hii ya kuleta mabadiliko haraka kuwa ni kichocheo muhimu cha kuwavutia watu wengi zaidi kuweza kurejea makwao kutoka ukimbizini, "Tunaamini kuwa tutaweza kukuza hali ya kudumu ya watu kurejea makwao na kuwaunganisha wakimbizi hawa wa ndani pamoja na waliokimbilia nje ya mipaka ya nchi. Tunataka waweze kujisikia kulindwa na kujua kwamba hawata pokonywa mali zao kiholela. Pia tunataka wajue watalipwa ikiwa, walipokuwa wakikimbia mzozo baadhi ya mali zao zilichukuliwa na watu wengine. Kwa hivyo, taratibu zote hizi kama ujenzi wa mahakama na jela zinategemeana. Tunaamini kuwa mfumo madhubuti wa haki utawasaidia sana watu wanaotafuta haki.”Ujumbe wa Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini humo, UNMISS haujajitolea tu kuboresha uwezo wa mfumo wa haki nchini Sudan Kusini, bali pia kukuza heshima na kufuata matakwa ya haki za binadamu.Jamii ikiwa imewekewa mazingira bora ya kuwawajibisha wahalifu, ukiukaji wa haki za binadamu unatarajiwa kupungua.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia haiwezi kutatua changamoto kubwa inazokabiliwa nazo hivi sasa kuanzia mabadiliko ya tabianchi, vita ya Ukraine, mdororo wa uchumi na athari zinazoendelea za janga la COVID-19 katikia hali ya sasa ya mgawanyiko na kutokuwa na mshikamano hivyo wakati wa kufumbia macho changamoto hizi umepita na wanaochangia wawajibishwe.Katibu Mkuu Guterres ameyasema hayo mjini Davos Uswis katika hotuba yake kuhusu hali ya dunia kwenye siku ya pili ya jukwaa la uchumi duniani akibainisha kwamba wakati dunia inahitaji ushirikiano zaidi katika masuala ya mabadiliko ya tabianchi , upunguzaji wa mzigo wa madeni na afya uya kimataifa kuna mgawanyiko na changamoto inaongezeka linapokuja suala ya vita ya Ukraine akisema "Hasa uvamizi wa Urusi kwa Ukraine sio tu kwa sababu ya mateso yasiyoelezeka kwa watu wa Ukraine, lakini kwa sababu ya athari zake kubwa za kimataifa kwa bei ya chakula na nishati, kwenye minyororo ya biashara na usambazaji na maswala ya usalama wa nyuklia, kwa misingi hiyo hiyo ya sheria za kimataifa”. Akisisitioza kuhusu suala la mabadiliko ya tabianchi amelaani makampuni makubwa ya mafuta kwa kupuuza sayansi kuhusu mabadiliko ya tabianchi, na kushutumu sekta ya mafuta na gesi kwa kutafuta kupanua zaidi wigo wa uzalishaji licha ya kujua kwamba kwamba mtindo wao wa biashara hauendani na maisha ya binadamu. Amesema"Baadhi ya makampuni makubwa ya mafuta wanadanganya kwa kiasi kikubwa na kama vile ilivyo kwa sekta ya tumbaku, wale wanaohusika kuchochea mabadiliko ya tabianchi lazima wawajibishwe." Pia amezungumzia migawanyiko ikiwemo baina ya Mashariki na Magharibi hasa Marekani na Uchina hususan katika suala la haki za binadamu na usalama wa kikanda na Kaskazini na Kusini ambao amesema hashawishiki kwamba Kaskazini inatambua kiwango cha madhila yanayowakabili watu wa Kusini hasa linapokuja suala la afya kuhusu usawa wa usambazaji wa chanjo. Amehitimisha hotuba yake kwa kutoa wito kwa serikali zote, sekta binafsi na wadau wote kuunda njia za ushirikiano zaidi, ikisisitiza haja ya kuziba pengo la migawanyiko yote kwa kurekebisha na kujenga usawa katika mfumo wa fedha wa kimataifa, Kuchukua hatua za maana dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, Kurekebisha muundo wa biashara na mazoea ili kuendeleza malengo ya maendeleo endelevu, kuongoza njia ya kufikia fursa za kiuchumi kwa wanawake, na kufikia lengo la uhakika wa chakula duniani . Hivyo amesisitiza kwamba “Sasakuliko wakati mwingine wowote, ni wakati wa kutengeneza njia za ushirikiano katika dunia yetu lililogawanyika kwani dunia haiwezi kusubiri."
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Nchi za Afrika zimezidi kukopa kutoka kwa shirika la fedha duniani IMF ,vilevile Rais wa Ghana amewataka viongozi wa Afrika kuacha kuomba mikopo kutoka kwa nchi za Magharibi. Tumekuuliza Kwa nini unafikiri Afrika inahitaji mikopo zaidi? je, nini athari za mikopo hii kwa uchumi?Sikiliza makala habari rafiki kwa mengi zaidi
Nchi za Afrika zimezidi kukopa kutoka kwa shirika la fedha duniani IMF ,vilevile Rais wa Ghana amewataka viongozi wa Afrika kuacha kuomba mikopo kutoka kwa nchi za Magharibi. Tumekuuliza Kwa nini unafikiri Afrika inahitaji mikopo zaidi? je, nini athari za mikopo hii kwa uchumi?Sikiliza makala habari rafiki kwa mengi zaidi
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Katika mkutano wa mazingira wa COP 27 nchini Misri, Afrika kwa sauti moja inayataka mataifa ya Magharibi yanayochagia asilimia 80 ya uchafuzi wa hewa kuheshimu ahadi zao na kutoa fedha za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Katika mkutano wa mazingira wa COP 27 nchini Misri, Afrika kwa sauti moja inayataka mataifa ya Magharibi yanayochagia asilimia 80 ya uchafuzi wa hewa kuheshimu ahadi zao na kutoa fedha za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Mamia ya Wazimbabwe walijitokeza Jumanne katika maandamano ya kupinga vikwazo vya Magharibi, ambavyo serikali imekuwa ikivilaumu kwa muda mrefu kuwa sababu ya matatizo ya kiuchumi ya nchi hiyo.
Karibu Jumapili hii kuwa nami katika Makala Changu Chako Chako Changu, ambapo leo nakuletea Historia watu wa Kabila la Waturukana. Na kwenye kipengele cha le parler francophone nakuletea ratiba kwenye Institut francais yta Lubumbashi na Nairobi nchini Kenya lakini pia Dar es salaam Tanzania, na kwenye Muziki nakuletea kumbukumbu ya miaka 33 tangu kutokea kifo cha hayati Franco. Mimi naitwa Ali Bilali Bienvenue et Bon reveil Matinale.
Burkinafaso imeshuhudia mapinduzi ya kijeshi mara mbili mfululizo kwa kipindi kisichozidi mwaka mmoja, na kushuhudia kiongozi wa kijeshi Paul Henri Damiba akipinduliwa.Unafkiri mapinduzi haya ya kijeshi yanauwa demokrasia katika nchi za Afrika Magharibi ?Nini mchango wa jumuiya ya kimataifa katika kukomesha matukio kama haya ya mapinduzi ?
Burkinafaso imeshuhudia mapinduzi ya kijeshi mara mbili mfululizo kwa kipindi kisichozidi mwaka mmoja, na kushuhudia kiongozi wa kijeshi Paul Henri Damiba akipinduliwa.Unafkiri mapinduzi haya ya kijeshi yanauwa demokrasia katika nchi za Afrika Magharibi ?Nini mchango wa jumuiya ya kimataifa katika kukomesha matukio kama haya ya mapinduzi ?
Takriban asilimia 60 ya nchi za kipato cha chini barani Afrika hivi sasa ziko kwenye mzigo wa madeni, shinikizo kubwa au katika hatari ya kuingia kwenye madeni huku mamilioni ya Waafrika wakitumbukia tena kwenye umasikini wakati huu wakiwa kwenye hatari kubwa ya kutokuwa na uhakika wa chakula, imeonya ripoti mpya ya biashara na maendeleo kwa mwaka 2022 iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD. Flora Nducha na taarifa kamili Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa mjini Geneva Uswis kiwango cha ukuaji uchumi cha Afrika kimeshuka na mwaka huu wa 2022 kinatarajiwa kukua kwa asilimia 2.7 huku 2023 kikikuwa wa asilimia 2.4 ukiulinganisha na ukuaji wa asilimia 5.1 uliokuwa mwaka 2021. Na matokeo yake watu wengine milioni 58 barani Afrika watalazimia kutumbukia kwenye umasikini uliokithiri mwaka huu na kujiunga na wengine milioni 55 ambao tayari wako kwenye ufukara. Katibu Mkuu wa UNCTAD Rebeca Grynspan amesema”Kuzorota huku kwa uchumi kunasababisha mkwamo wa kufikia agenda ya 2030 ya maendeleo endelevu. Na madeni yanazikabili sekta zote Afrika kuanzia za umma na sekta binafsi.” Mbali ya mzigo wa madeni ripoti hiyo ya UNCTAD inasema zaidi ya asilimia 60 ya nchi za Afrika zinahitaji msaada wa chakula kutoka nje wakati huu njaa ikisambaa haraka kwenye bara hilo. Imeongeza kuwa kudorora huko kwa uchumi kunaleta changamoto zingine lukuki ikiwemo ongezeko kubwa la bei za mafuta na chakula, shinikizo katika sera za fedha kwa nchi zilizoendelea na hatari kubwa ya kutokuwa na uhakika wa chakula katika maeneo mengi ya kanda hiyo. Katika nchi tatu za Africa ambazo uchumi wake ndio unashikilia asilimia 60 ya pato la bara hilo Nigeria, Misri na Afrika Kusini ripoti inasema ukuaji wa uchumi umeshuka ikilinganishwa na mwaka 2021. Kwingineko kwa mujibu wa ripoti " Shirika la fedha duniani IMF na Benki ya Dunia wameingilia kati kwa programu maalum kuzisaidia nchi 16 za kipato cha chini Afrika zilizo na mzigo mkubwa wa madeni na zilizo katika hatari ya mzigo huo ili kupunguza mzingo huo zikiwemo Zambia, Ghana na Tunisia. " Wakati huohuo shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limekadiria kuwa nchini 33 za Afrika zinahitaji msaada wa chakula toka nje wakati hali ya kutokuwa na uhakika wa chakula ikitarajiwa kuwa mbaya zaidi katika miezi 18 ijayo katika nchi hizo. “Kupanda kwa bei ya mbolea kwa sababu ya vita inayoendelea Ukraine kunatishia kupunguza uzalishakji wa chakula na kuongeza mgogoro wa chakula duniani huku wakulima wadogo wakiwa ndio waathirika zaidi. Hali ni mbaya zaidi hususan Mashariki na Magharibi mwa Afrika kutokana na uzalishaji mdogo wa kilimo , ukame, na migogoro”. Amesema Rebeca Grynspan.
Katika Jarida la habari la Umoja wa Mataifa leo Ijumaa Flora Nducha anakuletea -Katika siku ya kimataifa ya kulinda shule dhidi ya mashambulizi mashirika ya Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na la elimu sayansi na utamaduni UNESCO yanasema Afrika ya Kati na Magharibi ni nyumbani kwa karibu robo ya watoto wote duniani wasiokwenda shule -Taasisi ya Molteno ya lugha, kusoma na Kuandika kutoka nchini Afrika Kusini imetunukiwa tuzo ya kujua kusoma na kuandika ya mwaka 2022 ijulikanayo kama confucius ambayo hutolewa na shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO. -Makala yetu leo inatupeleka kuangazia wahamiaji na changamoto wanazopitia kwenda kusala hifazi hasa raia wa Venezuela wanapoikimbia nchi yao kuingia Chile -Mashinani inaturejesha Makao Makuu ya Un kwenye mkutano wa waathirika wa ugaidi na mmoja wao anakumbuka siku ambayo hatoisahau maishani shambulio la ugaidi lilipobisha hodi kwenye sherehe ya harusi yake
Mjadala wa kila Ijumaa "Live Talk" unaangazia namna Afrika inaweza kujiondoa katika ushawishi wa mataifa ya Magharibi na yaliyo endelea kiujumla.
Lavrov amesema hayo wakati wa kumaliza ziara yake ya siku nne barani Afrika Jumatano kwenye ubalozi wa Russia mjini Addis Ababa, Ethiopia. Amelaumu vikwazo vilivyowekewa taifa lake na mataifa ya magharibi.
Waziri wa mambo ya nje wa Russia Sergei Lavrov alikamilisha ziaara yake baran Afrika kwa kukutana na viongozi serikali ya wa Ethiopia mkjini Addis Ababa huku akikosolewa na baadhi ya mataifa ya Magharibi.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov anafanya mazungumzo mjini Cairo na maafisa wa Misri wakati nchi yake ikijaribu kukabiliana na hatua ya kutengwa kidiplomasia na kuwekewa vikwazo na nchi za Magharibi kutokana na uvamizi wake wa Ukraine. Lavrov pia atazuru Ethiopia, Uganda na DRC.
Jamii zawatu wenye tamaduni mbali mbali wanao ishi Magharibi Australia, wamepata sehemu mpya yakupokelea huduma, kuchangia taarifa nakuendesha shughuli zao.
Ni Jumapili nyingine tunakutana tena katika Makla haya ya Changu chako Chako changu rfi kiswahili leo nakuletea hitoria ya jiji la Kisumu, nitaungana naye mwenzangu Victor Abuso aliekuwepo huko Kisumu na kwenye kipengele cha Muziki nitakuletea mwanamuziki muasisi wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania Mr Sugu mimi ni Ali Bilali bienvenue.
Kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi kusababisha ukame katika maeneo mbalimbali ya dunia, kusababisha kupungua kwa mvua za masika, baadhi ya wakulima wa wilaya ya Uyui mkoani Tabora, nchini Tanzania wanasema hawajasazwa katika kukumbana na athari za mabadiliko hayo kwani hata mvua za masika walizokuwa wanazitegemea kukuzia mazao yao, zimekuwa za kusuasua. Kwa sababu hiyo wameamua kujikita katika kilimo cha muda mfupi katika bustani ndogondogo ili waweze kujikumu kimaisha lakini bado wanakumbana na changamoto nyingine ikiwemo kukosa mbegu na pembejeo, na kulazimika kutumia sumu nyingi ambazo ni hatari kwa mazingira na afya. Hamad Rashid wa Redio washirika Tanzania kidstime fm kutoka Mkoa wa Morogoro amesafiri hadi Magharibi mwa Tanzania Kata ya Ibelamilundi Wilaya ya Uyui Mkoa wa Tabora na kuzungumza na wakulima.
Kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi kuleta ukame katika maeneo mbalimbali ya dunia, kusababisha kupungua kwa mvua za masika, baadhi ya wakulima wa wilaya ya Uyui mkoani Tabora, nchini Tanzania wanasema hawajasazwa katika kukumbana na athari za mabadiliko hayo kwani hata mvua za masika walizokuwa wanazitegemea kukuzia mazao yao, zimekuwa za kusuasua. Kwa sababu hiyo wameamua kujikita katika kilimo cha muda mfupi katika bustani ndogondogo ili waweaze kujikumu kimaisha lakini bado wanakumbana na changamoto nyingine ikiwemo kukosa mbegu na pembejeo, na kulazimika kutumia sumu nyingi ambazo ni hatari kwa mazingira na afya. Hamad Rashid wa Redio washirika Tanzania kidstime fm kutoka Mkoa wa Morogoro amesafiri hadi Magharibi mwa Tanzania Kata ya Ibelamilundi Wilaya ya Uyui Mkoa wa Tabora na kuzungumza na wakulima.
Rais wa Rwanda, Paul Kagame Alhamisi aliikosoa Jumuiya ya kimataifa kwa "kukaa kimya wakati wa mauaji ya kimbari ya mwaka wa 1994," ambapo inaaminika kwamba takriban watu laki nane walipoteza maisha yao katika mashambulizi yaliyowalenga zaidi Watutsi.
Viongozi wa mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi na lile la Uhamiaji IOM Antonio Vittorino wamefanya ziara nchini Niger, huko Agadez ambalo ni eneo la mpito la watu wanaotafuta hifadhi na wahamiaji nchini Niger ambalo limeongezeka kuwa na idadai kubwa ya watu wenye kuhitaji msaada wa usalama na fursa. Taarrifa ya UNHCR inasomwa studioni na Evarist Mapesa wa redio washirika Redio SAUT ya Mwanza, Tanzania. Jamhuri ya Niger, taifa hili lisilo na bahari lililopo Magharibi mwa Afrika limepakana na mataifa saba ya ambayo ni Chad, Benin, Algeria, Nigeria, Mali, Burkina Faso na Libya. Kupakana na mataifa hayo kumeifanya nchi hii kuwa kitovu au njia ya wanaoelekea kaskazini mwa Libya, Algeria, na Bahari ya Mediterania. Kwa sasa nchi hii inashuhudia kuongezeka kwa idadi ya watu wanaokimbia Libya au kufukuzwa kutoka Algeria. Mmoja wa watu hao ni Safa Ahmed yeye alikimbia Sudan miaka mitano iliyopita na kukwama nchini Libya. Lakini sasa amefanikiwa kusafiri hadi hapa Agadez nchini Niger. “Kusema ukweli maisha ya hapa, mbali na kwamba sina mama na baba yangu ni mazuri. Asante Mungu. Ninafanya kazi, binti zangu wanasoma tena kwa Kiingereza. Nina biashara ya kuuza nguo na manukato. Naweza kufanya kazi. Sitarajii chochote kutoka kwa mtu yeyote. Nina kila kitu. Kwenye fikra zangu nimeshaachana na Libya.” Kauli yake inaungwa mkono na Mkimbizi huku kutoka Cameroon ambaye anasema, “Tunamshukuru Mungu kwamba serikali ya Niger ilitupokea na kutupa mahali pa kulala na tunashukuru sana lakini sisi hapa, shida yetu kuu ni maisha yetu ya baadaye.” IOM Ukarimu wa Niger unamfurahisha Filippo Grandi, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa anahusika na Wakimbizi ambaye anasema lengo kuu la UNHCR ni kuhakikisha wale wanaotafuta ulinzi wanapata usaidizi na wanapata hifadhi. “Nimefurahi sana, tumekuja hapa kujaribu kuona majukumu yetu ni nini na jinsi ambavyo kwa pamoja, tunaweza kusaidia watu hawa katika harakati zao, wakazi wa eneo hili na mamlaka ya nchi ambayo inabaki kuwa wakarimu sana na iko tayari kukaribisha kila mtu.” Pamoja naye ni Antonio Vittorino, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM ambaye anasema, "UNHCR na shirika letu (IOM) kama sehemu ya Umoja wa Mataifa, kufuatia uamuzi wa Katibu Mkuu, tuna jukumu la kushiriki zaidi kushughulikia mahitaji ya wasaka hifadhi.” Wengi wa wasaka hifadhi wamepokelewa katika Kituo cha misaada ya Kibinadamu, eneo lililopo nje kidogo ya Agadez ambapo wanapata huduma za afya, shughuli za kiuchumi, maji, makazi na chakula yakiwa ni miongoni mwa mahitaji mengine ya kimsingi.
Baada ya wimbi la ugonjwa wa Covid-19 lililodumu kwa takribani wiki sita, wimbi hilo la nne barani Afrika ambalo kimsingi lilichochewa na mnyumbuliko wa virusi vya corona kwa jina Omicron, sasa linapungua na hivyo kulifanya kuwa wimbi lililodumu kwa muda mfupi zaidi katika bara hilo ambako jumla ya maambukizi hivi sasa tangu kuibuka kwa ugonjwa huo limezidi milioni 10. Imeeleza taarifa ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa kanda ya Afrika iliyotolewa hii leo Brazzaville nchini Congo. Leah Mushi anayo taarifa kamili. WHO inasema maambukizi ya kila wiki yaliongezeka katika siku saba hadi tarehe 9 Januari kutoka wiki iliyokuwa imetangulia. Kusini mwa Afrika, ambako kulishuhudiwa ongezeko kubwa la maambukizi wakati wa wimbi, taarifa njema ni kuwa kumerekodiwa kupungua kwa maambukizi kwa asilimia 14 katika wiki iliyopita. Afŕika Kusini, ambapo mnyumbuliko wa Omicron uliripotiwa kwa mara ya kwanza, imeshuhudia kushuka kwa asilimia 9 kwa maambukizi ya kila wiki. Kanda za Afrika Mashariki na Kati pia nazo zimeshuhudia kupungua kwa maambukizi. Hata hivyo, Afrika Kaskazini na Magharibi inashuhudia kuongezeka kwa maambukizi, huku Afrika Kaskazini ikiripoti ongezeko la asilimia 121 katika wiki iliyopita ikilinganishwa na ile wiki iliyopita. “Katika bara zima, hata hivyo, vifo viliongezeka kwa asilimia 64 katika siku saba zilizomalizika tarehe 9 ya mwezi huu wa Januari ikilinganishwa na wiki iliyotangulia hasa kwa sababu ya maambukizi miongoni mwa walio katika hatari kubwa. Pamoja na hayo, vifo katika wimbi la nne ni chini kuliko mawimbi ya awali. Idadi ya wagonjwa wanaolazwa imesalia chini kwa mfano nchini Afrika Kusini katika vitanda 5600 vya chumba cha wagonjwa mahututi, ni asilimia 9 tu ya vitanda hivyo imelaliwa na wagonjwa wa Covid-19.” Inaeleza WHO lakini ikionya kuwa, “wakati bara la Afrika linaonekana kukabiliana na wimbi la hivi karibuni la janga hili la Corona, waliochanjwa bado ni wachache. Ni takriban asilimia 10 tu ya wakazi wa Afrika wamechanjwa kikamilifu." Usambazaji wa chanjo kwa bara umeboreshwa hivi karibuni, na WHO inaongeza msaada wake kwa nchi ili kufikisha dozi kwa watu wengi zaidi barani humo.
Mhogo ni chakula kinachoenziwa na wengi na zao ambalo limewapa wakulima mapato humu nchini. Chakula chake ni maarufu katika baadhi ya mataifa ya bara la Afrika, Asia na Amerika Kusini. Kulingana na shirika la utafiti wa kilimo na mifugo humu nchini KALRO, mihogo inapandwa katika hekari laki moja na elfu sabini na mbili nchini ambapo asilimia 60 hupandwa kutoka eneo la Magharibi, Pwani asilimia 30 na eneo la Mashariki likiwa na asilimia 10. Licha ya kuwa tegemeo kwa wakulima, ukulima huo unakabiliwa na changamoto za maradhi ya aina mbili na kusababisha hasara ya mapato kwa wakulima. Moja wapo ya maradhi hayo ni yale ya cassava brownstreak disease yanayofanya mhogo kuwa rangi ya kahawia na yale ya cassava mosaic ambayo yanaweza kudhibitiwa. By:Ali Mwalimu
siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Scotland, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi. (Taarifa ya John Kibego) “Hatujawahi kuona mwaka kama 2021. Huu ni mwaka wenye mioto mingi ya nyika.” Anasema Ahmedou El-Bokhary, Rais wa Kikosi cha zima moto kinachoundwa na wakimbizi. Andrew Harper, Mshauri Maalumu wa masuala ya hatua dhidi ya tabiachi kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, amejionea hali hiyo inayosemwa na anasema, “hii sio vita ambayo kunaweza kuwa na makubaliano ya amani nayo,” na anaongeza akisema, “Mauritania siyo tu ni mwenyeji wa maelfu ya wakimbizi, lakini moja ya nchi ambazo zimathiriwa zaidi na mabadiliko ya tabianchi.” Yahya Koronio Kona yeye ni mkimbizi kutoka Mali anasema, “mito inapungua kina cha maji. Idadi ya samaki inakuwa ndogo, inasababisha matatizo.” Bwana Harper anaendelea kueleza hali ilivyo mbayá akisema, "kuzunguka mito hii, kuna mifugo na hii mifugo inagombea vyanzo hivi vya maji. Na kwa hivyo moja ya changamoto kubwa sasa ni tuna ushindani kwenye rasilimali hizo zinazopungua, na maji pengine ni dalili zaidi ya changamoto za mabadiliko ya tabianchi. Na kwa hivyo tunatakiwa kufikiria kinachofuata.” Wakimbizi wanasema wakati jua kali linapowaka, nyasi zinakauka na kushika moto. Na hapo kikosi chao cha kuzima moto kinaingilia kwani hawana namna nyingine. “Pamoja na changamoto zote,” anasema Bwana Harper, “pamoja na kile watu wanachofanya katika nchi za Magharibi kuiharibu dunia, watu wanaoteseka zaidi wanajaribu kufanya uamuzi sahihi ili kuyalinda mazingira na kutoa karibu muongozo ambao ni, ‘Kama tunaweza kufanya, kwa nini wengine duniani wasiweze?'”
Tunaangazia juu ya changamoto za ujasiriamali kwenye vikundi vya walemavu nchini Tanzania. Kwa namna ya pekee tutawasikia baadhi ya walemavu na wadau wengine wanaohusika kuhakikisha mlemavu anajiwezesha kiuchumi huko mjini Bukoba, mkoani Kagera, Magharibi mwa Tanzania.
Kikoshi cha kulinda amani cha Tanzania nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR kijulikanacho kama TANZBAT4 kimetunukiwa nishani ya utendaji bora katika halma maalum iliyofanyika kwenye eneo la Berberati Magharibi mwa nchi hiyo. Luteni Noela Julius Nyaisangah afisa Habari wa TANZBAT 4 ameshuhudia na kuandalia taarifa hii (TAARIFA YA LT NOELA JULIUS NYAISANGAH) ….. Gwaride la walindamani with sound…… Ni sherehe maalum za kuwatunukia nishani maafisa walindamania wa kutoka Tanzania wa kikosi cha 4 au TANZBAT 4 wanaohudumu kupitia mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR uitwao MINUSCA. Kikosi hicho kinachoongozwa na Luteni Kanali Alexander Edward Masangura kiliwasili CAR mwezo Novemba mwaka 2020 Magharibi mwa nchi hii na sasa kimehitimisha miezi 9 ya ulinzi wa amani na kutunukiwa nishani ya Umoja wa Mataifa kutokana na weledi wao mkubwa. Sherehe hizo zimeambatana na shamrashamra mbalimbali ikiwemo gwaride maalum lililoongozwa na Meja Baraka Songoro. Katika hafla hiyo mwakilishi na mkuu wa vikosi vya ulinzi wa amani vya MIUNUSCA Meja Jenerali Paulo Maia Pereira amewapongeza maafisa wa TANZBAT 4 kwa utendaji wao mzuri wenye tija katika shughuli za ulinzi wa amani kwenye Umoja wa Mataifa. Itakumbukwa kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika medani za kimataifa kwenye ulinzi wa amani, ambapo inashiriki katika opereshani mbalimbali duniani ikiwemo hapa CAR, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Dafur Sudan na Lebanon. Natss… with sound, wanajeshi mazoezi utoka hapa Berberati Magharibi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati mimi ni Luteni Noela Julius Nyaisangah.
Je, unafahamu historia ya jiji kuu la Kenya Nairobi ? Tunakufahamisha pia kuhusu utamaduni wa mafali kupambanishwa, Magharibi mwa nchi hiyo.
Wakazi wa jimbo la Magharibi Australia wameishi, kwa muda mrefu bila vizuizi vyovyote vya Coronavirus tofauti na wenzao kote nchini Australia.
Chama cha Labor kimeshinda muhula wa pili serikalini, katika uchaguzi wa jimbo la Magharibi Australia uliofanyika wikendi hii.
Watu zaidi ya 5,000 wamefungasha virago siku za karibuni wakikimbia mashambulizi ya waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR hasa kwenye mji wa Magharibi wa Bouar na kuingia nchi jirani ya Cameroon kusaka usalama, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR. Jason Nyakundi na maelezo zaidi.
Kwa muda mrefu nimekua nikitaka kuongea na Mavoko ila ratiba zetu zilikua hazijawahi kuwa sawa na hivyo tukawa tunapishana tu. Kama mimi sina program naye basi yeye atakua free, na mimi nikiwa free basi yeye atakua na mipango ya kutoa kazi mpya ambayo itanifanya ningoje ili viende pamoja, au atakua kasafiri, au mimi nitakua nishaset watu wengine, ilikua kama tunacheza kidali po ila katikati ya mwezi wa kumi na mbili hatimaye yakatimia. Hakuna doubt juu ya uwezo wake popote pale utakapoenda ingawa baada ya yeye kuamua kuondoka kwenye label ya WCB kulikua na mengi yalosemwa na kutendwa na baadhi ya mashabiki yalikua yanaweza kukuaminisha jambo na mpaka kufikia pengine ku doubt huo uwezo wake. Mambo mengi yalisemwa, ya kusikitisha, ndoa haikuvunjika vizuri ila ambacho nilikiona kwake ni ustaarabu wa hali ya juu, wa kuwaacha walimwengu waseme na kufanya watakayo huku yeye akiwa ame focus kwenye kipaji chake na kujipanga upya. Moto wa Mama Richard anaujua mziki mwingi, ana uwezo mkubwa wa kuimba na kuandika na kucheza pia, ila kabla hajaingia kwenye label alikua anajulikana tu, ila kumfahamu vizuri na kuthamini kipaji chake kulikuja baada ya yeye kushirikiana na mmoja kama si msanii bora zaidi kuwahi kutokea na kuipeperusha zaidi bendera ya Tanzania ndani ya Diamond Platnumz. Ushirikiano wao ulitupa ‘anthem' kadhaa ambazo mpaka leo ukiziskiliza hazichuji. Ilikua kama team ya wenye vipaji pekee, kama ni mfuatiliaji wa mpira wa kikapu hii tunaweza kuifananisha na ile zile team mbili za Mashariki na Magharibi ambazo zinakusanya wachezaji wenye uwezo wahali ya juu. Saasa, ikawaje hasa mpaka akaona aachane na all star hiyo na kupeleka team yake uwanjani akiwa solo? Nini hasa kilifanya mpaka afikie maamuzi hayo? Kuna mtu au kitu kilimshinikiza? Je yalikua maamuzi sahihi? Pia kuna masuala binafsi ya kifamilia na suala la yeye kutomfahamu Baba yake takati anakua, elimu yeke, ndugu zake, Mama yake na muziki ulichomfanyia katika maisha yake. Mavoko huyu ambaye mimi namfahamu nilikutana naye Kampala, Uganda kama maka saba iliyopita na mazungumzo yetu yalikua yanahusu kipaji chake na jinsi ambavyo nilikua naona ‘hapewi' nafasi maana kama ngoma zake zilikua nzuri tu, video ndo usiseme ila hakuna na spotlight aliyokua anastahili, peleka mbele miaka mpaka 2021 ambapo alipata nafasi kwa miaka takriban miwili na nusu kufanya kazi na lebo bora zaidi ila baada ya muda akaamua kubwaga? Kwanini hasa? Sote tunajua kama nyasi za jirani huonekana zimestawi kweli kweli ila ukifika na kuziona kwa ukaribu utaelewa kwamba si kila kitu kina fanana na kionekanavyo. Ila mpaka kuamua kukusanya na mabegi na kuondoka kwenye ‘jumba kali'? Majubu yake yalikua ya moja kwa moja tu na nafsi yake ilikua tayari kuhamia nyumba nyengine mwenzangu. Natumai kwa kiasi flani utasoma jambo, ingawa kwangu mimi natamani ningepata zaidi na zaidi ila inaonekana bado hakua tayari kutufungukia mazima. Binafsi namshkuru kwa kuja mezani kwetu na pengine tutaweza kukutana tena mbeleni In Shaa Allah. Yangu matumaini bado utaokota mawili matatu. Love, Salama. --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu katika Jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini hivi karibuni wakati wakiwa kwenye doria ya umbali mrefu, wametembelea jamii kadhaa za vijijini ili kufahamu kuhusu changamoto zao na kuwaelimisha kuhusu COVID-19.
Jeshi la jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, juma hili lilifahamisha kuwa limedhibiti ngome muhimu ya Madina baada ya kuwatimua waasi wa ADF, huko Kenya waalimu watishia kuondoka katika eneo la Garissa kwa sababu za kiusalama, viongozi wa mataifa ya Sahel walikubaliana kuhusu kuimarisha mapambano dhidi ya magaidi, na huko Marekani mchakato wa kumuondoa madarakani rais Donald Trump washika kasi
Kilimo Ajira 5: Making a living of Sweet Potato vine production Growing Sweet Potato can not only help to feed your family or be grown to sell. In Western Kenya, there also is a market for Sweet Potato vines. If done right, this can be a lucrative business. The professional vine multiplier Ruth Maruti from Bungoma County explains how her business works. Kilimo Ajira 5: Kujikimu ki maisha kwa uzalishaji wa mbegu za viazi vitamu Ukulima wa viazi vitamu haiwezi tu kulisha familia yako au kuuza. Magharibi mwa Kenya, kuna soko kubwa ya mbengu za viazi vitamu. Ikitekelezwa kwa njia sawa, inaweza kuwa biashara yenye mapato makubwa. Mtaalamu wa ukuzaji wa mbegu za viazi vitamu Ruth Maruti kutoka kaunti ya Bungoma anaeleza jinsi biashara yake huenda.
The Prime Minister and Opposition Leader will hold the first debate of the election campaign in Perth next week, where as many as six marginal seats are up for grabs. - Waziri Mkuu na kiongozi wa upinzani wata fanya mjadala wa kwanza katika kampeni ya uchaguzi mjini Perth wiki ijayo, ambako chama chochote kinaweza shinda takriban maeneo bunge sita.
1 - Quenacho (Sahalé Nightline Edit) - erik the flutemaker 2 - Sahalé & Samarana - Ntaolo - tropical twista records 3 - Dakha Brakha Yagydku (Remix) - sahale 4 - Erzeroumi Shoror - arax 5 -Mah Sheed - sahale 6 - Tarlabasi - Be Svendsen Remix - oceanvs orientalis 7 - Saana - sahale 8 - Magharibi - sahale 9 - Isra (Original Mix) - azur 10 - Tortuous Maze (Original Mix) - sahale 11 - Middle Eastern Promises - sahale 12 - Esfahran - sahale 13 - Phara Oh - dole & kom 14 - dijin (original mix) - sahale 15 - surrender - (andre winter remix )
Makala ya Wimbi la Siasa Juma Hili Inaangazia Hali ya Kisiasa Nchini Iran Ambayo Kwa Majuma Kadhaa Imeshuhudia Maandamano ya Wananchi Wakipinga Hali Ngumu ya Maisha. Hata Hivyo Juma Hili Pia Wafuasi Wanaoiunga Mkono Serikali Nao Walifanya Maandamano Kuonesha uungaji Mkono Wao Kwa Serikali. Nini Hatma ya Siasa ya Nchi ya Iran? Ni Kweli Nchi za Magharibi Zina Mkono na Vurugu Zilizoshuhudiwa Iran?
Makala haya ya Afrika ya Mashariki yanaangazia juu ya changamoto za mauaji ya walemavu wa ngozi (Albino), ambayo yamekithiri katika kanda ya ziwa Magharibi mwa Tanzania.
Mission Europe - Mission Berlin | Kujifunza Kijerumani | Deutsche Welle
Katika Berlin iliyogawanyika, Anna anapaswa kutoka Mashariki kwenda Magharibi. Hilo silo tatizo la pekee. Ana muda wa dakika 55 kuchunguza lengo la RATAVA. Je ni ujenzi au kubomolewa ukuta? Mwaka 1961, Anna anajaribu kufika Kantstraße. Lakini Kantstraße iko Berlin Magharibi na yeye yuko Berlin Mashariki. Anna hawezi kwenda Magharibi kwa sababu serikali ya Ujerumani Mashariki imeanza kujenga ukuta. Baada ya kuanzishwa upya kwa mchezo, mchezaji na Anna wanagundua kuwa huenda malengo ni mawili: ujenzi au kubomolewa Ukuta wa Berlin. Wanabakiwa na dakika 55 kuchunguza kujua lengo la RATAVA.
Deutsch – warum nicht? Fungu 4 | Kujifunza Kijerumani | Deutsche Welle
Mkoa unajitangaza: Muhtasari wa sarufi: Hakuna sarufi mpya